Tiba mbadala ya chumvi: Sehemu ya kwanza

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,605
696,697
Habarini za usiku huu
Ningependa kushare nanyi hii tiba mbadala ya chumvi kwa wale waamini na wenye uhitaji, hii si uchawi ushirikina wala ulozi na wala huhitaji kwenda kwa 'mtaalam' kupoteza pesa na muda wako huku ukiwa kwenye hatari ya kutapeliwa nk

Chumvi yenye matokeo bora ni chumvi ya mabonge, au ile chumvi ya kuchimba kwa vifaa vya kawaida (epuka chumvi ya viwandani ni mfu) japo inaweza kusaidia kwa kasi chake

Chumvi ni kinga bora kwa nguvu hasi zote ushirikina na nguvu nyingine za giza! Hata wale wanaohisi kuibiwa ama kuchafuliwa nyota zao, stimulus bora ni chumvi... Hata zile hatari nyingine katika ulimwengu wa roho, zote zinazokunyelemea kinga kuu pamoja na sala na imani yako kwa Mungu ni chumvi

MATUMIZI
Chukua kiasi kidogo cha chumvi nyunyizia kuzunguka kitanda, chumba au hata nyumba yako, fanya hivyo huku ukinia ama kunuizia yale utakayo... Fanya ukiamini na kumaanisha.

Hapo hiyo ni kinga ya kujikinga na nguvu hasi lakini ukitaka kusafisha nyota yako(mtima/aura) kila uogapo weka chumvi kidogo kwenye maji kisha ogea..... Masharti ya kuoga ni siku 7 14 au 21 ama la mara 7 14 au 21
Nb: hii haipingani na imani yako kwakuwa hata kwenye maandiko tunaona chumvi ilivyotumika kutakasa
a7a04db0b1254ba994fe9e7e3de1522c--magical-herbs-witchcraft-wiccan-herbs.jpg


Mubashara:
Pamoja na kwamba mada yetu ni ya chumvi lakini nakupa nyongeza ya hii ya kipande cha mkaa kwa wale wenzangu wa Uswazi kwenye chumaulete zongo na kulogana kusikoisha
1799584c214ef3a2268d4feb911aabe0.jpg


Alamsiki.......!!!!!!


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hahaahahaha. bac hakuna shida. mimi mgeni kabisa humu. na mimi nataka nikwambie kitu kimoja
chumvi ni kweri tiba na ni dawa ila tunapokosea kusema unapaswa uwe na imani fulani ndiyo ifanye kazi. mimi najua ukitumia siku7, 14 au 21 kwa utaratibu wa formula fulani itakutibu tu. hizo zingine huwa mbwembwe tu wala azisaidiii kabisa
 
141 Reactions
Reply
Back
Top Bottom