Game Theory
Platinum Member
- Sep 5, 2006
- 8,545
- 835
Tido Mhando ambaye alipewa nafasi aliyonayo baada ya kufanya kazi kule BBC SWAHILI, aliingia TBC kwa manjonjo yasiyo na kifani na sasa kuna habari kuwa apart from UFISADI uliokuwa unaendelea chini yake pale TBC.
Huyu mheshimiwa amekuwa akiinfluence ajira UNFAIRLY na ufisadi ulioipelekea TBC kupoteza mabilioni ya shilingi na hakuna aliyechukuliwa hatua yoyote ile.
Sasa kuna hii ya TBC 'kuuzwa' kinyemela chini yake kwa Wachina na yeye kama kiongozi kwa kusudi ameamua kukaa kimya bila kuwaarifu wananchi ambao ni wadau wa hii TBC kulikoni?
Lakini kabla hatujaendelea na hayo hebu turudi nyuma kidogo na kumtazama TIDO alikuwa na vision ya namna gani kuhusu TBC ndipo tutaamua kuendelea
Kwa kuanza tu, Tido kwa sababu alitokea BBC, akili yake alijiona kuwa anaweza akairestructure TBC katika mfumo wa BBC na zaidi huyu mheshimiwa alijiona kuwa yeye ndiye atakayekuwa ni REITH wa Tanzania..
Lakini akasahau kuwa huko alikotoka (BBC), pamoja na wengine lakini mission statement yao iko wazi kuwa wana EDUCATE, INFORM and ENTERTAIN the public, lakini kwa Tido hilo halipo, sana sana TBC imekuwa kama vile chaka la ma incompetents. Pesa na vifaa vya kisasa vyote walivyonavyo wameshindwa kutengeneza vipindi ambavyo vinamvuto kwa walipa kodi ambao walitakiwa kuwa ma stakeholders wakubwa wa TBC!
Mbaya zaidi, ukitazama TBC zote 1 & 2 utafikiri unatazama zile documentary za 1980's ambazo unaona kabisa sauti na picha haziendani... Ukitazama KTN ya Kenya na TBC, utaona wazi kuwa tofauti zao ni sawa na mbingu na ardhi! Inshort, TBC inatia kichefu chefu kuitazama na hiyo redio ndio siwezi kuzungumzia kwani its not the same RTD tuliyoizowea.
Yes kulikuwa na mabadiliko ya lazima lakini Tido kwa kukaa kwake nje muda mrefu kasahau attachment wananchi wa kawaida waliyokuwa nayo na vipindi kama vya malenga wetu na kadhalika na kaamua kutuletea watangazaji ambao hata Kiswahili hawajui... Kiswahili cha watangazaji kinatia kinyaa kusema ukweli... Saa zingine ukisikiliza redio utafikiri unasikiliza FM stations za wa Kenya kwani Kiswahili sanifu hakipo, na wameingiwa na hiyo inferiority complex ya kuchanganya Kiswahili na Kiingereza kule Kenya wanaita "Sheng".
Ukiuliza average Juma wa mtaani kuhusu TBC atakwambia kuwa its useless and its not woth the public funds! Cha ajabu, for someone like Tido, one would have thought kuwa anaelewa the meaning of PUBLIC SERVICE BROADCASTING lakini wapi!
Sasa hivi kupitia ma swahiba zake, wameamua kuiuza TBC kinyemela and i wonder whats gonna be next for Tido and his team of mediocres ambao wanakula pesa zetu kusaidiana na MKUCHIKA... Stay tuned kuona watakavyoita press conferences za kutetea huu utumbo wao.
@Hlaisi ameuliza maswali haya kwa Mkuchika ambaye sasa hivi kaweka JF kama main page ya computer yake. Tayari Mkuchika ameibuka na kutoa ufafanuzi lakini hakuna popote alipozungumzia kuhusu mambo makubwa ya msingi;
- Hakusema kwanini wamewapa Wachina 100% na badala yake amesema kwamba TBC haijauzwa bali imeingia ubia
- PPRA wamenukuliwa wakisema hawana taarifa, Mkuchika anadai sheria za PPRA zimefuatwa, na kutaja mamlaka kadhaa zilizohusika.
- Mkuchika hakusema kuhusu matumizi ya Dola badala ya Shilingi
- Mkuchika hakusema kuhusu kusajiliwa chapuchapu na hata kukosewa
- Mkuchika hakusema kuhusu kuzuiwa kwa hisa kuuzwa katika soko la hisa
- Mkuchika hakusema kuhusu usalama wa masafa yetu kama 65% ziko kwa Wachina
- Mkuchika hakusema kuhusu Waislamu kutengwa na Agape kujibebesha jukumu
- Mkuchika hakusema lolote kuhusu TBC kuomba lakini Star Media kumilikishwa
- Mkuchika hakusema kuhusu maana ya masafa ya umma ni nini
Hii docs ni kwa hisani ya mwenzetu humu bwana Halisi
Last edited: