The SGR War: Wakati Kenya wakisuasua, Uganda wameamua kujenga SGR. Hii ni fursa kwa SGR ya Tanzania. Is it viable? Tuichangamkie?

nadhani wasiwasi wa nchi zote za magharibi ni kwamba Tanzania ikiweza kuwa vizuri kwenye uchumi itapelekea nchi nyingi sana za ukanda wetu kuwa huru kiuchumi na hii haitokuwa vizuri sana kwao maana kuna vikwazo lazima tutakuwa tuna vipunguza kutokana na uchumi wetu kuimarika na nchi za jirani

Na hili litaweza kuwafanya wao waingize propaganda kwasababu sidhani kama Tanzania tulishawahi fuata na kuwa kwenye nyayo zao muda mrefu ikipelekea hii miradi kumalizika na kilimo kikawa vizuri jumlisha na umeme imported goods zitapungua na wazee huku hawatokubali maana economic yao ina tegemea sana bara la Africa hasa sub saharan countries

Nadhani kwa hili tuombe MUNGU tufanikiwe maana adui anaweza kutokea popote na huenda hata akawa rafiki wa karibu

National interests kwa Africa ni changamoto na ni vita kubwa sana mzungu kukubali si rahisi na zijengwe kutokana na matumizi ya sisi wa Africa isije ikawa ndio njia za ku lubricate exports ya raw materials kwenda mataifa ya magharibi tutakuwa hatujafanya kitu

ikiwezekana viwanda navyo tuangalie viwepo hata processing na manufacturing industries

We Africans need to produce things we consume and consume things we produce without awareness nothing gonna change,it's a war and in these issues Africa needs to become one without any country being a traitor pasipo hivyo kuna watu wanaweza kuja kuwekwa kwenye kikaangoo kama Gaddafi na wengine being economically independent inawapa wazungu hasira sana sanaaa

There's is no a place that loves you the most like your country Africa is home we need to rebuild it again!
Mkuu Rijali jandoni, thanks for this, huu ndio uzalendo!.
P
 
Mkuu Mmawia, hakuna mtu anayejua kila kitu, kitu kama hujui sio lazima kuchangia!. SGR haiwezi kujiendesha kwa faida hata ikipata abiria 100%. The plan ya SGR ya Mombasa ni kwenda mpaka Malaba, hivyo kubeba mzigo wa Uganda, Rwanda, DRC na Southern Sudan. SGR ya Uganda ili ilete faida ni kupokea mzigo wa Rwanda, Burundi, DRC na Southern Sudan. Kitendo cha SGR ya Rwanda kuunganisha na ya Tanzania, kukaifanya SGR ya Kenya a white elephant, kwasababu bila mzigo wa Rwanda, SGR ya Uganda hailipi, bila mzigo wa Uganda, SGR ya Kenya hailipi, hivyo sasa SGR ya Kenya itaishia Naivasha and will never pay!.
Jielimishe zaidi hapa
P
Sasa hiyo comparison uliyo ionyesha inatoka wapi juu ya Kenya? Kwani Tanzania tuna mashindano ya kiuchumi na Kenya?
 
Mkuu Kishina cha Mshahara, naunga mkono hoja, naunga mkono hoja, nchi inaendeshwa kwa mujibu wa katiba, sheria, taratibu na kanuni, na sio kwa utashi tuu wa kiongozi aliyepo madarakani. Mfano, haiwezekani nchi itumie bilions kuanzisha mchakato wa katiba, na baada kula ngombe mzima, na kubakisha mkia, kiongozi anafuata, ana abandon kila kitu kwa hoja sio kipaumbele changu!.

Kufuatia uzoefu huu, JPM ndie rais wa mwisho Tanzania, kuwa rais kwa kubeeb tuu, kuanzia sasa, tutahakikisha anayempokea Magufuli, anasainishwa "a continuity clause", kuyaendeleza yote ya mtangulizi wake, na anayempokea ni yule atakayeyaendeleza mazuri yote ya Magufuli, na tukijiona tuna mashaka, then, Magufuli alazimishwe kuendelea, hadi akamilishe miradi yake yote ya kimkakati, hata kama it will take some ten extra years, let it be!.
P
Akisaini na asipotekeleza tutamfanya nini wakati Raisi wa nchi hii hashitakiwa na juzi tu wamepitisha sheria ya kuwalinda zaidi?
 
Hizi concept hazipo duniani zipo Afrika peke yake kuhusu ujenzi was SGR, sio Europe, America and Asia nchi zimejenga reli ya SGR eti kuhudumia mizigo ya nchi jirani ndio ziwe economically viable! Paskali utambue kuwa SGR inatakiwa iwe socio-economically viable kwa nchi yenyewe kwanza kabla ya hizo siasa za kubeba mizigo ya nchi jirani. Ni bahati mbaya uendeshji was uchumi wet sio was kimkakati, laminitis ungekuwa hivyo tulitakiwa kuwa na manufacturing/production clusters ambazo tulitakiwa kuzinganisha na Sgr kabla ya kukimbilia kwa majirani wakati uchumi wetu haujaunganishwa. Na huu ni mwenndelezo wa colonial economic concept!
Paskali, a project of SGR type that is socio-economic inaanza kurudisha mtaji/ uwekezaji wake kuanzia miaka 50 sio huo uongo mnaojazwamchina
Wachumi wenzangu tungejitahidi kufanya synthesis analysis ya mradi huu kabla ya kuandika hasa figures. Matokeo yake ama tutakuwa wapotoshaji au hatuna uhakika na tunacho chambua.

Deni lolote muda unategemea na utakavyo structures loan repayments. Project inaweza ukaitafakari haraka haraka unaweza usipate ecomomic viability yake, lakini social viability ya huu mradi iko wazi kabisa.
Complex Consequential economic benefit analysis lazima uifanye ili upate usahihi wa economic viability. The Government is enabler, Haifanyi biashara.
 
Sasa hiyo comparison uliyo ionyesha inatoka wapi juu ya Kenya? Kwani Tanzania tuna mashindano ya kiuchumi na Kenya?
Huwezi kufanya comparison kwa kitu ambacho hakipo!, hivyo sijafanya comparison yoyote, nilichofanya ni kutoa angalizo la projected trends za SGR ya yetu, kwa kuitumia SGR ya Kenya. Japo hatuna mashindano ya wazi, like like entities zinashindana, Bandari ya Dar na Bandari ya Mombasa zinashindana kugombania wateja. Mzigo unaupita bandari ya Mombasa, ndio unailisha SGR ya Kenya, Kama bandari ya Mombasa, inapokea mzigo mkubwa kuliko bandari ya Dar, lakini SGR yao haishibi, sisi sasa tunapojenga SGR yetu, tusisubiri ije kushinda njaa, pia tujipange, tutaishibishaje SGR yetu?.
P
 
My Take
Kama tumeweza kuwapiga Tanchi kwenye SGR ya kuunganisha na Rwanda, kisha tukawapiga Tanchi kwenye bomba la mafuta la Uganga, Tanzania tukifanikiwa kuifikisha SGR yetu, Mwanza, hadi Kigoma, na pia tukajenga SGR to Tunduma, Tanzania ndio itakuwa the super power of EAC Region, na kama tukiifanya Dar Port kuwa a free port kwa baadhi ya bidhaa, with The AfCFTA in place!, Tanzania will fly!, no one will catch us!.

Nawatakia Jumapili Njema.

Paskali
Bahati nzuri niko kwenye hii industry na kuna mambo mawili au matatu nayaelewa...kwa hapa nataka kusema Tanzania imelala usingizi wa pono kwenye kupigania shehena kubwa zaidi kupita Dar port, miundombinu ni mibovu mno na badala ya Magufuli kuhangaika na 10% zake kwenye biashara Kichaa ya ndege, ni heri angewekeza nguvu kuikamilisha SGR..

Lkn Sasa tumbo la mwanadamu halishibi, hadi Mhutu aje ashibishwe na 10% za dili za ndege Kenya watakuwa wameikamilisha SGR yao kuingia Uganda, Namibia Watakuwa wameifikisha SGR yao Zambia, na Angola Watakuwa wameifikisha SGR yao Lubumbashi.

Then Tanzania/dar port itaendelea tu kuwa ki-bandari kidogo kinachohudumiwa na bandari ya Mombasa
 
Wanadodi,

Leo nimepata fursa ya kuendelea na zile makala zangu za kwa Maslahi ya Taifa, leo nikianzia kuibuka kwa fursa mpya kwenye reli ya SGR ya Tanzania, karibu.

Wakati Tanzania tukiendelea na ujenzi wa reli yetu ya SGR, shughuli nzito kwenye SGR sio ujenzi, bali ni kuiendesha kwa faida. Ili SGR iendeshwe kwa faida, ni lazima iwe na kitu kinachoitwa linkages, yaani muunganisho kati ya nchi moja na nyingine, ili hiyo SGR ipate mzigo wa kushiba na ku operate kwa faida.

Kwa nchi za Afrika Mashariki, Kenya ikitumia mtindo wa "ujanja kuwahi", ikawa ndio nchi ya kwanza kuchangamkia fursa hivyo ikajenga SGR ya Mombasa-Nairobi-Naivasha-Malaba, ili mzigo wa Uganda na Rwanda upitie bandari ya Mombasa, na Uganda ingejenga SGR kupokea mzigo wake na wa Rwanda na kuufikisha Kigali. Hivyo the linkaje ya mzigo wa Uganda na Rwanda, ndio roho ya SGR ya Kenya, Mchina kupitia benki yake ya EXIM akakubali kugharimia kila kitu.

Kumbe "ujanja nsi kuwahi, ni kupata", JPM baada tuu ya kuchaguliwa,ziara yake ya kwanza nje ya nchi, ni kutembelea Rwanda, wakakubaliana SGR ya Tanzania itaungana na ya Rwanda. Hivyo kitendo tuu cha kukubaliana SGR ya Tanzania itajiunga na Rwanda, ile linkages ya SGR ya Uganda kwenda Rwanda, ikakatika, hivyo SGR ya Kenya kuunga Uganda haitakuwa na faida, hali hiyo ikikapelekea mfadhili kujitoa kuendeleza SGR ya Kenya sasa itaishia Naivasha, na hakuna funding tena ku fund SGR ya Uganda!.

Baada ya mchina kugoma kugharimia SGR ya Uganda, MU7, nae kaamua kumfuatilisha JPM kwa kuamua kujenga SGR ya Uganda hata kama Kenya anasuasua. Uamuzi huu wa Uganda kujenga SGR yake bila kuitegemea Kenya ni fursa nyingine kubwa kwa SGR ya Tanzania na Bandari ya Dar es Salaam kubeba mzigo wote wa Uganda.

Ili sisi Tanzania kuweza kuichangamkia fursa hii mpya, sasa hapa ndio "ujanja kuwahi", kwa kujenga SGR ya Mwanza fasta, ili mzigo wa Uganda ushuke Dar, ukimbizwe Mwanza, uvushwe ziwa Victoria hadi Uganda. Hili likifanyika, sio tuu, Bandari ya Dar itabeba cargo ya Uganda tuu, bali cargo kutoka South Sudan na North Eastern DR Congo itapitia bandari ya Dar es Salaam kupelekwa Mwanza. Changamoto pekee, in umbali wa route hii, kama italipa, na changamoto ya hatari zaidi, ni bada ya MU7 kuamua kujenga SGR, Kenya anaweza na yeye kuamua kukijenga kipande cha Naivasha-Malaba.

Background.
Taarifa za Uganda kujenga nmezisoma hapa Uganda plans to go it alone and build 2,700km-long standard gauge railway.

SGR ndio kipimo cha the economic super power of EAC, hivyo ni vita kubwa.




My Take
Kama tumeweza kuwapiga Tanchi kwenye SGR ya kuunganisha na Rwanda, kisha tukawapiga Tanchi kwenye bomba la mafuta la Uganga, Tanzania tukifanikiwa kuifikisha SGR yetu, Mwanza, hadi Kigoma, na pia tukajenga SGR to Tunduma, Tanzania ndio itakuwa the super power of EAC Region, na kama tukiifanya Dar Port kuwa a free port kwa baadhi ya bidhaa, with The AfCFTA in place!, Tanzania will fly!, no one will catch us!.

Nawatakia Jumapili Njema.

Paskali
Brother Mayala Leo umetema madini ya maana kwenye Transport Economy, ubarikiwe sana kwa uwezo wa kuchambua masuala yenye tija na mshikamano kwa Nchi yetu Tanzania
 
Wanadodi,

Leo nimepata fursa ya kuendelea na zile makala zangu za kwa Maslahi ya Taifa, leo nikianzia kuibuka kwa fursa mpya kwenye reli ya SGR ya Tanzania, karibu.

Wakati Tanzania tukiendelea na ujenzi wa reli yetu ya SGR, shughuli nzito kwenye SGR sio ujenzi, bali ni kuiendesha kwa faida. Ili SGR iendeshwe kwa faida, ni lazima iwe na kitu kinachoitwa linkages, yaani muunganisho kati ya nchi moja na nyingine, ili hiyo SGR ipate mzigo wa kushiba na ku operate kwa faida.

Kwa nchi za Afrika Mashariki, Kenya ikitumia mtindo wa "ujanja kuwahi", ikawa ndio nchi ya kwanza kuchangamkia fursa hivyo ikajenga SGR ya Mombasa-Nairobi-Naivasha-Malaba, ili mzigo wa Uganda na Rwanda upitie bandari ya Mombasa, na Uganda ingejenga SGR kupokea mzigo wake na wa Rwanda na kuufikisha Kigali. Hivyo the linkaje ya mzigo wa Uganda na Rwanda, ndio roho ya SGR ya Kenya, Mchina kupitia benki yake ya EXIM akakubali kugharimia kila kitu.

Kumbe "ujanja nsi kuwahi, ni kupata", JPM baada tuu ya kuchaguliwa,ziara yake ya kwanza nje ya nchi, ni kutembelea Rwanda, wakakubaliana SGR ya Tanzania itaungana na ya Rwanda. Hivyo kitendo tuu cha kukubaliana SGR ya Tanzania itajiunga na Rwanda, ile linkages ya SGR ya Uganda kwenda Rwanda, ikakatika, hivyo SGR ya Kenya kuunga Uganda haitakuwa na faida, hali hiyo ikikapelekea mfadhili kujitoa kuendeleza SGR ya Kenya sasa itaishia Naivasha, na hakuna funding tena ku fund SGR ya Uganda!.

Baada ya mchina kugoma kugharimia SGR ya Uganda, MU7, nae kaamua kumfuatilisha JPM kwa kuamua kujenga SGR ya Uganda hata kama Kenya anasuasua. Uamuzi huu wa Uganda kujenga SGR yake bila kuitegemea Kenya ni fursa nyingine kubwa kwa SGR ya Tanzania na Bandari ya Dar es Salaam kubeba mzigo wote wa Uganda.

Ili sisi Tanzania kuweza kuichangamkia fursa hii mpya, sasa hapa ndio "ujanja kuwahi", kwa kujenga SGR ya Mwanza fasta, ili mzigo wa Uganda ushuke Dar, ukimbizwe Mwanza, uvushwe ziwa Victoria hadi Uganda. Hili likifanyika, sio tuu, Bandari ya Dar itabeba cargo ya Uganda tuu, bali cargo kutoka South Sudan na North Eastern DR Congo itapitia bandari ya Dar es Salaam kupelekwa Mwanza. Changamoto pekee, in umbali wa route hii, kama italipa, na changamoto ya hatari zaidi, ni bada ya MU7 kuamua kujenga SGR, Kenya anaweza na yeye kuamua kukijenga kipande cha Naivasha-Malaba.

Background.
Taarifa za Uganda kujenga nmezisoma hapa Uganda plans to go it alone and build 2,700km-long standard gauge railway.

SGR ndio kipimo cha the economic super power of EAC, hivyo ni vita kubwa.




My Take
Kama tumeweza kuwapiga Tanchi kwenye SGR ya kuunganisha na Rwanda, kisha tukawapiga Tanchi kwenye bomba la mafuta la Uganga, Tanzania tukifanikiwa kuifikisha SGR yetu, Mwanza, hadi Kigoma, na pia tukajenga SGR to Tunduma, Tanzania ndio itakuwa the super power of EAC Region, na kama tukiifanya Dar Port kuwa a free port kwa baadhi ya bidhaa, with The AfCFTA in place!, Tanzania will fly!, no one will catch us!.

Nawatakia Jumapili Njema.

Paskali

Nime kuja kugundua kitu kuna mahusiano makubwa sana kati ya CCM na ujinga, simtukani mtu ila huo ndio ukweli tujitahidi sana kuwapa ndugu zetu somo Folded hands. madhara ya kukubali kumtegemea mtu kua kinga yako ndio hayo nilazima uwe kama zombie kila kitu unashabikia tuwasaidie wenzetu.
 
Huwezi kufanya comparison kwa kitu ambacho hakipo!, hivyo sijafanya comparison yoyote, nilichofanya ni kutoa angalizo la projected trends za SGR ya yetu, kwa kuitumia SGR ya Kenya. Japo hatuna mashindano ya wazi, like like entities zinashindana, Bandari ya Dar na Bandari ya Mombasa zinashindana kugombania wateja. Mzigo unaupita bandari ya Mombasa, ndio unailisha SGR ya Kenya, Kama bandari ya Mombasa, inapokea mzigo mkubwa kuliko bandari ya Dar, lakini SGR yao haishibi, sisi sasa tunapojenga SGR yetu, tusisubiri ije kushinda njaa, pia tujipange, tutaishibishaje SGR yetu?.
P
Wakati bandari yenu inapiga miayoo
 
Tanz is a sleeping giant km gesi tukiitumia vizuri kiuchumi tutakuwa economic power house shida hatujaukamilisha vizuri mradi huu. Tunayo mengi ya kujikwamua tayari tuko uchumi wa kati sawa na Kenya.
 
Nime kuja kugundua kitu kuna mahusiano makubwa sana kati ya CCM na ujinga, simtukani mtu ila huo ndio ukweli tujitahidi sana kuwapa ndugu zetu somo Folded hands. madhara ya kukubali kumtegemea mtu kua kinga yako ndio hayo nilazima uwe kama zombie kila kitu unashabikia tuwasaidie wenzetu.
Hongera sana mkuu kwa somo zuri sana
 
Tanz is a sleeping giant km gesi tukiitumia vizuri kiuchumi tutakuwa economic power house shida hatujaukamilisha vizuri mradi huu. Tunayo mengi ya kujikwamua tayari tuko uchumi wa kati sawa na Kenya.
Unaizungumzia ges ipi hiyo?
 
Mkuu Kishina cha Mshahara, Salary Slip , naunga mkono hoja, naunga mkono hoja, nchi inaendeshwa kwa mujibu wa katiba, sheria, taratibu na kanuni, na sio kwa utashi tuu wa kiongozi aliyepo madarakani. Mfano, haiwezekani nchi itumie bilions kuanzisha mchakato wa katiba, na baada kula ngombe mzima, na kubakisha mkia, kiongozi anafuata, ana abandon kila kitu kwa hoja sio kipaumbele changu!.

Kufuatia uzoefu huu, JPM ndie rais wa mwisho Tanzania, kuwa rais kwa kubeeb tuu, kuanzia sasa, tutahakikisha anayempokea Magufuli, anasainishwa "a continuity clause", kuyaendeleza yote ya mtangulizi wake, na anayempokea ni yule atakayeyaendeleza mazuri yote ya Magufuli, na tukijiona tuna mashaka, then, Magufuli alazimishwe kuendelea, hadi akamilishe miradi yake yote ya kimkakati, hata kama it will take some ten extra years, let it be!.
P

Kwa katiba ipi ya kumbana rais atakayekuwa madarakani? Katiba yetu inampa rais uwezo wa kuamua ni mradi gani ni mzuri na sio mipango. Kwa katiba hii ya rais kuamua nani awe mbunge, na nani afungwe au asifungwe, sioni tukipiga hatua. Kama unataka Magufuli aongezewe muda sio kwasababu anayotekeleza sasa ni mazuri, bali una maslahi naye binafsi. Kama ni mazuri hata akitoka, uwe unaanzisha makala hata ikibidi kuuwawa ili hayo mazuri yatekelezwe. Sio leo tunaimbishwa kama watoto wadogo kuwa gas ndio muarubaini wa matatizo ya umeme, haijapita hata miaka 10, tunaambiwa gas tumepigwa, ila umeme wa maji ndio sahihi!
 
Mkuu nafahamu kabisa kuwa mada iliyoko mezani ni SGR japo nayo naona unababaisha tu. Nilitaja mradi wa bomba la mafuta kama mfano kukuonyesha kiwango cha utapeli tu kwenye hii miradi. Lengo la mimi kutaja mfano wa bomba la mafuta, na mfano wa sarafu ya pamoja ya East Afrika, ni kukuonyesha kuwa hatuna vipaombele vya hivyo. Ila huyo Mataga akaingilia hapo kati ikabidi nimpe zaidi.

Huku kwenye SGR nilipoona tu unasema kipande cha Dar-Moro tatizo lilikuwa ni Corona, nikajua umeamua kuleta uongo usio na tija, ndio maana ndani ya hii mada yako naendelea kujadili kiwango cha utapeli wa hii miradi, na sio kubaki kwenye hoja iliyo mezani, maana hata ww mwenyewe huna utetezi wenye mashiko zaidi ya porojo za kufurahisha genge.
Na ni kweli pasco kutaja corona kama kikwazo kipande hicho cha km300 na kimeanza kujengwa miaka kadhaa nyuma huo ni uongo kama sio hoja ya kitoto kutoka kwa Pasco

Sent from my TECNO-N2 using JamiiForums mobile app
 
Umewahi kutembelea maeneo ya hii miradi ukaona kazi zinazofanyika?? Kama la basi tembelea kwanza then ndo uje uwazodoe hapa. Huwa nawapinga sana MATAGA ila kwenye hili napingana na wewe. Fanya kwenda kuangalia naamini utabadilisha maoni yako. Btw soon kipande cha mwanza kitaanza kujengwa.
Nimepita sehemu kadhaa na kuna kazi kweli inafanyika, sina tatizo kabisa na kazi kufanyika, ninahoji muda wa kumalizika kwa mradi kutokana na ahadi zinazotoka. Dar-Moro ilikuwa ikamilike Nov 2019. Lakini sasa tunaambiwa itakamilika Aprili 2021. Na je kweli ni fedha za ndani?
 
27 Reactions
Reply
Back
Top Bottom