pinno
JF-Expert Member
- Jan 17, 2013
- 1,213
- 1,228
Ni one of the short docuseries on Netflix sasa hivi, imeanza kuruka nadhani last week,
Nimekuwaga nikisoma habari za Majasusi wa Mossad, na namna ambavyo Mossad ni moja ya Intelligence Unit inayoheshimika zaidi duniani, along with CIA,M16 KGB na nyingine. Humu Jf na hata kwingineko.
Sasa this weekend katika kushanga shangaa mtandaoni nikakutana na kitu "The SPY" japonajua kutakuwa na vi propaganda kama kawaida, Jews wanajua kusimulia habari zao vizuri kuliko habari za wengine, so najua watakuwa wamejichotea sana, ila nimewakubali sana.
AGENT Recruitment
Jamaa Eli Cohen, kajaribu mara kadhaa kuomba kazi Mossad, anatoswa kwa kuwa hana vigezo, later on, kutokana na vita inayoendelea kati ya Syria na Israel, Mossad wanalazimika kufanya juu chini, ili wawe na agent wao, Syria, shinikizo toka kwa waziri mkuu na wakuu wote wa usalama, wanataka apatikane agent haraka sana, ambae atafaa kwa mahitaji ya eneo hilo la Syria
Jamaa katika kupitia mafile ya potential people wanakutana na file la Eli Cohen, ambae ni mzaliwa wa Misri, kwa hyo ana element na lafudhi ya kiarabu arabu kidogo, na mambo mengine. Anapitia mafunzo ya muda kidogo ili awe tayari kwa kazi.Mchakato na mitihani anayopewa ili aonekane kama atafaa au lah, inakuonesha namna gani jamaa wapo makini katika kuspot potential candidate na kurecruit.
Usiri Mkubwa
Pamoja na kuwa jamaa alikuwa yupo in very good term na mke wake, full kupendana, wife hakuwahi wala hata ndugu zake,kuwa jamaa kaitwa na Mossad, na amepewa kazi maalumu, kwa mke wake na ndugu zake, alizuga yeye ni afisa manunuzi wa jeshi la Israel, kwa hyo anazunguka dunia nzima, na hasa ana spent more time Uswisi, Karibu na mwishoni, mwishon mmoja wa kaka ake, amabe nae ni afisa usalama, ila alikuwabased home, ndo anakuja hisi kuwa jamaa ndo atakuwa yule the famous agent 88. Kwa hiyo kiufupi nikuwa hata kaka mtu ambaye nae alikuwa ni agent mwana usalama, hakuwa anajua, wala hakujua, ilibidi afanye jitihada binafsi kujua, hasa pale ambapo kimakosa, alipewa nafasi ya kumshikia mtu anae pokea taarifa toka kwa agent Eli cohen.
Cover Establishemnt:
Kwamba ilipanga jamaa ,aonekane kuwa ni mfanyabiashara mkubwa wa Kisyria, anaeishi Argentina anaetaka kurud home ili kutumikia taifa lake, ikabid kweli jamaa aende Argentina, aishi muda kadhaa, ajenge urafiki na balozi wa Syria Argentina, anazuga wazazi wake walikufa wakazikwa , makaburi yakaandaliwa kabisa, kwamba biashara yake ya export-Import ipo Uswisi, nayo ikawekwa vzuri. yaani kwenye kutengeneza identity ya uongo, jamaa waliweza. Akaanza julikana kama Kamel Amin Thaabet
Jitihada Binafsi+Kujiongeza+Resources +Uimara wa Mossad
Utapewa mafunzo, ndiyo, utapewa vitendea kazi ndiyo vyote pamoja na hela, lakini kufanikiwa kwa mission bado kunahitaji jitihada zako binafsi, jamaa Kamel Amin Thaabet alijijenga vzuri ,analifanya kazi ambayo hadi wakuu wa Mossad wenyewe walikuwa wanashangaa, ni zao la jitihada zake binafsi na uwezo wake wa kuweza kujipenyeza
Kuchaguliwa kuwa Naibu wizara ya Ulinzi
Hapo ndipo nilipokuja kumvulia kofia jamaa, ilifika kipindi , Rais anamteua awe naibu wa wizara ya ulinzi, na ofcourse hiki ndo kitu kilichomcost ,kwani ilibid airudi tena Syria, ila kurud kwake ni baada ya Wakuu wa Mossad kuona, tunanafasi ya kuwa na naibu wizara ya Ulinzi amabe ni wetu, hebu arudi tu, japo jamaa, alikuwa ameshaona kuwa kazi kubwa imefanyika na sirudi, na kweli aliporud, ndo akakamwata
Osama Bin Laden na Baba ake:
Kwenye series, anaoneka Baba ake Osama, ambae kampuni yake ilipewa tenda na serikali ya Syria kujenga project ambayo ingewaathiri vyanzo vya maji ekee vuya Israel na kuwafanya washindwe kuendesha nchi, Anaonekana Osama, akiwa mdogo, wakati Baba ake Osama akiongea na Kamel Amin Thaabet "Jasusi Eli cohen" Mipango ya kuingiza ndani hiyo mitambo.
Mafanikio
Mafanikio ya kazi yake jamaa, yalikuwa ni makubwa, inasememakana, ile vita ambayo Waisrael huwa wanajisifia sana kuwa waliwatandika waarabu kwa siku 6 tu, Six days war, ilitokana na taarifa kuntu alizozikusanya bwana Eli Cohen.
Kunyongwa na Tusi kubwa kwa Wasyria.
Ilikuwa ngumu kwa Wasyria kumsahehe jamaa, hata maiti yake hawaja isamehe, na Ndo maana hata leo hii mke wa Eli Cohen, Bibi Nadia, bado huwa analia kuomba mabaki ya maiti yake yarudishwe, Hadi 2001 bado waziri aliepita wa Syria Bwana Hafiz, alikuwa bado kwenye vyombo vya habari anaongelea ishu ya Eli cohen, Ilikuwa ni aibu kwa Taifa.
Nimekuwaga nikisoma habari za Majasusi wa Mossad, na namna ambavyo Mossad ni moja ya Intelligence Unit inayoheshimika zaidi duniani, along with CIA,M16 KGB na nyingine. Humu Jf na hata kwingineko.
Sasa this weekend katika kushanga shangaa mtandaoni nikakutana na kitu "The SPY" japonajua kutakuwa na vi propaganda kama kawaida, Jews wanajua kusimulia habari zao vizuri kuliko habari za wengine, so najua watakuwa wamejichotea sana, ila nimewakubali sana.
AGENT Recruitment
Jamaa Eli Cohen, kajaribu mara kadhaa kuomba kazi Mossad, anatoswa kwa kuwa hana vigezo, later on, kutokana na vita inayoendelea kati ya Syria na Israel, Mossad wanalazimika kufanya juu chini, ili wawe na agent wao, Syria, shinikizo toka kwa waziri mkuu na wakuu wote wa usalama, wanataka apatikane agent haraka sana, ambae atafaa kwa mahitaji ya eneo hilo la Syria
Jamaa katika kupitia mafile ya potential people wanakutana na file la Eli Cohen, ambae ni mzaliwa wa Misri, kwa hyo ana element na lafudhi ya kiarabu arabu kidogo, na mambo mengine. Anapitia mafunzo ya muda kidogo ili awe tayari kwa kazi.Mchakato na mitihani anayopewa ili aonekane kama atafaa au lah, inakuonesha namna gani jamaa wapo makini katika kuspot potential candidate na kurecruit.
Usiri Mkubwa
Pamoja na kuwa jamaa alikuwa yupo in very good term na mke wake, full kupendana, wife hakuwahi wala hata ndugu zake,kuwa jamaa kaitwa na Mossad, na amepewa kazi maalumu, kwa mke wake na ndugu zake, alizuga yeye ni afisa manunuzi wa jeshi la Israel, kwa hyo anazunguka dunia nzima, na hasa ana spent more time Uswisi, Karibu na mwishoni, mwishon mmoja wa kaka ake, amabe nae ni afisa usalama, ila alikuwabased home, ndo anakuja hisi kuwa jamaa ndo atakuwa yule the famous agent 88. Kwa hiyo kiufupi nikuwa hata kaka mtu ambaye nae alikuwa ni agent mwana usalama, hakuwa anajua, wala hakujua, ilibidi afanye jitihada binafsi kujua, hasa pale ambapo kimakosa, alipewa nafasi ya kumshikia mtu anae pokea taarifa toka kwa agent Eli cohen.
Cover Establishemnt:
Kwamba ilipanga jamaa ,aonekane kuwa ni mfanyabiashara mkubwa wa Kisyria, anaeishi Argentina anaetaka kurud home ili kutumikia taifa lake, ikabid kweli jamaa aende Argentina, aishi muda kadhaa, ajenge urafiki na balozi wa Syria Argentina, anazuga wazazi wake walikufa wakazikwa , makaburi yakaandaliwa kabisa, kwamba biashara yake ya export-Import ipo Uswisi, nayo ikawekwa vzuri. yaani kwenye kutengeneza identity ya uongo, jamaa waliweza. Akaanza julikana kama Kamel Amin Thaabet
Jitihada Binafsi+Kujiongeza+Resources +Uimara wa Mossad
Utapewa mafunzo, ndiyo, utapewa vitendea kazi ndiyo vyote pamoja na hela, lakini kufanikiwa kwa mission bado kunahitaji jitihada zako binafsi, jamaa Kamel Amin Thaabet alijijenga vzuri ,analifanya kazi ambayo hadi wakuu wa Mossad wenyewe walikuwa wanashangaa, ni zao la jitihada zake binafsi na uwezo wake wa kuweza kujipenyeza
Kuchaguliwa kuwa Naibu wizara ya Ulinzi
Hapo ndipo nilipokuja kumvulia kofia jamaa, ilifika kipindi , Rais anamteua awe naibu wa wizara ya ulinzi, na ofcourse hiki ndo kitu kilichomcost ,kwani ilibid airudi tena Syria, ila kurud kwake ni baada ya Wakuu wa Mossad kuona, tunanafasi ya kuwa na naibu wizara ya Ulinzi amabe ni wetu, hebu arudi tu, japo jamaa, alikuwa ameshaona kuwa kazi kubwa imefanyika na sirudi, na kweli aliporud, ndo akakamwata
Osama Bin Laden na Baba ake:
Kwenye series, anaoneka Baba ake Osama, ambae kampuni yake ilipewa tenda na serikali ya Syria kujenga project ambayo ingewaathiri vyanzo vya maji ekee vuya Israel na kuwafanya washindwe kuendesha nchi, Anaonekana Osama, akiwa mdogo, wakati Baba ake Osama akiongea na Kamel Amin Thaabet "Jasusi Eli cohen" Mipango ya kuingiza ndani hiyo mitambo.
Mafanikio
Mafanikio ya kazi yake jamaa, yalikuwa ni makubwa, inasememakana, ile vita ambayo Waisrael huwa wanajisifia sana kuwa waliwatandika waarabu kwa siku 6 tu, Six days war, ilitokana na taarifa kuntu alizozikusanya bwana Eli Cohen.
Kunyongwa na Tusi kubwa kwa Wasyria.
Ilikuwa ngumu kwa Wasyria kumsahehe jamaa, hata maiti yake hawaja isamehe, na Ndo maana hata leo hii mke wa Eli Cohen, Bibi Nadia, bado huwa analia kuomba mabaki ya maiti yake yarudishwe, Hadi 2001 bado waziri aliepita wa Syria Bwana Hafiz, alikuwa bado kwenye vyombo vya habari anaongelea ishu ya Eli cohen, Ilikuwa ni aibu kwa Taifa.