Mbu
JF-Expert Member
- Jan 11, 2007
- 12,753
- 7,844
Kimbembe kimeanza miaka mitatu iliyopita. Mke amebahatika kupangiwa ofisi nyeti ambayo inajihusisha na upatikanaji wa mapato ya serikali. Kufumba na kufumbua, mke kajenga nyumba mbili za kisasa kisha kazipangisha. Nyumba waliyokuwa wanaishi ameiongezea vyumba vingine vinne pamoja na vikorombwezo na nakshi mbali mbali. Almuradi maisha yao shwari mara kumi ya hapo awali.
Kama hilo halitoshi, kawahamisha watoto public school na kuwapeleka kwenye Academy ambako kwa mwaka pamoja na vikorombwezo vingine, anawalipia mara kumi ya mshahara wake. Haikupita muda, kanunua brand New Toyota VX, na sasa ameagiza Range Rover Vogue (Sport) toka Uingereza kwa ajili ya mumewe.
Jamaa (mume) pamoja na unafuu wa maisha, roho yake haimpi! anaona "likibumbuluka" ofisini kwa mkewe, watakumbwa waliokuwamo na wasiokuwamo. Kajaribu kumsahuri mkewe aachane au apunguze mabomu kazini, Mke hasikii la mwadhini wala mnadi swala!... anasema "tumeteseka sana kimaisha, acha nasi tujiliwaze kidogo!"
Jamaa hajielewi elewi kabisaaa. Akifikiria ndoa, yake haijwahi yumbishwa kwa lolote miaka yote kumi na tano. Lakini, kasi ya mkewe na likilipuka, watataifishwa mali zote na huenda mkewe akaishia jela. Mzee wa watu anafikiria aanzie wapi kuepusha 'bomu hili la kutega'
Mna maoni gani.