Tido Mhando nae Ang'oa

KakaJambazi

JF-Expert Member
Jun 5, 2009
18,711
12,067
Kuna tetesi kuwa aliyekua bosi wa TBC Tido Mhando naye ameng'oa vitasa na kukwapua mapazia ya ofisi.
Mwenye tetesi kamili atujuze.
 
Mh pole sana mkurugenzi tbc,sasa anza kuaply kazi nyingine bbc walau ya ufreelancer
 
Mimi namshauri apumzike au afungue kampuni ya ushauri kuhusu media comm. At his age haina haja kuzungusha cv kama vijana wadogo. Vinginevyo nitamfanisha na wale wanaosema hatuendi kubeba mawe au zege!
 
hivi tido hajafikia umri wa kustaafu aishi kwa pensheni yk kulikoni kuhangaika ameshafanya aache na wengine nao watoe mchango wao
 
Jana nilimsikia akilialia TBC eti amepewa barua ghafla ya kuachia ulaji, japo alijua mkataba unaisha Dec 15.Alitegemea kwa kazi aliyofanya angeendelea kuula kwa miaka 4 ijayo.
 
Kilichonisikitisha ni jinsi alivyojieleza... kwangu binafsi sioni kama ni professionalism imetumika pale, nadhani ameweka siasa na kuthibitisha majungu, IF YOU ARE GOOD, YOU ARE GOOD REGARDLESS YA KAMA UMEONDOLEWA AU KUONDOKA

kama wote wangekua wanajieleza hivi basi radio na TV zingekua na vipindi maalum kwa wakubwa walioondolewa au kuondoka kwenye mashirika ya umma... Tusitafute mchawi, mchawi ni yeye mwenyewe kukubali hiyo kazi in the first place

Hayo ya kungoa vitasa naona in rumours kama ambavyo some members of JF kwa sasa ni rumour mongers, na hawataki kuwa serious kwa chochote zaidi ya kuandika wadhaniacho

I WISH HIM ALL THE BEST, HE WAS BROUGHT FOR A SPECIFIC PURPOSE AND I AM SURE HE HAS FULFILLED IT
 
Jana nilimsikia akilialia TBC eti amepewa barua ghafla ya kuachia ulaji, japo alijua mkataba unaisha Dec 15.Alitegemea kwa kazi aliyofanya angeendelea kuula kwa miaka 4 ijayo.
anacho lalamika ni nijinsi ulivyo kiukwa mkataba wake walitakiwa wamjulishe miezi 6 kabla ya mkataba wake kuisha kuwa hawataongeza mkataba hivyo kukaa kwao kimya kulishalia mambo safi kwake...
 
ila hawako fair, tbc bila TIDO Mhando ilikuwa haiangaliki na kwa kweli ilikuwa hana wapenzi wengi, labda wale makada wa ccm tu ndio walikuwa wanaifuatilia
 
ila hawako fair, tbc bila TIDO Mhando ilikuwa haiangaliki na kwa kweli ilikuwa hana wapenzi wengi, labda wale makada wa ccm tu ndio walikuwa wanaifuatilia
ze comedy hawajachangia kuleta wapenzi kwenye hii tiivii?:embarrassed:
 
Kilichomuondoa TBC1 ni kuendelea kuonyesha vipindi vya kampeni za vyama vya upinzani ili khali CCM walishajitoa....
 
Hakupasa kutolewa jinsi walivyomtoa hata kama mkataba uliisha.swala la kua na kipindi maalumu kuongelea swala lake tbc ni sahihi kabisa.yeye ni staff wa ile organization so anayo haki ya kui2mia,kama tu staff wengine wakifunga ndoa wanavyo 2mia tbc kutangaza.serikali imechemka.na kuchemka kwake ni kudhihirisha kua haitaki wachapa kazi wanaoleta positive changes,wao wanataka puppets wa kila wakati ndio mzee.
 
Back
Top Bottom