Theresa Shayo: Miss Tanzania Mwafrika wa kwanza 1967 katika historia ya Tanzania

Marhum Theresia Shayo alikua muungwana sana. Nilipata sikia habari zake kutoka kwa bi. Halima bint Mustafa Baraza. Mola Mlezi awaweke salama ndugu zetu kwenye makaburi yao.
 
M's Tanzania wa Kwanza (Hayati Theresa)

Mwaka 1960 ndipo Mashindano ya urembo nchini yalipoanza na hayatakuwa na muonekano wa kimataifa kwa sababu yalifanyika kwenye maeneo machache.

Kwani kumbukumbu zilizopo zinaonyesha kwamba mrembo wa kwanza kunyakua taji hilo la Miss Tanzania, si mwingine bali alikuwa Theresa Shayo.

Kutokana na maadali na utamaduni ya mtanzania serikali ililazimika kuyapiga marufuku mashindano hayo ilipofika tu mwaka 1967, kabla ya Rais wa awamu ya pili Alhaj Ali Hassan Mwinyi kuyaruhusu kuendelea kutokana na utandawazi kuanza kushika kasi ya ajabu.

Tangu kipindi hicho nchi yetu ya tanzania iliweza kufanikiwa kutoa warembo kadhaa walioshiriki mashindano ya kumtafuta mrembo wa dunia, wakiwemo Emil Adolf, Nancy Sumary, Saida Kessy, Basila Mwanukuzi, Hoyce Temu, Jacqueline Ntuyabaliwe na wengineo.

Mshindi huyo wa kwanza kushiriki mashindano hayo ya urembo ya Miss Tanzania Theresa Shayo, alifariki dunia huko Augburg Munich Ujerumani na kuzikwa uko uko alikokuwa akiishi miaka yote hiyo.

Mwaka 1967 ndipo hayati Theresa alitwaa taji hilo kwenye shindano lilofanyika hoteli ya Kilimanjaro, alifariki dunia january 26 mwaka 2007 na maradhi ya kansa ya tumbo huku akiwa na umri wa miaka 61.

Theresa hakubahatika kupata mtoto na alikuwa akiishi mjini Augsburg ambako aliolewa na mjerumani aitwaye Chrstian Rieger ambaye waliachana na hadi anakufa alikuwa akiishi na boy friend aitwaye Tonny.

Kabla ya hapo Theresa alikuwa akiishi peke yake mtaa wa Schmiedberg namba 9 katikati ya mji wa Augsburg na alimwachia nyumba hiyo mtanzania aitwaye Othman Lukindo.

Kwani alikuwa ni mtu mwenye huruma sana pamoja na kwamba alijiengemeza zaidi kwa ndugu zetu wa Kenya, alikuwa na upendo na kila mmoja uko alikokuwa akiishi alimpenda.


View attachment 348689
Miss Zanzibar wa kwanza Hediye Khamis Mussa (kati) akiwa na washindi wa pili na wa tatu January 13, 1968.

Mashindano haya yamekuwa yakitia fora na kujizolea umaarufu mkubwa ndani ya jamii ya watanzania, hasa baada ya kuwa chini ya uratibu wa Hashim Lundega, ambaye alianza kuyaendesha tangu mwaka 1994.

Kwani kupitia Lundega, kampuni mbalimbali zimekuwa zikijitokeza kudhamini mashindano hayo na kutoa zawadi zikiwemo za magari ya kisasa kwa washindi, hali iliyoyafanya yawe na ushindani mkali.

Ukuaji wa Mashindano haya ulikuwa ni wa kasi kubwa kwani watu wengi kama ilivyo kwa mchezo wa soka ama muziki, hasa baada ya muziki wa kitanzania kuingiliwa na vionjo vya kutoka nchi jirani ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo).

Mkoa wa Mbeya nao haupo nyuma katika mashindano hayo.

Umekuwa unapita katika hatua hizo kwa kupata warembo mbalimbali walioibuka washindi kuanzia ngazi ya mkoa, kanda hadi kufikia hatua ya kushiriki shindano la 'Miss Tanzania'.



View attachment 259245

View attachment 259249
Hizo zama hapakua na inchi inayoitwa tanzania,,,Tanganyika kama nitakua sahihi sijui
 
Sasa na hao wazungu walikuwa wanagombea miss europe in tanganyika au
Alikuwa anatafutwa miss tanganyika maana sijawaelewa na walivyo rundo

MKuu Kulikua na wazungu wengi ambao ni raia wa Tanganyika, wengi walizaliwa Bongo na wengine walikulia toka wadogo. Baada ya Azimio la Arusha La Nyerere wazungu wengi na wahindi waliingia mitini, mana walijua kuwa hii nchi sio salama tena.
 
Tatizo sio alitwaa lini. Alitwaa 1967, okay, mashindano yalianza lini?

Bado unasomeka kwamba mashindano yalianza 1960, mrembo wa kwanza kunyakua akaja 1967. Walikuwa wanatoka draw miaka yote saba kabla ya '67?

Wasema "hakubahatika" kupata mtoto. Aliwahi kusema kwamba alitaka watoto?

Wadai alikuwa mpole mwenye huruma "pamoja na kwamba alijiegemeza zaidi na ndugu zetu wa Kenya." Kwa hiyo ku hang na Wakenya kunatia hitilafu katika upole wa mtu?

Na ulipochomekea kwamba mkoa wa Mbeya hauko nyuma katika mashindano hayo, what is special about mashindano au warembo wa Mbeya? Hiyo sifa ya Mbeya kutoa mshindi, sio Mbeya peke yake wanayo.
Aisee...
 
Back
Top Bottom