The Weekend that Lasts ......

Kasie

Platinum Member
Dec 29, 2013
21,222
36,238
Habari za mwisho wa wiki waungwana,

Hiki kisa ninachokisimulia hapa naona kama kinataka kujirudia na tukio lililotukia nikiwa mwanamke wa makamo I was in my last 30s year....

Ni miaka 10 iliyopita ilikuwa naishi Mwenge na kibarua changu kilikuwa mjini posta. Kila siku nikiwa naelekea kazini nikawa najikuta naongozana na watu ambao tunatoka eneo moja hadi tunaingia mjini pamoja na tukishaingia viunga vya posta kila mmoja anenda kibaruani kwake.

Ilikuwa tunajikuta tunatoka mida hiyo hiyo, japo hakujua nkaa wapi wala mie sikujua anaishi wapi ni kuwa tubnakutana barabarani na tunaongozana hadi mjini, kwa sura hatujuani ila kwa aina ya magari ndo najua yulee nikimfata anaelekea mjini.

Kati ya hao tunaoongozana kuna ambao wao wanafata sheria siku zote iwe foleni watakaa hawatanui wala kuchomekea chomekea hovyo. Kuna akina sie mavurugu hadi barabarani, foleni ikikaa barabarani tushaingia panya road kukwepa foleni.

Sasa kuna huyu kaka mmoja nakumbuka alikuwa anaendesha Rav 4, siku hiyo nimetoka zangu nyumbani kwa kuchelewa kidogo kama dakika 15 ya muda ninaoondokaga siku zote. Kufika Morocco nikaona Rav 4 imepaki pembeni imewasha hazard na mwenyewe amesimama nje yuko na simu kana kwamba vile anawasiliana na mtu aje kumtatua hapo alipo na anaonekana alikuwa na msongo wa kuwahi anakokwenda wakati gari ndo ishabuma. Nikajikuta tuu nimesimama pembeni nikashusha kioo nikapiga honi, habari yako... (Kichwani lengo langu nitoe msaada wa lifti maana najua anenda mjini).

Kweli kaka akaja nikamwambia pole jirani naona gari imegoma kwenda, akasema yeah fundi keshafika hapa nilikuwa nampigia mtu aniletee gari ingine nyumbani niwahi kibaruani ila muda umeenda na leo nna kikao asubuhi daah. Nikamwambia jirani kazi yake ni nini, panda twende, sitakufikisha kazini ila nikikuacha maeneo ya Posta najua utafika tuu ofisini kwako. Yule kaka kusikia vile akarudi kwenye gari lake kachukua mkoba wake (seems kama ni wa laptop au nyaraka) akaingia kwenye gari haoo tukaondoka. Njia nzima tulikuwa kimya mie nikikosentreti kuwahi mjini nayeye ile tension ya asichelewe na awahi kikao asubuhi.

Tukafanikiwa kufika mjini nusu saa kabla ya kikao chake kuanza, mie nilikuwa naishia jengo la PPF yeye nikamuacha kona ya kwenda kanisani. (nimeacha hivi makususdi kupunguza dotisi)
Wakati namshusha akanipa mkono na kutamka jina lake Wycliff huku akitabasamu nami nikampa mkono na kusema Kasinde. Akaniambia naomba leo jioni tuonane angle thita tafadhali usikatae, nikawambia bila hofu.

Baada ya muda wa kazi nikafika angle thita na kukuta Wycliff ameshafika, maongezi ya hapa na pale yakaanza tukala dinner tukanywa, mziki ukaanza na dancing juu. Tulikaa pale hadi saa sita kasoro usiku ndo kila mmoja akarudi kwake bila kutokea madhara yeyote yale. Usiku ule tulicheza sana mziki kumbe nae ni mpenda mziki kama Kasie, na alinishukuru sana kwa kumpa lifti ile asubuhi maana alishakata tamaa ya kuwahi kikao.

Sasa wiki iliyopita jumatano, tukio hili limejirudia kwa mwanaume mwingine huku S.A. Mkaka huyu wa kizulu huwa tunaongozana kuelekea uelekeo mmoja asubuhi na jumatano hiyo alipata shida ya gari, nikampa lifti hadi maeneo anayofanyia kazi na jioni yake tukawa na heavy night, tulicheza mziki tukala tukanywa hadi usiku mnene. Kisha bila madhara kila mmoja alirudi kwake kivyake maana akiwa kazini aliletewa gari yake ikiwa ishakuwa fixed.

Moja ya wimbo tulioucheza kama vile hakuna kufa ni hii wa shakira....



It was hot asieeh...

Nimeelezea kwa kirefu, na hapo nimejitahidi kufupisha. Natumai sio crush...

Kasinde Matata.
 
Habari za mwisho wa wiki waungwana,

Hiki kisa ninachokisimulia hapa naona kama kinataka kujirudia na tukio lililotukia nikiwa mwanamke wa makamo I was in my last 30s year....

Ni miaka 10 iliyopita ilikuwa naishi Mwenge na kibarua changu kilikuwa mjini posta. Kila siku nikiwa naelekea kazini nikawa najikuta naongozana na watu ambao tunatoka eneo moja hadi tunaingia mjini pamoja na tukishaingia viunga vya posta kila mmoja anenda kibaruani kwake.

Ilikuwa tunajikuta tunatoka mida hiyo hiyo, japo hakujua nkaa wapi wala mie sikujua anaishi wapi ni kuwa tubnakutana barabarani na tunaongozana hadi mjini, kwa sura hatujuani ila kwa aina ya magari ndo najua yulee nikimfata anaelekea mjini.

Kati ya hao tunaoongozana kuna ambao wao wanafata sheria siku zote iwe foleni watakaa hawatanui wala kuchomekea chomekea hovyo. Kuna akina sie mavurugu hadi barabarani, foleni ikikaa barabarani tushaingia panya road kukwepa foleni.

Sasa kuna huyu kaka mmoja nakumbuka alikuwa anaendesha Rav 4, siku hiyo nimetoka zangu nyumbani kwa kuchelewa kidogo kama dakika 15 ya muda ninaoondokaga siku zote. Kufika Morocco nikaona Rav 4 imepaki pembeni imewasha hazard na mwenyewe amesimama nje yuko na simu kana kwamba vile anawasiliana na mtu aje kumtatua hapo alipo na anaonekana alikuwa na msongo wa kuwahi anakokwenda wakati gari ndo ishabuma. Nikajikuta tuu nimesimama pembeni nikashusha kioo nikapiga honi, habari yako... (Kichwani lengo langu nitoe msaada wa lifti maana najua anenda mjini).

Kweli kaka akaja nikamwambia pole jirani naona gari imegoma kwenda, akasema yeah fundi keshafika hapa nilikuwa nampigia mtu aniletee gari ingine nyumbani niwahi kibaruani ila muda umeenda na leo nna kikao asubuhi daah. Nikamwambia jirani kazi yake ni nini, panda twende, sitakufikisha kazini ila nikikuacha maeneo ya Posta najua utafika tuu ofisini kwako. Yule kaka kusikia vile akarudi kwenye gari lake kachukua mkoba wake (seems kama ni wa laptop au nyaraka) akaingia kwenye gari haoo tukaondoka. Njia nzima tulikuwa kimya mie nikikosentreti kuwahi mjini nayeye ile tension ya asichelewe na awahi kikao asubuhi.

Tukafanikiwa kufika mjini nusu saa kabla ya kikao chake kuanza, mie nilikuwa naishia jengo la PPF yeye nikamuacha kona ya kwenda kanisani. (nimeacha hivi makususdi kupunguza dotisi)
Wakati namshusha akanipa mkono na kutamka jina lake Wycliff huku akitabasamu nami nikampa mkono na kusema Kasinde. Akaniambia naomba leo jioni tuonane angle thita tafadhali usikatae, nikawambia bila hofu.

Baada ya muda wa kazi nikafika angle thita na kukuta Wycliff ameshafika, maongezi ya hapa na pale yakaanza tukala dinner tukanywa, mziki ukaanza na dancing juu. Tulikaa pale hadi saa sita kasoro usiku ndo kila mmoja akarudi kwake bila kutokea madhara yeyote yale. Usiku ule tulicheza sana mziki kumbe nae ni mpenda mziki kama Kasie, na alinishukuru sana kwa kumpa lifti ile asubuhi maana alishakata tamaa ya kuwahi kikao.

Sasa wiki iliyopita jumatano, tukio hili limejirudia kwa mwanaume mwingine huku S.A. Mkaka huyu wa kizulu huwa tunaongozana kuelekea uelekeo mmoja asubuhi na jumatano hiyo alipata shida ya gari, nikampa lifti hadi maeneo anayofanyia kazi na jioni yake tukawa na heavy night, tulicheza mziki tukala tukanywa hadi usiku mnene. Kisha bila madhara kila mmoja alirudi kwake kivyake maana akiwa kazini aliletewa gari yake ikiwa ishakuwa fixed.

Moja ya wimbo tulioucheza kama vile hakuna kufa ni hii wa shakira....



It was hot asieeh...

Nimeelezea kwa kirefu, na hapo nimejitahidi kufupisha. Natumai sio crush...

Kasinde Matata.


Anaitwa nani huyo Msauzi? Dumisane Dube?
 
Naanzia wapi kwanza kumchunia Toto la Kinyamwezi!! Usicheze na utamu wa asali tena ile mbichi ya Tabora weeeee!


Aahahahahaaaaahahahahaa kiasaliii

Umenifanya nipange mkakati wa mashambulizi ya asali kwa tukio lijalo...

Waalaaah itakuwa mavurugu plus plus bin square eehhehehheeeee.

Na wewe ni mtaalam wa kurina asali??!

Matata K.
 
K matata mpenda kujirusha kwa namna mbali mbali ikiwemo muziki. 😜




B to the K, how are you handsome...

You once tell me not to read between the lines,so do you....

Sean on the line below.....



Baby please come over...

Kasinde.
 
Aahahahahaaaaahahahahaa kiasaliii

Umenifanya nipange mkakati wa mashambulizi ya asali kwa tukio lijalo...

Waalaaah itakuwa mavurugu plus plus bin square eehhehehheeeee.

Na wewe ni mtaalam wa kurina asali??!

Matata K.
Ahahaaahahaaaaaaaaaaaaaaa......

Nilifunzwa kurina asali na kwa sasa nikiukuta mzinga wa kiasali sio kwamba nitarina tu asali bali napakua kabisaaaaaaa kiasali
 
Mambo ya weekend hayooo! I can’t complain God is always GREAT and I am very appreciative. Life is GOOD!



B to the K, how are you handsome...

You once tell me not to read between the lines,so do you....

Sean on the line below.....



Baby please come over...

Kasinde.
 
Ahahaaahahaaaaaaaaaaaaaaa......

Nilifunzwa kurina asali na kwa sasa nikiukuta mzinga wa kiasali sio kwamba nitarina tu asali bali napakua kabisaaaaaaa kiasali


Aahahahahhahahahaaa unaniamsha kiasali, weekend hii, isije ikawa the weekend that lasts....
 
Back
Top Bottom