This is it!.. I'm @!#% Fed up.. atapokeaje tuzo kwa niaba yangu?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,463
39,929
Siku chache zilizopita Rais Mstaafu Ndg. Benjamin Mkapa alipokea tuzo ya Uongozi Duniani kutoka Taasisi ya mhifadhi wa sokwe-mtu Dr. Jane Goodall katika maadhimishisho ya miaka 30 the taasisi hiyo. Rais Mkapa aliipokea tuzo hiyo "kwa niaba ya Watanzania" kwa maneno yake mwenyewe.

Sasa, sipendi tena sitaki Rais Mkapa aendelee kuzungumza kwa niaba yangu huko nje ya nchi na kupokea tuzo kwa niaba ya Watanzania wakati ameamua kuwadharau na kuwaona hawana mpango. Kitendo cha yeye kuendelea kukaa kimya dhidi ya tuhuma mbalimbali zinazomkabili ni kitendo cha dharau, kiburi, na kisicho cha kiungwana dhidi ya watu waliompatia nafasi hiyo aliyonayo leo!!

Wakati umefika Rais Mkapa azungumzie tuhuma zote zinazomkabili zinazohusiana na utendaji kazi wake akiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano.

a. Kutumia vibaya ofisi yake kwa kufanya biashara akiwa Ikulu
b. Kutumia madaraka yake vibaya kujipatia mali kwa kutumia cheo chake na kujiingizia biashara kutoka fedha za serikali
c. Kujichumia mali za haraka haraka kwa kutumia cheo chake kama Rais

Na aseme sasa, au anyamaze milele!
 
Siku chache zilizopita Rais Mstaafu Ndg. Benjamin Mkapa alipokea tuzo ya Uongozi Duniani kutoka Taasisi ya mhifadhi wa sokwe-mtu Dr. Jane Goodall katika maadhimishisho ya miaka 30 the taasisi hiyo. Rais Mkapa aliipokea tuzo hiyo "kwa niaba ya Watanzania" kwa maneno yake mwenyewe.

Sasa, sipendi tena sitaki Rais Mkapa aendelee kuzungumza kwa niaba yangu huko nje ya nchi na kupokea tuzo kwa niaba ya Watanzania wakati ameamua kuwadharau na kuwaona hawana mpango. Kitendo cha yeye kuendelea kukaa kimya dhidi ya tuhuma mbalimbali zinazomkabili ni kitendo cha dharau, kiburi, na kisicho cha kiungwana dhidi ya watu waliompatia nafasi hiyo aliyonayo leo!!

Wakati umefika Rais Mkapa azungumzie tuhuma zote zinazomkabili zinazohusiana na utendaji kazi wake akiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano.

a. Kutumia vibaya ofisi yake kwa kufanya biashara akiwa Ikulu
b. Kutumia madaraka yake vibaya kujipatia mali kwa kutumia cheo chake na kujiingizia biashara kutoka fedha za serikali
c. Kujichumia mali za haraka haraka kwa kutumia cheo chake kama Rais

Na aseme sasa, au anyamaze milele!

Duuh Mwanakijiji nilifikiria kachua radio/podomatic awards kwa niaba yako...hehee.
Pole bana. Ila nakusikia huku usawa wa mita bandi za broadband.
 
Siku chache zilizopita Rais Mstaafu Ndg. Benjamin Mkapa alipokea tuzo ya Uongozi Duniani kutoka Taasisi ya mhifadhi wa sokwe-mtu Dr. Jane Goodall katika maadhimishisho ya miaka 30 the taasisi hiyo. Rais Mkapa aliipokea tuzo hiyo "kwa niaba ya Watanzania" kwa maneno yake mwenyewe.

Sasa, sipendi tena sitaki Rais Mkapa aendelee kuzungumza kwa niaba yangu huko nje ya nchi na kupokea tuzo kwa niaba ya Watanzania wakati ameamua kuwadharau na kuwaona hawana mpango. Kitendo cha yeye kuendelea kukaa kimya dhidi ya tuhuma mbalimbali zinazomkabili ni kitendo cha dharau, kiburi, na kisicho cha kiungwana dhidi ya watu waliompatia nafasi hiyo aliyonayo leo!!

Wakati umefika Rais Mkapa azungumzie tuhuma zote zinazomkabili zinazohusiana na utendaji kazi wake akiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano.

a. Kutumia vibaya ofisi yake kwa kufanya biashara akiwa Ikulu
b. Kutumia madaraka yake vibaya kujipatia mali kwa kutumia cheo chake na kujiingizia biashara kutoka fedha za serikali
c. Kujichumia mali za haraka haraka kwa kutumia cheo chake kama Rais

Na aseme sasa, au anyamaze milele!

Huyu anafikiri bado ni Rais na ndio maana anakuwa na kiburi cha hali ya juu. Tunamtaka akajibu kwa Watanzania wote tuhuma nzito za madudu aliyoyafanya akiwa Rais wa Tanzania, pia kama kuna mali alizozipata kwa njia za haramu azirudishe zote kwa Watanzania.

Na hii tabia "ya kiguu na njia" kila wakati yuko nje ya nchi ni nani anamlipia? kama anatumia pesa za walipa kodi Watanzania ni bora aache kabisa kufuja pesa za walala hoi.
 
Yaani, anachoonesha ni kilele cha kiburi.. hizi sisi watanzania wote tuna wivu au wajinga kiasi cha kwamba tunashindwa kumhoji. Nadhani Rais Kikwete aulizwe kama anaona ipo haja ya Rais Mkapa kujibu tuhuma zilizoinuliwa juu yake..
 
Taratibu tutafika Ukonga au Segerea tu, na itabidi wakalale kule.
 
Kuna siku atasimama kizimbani na hapo ndipo watakapojua kuwa embe ni tunda na nyanya ni kiungio!
 
Kwa niaba ya watanzania au kwa niaba ya familia yake na Yona? El gordo loco haoni hata aibu.
 

...poa moto mzee mwkjj, tuzo toka Taasisi ya 'mhifadhi wa sokwe-mtu', ni ujumbe tosha!!
 
mwalimu hakujua kuwa chinga haswaa chinga wa age kama ya bw mkapa ni dam dam na wazungu! Jamaa alikuwa anauza nchi kwa kusifiwa tu...
 
Mwanakijiji,
Umeshasahau Rais Kikwete alishasema kuwa Mkapa asishtakiwe, aachwe apumzike? Ndio hivyo tena...
 
Yaani, anachoonesha ni kilele cha kiburi.. hizi sisi watanzania wote tuna wivu au wajinga kiasi cha kwamba tunashindwa kumhoji. Nadhani Rais Kikwete aulizwe kama anaona ipo haja ya Rais Mkapa kujibu tuhuma zilizoinuliwa juu yake..

Jamani kikwete was very clear aliposema yeye hafikirii kuchunguza wala kuwashtaki marais waliopita, that means hana huo mpango kabisa. By the way Mkapa yuko busy kweenye seminar na wafanyakazi wake wa Mkapa AIDS Foundation alhamis na ijumaa kunduchi beach hotel, muda wa kujibu tuhuma hana i think.
 
Jamani kikwete was very clear aliposema yeye hafikirii kuchunguza wala kuwashtaki marais waliopita, that means hana huo mpango kabisa. By the way Mkapa yuko busy kweenye seminar na wafanyakazi wake wa Mkapa AIDS Foundation alhamis na ijumaa kunduchi beach hotel, muda wa kujibu tuhuma hana i think.

Inabidi apokelewa na mabango hapo kwenye eneo la mkutano.
 
inakatisha tamaa kwamba tanzania tu ndio sehemu ambapo kama ulikuwa rais au waziri unaachwa uumzishwe! kwa maana hiyo mkubwa zaidi asieipendelea mema nchi ni kikwete alithubutu kukiri mbele ya wananchi wake kuwa hatochukuwa hatua yyote hata kama huyo rais mstaafu alimega nchi na kuitafuna:mad:
 
JF ni venue ya wadadavuzi kweli? Kuna shari gani kupokea tuzo ya wanayamapori kwa niaba yetu? Pengine ingalikuwa madini ningethubutu kujiuliza rohoni.

Hana la kujibu,huyu jamaa alishasema when a'm done with Tz na CCM sintajihusisha na siasa za ndani na hiyo ndio tafsiri ya ukimya wake.

Heri yenu mnaokomalia kumshinikiza bubu wa siasa za Bongo toka 2006 alipoacha u-chairman wa chichiem aongee. Sahauni hilo halitatokea,maandamo dhidi ya mtu asiye dola wala mamlaka ni matumizi mabaya ya nguvu ya umma.
 
JF ni venue ya wadadavuzi kweli? Kuna shari gani kupokea tuzo ya wanayamapori kwa niaba yetu? Pengine ingalikuwa madini ningethubutu kujiuliza rohoni.

Hana la kujibu,huyu jamaa alishasema when a'm done with Tz na CCM sintajihusisha na siasa za ndani na hiyo ndio tafsiri ya ukimya wake.

Heri yenu mnaokomalia kumshinikiza bubu wa siasa za Bongo toka 2006 alipoacha u-chairman wa chichiem aongee. Sahauni hilo halitatokea,maandamo dhidi ya mtu asiye dola wala mamlaka ni matumizi mabaya ya nguvu ya umma.

Well said mkuu, huyo Mwakjj naona amedata sasa...
 
hahaha imetulia hiyo. naungana na Mzee wa kijiji kukataa kuwakilishwa na mtu ambaye sina imani wala amani naye.
 
Tunataka ajibu, kiburi akamfanyie super model wa old moshi. Siyo watanzania wa leo.. Tunataka aje atuambie ili tuelewe ukweli asijifanye mbabe kabisaaa
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom