The Silence Is Killing Me

BadoNipo

Senior Member
Jul 4, 2008
170
28
Jamani wanaJF tumsaidie binti huyu, mawazo yenu ni muhimu sana kwake.

'I have been in my relationship with this man for eight months, and I am in love with him. But, my question or concern is when I say to him, "I love you." There is nothing -- just silence. I don't care if he doesn't say it back, however, something kind or caring stated back would be appreciated. What is the problem? What should I do? Am I just fooling myself? '
 
Dada Yangu Neno I Love You Ni Neno Tu , Kwa Taarifa Yako Siku Hizi Hata Watoto Wadogo Wanataniana Kwahiyo Hilo Ni Neno Tu Mapenzi Ni Zaidi Ya I Love You Ni Zaidi Ya Unavyofikiria Wewe Ni Zaidi Ya Kila Kitu Ni Kazi Yako Wewe Kujua Mpenzi Wako Anataka Nini Katika Wakati Gani Ili Mufurahie Maisha Yenu

Mchana Mwema Mbona Mie Sijawahi Kumwambia Naima I Love You ?
 
Nimuulize swali kabla sijatoa ushauri. Uhusiano wao ulianzaje? ni huyo demu alimuomba urafiki au ni huyo jamaa? Nauliza hivi kwa sababu wakati mwingine kama ni msichana amemtongoza mwanaume inakuwaga kama mwanaume ameshikwa na bubmbuwazi flani anapoambiwa nakupenda hadi anasita kurudisha!!!!
 
Mchola Hiyo Unayosemea Wewe Imepitwa Na Wakati Na Hiyo Ni Unyanyasaji Kijinsia Wewe Soma Alama Za Nyakati Utaona Ninachosema Nina Maanisha Nini
 
Nimuulize swali kabla sijatoa ushauri. Uhusiano wao ulianzaje? ni huyo demu alimuomba urafiki au ni huyo jamaa? Nauliza hivi kwa sababu wakati mwingine kama ni msichana amemtongoza mwanaume inakuwaga kama mwanaume ameshikwa na bubmbuwazi flani anapoambiwa nakupenda hadi anasita kurudisha!!!!

Mwanamume ndo aliyeomba urafiki
 
mkalishe chini mwambiye how you feel .. sometimes watu wanajiongopea kwamba wanafanya kile ambacho mwenzake anakihitaji kwake 100% na hata baadae huyo asieridhika akija kukatisha uhusiano mwengine anajiuliza hivi ni kitu gani ambacho sijampa yule mwanamke au mwanaume na nimekosea wapi ... sasa if you dont take the trouble to tell him .. wewe ukifahamu vyema kwamba he cant read the signs utakuwa umemuonea .. please mkalishe chini umwambie kwa upendo na upole dont try to hide your feelings muonyeshe kwamba unaumia waziwazi .. atakuelewa halafu he will reciprocate definately
 
Sawa Shy lakini haikutakiwa iwe hivyo basi ni kwa vile wanaforce na matokeo yake ndio kama ya kule Urusi. Mtanzania akienda kusoma Urusi kama haji na mrusi basi utasikia kazaa nae akamtoroka siku ya kurudi. Kisa ni wanawake wanawang'ang'ania wanaume. Sasa naona taratibu inaingia hapa kwetu. Raha ya mwanamke ni Mwanaume amtongoze kwa maneo laini, oh nakupenda kama mboni ya jicho langu, nikilala nakuota wewe...
Kumbuka, mwanamke hata kama anajua unamdanganya lakini kumwambia nakupenda inamsuuza roho yake. Wewe ukiona huwezi kumtamkia mwnamke neno 'nakupenda' basi ujue hayupo moyoni bali unamtumia tu



Daaa! sasa wewe unataka kuturudisha wapi sijui,kwa zama hizi za uhuru wa kueleza hisia zako wacha wakina dada wawatokee hao wanaume.

Ukisubiri kufuatwa nawe ndo umezimika utaula wa chuya,atatokea mjanja amchukue umpendae ubaki ningejua ningejua.
 
Daaa! sasa wewe unataka kuturudisha wapi sijui,kwa zama hizi za uhuru wa kueleza hisia zako wacha wakina dada wawatokee hao wanaume.

Ukisubiri kufuatwa nawe ndo umezimika utaula wa chuya,atatokea mjanja amchukue umpendae ubaki ningejua ningejua.

mmmmmmmh......hii imetulia mkuu
 
Kama mtu hawezi hata ku fake "I love you too" anaweza kufanya sacrifices zinazotakiwa na mapenzi ya kweli?
 
Jamani wanaJF tumsaidie binti huyu, mawazo yenu ni muhimu sana kwake.

'I have been in my relationship with this man for eight months, and I am in love with him. But, my question or concern is when I say to him, "I love you." There is nothing -- just silence. I don't care if he doesn't say it back, however, something kind or caring stated back would be appreciated. What is the problem? What should I do? Am I just fooling myself? '

Kama alivyosema Shy love goes beyond words!!! Yawezekana huyu binti yeye mapenzi yake anayaonyesha kwa huyu jamaa through words saying "I love you" wakati jamaa anaonyesha mapenzi through deeds!!! I think its better huyu binti akajaribu kujifanyia evaluation kujua is she worth what she says au anaongea hili na kutenda lile!!

Kingine ambacho napenda mkifahamu mabinti humu ndani ni kwamba in most cases msichana akisema i love you yawezekana kuna kitu anahitaji atimiziwe kwa hiyo anajaribu kwanza kuinfeluence/kumintimidate jamaa yake ili chochote atakachohitaji kitimizwe!!! I hope this is not the case for you coz kama ni hivyo ujue jamaa ashajua janja yako na kachoka!!!!!!

kuna wakati utapewa jibu la...
Girl says: I love you
Man replies: What is it now??

Just be careful love is not in words but in every little thing you do!!!
 
Dont push pengine he is afraid of saying something without being very sure of it... Anapractice ile kusema dont say I love you unless you mean it. mchunguze matendo yake na feelings zake kwako then utajua kwa nini hasemi. Pengine anasubiri kuwa haika .
 
Hivi neno I LOVE YOU, linatosha kabisa kukuonyesha kuwa unapendwa? mbona kuna njia nyingi tu. Inawezekana kuna mmoja wao anapendelea mapenzi ya kuangalia kwenye series (ISIDINGO).

Muulize huyo dada kama kuna dalili zozote za kupendwa au kutopendwa ukiachilia kuambiwa neno I LOVE YOU.
Ni hayo tu ngoja nimalize kabla muajiri hajanifumania.
 
sasa naona mwaongea mengi kwani kusema nakupenda ni dhambi? sasahivi msichana anauwezo wa kusema nakupenda kwani aibu imeisha au unasemaje?

mama wa ushauri
 
Jibu linajulikana "I love you too".
Sasa akishaambiwa inakuwaje?
Nahisi huyo kaka anashangaa hiyo sinema ya kihindi hajaiona.
anataka umuonyeshe mapenzi siyo umuambie mapenzi.
Nina uhakika matendo husema mengi kuliko maneno.
Hata macho tu husema zaidi.
Hasa kama ni watanzania ambao hatuaminiki maneno yetu!!!! wala simshangai huyo kijana.
 
Jibu linajulikana "I love you too".
Sasa akishaambiwa inakuwaje?
Hata macho tu husema zaidi.
Hasa kama ni watanzania ambao hatuaminiki maneno yetu!!!! wala simshangai huyo kijana.

Umeshamaliza haika,hamna cha kuongeza
 
Mwambie kwa kiswahili....

Weeeee!, basi kama kuna neno gumu wa wapendanao kulilitamka ni hilo la 'nakupenda' ila 'i love you' hilo mbona kama unakunywa juisi ya ubuyu!, just imagine for urself how many times have you semad 'nakupenda' vis a vis ' i love you' ?...jibu unalo!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom