Tido Mhando na Ubinafsishaji wa TBC kwa StarTimes

Halisi, kama sheria itakuwa kushoto kwao, je nani anaweza kutengua ubia huu.. TCRA, Bunge au Mahakama ndiyo wanaweza?!

Kwa ninavyofahamu ni kwamba kwa sasa tayari watu kadhaa wamewasilisha pingamizi TCRA kwa mujibu wa sheria, ambako siku ya mwisho ilikua Ijumaa iliyopita. Waliowasilisha malalamiko hayo ni Watanzania wakiwamo viongozi wa Kiislamu ambao nao wana hoja nzito ya kutengwa katika masafa na wengine walioona kasoro hizo.

Lakini kwa maelezo yangu hapo juu, sidhani kama kuna mtu mwenye kuitakia mema nchi hii atakayeendelea na zoezi hili labda iwe ile ile hali ya kusema "This is Made in Tanzania Only" hapo nitaelewa. Kuna mapungufu mengi ya kiutendaji, kisheria na kiusalama ambayo yanalifanya zoezi zima liweze kurudiwa na TBC watapata nafasi ya kujipanga upya kwa kuzingatia maslahi ya umma.

Hapo juu nimezungumzia Waislamu lakini sijasema ni kitu gani. Ukisoma waraka wa TCRA kuna masafa ya aina tatu, ya kwanza ni ya UMMA yaliyopewa TBC na mawili ni ya "KIBIASHARA" ambayo vyombo vya habari vimewakilishwa na MOAT iliyounda kampuni na taasisi za dini zimeunda kampuni chini ya Agape. Sasa Waislamu wameshituka maana walikuwa katika majadiliano na wenzao wa Kikristo lakini kwa bahati mbaya wamejikuta wenzao wamesajili kampuni kinyemela na kupewa masafa na TCRA kwa kigezo cha kuwakilisha taasisi za dini. Sasa Waislamu wamelalamika rasmi na kupinga mchakato mzima kisheria.
 
Kwa ninavyofahamu ni kwamba kwa sasa tayari watu kadhaa wamewasilisha pingamizi TCRA kwa mujibu wa sheria, ambako siku ya mwisho ilikua Ijumaa iliyopita. Waliowasilisha malalamiko hayo ni Watanzania wakiwamo viongozi wa Kiislamu ambao nao wana hoja nzito ya kutengwa katika masafa na wengine walioona kasoro hizo.

Lakini kwa maelezo yangu hapo juu, sidhani kama kuna mtu mwenye kuitakia mema nchi hii atakayeendelea na zoezi hili labda iwe ile ile hali ya kusema "This is Made in Tanzania Only" hapo nitaelewa. Kuna mapungufu mengi ya kiutendaji, kisheria na kiusalama ambayo yanalifanya zoezi zima liweze kurudiwa na TBC watapata nafasi ya kujipanga upya kwa kuzingatia maslahi ya umma.

Hapo juu nimezungumzia Waislamu lakini sijasema ni kitu gani. Ukisoma waraka wa TCRA kuna masafa ya aina tatu, ya kwanza ni ya UMMA yaliyopewa TBC na mawili ni ya "KIBIASHARA" ambayo vyombo vya habari vimewakilishwa na MOAT iliyounda kampuni na taasisi za dini zimeunda kampuni chini ya Agape. Sasa Waislamu wameshituka maana walikuwa katika majadiliano na wenzao wa Kikristo lakini kwa bahati mbaya wamejikuta wenzao wamesajili kampuni kinyemela na kupewa masafa na TCRA kwa kigezo cha kuwakilisha taasisi za dini. Sasa Waislamu wamelalamika rasmi na kupinga mchakato mzima kisheria.

Ahsante sana Mkuu kwa habari hii. Inafariji.
 
Tayari Mkuchika ameibuka na kutoa ufafanuzi lakini hakuna popote alipozungumzia kuhusu mambo makubwa ya msingi.
-Hakusema kwanini wamewapa Wachina 100% na badala yake amesema kwamba TBC haijauzwa bali imeingia ubia.
_PPRA wamenukuliwa wakisema hawana taarifa, Mkuchika anadai sheria za PPRA zimefuatwa, na kutaja mamlaka kadhaa zilizohusika.
_Mkuchika hakusema kuhusu matumizi ya Dola badala ya Shilingi
_Mkuchika hakusema kuhusu kusajiliwa chapuchapu na hata kukosewa
_Mkuchika hakusema kuhusu kuzuiwa kwa hisa kuuzwa katika soko la hisa
_Mkuchika hakusema kuhusu usalama wa masafa yetu kama 65% ziko kwa Wachina
_Mkuchika hakusema kuhusu Waislamu kutengwa na Agape kujibebesha jukumu
_Mkuchika hakusema lolote kuhusu TBC kuomba lakini Star Media kumilikishwa
_Mkuchika hakusema kuhusu maana ya masafa ya umma ni nini
 
MKUCHIKA anasema TBC ni mali ya umma na itaendelea kuwa hivyo kama shirika la umma linalomilikiwa na serikali kwa asilimia 100 na kuongeza kuwa Star Media Tanzania
Limited ni Kampuni tanzu ya TBC.??????!!!!!


Jamani nadhani alikuwa hajaingia JF
 
Last edited:
story kamili ya Mkuchika hii hapa:

Serikali imekanusha madai ya shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) kuuzwa kinyemela kama ilivyoonyeshwa katika taarifa iliyotolewa na chombo kimoja cha habari hapa nchini.

Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar esa Salaam na Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo George Mkuchika wakati wa mkutano na waandishi wa habari kuhusu hatua iliyochukuliwa na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) kuunda kampuni mpya iitwayo Star Media (Tanzania) Limited kwa ubia na mwekezaji.

Amesema Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) kama shirika la umma halijauzwa na kuwataka wananchi kutoamini taarifa zozote zinazotolewa kuhusu kuuzwa kwa namna yoyote kwa shirika hilo.

“ Nawathibitishieni leo kuwa shirika la Utangazaji (TBC) halijauzwa ,bado ni la wananchi na kamwe halitauzwa” amesisitiza.

Ameongeza kuwa TBC ni mali ya umma na itaendelea kuwa hivyo kama shirika la umma linalomilikiwa na serikali kwa asilimia 100 na kuongeza kuwa Star Media Tanzania Limited ni Kampuni tanzu ya TBC.

Amefafanua kuwa TBC imeunda kampuni hiyo mpya kwa ubia na mwekezaji aliyeteuliwa kihalali ili kutekeleza mabadiliko ya Digitali na kuendesha mitambo ya kurushia matangazo yake nchi nzima kazi ambayo itakamilika mwaka 2012 kwa gharama ambazo TBC isingeweza kuzimudu yenyewe kutokana na jukumu hilo kuhitaji utaalam mkubwa wa kiufundi ili kukamilisha ufanisi.

Waziri Mkuchika ameendelea kufafanua kuwa Serikali ina jukumu la kuhakikisha inaiwezesha TBC kutekeleza wajibu wake wa kufikisha matangazo yake nchi nzima na kuongeza kuwa ililiruhusu Shirika hilo kutafuta mwekezaji ili kutekeleza mradi wa mabadiliko ya mfumo wa utangazaji kutoka analojia kwenda digitali na kukuza mtandao wake kuenea nchi nzima jambo ambalo limefanyika na kutekelezwa kwa kufuata taratibu zote zinazostahili.

“ Kampuni hii si ya matapeli ,uteuzi wake hii ulifuata taratibu uwekezaji, taratibu za manunuzi ya umma kutoka mamlaka husika kwa maandishi (Public Procurement Regulatory Authority) na pia ushauri wa wataalam wa mamlaka mbalimbali husika”

Akizungumza kuhusu mradi huo amesema kuwa utaiwezesh TBC kubadilisha mfumo mzima wa utangazaji wa televisheni kuwa digitali na kusamabaza matangazo yake na ya watangazaji wengine kufika maeneo yote nchini na kuongeza kuwa ifikapo mwaka 2012 matangazo ya televisheni ya digitali yatafika kote nchini yakiwemo maeneo yote ambako matangazo hayafiki kwa sasa.

Kuhusu uteuzi wa mbia waziri Mkuchika amesema ulifanywa na Bodi ya wakurugenzi ya TBC baada ya tathmini ya kina iliyowashrikisha wataalam kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo, Wizara ya Mwasiliano, Sayansi na Teknolojia , COSTECH, TCRA na Kituo cha Taifa cha Uwekezaji (TIC) kuchambua na kupendekeza mbia anayefaa .

Ameendelea kufafanua kuwa makampuni 5 ya kimataifa yalionyesha nia ya kushirikiana na TBC katika kutekeleza mradi huo wa digitali na kuombwa kuwasilisha michanganuo yao ya utekelezaji na baadye kampuni ya Star Communication Network Technology Co. Ltd ya China iliteuliwa kwa kufuata taratibu.

Aidha tathmini na uwezo halisi wa mwekezaji ulifanywa na ujumbe wa wataalam kutoka TBC wakiongozwa na katibu mkuu Wizara ya Habari na Utamaduni na Michezo kwa kushirikiana na ubalozi wa Tanzania nchini China waliitembelea kampuni hiyo iliyoko Beijing China ili kuhakiki uwezo wake kabla ya kusaini mkataba.

Hata hivyo waziri Mkuchika amevitaka vyombo vya habari nchini kuzingatia weledi katika taaluma ya uandishi wa habari na kusisitiza kuwa mchakato mzima ulikuwa wazi na mkataba wa ubia uliandaliwa kwa pamoja kwa kufuata taratibu zote ikiwemo kumshirikisha mwanasheria mkuu wa serikali kabla ya kusainiwa.
 
jamani hiyo $1m ni bei ya TBC yote au ni kiwanja cha TBC.....
jamani hiyo TBC ni mbaya kiasi gani mpaka ikawa valued $1m..
yaani hiyo TBC ni cheap kulikoni nyumba za mafisadi wailzoweka bond kwenye kesi zao....
 
jamani hiyo $1m ni bei ya TBC yote au ni kiwanja cha TBC.....
jamani hiyo TBC ni mbaya kiasi gani mpaka ikawa valued $1m..
yaani hiyo TBC ni cheap kulikoni nyumba za mafisadi wailzoweka bond kwenye kesi zao....

Mkuchika amekuwa mkali na sasa wameamua kuwatishia hata MwanaHalisi!!!!
 
Kila Waziri au Kiongozi wa GOT anakula sehem yake....!!!! wana "vibuzwagi" au vi-"EPA" vyao vya kimtindo...!!!
 
Hwa watu bwana unashindwa hata pa kuanzia... hivi hii serikali inaipeleka wapi hii nchi.. hivi hii CCM itanawa hizi damu za watanzania zitakazo mwagika?????
 
Je tunaweza kumtafuta mwanasheria na tukaingia mahakamani kupinga udhalilishwaji wa namna hii ama we will need a 90days notice kama tunataka kuishitaki serikali ? Maana JF we can do it tumlipe Tundu Lissu wengine wote ni waoga na wana nunulika .

Swali tunaweza ? Je tukiweza kisheria tuchangishaje ? Maana ukikaa namna hii kesho utafungwa kamba mbele ya mkeo na watoto kwa kuambiw CCM wamesha weka sahihi wewe twende ukalime tu .
 
mh, wewe GT!
TBC imeuzwa kwa wachina?!!!
lini? kwa nini iuzwe?
chanzo cha habari yako ni wapi?
maana hapa usilete habari zisizo na uhakika.

Kama maelezo yanavyosomeka hapo juu, haijauzwa jumla, ila wachina wana hisa 65% katika TBC. Kimsingi kinacholalamikiwa na Watanzania ni kwamba hakukutangazwa tenda ya ushindani chini ya PPRA ili kuwashindanisha wabia wa kuwekeza ktk masafa ya TBC. Wachina walipewa tu kimya kimya kazi hii! Na hio ni kinyume cha sheria kwa Tanzania.

Mbona hakuna habari ya kuuzwa? Inaonekana ni partnership. Sasa sijui tukifika kwenye digital inamaana ndio mambo ya TV licence? Kazi kweli au ndio subscrptions kwenye channels. Nadhani hawataminya matangazo yoote na wanania ya kuongeza channels. Tafsiri ya kuuzwa na ufisadi ni ya mbali saana

Kaka,
kinacholalamikiwa hapo ni kwamba, huo ubia ulitangazwa wapi? Wangapi walishindana ili kupata mbia stahiki wa kuwekeza ktk TBC? Je wakati wa kuwapa wachina kazi hii, je sheria za PPRA zilifuatwa? Haya ndio maswali ambayo Watanzania wanataka kujua.


jaribu kutoa habari zenye uhakika zingatia sana vyanzo vya habari
usipotoshe jamii kuwa mwangalifu.

Bro, usidandie gari kwa mbele!
JF inaenda kwa facts na si kutishana. You are in a wrong place!
Habari hizi ni za uhakika. Mwanahalisi wamemhoji Tido Mhando na amekiri kufanya kitu hicho, na wamawahoji pia watu wa hazina na wakakiri kwamba Tido hakuwahusisha ktk dili nzima. Soma gazeti la Mwanahalisi la jana juma5, kuna habari nzima ya sakata hili.


Sikuamini mzoefu kama GT anaweza andika utumbo kama huu alioutoa hapa!

Kaka, sio utumbo, haya masuala ni real. Soma attached PDF docs hapo juu ujue ukweli halisi!
 
halafu kuna habari kuwa kutokana na huo mkwara wa Mkuchika imebidi uongozi wa JF ubadili header ya thread from TIDO MHANDO NA UFISADI TBC to tido mhando na ubinafsishaji tbc...wakulu tuna kazi na mwendo mrefu sana kwenye hivi vita dhidi ya UFISADI maana hata katika hizi hizi platforms za kupiga vita ufisadi mafisadi tayari wanawainvfluence owners

sijui kama tutafika

nilipoleta hii habari nikaambiwa naleta uzushi haya kiko wapi?

Halisi tayari keshaleta nondo hizo hapo na bado msimamo wangu uko pale pale...napinga kuuzwa kwa TBC ...kuna instutions ambazo hazitakiwi kuguswa and one of them is this
 
halafu kuna habari kuwa kutokana na huo mkwara wa Mkuchika imebidi uongozi wa JF ubadili header ya thread from TIDO MHANDO NA UFISADI TBC to tido mhando na ubinafsishaji tbc...wakulu tuna kazi na mwendo mrefu sana kwenye hivi vita dhidi ya UFISADI maana hata katika hizi hizi platforms za kupiga vita ufisadi mafisadi tayari wanawainvfluence owners

sijui kama tutafika

nilipoleta hii habari nikaambiwa naleta uzushi haya kiko wapi?

Halisi tayari keshaleta nondo hizo hapo na bado msimamo wangu uko pale pale...napinga kuuzwa kwa TBC ...kuna instutions ambazo hazitakiwi kuguswa and one of them is this

Ingawa mara nyingi sikubaliani nawe hapa (hasa katika mambo ya udini) lakini katika hili nakuunga mkono asilimia mia moja. Ni makosa na ni ufisadi kuiuza TBC kinyemela.
 
Kuna uwezekano ukawa na shares nyingi lakini ukawa huna sauti. hii inategemea mkataba umetengenezwaje (mwenye shares nyingi anakuwa na maamuzi katika bodi lakini sio guarantee that kila mwenye share nyingi anakuwa na sauti na maamuzi katika bodi).
 
Tido Mhando ambaye alipewa nafasi aliyonayo baada ya kufanyakazi kule BBC SWAHILI aliingia TBC kwa manjonjo yasiyo na kifani na sasa kuna habari kuwa apart from UFISADI uliokuwa unaendelea chini yake pale TBC huyu mheshimiwa amekuwa akinfluence ajira na ufisadi ulioipelekea TBC kupoteza mabilioni ya shilingi na hakuna aliyechukuliwa hatua yoyote ile.

Sasa kuna hii ya TBC kuuzwa kinyemela chini yake kwa waChina na yeye kama kiongozi kwa kusudi ameamua kukaa kimya bila kuwaarifu wananchi kulikoni. Lakini kabla hatujaendelea na hayo hebu turudi nyuma kidogo na kumtazama TIDO alikuwa na vision ya namna gani kuhusu TBC ndipo tutaamua kuendelea

Kwa kuanza tuu TIDO kwa sababu alitokea BBC akili yake alijiona kuwa anaweza akairestructure TBC katika mfumo wa BBC na zaidi huyu mheshimiwa alijiona kuwa yeye ndiye atakeykuwa ni REITH wa Tanzania..lakini akasahau kuwa huko alikotoka BBC pamoja na wengine lakini mission statement yao iko wazi kuwa wana EDUCATE,INFORM and ENTERTAIN the public lakini kwa Tido hilo halipo sana sana TBC imekuwa kama vile chaka la ma incompetents. Pesa na vifaa vya kisasa vyote walivyonavyo wameshindwakutengeneza vipindi ambavyo vinamvuto kwa walipa kodi ambao walitakiwa kuwa ma stakeholders wakubwa wa TBC !

Mbaya zaidi ukitazama TBC zote 1 & 2 utafikiri unatazama zile documentary za 1980's ambazo unaona kabisa sauti na picha haziendani...ukitazama KTN ya Kenya na TBC utaona wazi kuwa tofauti zao ni sawa na mbingu na ardhi! in short TBC inatia kichefu chefu kuitazama na hiyo redio ndio siwezi kuzungumzia kwani its not the same RTD tuliyoizowea, yes kulikuwa na mabadiliko ya lazima lakini Tido kwa kukaa kwake nje muda mrefu kasahu attachment wananchi wakawaida waliyokuwa nayo na vipindi kama vya malenga wetu na kadhalika.

Ukiuliza avaraje Juma wa mtaani kuhusu TBC atakwambia kuwa its useless and its not woth the public funds, cha ajabu for someone like Tido one would have thought kuwa anaeleewa the meaning of PUBLIC SERVICE BROADCASTING lakini wapi!

sasa hivi kupitia ma swahiba zake wameamua kuiza TBC kinyemela and i wonders gonna be next for Tido and his team of mediocres

Sina uhakika na data zako ila nakubaliana nawe kabisa kuwa Tido ameshindwa kabisa kuiongoza TBC iweze kuendana na karne hii. Alitakiwa atumie uzoefu wake wa nje kuonyesha pia kuwa vyombo vya habari vya umma havitumiwi na wachache kwa sababu za kisiasa.
 
Hivi jioni nimemwona Mkuchika kwenye TBC ana bwabwaja na maswali aliyoyauliza HALISI sidhani kama atayajua

Mbaya zaidi I doubt kama anajua kuna kitu kinaitwa JF kina exist

Na kwa kuongeza tuu sijui kama najua kama huku watu watamwaga upupu mpaka aseme hii ni nini

Najua Tanzania the only institution tuliyobaki nayo ilikuwa ni RADIO TANZANIA au TBC, na MWALIMU NYERERE na ni institution ambazo ilitakiwa tuzipe heshima zinazostahili

Kama ikifika weekend basi nitaanzisha Kampeni ya kupinga kubinafsishwa kwa TBC na MKUCHIKA, TIDO na wahuni wenzao wajiandae kwani kama nitahitajika then i will even go personal

Sisi wote tumekuwa kwa kusikiliza Radio Tanzania na labda kwa hawa watawala kwao itakuwa imepitwa na wakati lakini sisi kwetu ni muhimu sana na si kitu cha kuchezea chezea as if ni mali binafsi

Kwa mlio tayari kumtetea Mkuchika na Tido jiandaeni na nondo za kutosha na Invisible kama unaona hii itakuharibia then be it I am even ready kuihamisha hii vita kwenda kwenye terrain tofauti kabisa

Huu ni upuuzi na hatuwezi kuukubali
 
Back
Top Bottom