THREAD zenye MAMBO YA KITOTO ziachwe

kumbuka msuli hauna lups,na kitovu hakikai nyuma. We nenda kale maembe kibada na mchicha pia maana huna macho au sijui ndo akili mbili mmmh sikuisomaga hii kumbe ndivyo ulivyo hebu omba mods wakupeleke jf nyingne, ukakutane nawakubwa wenzako wengine ili uweze toa commends zingine heheee tuonane dk chache zingineeee

Ameeeeeen
 
Wakuu heshima mbele,

Ni muda mrefu sijapita huku, lakini leo nimeingia, na nimekutana na hii thread, na nimesoma kila post mpaka mwisho bila kuruka, naomba nizungumze kama mwangalizi wa nje tafadhali.

1. Wanafunzi, pia ni sehemu ya watuamiaji wa JF, na pia CC wamo hapana shaka. Na at the same time, watumiaji wa FB pia wamo sana tu humu. kiufupi, walio timamu na wasio timamu wapo humu ndani.

2. Arushaone ametoa angalizo kwa post za kitoto kuachwa, yet humu ndani kuna majibu yamekuja, na wengine wakijadiliana off topic (wanaenda chaka na mambo yao tofauti na topic), na bado karibu post zote zimekuwa liked na muanzilishi wa mada. Nimeshindwa kuelewa mantiki ya likes.

3. Kuanzia ukurasa wa 1-15, sijaona resolution zaidi ya kurushiana vijembe na kutishiana BAN, kitu ambacho kwa yeyote atakayesoma ni lazima ajiulize mara mbili mbili dhana ya post.

4. MEE, naukumbuka huu mfumo nikiwa shule, mwalimu alikuwa akisema mention, explain, example. Sasa katika hii mada sijaona example ya post ambayo angekuwa anarefer (unless anaogopa kutokana na jina la mtu alitengeneza hiyo post, pengine ni best yake na anashindwa kumuambia live), leave alone explanation, ambayo kimsingi pia sijaelewa post a kitoto ni zipi, ama post yenye maana ni ipi, mathalani kuna mchangiaji mmoja ameweka bayana kuwa kinacholeta maana kwake ni tofauti na kinacholeta maana kwa mtu mwingine - which makes sense.

5. Na hii post imewekwa kama sticky, na yet haipati heshima yake kama ambavyo ililengwa, ndo nazidi kuchanganyikiwa nguvu ya umma iko wapi, na hata nguvu ya dola (aka mods) iko wapi.

Naiheshimu CC, ndio hapa hapa nilikuja kuomba ushauri wa dogoro zuri, na nikapata suggestions za kutosha tu, (utani pia ulikuwemo though) https://www.jamiiforums.com/jf-chit-chat/311884-msaada-godoro-gani-zuri-3.html

Uwepo wa hii post ambayo pia bado haina resolution, unaifanya iendelee kuhang na kila atakayeisoma ataamini kuwa hakuna solution, ilhali kuna vichwa vizuri tu humu ambavyo vinaweza kumaliza hili suala, kwa kueleza wazi mantiki ya jukwaa hili, na mipaka yake vile vile ambayo watu wata-adhere to. Ama ikishindikana basi ni kukusanya maoni, watu wanaidefine vipi CC, maana kama wanataka CC iwe ya mrengo fulani, na ni asilimia kubwa ya watumiaji, ya nini wanyimwe? naamini maelewano hayajashindikana. vinginevyo kuna watu wataendela kukwazika kwa kuona kile ambacho wanaamini hakistahili hapa jukwaani.

Ni mtazamo wangu tu huu, salamu kwa wote,

carbon copy: watu8, FirstLady1, Catherine, Naipendatz, Baba V, Raiza, Erickb52, Filipo, HEART, madame M, chardams, ummu kulthum, sweetlady, Mpenda Yesu, Nicas Mtei, Chilli, Chimbuvu, Madam B et.al
 
Last edited by a moderator:
10 Reactions
Reply
Back
Top Bottom