The SGR War: Wakati Kenya wakisuasua, Uganda wameamua kujenga SGR. Hii ni fursa kwa SGR ya Tanzania. Is it viable? Tuichangamkie?

Vipi umeanza kupewa posho ?


Mkuu!! Ukiweza kujiaajiri utakuwa na maisha ya Raha Sana aisee
 
Sasa kuna umbali gani kutoka KIA mpaka Machame route ? Au kufika mt Kilimanjaro? .Hujui kuwa hata Kenya wangejenga uwanja hakuna uwezekano wakupanda mlima , kwasababu routes zote zipo Tanzania. Na lazima mtalii awe na vibali ndo aruhusiwe kupanda huo mlima na vibali lazima avipate Tanzania. So Tanapa wanajitahidi sana ,sio kama zamani
Mkuu victor mboro, the best way kupanda Mlima Kilimanjaro inayopendwa sana na watalii ni route ya Marangu, kuanzia Marangu National Park. Kenya walipanga kujenga uwanja Taveta, kutoka Taveta hadi Marangu national park ni 20 KM, just 30 min drive, wakati kutoka KIA to Marangu ni 80km, 2hrs drive, hivyo Kenya wakijenga uwanja Taveta, watalii wa Marangu route watapitia Kenya. Japo route ya Machame ni fupi, kupanda Mlima Kilimanjaro kupitia Machame ni 7 days wakati Marangu ni 6 days kutokana na vilima vikali kuliko Marangu.
P
 
Aliandika PseudoDar186


Nimepitia takwimu kutoka the National Bureau of Statistics (NBS) na Tanzania Ports Authority (TPA) kuhusu mizigo / shehena yanayopitia bandari za Tanzania kwenda au kutoka nchi za jirani.

Kwa mwaka 2017/18, jumla ya tani 5.6 million zilipitia Tanzania (bandari ya Dar es Salaam pekee) kwenda au kutoka nchi za jirani, ikilinganishwa na tani 4.8 million mwaka 2016/17. Hili ni ongezeko la asilimia 17.1 na ni habari njema kabisa kwa TPA na nchi yetu kwa ujumla.

Ukiangalia mchanganuo wa shehena zinazoenda au kutoka nchi za jirani, asilima 61.1% ni za Zambia (36.6%) na J.D. Kongo (24.4%). Hii ni zaidi ya tani 3.4 million ambazo kwa asilimia kubwa zinawafikia jirani zetu kupitia barabara zetu hapa Tanzania. Ukipitia takwimu za 2017/18, TAZARA imefanikiwa kusafirisha mizigo ya tani 187,558 tu (3.4% ya 5.6 million) kwa njia ya reli.

Shehena za Rwanda ni asilimia 16.5% pekee (au tani 922,134) kwa mwaka wa 2017/18. Ukilinganisha na 2016/17, kuna upungufu wa 9.0% - kitu ambacho kinaashiria kuwa mizigo ya Rwanda inawezekana kuwa inapitia Kenya na Uganda.

Kwa kutumia akili za kawaida (common sense), kuna haja ya kuwekeza reli ya SGR kuunganisha Tanzania na Zambia na J.D. Kongo kwa sababu business case (volume of cargo) ni kubwa mno (kwa mara 3.7) kuliko Rwanda. Pia, tukiweza kuondoa hata tani 2 million barabani, TANROADS watapumua kidogo na matengenezo ya kila mara yanayotokana na uharibifu wa baraba zetu. Hii ni kwa mujibu ya data za NBS na TPA wenyewe.

Naomba mwenye taarifa kuhusu ya haya maamuzi ya kupeleka SGR Rwanda atujulishe
 
Paskali nahisi umemka umelewa, umeamka na mada za propaganda si propaganda bali vichekesho vitupu. SGR yetu kipande cha Dar-Moro tuliambiwa mwezi wa Nov 2019 kitakuwa kimekamilika, hadi sasa hakijakamilika na tunaambiwa kitakamilika Aprili 2021! Na kuna tetesi kuwa fedha zinasumbua kwenye huo mradi ndio maana simu ilipigwa kwa rais wa China. Unazungumzia mradi kufika Mwanza huku hata kipande cha 300km kimechekua zaidi ya 3yrs na bado hakijamilika!

Hao Uganda wana mradi wa bomba la mafuta, ilisainiwa toka 2017, na matarajio ingekamilika 2020. Lakini mpaka sasa haujaanza na hata kama ni kuanza ni kwa kusuasua. Sasa hapo unaoongelea mambo ya mradi wa SGR si vichekesho hivyo? Nikikumbuka ule utapeli wa sarafu ya pamoja ya E. Africa, kisha nikiona hizi mada zako kuhusu hawa matapeli, nacheka kwa nguvu.
Hili kabila limejaa watu wa hovyo sn, Jiwe, Paschal, Mnyeti, Makonda n.k sijui kwanini?
 
Mkuu Paskali,
Mseven anakenga SGR sio kwenda port bell ambapo kuna port toka Mwanza;
Anajenga reli kwenda Malaba ambako ni mpakani na Kenya;

On the other hand labda tujiulize Kenya SGR yao, unawapatia/inaleta nini kwa Kenya.

Ukisoma vyanzo mbalimbali ambavyo ndicho kinaendelea kwenye akili zetu; Kenya wana import zaidi bidhaa toka nje ya nchi kuliko wanavyo export.

Je na sisi SGR ikikamilika itakuwaje, tuta import zaidi au tutaitumia ku-export zaidi; kiuchumi ni faida (trade surplus) kuliko kuwa na hasara (trade deficit).
Nchi hizi zetu ikiwamo Congo, Burundi, Rwanda, Uganda, Malawi na Zambia zina import nini?
Dawa za mswaki
Miswaki
Mopers
Mifagio (soft brooms)
Toothpick
Penseli
Kalamu za kuandikia
Pedi za wanawake
Toilet paper
Cornflakes
Superghet
Nyama za makopo
Samaki za makopo
Vitunguu swaumu
Fanicha zilizotengenezwa kwa unga/vumbi la mbao;

Sasa hata lini tutajivunia kupitisha containers zenye vitu hivi na kupata tozo bandarini/kwenye SGR;

Kuna rocket sayansi kutengeneza chupi za kiume na handkerchief?

Hapa ndipo dhana ya kujenga viwanda inakuja na hata mjerumani alijenga reli ya kwanza yeye Ujerumani a-import raw materials kwa ajili ya viwanda vya Ujerumani na sio vinginevyo.

Reli ni kama mishipa ya damu, uzalishaji wa ndani una tija zaidi ku-cut down imports ya vitu basic kama nyama za kopo au samaki wa kopo?

Tusitumie sana model za World bank, baadhi kama sio nyingi zina tu-mislead.

Tutafute Japanese economic miracle
Malaysian economic miracle
Wote hawa waliona faida ya kukuza uchumi baada ya kuwa na surplus kwenye manufacturing kwa kutumia raw material toka ndani au nje ya kuonegeza export.

Tunapojenga SGR macho yetu yawe focused on prize; lazima tuwe na right model ya PPP; otherwise JPM ataondoka then tutabaki tunashangaa huyo anaekuja nae aje na vipaumbele vyake.
 
Ni jambo jema!

Lakini sidhani kama tuna mashindano na Kenya mkuu Pascal!
Sahihi. Lengo kubwa siyo kushindana ila ushindani hauepukiki. Mimi hupenda kuitazama hii 'vita' ya SGR kwa muktadha wa maendeleo ya viwanda kuliko biashara ya uchukuzi. Na hapa ndipo kwenye manufaa makubwa zaidi ya vile wanavyodhani watu. Mtandao wetu wa reli ya kisasa ukiwafikia majirani wengi kwa ufanisi mkubwa kuliko ule wa Kenya maana yake bidhaa zetu zitakuwa na competitive advantage dhidi ya zile za Kenya.

Tuwatazame hawa majirani kama masoko ya bidhaa zetu kuliko kama wateja wa huduma ya uchukuzi.
 
Kwani ccm wanazo au nyingi wamerithi toka mfumo wa chama kimoja? Ccm wana ofisi kwa sababu chama chao kiko madarakani, hivyo wanatumia nafasi hiyo kujipatia ofisi. Zunguka kwenye majengo ya ccm nchi nzima uone zilivyochoka, na hapo wako madarakani na walizirithi kisha uje ujisifie.
Kwa hiyo hiyo ndiyo sababu inayoifanya chadema isiwe na angalau kiwanja tu 🤔😅😅
 
mada nzuri , inahitajika time frame ya kukamilisha miradi kama hii yenye tija kubwa. siku SGR ikifika Mwanza na Kigoma ni siku ya kihistoria kwa bongo! penye nia pana njia! wakope kokote kiasi chochote reli iishe pesa itarudi tu! hata wajukuu wakilipa si tatizo! vitu viwili tu hupaisha uchumi wa nchi reli ya umeme na umeme wa bei rahisi na wa kutosha!
 
Aliandika PseudoDar186


Nimepitia takwimu kutoka the National Bureau of Statistics (NBS) na Tanzania Ports Authority (TPA) kuhusu mizigo / shehena yanayopitia bandari za Tanzania kwenda au kutoka nchi za jirani.

Kwa mwaka 2017/18, jumla ya tani 5.6 million zilipitia Tanzania (bandari ya Dar es Salaam pekee) kwenda au kutoka nchi za jirani, ikilinganishwa na tani 4.8 million mwaka 2016/17. Hili ni ongezeko la asilimia 17.1 na ni habari njema kabisa kwa TPA na nchi yetu kwa ujumla.

Ukiangalia mchanganuo wa shehena zinazoenda au kutoka nchi za jirani, asilima 61.1% ni za Zambia (36.6%) na J.D. Kongo (24.4%). Hii ni zaidi ya tani 3.4 million ambazo kwa asilimia kubwa zinawafikia jirani zetu kupitia barabara zetu hapa Tanzania. Ukipitia takwimu za 2017/18, TAZARA imefanikiwa kusafirisha mizigo ya tani 187,558 tu (3.4% ya 5.6 million) kwa njia ya reli.

Shehena za Rwanda ni asilimia 16.5% pekee (au tani 922,134) kwa mwaka wa 2017/18. Ukilinganisha na 2016/17, kuna upungufu wa 9.0% - kitu ambacho kinaashiria kuwa mizigo ya Rwanda inawezekana kuwa inapitia Kenya na Uganda.

Kwa kutumia akili za kawaida (common sense), kuna haja ya kuwekeza reli ya SGR kuunganisha Tanzania na Zambia na J.D. Kongo kwa sababu business case (volume of cargo) ni kubwa mno (kwa mara 3.7) kuliko Rwanda. Pia, tukiweza kuondoa hata tani 2 million barabani, TANROADS watapumua kidogo na matengenezo ya kila mara yanayotokana na uharibifu wa baraba zetu. Hii ni kwa mujibu ya data za NBS na TPA wenyewe.

Naomba mwenye taarifa kuhusu ya haya maamuzi ya kupeleka SGR Rwanda atujulishe
Tanzania hawapeleki SGR Rwanda, bali Rwanda wanaunganisha SGR yao mpakani mwa Tanzania na Rwanda ambapo wamepata mkopo kutoka AfDB.

AfDB wanafadhili miradi ya kimkakati nchini Tanzania. SGR yetu ni kuwezesha usafiri wa haraka na wa chini zaidi kwa abiria/bidhaa kutoka mikoa ya Mwanza, Kigoma, Geita, Tabora na mikoa yote ambayo inapita nk. Sio lazima upande ndege ili usafiri kwa haraka zaidi, SGR itachangia uchumi wa Tanzania kwa ujumla na kupunguza uharibifu wa barabara pamoja na ajali. In a long run its cheaper to have SGR.

Zambia tayari ipo reli ni swala la kuiimarisha na kuifanya ifanye kazi kwa faida zaidi. Tanzania tulichelewa sana inabidi tukimbie.
 
Wanabodi
Bandari ya Mombasa is very busy kwa sababu ya mizigo ya Uganda, Sudan ya Kusini na Tanzania. Hata kama tutaboresha efficiency ya Bandari ya Dar, mizigo yote ya Tanzania itapitia Dar, hivyo bandari yetu ikifanikiwa kwenye hili, mizigo yote ya DRC, Rwanda na Burundi itapita Dar na kuifanya Dar port kuwa the biggest, the busiest na the most profitable kuliko bandari ya Mombasa, lakini bado haiwezi kushibisha SGR ikajiendesha kwa faida, ndio maana wenye kuona mbali, wakaamua tujenge bandari ya kisasa Bagamoyo, na kuziboresha Bandari za Dar, Tanga na Mtwara na ndipo tutakuwa na mzigo wa kutosha kuishibisha SGR na kuiendesha kwa faida. Lakini wakatokea wenye uoni wa mpaka mwisho tuu wa pua zao, wakaambizana eti bandari ya Bagamoyo atafaidi Mkwere, waka abandon hii project.

Paskali
Wanabodi, Tanzania ni nchi yetu sote, viongozi wetu wana wajibu wa kutusikiliza sisi wananchi wao tunasema nini na kushauri nini, kama ushauri wetu ni mzuri, wauzingatie, kama ni ushauri wa hovyo, wau puuzie.

Ushauri huu ulitolewa miaka 3 iliyopita, ulipuuzwa!. Leo Spika kaenda China, akaonyeshwa na Wachina umuhimu wa bandari ya Bagamoyo, sasa ndio leo, Spika wetu anaongea Bungeni!.


Yaani kuna vitu wakishauri kina yakhe, vina puuziwa, lakini akishauri mchina, ndio Spika anaelewa!.
P
 
Wanadodi,

Leo nimepata fursa ya kuendelea na zile makala zangu za kwa Maslahi ya Taifa, leo nikianzia kuibuka kwa fursa mpya kwenye reli ya SGR ya Tanzania, karibu.

Wakati Tanzania tukiendelea na ujenzi wa reli yetu ya SGR, shughuli nzito kwenye SGR sio ujenzi, bali ni kuiendesha kwa faida. Ili SGR iendeshwe kwa faida, ni lazima iwe na kitu kinachoitwa linkages, yaani muunganisho kati ya nchi moja na nyingine, ili hiyo SGR ipate mzigo wa kushiba na ku operate kwa faida.

Kwa nchi za Afrika Mashariki, Kenya ikitumia mtindo wa "ujanja kuwahi", ikawa ndio nchi ya kwanza kuchangamkia fursa hivyo ikajenga SGR ya Mombasa-Nairobi-Naivasha-Malaba, ili mzigo wa Uganda na Rwanda upitie bandari ya Mombasa, na Uganda ingejenga SGR kupokea mzigo wake na wa Rwanda na kuufikisha Kigali. Hivyo the linkaje ya mzigo wa Uganda na Rwanda, ndio roho ya SGR ya Kenya, Mchina kupitia benki yake ya EXIM akakubali kugharimia kila kitu.

Kumbe "ujanja nsi kuwahi, ni kupata", JPM baada tuu ya kuchaguliwa,ziara yake ya kwanza nje ya nchi, ni kutembelea Rwanda, wakakubaliana SGR ya Tanzania itaungana na ya Rwanda. Hivyo kitendo tuu cha kukubaliana SGR ya Tanzania itajiunga na Rwanda, ile linkages ya SGR ya Uganda kwenda Rwanda, ikakatika, hivyo SGR ya Kenya kuunga Uganda haitakuwa na faida, hali hiyo ikikapelekea mfadhili kujitoa kuendeleza SGR ya Kenya sasa itaishia Naivasha, na hakuna funding tena ku fund SGR ya Uganda!.

Baada ya mchina kugoma kugharimia SGR ya Uganda, MU7, nae kaamua kumfuatilisha JPM kwa kuamua kujenga SGR ya Uganda hata kama Kenya anasuasua. Uamuzi huu wa Uganda kujenga SGR yake bila kuitegemea Kenya ni fursa nyingine kubwa kwa SGR ya Tanzania na Bandari ya Dar es Salaam kubeba mzigo wote wa Uganda.

Ili sisi Tanzania kuweza kuichangamkia fursa hii mpya, sasa hapa ndio "ujanja kuwahi", kwa kujenga SGR ya Mwanza fasta, ili mzigo wa Uganda ushuke Dar, ukimbizwe Mwanza, uvushwe ziwa Victoria hadi Uganda. Hili likifanyika, sio tuu, Bandari ya Dar itabeba cargo ya Uganda tuu, bali cargo kutoka South Sudan na North Eastern DR Congo itapitia bandari ya Dar es Salaam kupelekwa Mwanza. Changamoto pekee, in umbali wa route hii, kama italipa, na changamoto ya hatari zaidi, ni bada ya MU7 kuamua kujenga SGR, Kenya anaweza na yeye kuamua kukijenga kipande cha Naivasha-Malaba.

Background.
Taarifa za Uganda kujenga nmezisoma hapa Uganda plans to go it alone and build 2,700km-long standard gauge railway.

SGR ndio kipimo cha the economic super power of EAC, hivyo ni vita kubwa.




My Take
Kama tumeweza kuwapiga Tanchi kwenye SGR ya kuunganisha na Rwanda, kisha tukawapiga Tanchi kwenye bomba la mafuta la Uganga, Tanzania tukifanikiwa kuifikisha SGR yetu, Mwanza, hadi Kigoma, na pia tukajenga SGR to Tunduma, Tanzania ndio itakuwa the super power of EAC Region, na kama tukiifanya Dar Port kuwa a free port kwa baadhi ya bidhaa, with The AfCFTA in place!, Tanzania will fly!, no one will catch us!.

Nawatakia Jumapili Njema.

Paskali
Kiukweli kabisa, huyu mtu aliyeifanya kazi hii, akitokea kuja kuchaguliwa kuwa Mwakilishi wa Tanzania ndani ya EALA, you can just imagine atafanya nini!. Kama amaweza kufanya yote haya akiwa just a journalist, akitokea akawa mbumbe wa kitu kama EALA, si Tanzania itapaa?. Au mnasemaje wanabodi?.
P
 
Kwenye mambo ya SGR, Watanzania tunapaswa kuambiwa ukweli wa kila kitu!, serikali yetu lazima iwe very transparent see through kwenye kila kitu including mikataba na financial maters kufuatia kuwahi kupigwa huko nyuma kwenye rada, kwenye ndege, kwenye meli na sasa kwenye reli
Maswali haya yajibiwe kikamilifu
Wanabodi,
1. Taarifa ya TRC inasema vichwa vipya na mabehewa mapya, lakini ukweli ni kuwa ni vichwa mitumba na mabehewa mitumba kama ya mwaka '1947'!.

2. Ukiyaangalia kwa ndani, haya mabehewa ni kama yana madirisha only one sided!, hiki ni kuashiria originally haya ni mabehewa ya underground trains na sio ya terestrial train!. Sisi SGR yetu ni terestrial, moja ya faida kubwa kusafiri na treni ni pamoja na kuenjoy kitu kinachoitwa scenery enjoymement, madirisha makubwa both sides abiria kuona nje, hizi behewa za madirisha ya upande mmoja, hebu mfikirie abiria wa Kigoma, seat ya upande usio na dirisha!, kuna tofauti gani na chumba cha jela?.

3. Mkataba ni wa ukarabati na kutiwa nakshi nakshi kwa vichwa na mabehewa mitumba!, na sio kuundwa kwa vichwa na mabehewa mapya!, kwanini Watanzania hatuelezwi ukweli?.
Hakuna ubaya nchi kununua vichwa mitumba na mabehewa mitumba, kitu muhimu ni Watanzania tuelezwe ukweli!.

4. Je, hivyo vichwa viliundwa lini, wapi?, jee originally vimetumika wapi na kwa muda gani kabla sisi hatujauziwa?

5. Mitumba hiyo imenunuliwa kwa bei gani, ikakarabatiwa kwa bei gani, na kusafirishwa kwa gharama gani?

6. Tufanyiwe comparative analysis, kama tungenunua vichwa vipya na mabehewa mapya, tungetumia gharama kiasi gani, compared na kununua vichwa mitumba na mabehewa mitumba, ili tujue tumeokoa fedha kiasi gani kwa kununua mitumba hiyo?

7. Japo gharama za kununua vitu vipya ni juu ila maintance cost ni ndogo, unaweza kununua mitumba kwa bei poa kumbe ni mitumba choka mbaya, hivyo maintenance cost ikawa juu.

8. Sii wengi wanajua kazi ya CAG sio kutoa tuu zile ripoti za hesabu za serikali, CAG ni Mdhibiti na Mkaguzi, ufhibiti unafanywa kabla ya manunuzi, je, kulifanyika tathmini yoyote rail worthness report ya vichwa na mabehewa hayo mitumba kabla hayajanunuliwa?. Then CAG atufanyie value for money audit, msikute mitumba hiyo tumepewa bure, huku watu wakipiga kubwa tunauziwa kwa bei ya mapya!.

9. Ukiingia mkataba wa manunuzi, kwa matengenezo, mzigo ukanunuliwa, delivery ndio ikachelewa, huwezi kuvunja mkataba huo ukabaki salama, hivyo kesi ikifunguliwa, Tanzania tunashindwa hata kabla kesi haijaanza!.

10. Tulivunja mkataba wa Dowans, tulishitakiwa, tukashindwa, tukadaiwa tukasema hatulipi!, watu wakajiapisha "over my dead body", hatulipi!.
ukweli ni kuwa tumelipa kwa siri, Watanzania hatukuambiwa!.

11. Tulipo vunja mkataba wa Dowans, Zitto akashauri tuitaifishe mitambo ile, Wabunge wetu wakagoma kuwa Tanzania hatununui mitambo chakavu, mitambo mitumba!

12 Mitambo ile ikanunuliwa na Simbion, tukaingia nao mkataba ule ule wa Dowans, watu wale wale walio ikataa dowams, ndio hao hao danced to the tune na Hilary Clinton kuzindua Simbion kwa mkataba ule ule tuliovunja!, kwa gharama zile zile!, na capacity charge ile ile!, na tukawalipa!.

13. JPM alipoingia tukavunja mkataba wa Simbion, tukashitakiwa, tukashindwa, JPM akagoma kulipa!, ila baada tuu ya JPM kuitwa kule alipoitwa huku nyuma, sisi sio tuu tumelipa!, bali pia tumeinunua ile mitambo ya Simbion kwa bei ya ajabu!, sasa mitambo ile tuliosema ni chakavu, mtumba, na serikali yetu hatununui, mivitu chakavu, sasa ndio tumeinunua!, sasa mitambo ile ya Simbion ni mitambo yetu, ni mali yetu! na malipo yote yaliisha fanyika chap chap fasta fasta!, bila bajeti yake kuombwa popote!, bila Bunge letu kuijadili, bila CAG kuidhinisha malipo hayo!, na haya yote yamefanyika bila iWatanzania kuambiwa!.

14. NB. Unapohoji vitu kama hivi, huchelewi kunyooshewa vidole vya kukosa uzalendo au kutokuwa na nia njema!, no!, wala sijasema kilichofanyika ni wrong!, no!, ninachosema hapa ni sisi
Watanzania wa sasa ni waelewa, tuwe tuu tunaambiwa ukweli,

15. Kwa vile mambo kama haya kwenye manunuzi makubwa yaliwahi kutokea kule nyuma kwenye ununuzi wa Rada mtumba toka BAE, watu wakaweka cha juu kikubwa tuu, tukalipa fasta!, Mama Mzalendo wa kizungu, Linda Chalkel akabaini, akatupigania tukarudishiwa chenji ya Rada!.

16. Ununuzi wa ndege ya rais Gulf Steeam bei ikapaishwa zaidibya mara tatu!, John Cheyo akaonyesha bei ya kiwandaji watu wakatia pamba masikioni tukalipa fasta!.

17. Kuna vifaa vya kijeshi chakavu tumeuziwa hapa!, tangu vimenunuliwa havijawahi kutumika mpaka leo!. Hivi naomba nisivizungumzie wala msiniulizie!, maana hata sisi waandishi wa habari haturuhusiwi kuzungumzia mambo ya jeshi na usalama wa taifa, ila fedha zilizotumika sio fedha za jeshi au za usalama wa taifa, ni fedha za Watanzania, kuzungumzia vifaa vya jeshi, tuliuziwa nini mitumba ni vifaa vya nini na viko wapi, hii ni no!, hatuzungumzi, lakini tulilipia fedha kiasi gani, ni haki ya Watanzania kujua!.

18. Tukanunua Boti mtumba ya MV Bagamoyo, ikafanya safari moja tuu mahali pa 30 min, ilitumia masaa 3!, Hii pia sasa ni kufaa cha kijeshi!, isizungumzwe!, ila fedha zake ni fedha za Watanzania!.

19. Hivyo kweli hivi vichwa na mabehewa haya, ni bora tukaelezana ukweli tangia mwanzo!.

20. Namalizia kwa msisitizo, hakuna ubaya kutumia vitu used!, tena vingine ni vizuri, imara, bora, madhubuti kuliko hata vipya!, na Watanzania walio wengi, kutokana na low purchasing power due to umasikini uliotopea, wengi wetu affordability yetu ni mitumba kuanzia magar
i, nguo hadi mitambo, hivyo tumezoea, tunachohitaji ni kuambiwa ukweli tuu!,
tutaelewa tuu kuliko...

Wasalaam.
Paskali.
Maswali haya yanahitaji majibu ya kina na sio blah blah!.
Kama mtu kuuliza maswali kama haya, kutapelekea kuhojiwa uzalendo wake, mimi naomba kutumia kinga ya kihabari na kanuni ya kwanza ya mwandishi wa habari no seek the truth, and write nothing but the truth!, kuna kitu ninadhamiria sio tuu kuandika bali kukitengenezea a video documentary ya safari ya SGR ya Tanzania, tulipotoka, tulipo na tunapokwenda, ili huko mbele, likija kujitokeza liji white elephant fulani hivi ambalo sijui kama ni mimi tuu naliona, angalau dhamira yangu isinisute, niliona kabla, nikasema kabla, nikaandaa documentary kabla, nikaonyesha kabla, ili angalau jamii ya Watanzania wajue kuna watu waliona kabla na walisema kabla!.

Na labda kuwasaidia Watanzania wenzangu wasio jua, kwenye ile kashfa ya rada, BAE walikiri kutoa mlungula wa kickbacks, lakini sheria yao inawaruhusu non disclosure ya waliowapa mlungula, ilo usipoteze wateja wapya wapenda mlungula, kibiashara mlungula wa 10% ni halali!, ila ikijulikana kuwa umetoa mlungula, unapaswa ama uwataje uliowapa mlungungula, wakamuliwe wautapike huo mlingula, ama uwahifadhi usiwataje, na badala yake utozwe faini kwa uliowapa mlungula, na kuurejesha ule mlungula, na hicho ndicho kilichofanywa na BAE, kuwahifadhi waliowapa mlungula, na badala yake ikakubali kulipa faini na ndipo tukarejeshewa ile chenji ya rada.

Hii maana yake, kuna viongozi wetu walikula mlungula BAE akawakingia kifua kuwahifadhi kwa kulipia faini na ule mlungula ukarudishwa nchini kama chenji ya rada, endapo BAE wasinge wakingia kifua kuwahifadhi na kuwalinda, amini usiamini, hayo majina ya waliopokea mlungula na kuzihifadhi fedha zao kule Credit Suisse, yangetoka, Watanzania msinge amini macho na masikio yenu!.

Kashfa hii iliobuka kwasababu tuu kulitokea lijinga limoja, mgao wake yeye ukauhifadhi visiwa fulani ambavyo viko chini ya milki ya Uingereza, ndipo Muingereza akabaini, lakini kama wote wange bank Swiss banks, kule fedha zao ni very secure, hata bank manager, hajui majina ya customers na clients ni secret codes tuu zinatembea, hivyo wala kashfa ya rada isinge ibuka!.

Hivyo watu tunaoulizia kuhusu haya mabenewa, naomba mtuelewe ni wazalendo wa kweli wa nchi hii!.

Paskali
 
Kwenye mambo ya SGR, Watanzania tunapaswa kuambiwa ukweli wa kila kitu!, serikali yetu lazima iwe very transparent see through kwenye kila kitu including mikataba na financial maters kufuatia kuwahi kupigwa huko nyuma kwenye rada, kwenye ndege, kwenye meli na sasa kwenye reli
Maswali haya yajibiwe kikamilifu

Maswali haya yanahitaji majibu ya kina na sio blah blah!.
Kama mtu kuuliza maswali kama haya, kutapelekea kuhojiwa uzalendo wake, mimi naomba kutumia kinga ya kihabari na kanuni ya kwanza ya mwandishi wa habari no seek the truth, and write nothing but the truth!, kuna kitu ninadhamiria sio tuu kuandika bali kukitengenezea a video documentary ya safari ya SGR ya Tanzania, tulipotoka, tulipo na tunapokwenda, ili huko mbele, likija kujitokeza liji white elephant fulani hivi ambalo sijui kama ni mimi tuu naliona, angalau dhamira yangu isinisute, niliona kabla, nikasema kabla, nikaandaa documentary kabla, nikaonyesha kabla, ili angalau jamii ya Watanzania wajue kuna watu waliona kabla na walisema kabla!.

Na labda kuwasaidia Watanzania wenzangu wasio jua, kwenye ile kashfa ya rada, BAE walikiri kutoa mlungula wa kickbacks, lakini sheria yao inawaruhusu non disclosure ya waliowapa mlungula, ilo usipoteze wateja wapya wapenda mlungula, kibiashara mlungula wa 10% ni halali!, ila ikijulikana kuwa umetoa mlungula, unapaswa ama uwataje uliowapa mlungungula, wakamuliwe wautapike huo mlingula, ama uwahifadhi usiwataje, na badala yake utozwe faini kwa uliowapa mlungula, na kuurejesha ule mlungula, na hicho ndicho kilichofanywa na BAE, kuwahifadhi waliowapa mlungula, na badala yake ikakubali kulipa faini na ndipo tukarejeshewa ile chenji ya rada.

Hii maana yake, kuna viongozi wetu walikula mlungula BAE akawakingia kifua kuwahifadhi kwa kulipia faini na ule mlungula ukarudishwa nchini kama chenji ya rada, endapo BAE wasinge wakingia kifua kuwahifadhi na kuwalinda, amini usiamini, hayo majina ya waliopokea mlungula na kuzihifadhi fedha zao kule Credit Suisse, yangetoka, Watanzania msinge amini macho na masikio yenu!.

Kashfa hii iliobuka kwasababu tuu kulitokea lijinga limoja, mgao wake yeye ukauhifadhi visiwa fulani ambavyo viko chini ya milki ya Uingereza, ndipo Muingereza akabaini, lakini kama wote wange bank Swiss banks, kule fedha zao ni very secure, hata bank manager, hajui majina ya customers na clients ni secret codes tuu zinatembea, hivyo wala kashfa ya rada isinge ibuka!.

Hivyo watu tunaoulizia kuhusu haya mabenewa, naomba mtuelewe ni wazalendo wa kweli wa nchi hii!.

Paskali
Mambo mengi Magufuli alifanya lakini alitanguliza masilahi yake kwanza. Imagine ule mkataba wa SGR ya Mwanza - Isaka kupitia Chato aliosaini Desemba 2020 ulikuwa na maana gani?

Kumbuka kipande cha Makutopora- Tabora kilikuwa bado by then.

There is no way SGR ikawa na tija. Itbakia white elephant forever
 
27 Reactions
Reply
Back
Top Bottom