Kula hayo mapupu yanahitaji uwe serious!Hahahaa.......hapo Ufipa hakuna chai kuna supu ya mapupu tu!
Umesoma ukaelewa kweli? Kama hujaelewa kuwa msomaji na pita kimya!Ni upuuzi tu wa wasanii na kutaka kubebwa wakidhan Ruge ni baba yao
Sent using Jamii Forums mobile app
Ukweli ni kwamba kila kazi na fursa zake, palipo na fursa hapakosi changamoto na kila mtu na mazuri yake na mapungufu yake.
Ruge Mutahaba anaweza kuwa ametajwa kwenye masakata mengi ya ubaya dhidi ya wasanii, akibebeshwa lawama kuliko mtu mwingine yeyote kwenye tasnia ya muziki Tanzania.
THT, Tanzania House of Talent, ni kituo kilichoanzishwa mwishoni mwa mwaka 2005 kwa lengo la kuwasaidia vijana wenye vipaji, lakini wasio na uwezo wa kujiendeleza wenyewe kwenye sekta ya sanaa hapa nchini.
Mwaka 2005, baada ya Rais Jakaya Kikwete kufurahishwa na ushiriki wa wasanii kwenye kampeni za uchaguzi mkuu, aliwaahidi THT kuwajengea studio kubwa ya kisasa ili iweze kuwasaidia vijana wengi zaidi.
Baada ya serikali kutimiza ahadi yake na studio kukabidhiwa kwa THT, aliyekuwa Mkurugenzi mwanzilishi Ruge Mutahaba alianza kulalamikiwa na wasanii wenzake kuwa amejimilikisha studio hiyo kwa manufaa yake na rafiki zake, na ameifanya studio hiyo kama mali ya kampuni ya CMG inayomiliki vituo vya Clouds FM na Clouds TV, na kuwa anawabagua, kuwanyonya na kuwadhulumu wasanii wengine.
Baadhi ya wasanii ambao hawakukubaliana na Ruge ni Lady JD, Joseph Mbilinyi SUGU, Dudu Baya, Q Chief, Joseph Haule na wengine, walianzisha umoja wa kupinga unyonyaji huo uliopewa jina la Anti Virus.
Sugu na Ruge waliingia kwenye ugomvi baada ya Sugu kumtuhumu Ruge kujimilikisha Project ya Malaria iliyofadhiliwa na Serikali ya Marekani kupitia THT.
Lady JD aliwahi kumtuhumu Ruge na Kusaga kuwa ndio wanaonyonya jasho la wasanii, hadi kufikishana mahakamani kiasi kwamba waliapizana kutozikana, ugomvi uliopelekea Clouds kutopiga nyimbo za Lady JD na yeye kukimbilia EATV.
Q Chief naye alikwaruzana na Ruge kwa tuhuma za Ruge akishirikiana na BASATA kuzuia kibali cha mwimbaji wa Nigeria Davido.
Si hao tu, Ruge ameshawahi kukwaruzana na kundi zima la WCB linaloongozwa na Diamond Plutnamuz, ilifikia hatua wasanii walio chini ya WCB nyimbo zao kutopigwa na Clouds FM wala Clouds TV na hata kutoalikwa kwenye matamasha ya Fiesta yaliyokuwa yanaandaliwa na CMG. Leo WCB wameanzisha tamasha lao linalojulikana kama WASAFI Festival na TV yao ya Wasafi TV.
Karibu tujadili.
Ndiyo maana mods wamekuja kuificha huku hawajui hata sisi tunaisaidia JF kuisemea.WANAFIKI UKIWAAMBIA WANAKUPOOONDA!!!
East Africa Radio wakaanzisha nini????Clouds wakaanzisha team Kiba Hili kumkandamiza Diamond na watu wake
Sent using Jamii Forums mobile app
Umesoma ukaelewa kweli? Kama hujaelewa kuwa msomaji na pita kimya!
Kawanyanyua wapi! Wasanii walinyonywa tu. Au kwa vile unaona nyimbo zao kupigwa sana kwenye radio yake? Au kujulikana kwa msanii kwa promo zao!Amegusa watu wengi, wengi wanaomlalamikia ukiangalia vizuri, utagundua kuwa marehemu ana mchango kwenye kuwainua! Na kwa kuwa mabaya huwa yanavuma zaidi!
Naomba niungane na chid benzi kwa hili!
Tumuombee apumzike kwa amani!
Nasi tujiandae kwani njia yetu in moja!
R I P RUGE
Sent using Jamii Forums mobile app
Sasa Qchief na Davido wapi na wapi?Ukweli ni kwamba kila kazi na fursa zake, palipo na fursa hapakosi changamoto na kila mtu na mazuri yake na mapungufu yake.
Ruge Mutahaba anaweza kuwa ametajwa kwenye masakata mengi ya ubaya dhidi ya wasanii, akibebeshwa lawama kuliko mtu mwingine yeyote kwenye tasnia ya muziki Tanzania.
THT, Tanzania House of Talent, ni kituo kilichoanzishwa mwishoni mwa mwaka 2005 kwa lengo la kuwasaidia vijana wenye vipaji, lakini wasio na uwezo wa kujiendeleza wenyewe kwenye sekta ya sanaa hapa nchini.
Mwaka 2005, baada ya Rais Jakaya Kikwete kufurahishwa na ushiriki wa wasanii kwenye kampeni za uchaguzi mkuu, aliwaahidi THT kuwajengea studio kubwa ya kisasa ili iweze kuwasaidia vijana wengi zaidi.
Baada ya serikali kutimiza ahadi yake na studio kukabidhiwa kwa THT, aliyekuwa Mkurugenzi mwanzilishi Ruge Mutahaba alianza kulalamikiwa na wasanii wenzake kuwa amejimilikisha studio hiyo kwa manufaa yake na rafiki zake, na ameifanya studio hiyo kama mali ya kampuni ya CMG inayomiliki vituo vya Clouds FM na Clouds TV, na kuwa anawabagua, kuwanyonya na kuwadhulumu wasanii wengine.
Baadhi ya wasanii ambao hawakukubaliana na Ruge ni Lady JD, Joseph Mbilinyi SUGU, Dudu Baya, Q Chief, Joseph Haule na wengine, walianzisha umoja wa kupinga unyonyaji huo uliopewa jina la Anti Virus.
Sugu na Ruge waliingia kwenye ugomvi baada ya Sugu kumtuhumu Ruge kujimilikisha Project ya Malaria iliyofadhiliwa na Serikali ya Marekani kupitia THT.
Lady JD aliwahi kumtuhumu Ruge na Kusaga kuwa ndio wanaonyonya jasho la wasanii, hadi kufikishana mahakamani kiasi kwamba waliapizana kutozikana, ugomvi uliopelekea Clouds kutopiga nyimbo za Lady JD na yeye kukimbilia EATV.
Q Chief naye alikwaruzana na Ruge kwa tuhuma za Ruge akishirikiana na BASATA kuzuia kibali cha mwimbaji wa Nigeria Davido.
Si hao tu, Ruge ameshawahi kukwaruzana na kundi zima la WCB linaloongozwa na Diamond Plutnamuz, ilifikia hatua wasanii walio chini ya WCB nyimbo zao kutopigwa na Clouds FM wala Clouds TV na hata kutoalikwa kwenye matamasha ya Fiesta yaliyokuwa yanaandaliwa na CMG. Leo WCB wameanzisha tamasha lao linalojulikana kama WASAFI Festival na TV yao ya Wasafi TV.
Karibu tujadili.
Mimi napita njia!