Wiyelelee
JF-Expert Member
- Nov 9, 2012
- 1,071
- 347
Nikiwa mdau wa habari, nasikitika kusema kwamba pamoja na sifa zote alizojizolea, Bw. Tido Mhando alikosea sana kubadili jina kutoka RTD ililozoeleka sana kwenda TBC Taifa. Matokeo yake sasa, hiyo TBC Taifa imepoteza mvuto, mwelekeo na wasikilizaji wengi huko vijijini hawaipati. Wanashindwa kuitofautisha hiyo radio na FM stations!
Mi nadhani kwa mambo ya Kitaifa kama haya, siyo vizuri mtu akakurupuka tu na kuanza kubadilisha vitu ambavyo vilikuwepo hata kabla hajazaliwa. Kungelikuwa na maoni na mijadala ya Kitaifa kabla ya kufikia huo uamuzi. Napendekeza jina la RTD lirejeshwe maramoja.
Mi nadhani kwa mambo ya Kitaifa kama haya, siyo vizuri mtu akakurupuka tu na kuanza kubadilisha vitu ambavyo vilikuwepo hata kabla hajazaliwa. Kungelikuwa na maoni na mijadala ya Kitaifa kabla ya kufikia huo uamuzi. Napendekeza jina la RTD lirejeshwe maramoja.