Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,173
Tido na wenzake wangolewa MDTF
na Mwandishi wetu
MAMBO ndani ya Chama cha Maendeleo Muheza (MDTF), yamezidi kuharibika baada ya sekretarieti inayoongozwa na Tido Mhando, kupinduliwa rasmi na genge linalojiita wanachama wakereketwa.
Kupinduliwa kwa sekretarieti hiyo kumekuja mwezi mmoja baada ya wanachama hao chini ya uongozi wa, Halid Kibwana, kutoa kitisho cha kufanya mapinduzi hayo.
Waraka wa maandishi uliosambazwa kwa baadhi ya wakazi wa Muheza waishio jijini Dar es Salaam umetaja uamuzi huo unalenga kukinusuru chama ambacho kinaelekea kufa tangu kuingia madarakani kwa sekretarieti hiyo mwaka juzi.
Tumeamua kuingoa sekretarieti ya MDTF kutokana na kushindwa kazi kwani tangu iingie madarakani mwaka juzi chama hakina ofisi, hakina hata shilingi kwenye akaunti, shughuli za utawala zimesimama na mipango yote ya maendeleo ikiwemo kuanzisha saccos Muheza imekufa, inasomeka sehemu ya waraka huo.
Inaeleza pia kuwa alipoondoka Balozi Adadi Rajabu, aliacha chama kikiwa hai kwani alijenga shule ya sekondari na kufanya mambo mengine ya maendeleo tofauti na iliyo sasa ambayo ni mzigo.
MDTF inaundwa na sekretarieti inayoongozwa na Tido akiwa ni Mwenyekiti, Marry Chipungahelo- Makamu Mwenyekiti, Albert Semngindu Katibu.
Wengine ni Nehemia Mchechu ambaye ni Mweka Hazina na Mkurugenzi Mkuu Shirika la Nyumba (NHC) na Ramadhan Semtawa, Katibu Mwenezi huku Mkurugenzi Mtendaji akiwa ni Clement Mangenya.
Alipoulizwa jijini Dar es Salaam jana kwa njia ya simu, msemaji wa MDTF, Semtawa, alikiri kupata waraka huo na kuongeza kwamba bado anawasiliana na wenzake kuona namna ya kufanya.
na Mwandishi wetu
Kupinduliwa kwa sekretarieti hiyo kumekuja mwezi mmoja baada ya wanachama hao chini ya uongozi wa, Halid Kibwana, kutoa kitisho cha kufanya mapinduzi hayo.
Waraka wa maandishi uliosambazwa kwa baadhi ya wakazi wa Muheza waishio jijini Dar es Salaam umetaja uamuzi huo unalenga kukinusuru chama ambacho kinaelekea kufa tangu kuingia madarakani kwa sekretarieti hiyo mwaka juzi.
Tumeamua kuingoa sekretarieti ya MDTF kutokana na kushindwa kazi kwani tangu iingie madarakani mwaka juzi chama hakina ofisi, hakina hata shilingi kwenye akaunti, shughuli za utawala zimesimama na mipango yote ya maendeleo ikiwemo kuanzisha saccos Muheza imekufa, inasomeka sehemu ya waraka huo.
Inaeleza pia kuwa alipoondoka Balozi Adadi Rajabu, aliacha chama kikiwa hai kwani alijenga shule ya sekondari na kufanya mambo mengine ya maendeleo tofauti na iliyo sasa ambayo ni mzigo.
MDTF inaundwa na sekretarieti inayoongozwa na Tido akiwa ni Mwenyekiti, Marry Chipungahelo- Makamu Mwenyekiti, Albert Semngindu Katibu.
Wengine ni Nehemia Mchechu ambaye ni Mweka Hazina na Mkurugenzi Mkuu Shirika la Nyumba (NHC) na Ramadhan Semtawa, Katibu Mwenezi huku Mkurugenzi Mtendaji akiwa ni Clement Mangenya.
Alipoulizwa jijini Dar es Salaam jana kwa njia ya simu, msemaji wa MDTF, Semtawa, alikiri kupata waraka huo na kuongeza kwamba bado anawasiliana na wenzake kuona namna ya kufanya.