The SPY: Series inayoonesha Jinsi Jasusi la Mossad "Eli Cohen" Lilivyowachachafa wa Syria miaka ya 60.

Sasa kwann Israel isiingilie kati jamaa kuuwawa na mkewe anaishi nchi gan saa hz na ilikuwaje akanyakwa
Tuambie usije sema stry itakuwa ndefu
Ni Kama vile nilishawahi isoma Tena humuhumu ila hapo muandishi Kuna vitu vipya naona vimeongezeka.. kazi ya kijasusi si kazi ya hovyo inahitaji ujasiri,akili pana,ujuzi,uzalendo,kujiweza kihisia,uongo ambao mhusika anaweza kuuvaa.. kwa jicho la mbele binadamu tutakuja kupata changamoto zaidi pindi kutakapo kuwa na muingiliano na aina ya viumbe ambao watakuwa na ufahamu Kama sisi au zaidi huu ni mwanzo wa ukuaji wetu tu mambo yatakuja kuwa Moto.
kilichomponza no utumaji taarifa mfululizo huko Israel ambapo wakuu wa usalama Syria waligundua muingiliano wa mawasiliano usio wa kawaida hivyo wakafuatilia yankotokea ndipo walipo mnyaka kitu pekee familia yake ilichoambulia kutoka Syria in SAA ya mkononi
 
Duuh hatari sana
Ni one of the short docuseries on Netflix sasa hivi, imeanza kuruka nadhani last week,

Nimekuwaga nikisoma habari za Majasusi wa Mossad, na namna ambavyo Mossad ni moja ya Intelligence Unit inayoheshimika zaidi duniani, along with CIA,M16 KGB na nyingine. Humu Jf na hata kwingineko.

Sasa this weekend katika kushanga shangaa mtandaoni nikakutana na kitu "The SPY" japonajua kutakuwa na vi propaganda kama kawaida, Jews wanajua kusimulia habari zao vizuri kuliko habari za wengine, so najua watakuwa wamejichotea sana, ila nimewakubali sana.


AGENT Recruitment
Jamaa Eli Cohen, kajaribu mara kadhaa kuomba kazi Mossad, anatoswa kwa kuwa hana vigezo, later on, kutokana na vita inayoendelea kati ya Syria na Israel, Mossad wanalazimika kufanya juu chini, ili wawe na agent wao, Syria, shinikizo toka kwa waziri mkuu na wakuu wote wa usalama, wanataka apatikane agent haraka sana, ambae atafaa kwa mahitaji ya eneo hilo la Syria

Jamaa katika kupitia mafile ya potential people wanakutana na file la Eli Cohen, ambae ni mzaliwa wa Misri, kwa hyo ana element na lafudhi ya kiarabu arabu kidogo, na mambo mengine. Anapitia mafunzo ya muda kidogo ili awe tayari kwa kazi.Mchakato na mitihani anayopewa ili aonekane kama atafaa au lah, inakuonesha namna gani jamaa wapo makini katika kuspot potential candidate na kurecruit.

Usiri Mkubwa
Pamoja na kuwa jamaa alikuwa yupo in very good term na mke wake, full kupendana, wife hakuwahi wala hata ndugu zake,kuwa jamaa kaitwa na Mossad, na amepewa kazi maalumu, kwa mke wake na ndugu zake, alizuga yeye ni afisa manunuzi wa jeshi la Israel, kwa hyo anazunguka dunia nzima, na hasa ana spent more time Uswisi, Karibu na mwishoni, mwishon mmoja wa kaka ake, amabe nae ni afisa usalama, ila alikuwabased home, ndo anakuja hisi kuwa jamaa ndo atakuwa yule the famous agent 88. Kwa hiyo kiufupi nikuwa hata kaka mtu ambaye nae alikuwa ni agent mwana usalama, hakuwa anajua, wala hakujua, ilibidi afanye jitihada binafsi kujua, hasa pale ambapo kimakosa, alipewa nafasi ya kumshikia mtu anae pokea taarifa toka kwa agent Eli cohen.

Cover Establishemnt:
Kwamba ilipanga jamaa ,aonekane kuwa ni mfanyabiashara mkubwa wa Kisyria, anaeishi Argentina anaetaka kurud home ili kutumikia taifa lake, ikabid kweli jamaa aende Argentina, aishi muda kadhaa, ajenge urafiki na balozi wa Syria Argentina, anazuga wazazi wake walikufa wakazikwa , makaburi yakaandaliwa kabisa, kwamba biashara yake ya export-Import ipo Uswisi, nayo ikawekwa vzuri. yaani kwenye kutengeneza identity ya uongo, jamaa waliweza. Akaanza julikana kama Kamel Amin Thaabet

Jitihada Binafsi+Kujiongeza+Resources +Uimara wa Mossad
Utapewa mafunzo, ndiyo, utapewa vitendea kazi ndiyo vyote pamoja na hela, lakini kufanikiwa kwa mission bado kunahitaji jitihada zako binafsi, jamaa Kamel Amin Thaabet alijijenga vzuri ,analifanya kazi ambayo hadi wakuu wa Mossad wenyewe walikuwa wanashangaa, ni zao la jitihada zake binafsi na uwezo wake wa kuweza kujipenyeza

Kuchaguliwa kuwa Naibu wizara ya Ulinzi

Hapo ndipo nilipokuja kumvulia kofia jamaa, ilifika kipindi , Rais anamteua awe naibu wa wizara ya ulinzi, na ofcourse hiki ndo kitu kilichomcost ,kwani ilibid airudi tena Syria, ila kurud kwake ni baada ya Wakuu wa Mossad kuona, tunanafasi ya kuwa na naibu wizara ya Ulinzi amabe ni wetu, hebu arudi tu, japo jamaa, alikuwa ameshaona kuwa kazi kubwa imefanyika na sirudi, na kweli aliporud, ndo akakamwata

Osama Bin Laden na Baba ake:

Kwenye series, anaoneka Baba ake Osama, ambae kampuni yake ilipewa tenda na serikali ya Syria kujenga project ambayo ingewaathiri vyanzo vya maji ekee vuya Israel na kuwafanya washindwe kuendesha nchi, Anaonekana Osama, akiwa mdogo, wakati Baba ake Osama akiongea na Kamel Amin Thaabet "Jasusi Eli cohen" Mipango ya kuingiza ndani hiyo mitambo.

Mafanikio

Mafanikio ya kazi yake jamaa, yalikuwa ni makubwa, inasememakana, ile vita ambayo Waisrael huwa wanajisifia sana kuwa waliwatandika waarabu kwa siku 6 tu, Six days war, ilitokana na taarifa kuntu alizozikusanya bwana Eli Cohen.

Kunyongwa na Tusi kubwa kwa Wasyria.
Ilikuwa ngumu kwa Wasyria kumsahehe jamaa, hata maiti yake hawaja isamehe, na Ndo maana hata leo hii mke wa Eli Cohen, Bibi Nadia, bado huwa analia kuomba mabaki ya maiti yake yarudishwe, Hadi 2001 bado waziri aliepita wa Syria Bwana Hafiz, alikuwa bado kwenye vyombo vya habari anaongelea ishu ya Eli cohen, Ilikuwa ni aibu kwa Taifa.
 
Ujasusi bwana unaweza ukawa unafanyiwa vetting na mtu ambaye unamchukulia poa/humdhanii/humfikirii na unaishi nae katika jamii moja na akamaliza kuchota info zako zote na wee ukawa hujui/upo upo/hutambui lolote then ukaonekana hufai/hujatimiza vigezo wakakutosa/wakaachana na wewe na file lako linafungwa pasipo wewe kujua/kutambua nini kilitokea na tayari kimeshapita
 
Ukiachana na movie kama movie huyu Bwana aliwahi kuexist kweli kabisa. Kilichonisikitisha zaidi wakati Wasiria wanamu execute mataifa mengi yaliingilia bila mafanikio, hata papa mwenyewe hakufua dafu. Nime quote hii passage Wikipedia inasema hivi;

“Israel staged an international campaign for clemency, hoping to persuade the Syrians not to execute him. Israeli Foreign Minister Golda Meir led a campaign urging Damascus to consider the consequences of hanging him. Diplomats, prime ministers, and Pope Paul VI tried to intercede. Meir even appealed to the Soviet Union.[4] The governments of Belgium, Canada, and France tried to persuade the Syrian government to commute the death sentence,[17] but the Syrians refused”
 
Nimeitazama aisee ipo njema sana nillipenda sana NARCOS na hii THE SPY nimeipenda mno.
 
Moja ya series bora kabisa Netflix. Binafsi kati ya mengi yaliyonivutia ni aliyecheza nafasi ya Eli Cohen. Jamaa nilijua kama Borat na King Julien (the original). Nilitaka kuona kucheza serious character inakuwaje.

Ukiangalia na 'into the Mossad' documentary, 'Red Sea Diving Resort' movie. Zote zinasaidia kuielewa 'The Spy' na Mossad zaidi.
 
Moja ya series bora kabisa Netflix. Binafsi kati ya mengi yaliyonivutia ni aliyecheza nafasi ya Eli Cohen. Jamaa nilijua kama Borat na King Julien (the original). Nilitaka kuona kucheza serious character inakuwaje.

Ukiangalia na 'into the Mossad' documentary, 'Red Sea Diving Resort' movie. Zote zinasaidia kuielewa 'The Spy' na Mossad zaidi.
Sacha Baron Cohen.. very fun this guy..
Ref. Madagascar &The dictator
 
19 Reactions
Reply
Back
Top Bottom