The SGR War: Magufugame vs Musevenyatta ni Vita Kubwa!. It is a Win Lose War!. When One Wins, the Other Lose, No Win Win Situation!.

Haya mabandiko marefu tabu sana. Unatafuta pointi mpaka kuipata shatoka jasho tele.

Nimepitsha macho tu mahali nikakuta sehemu inasema "hakuna aliyejua Magufuli kwenda Rwanda, nk...) Mara hii umeme wa maporomoko ya Rusumo huyakumbuki?

Mengine sikusoma, lakini kutokana na kichwa cha habari kuna ninayounga mkono kuhusu 'vita'.

Siyo siri hata kidogo kuwa kuna vita, sio iliyoanza leo. Ni vita ya siku nyingi, na inapiganwa kwa njia mbalimbali.

Rwanda na Uganda ni Jiografia tu ndio inayoamua. Rwanda hadi leo hii anafanya biashara nyingi zaidi na Kenya kuliko Tanzania. Baadhi ya mizigo yake bado anapitisha Mombasa, hii sio kwa sababu anapenda kufanya hivyo, ni kwa sababu ya ubovu uliokuwepo bandarini Dar es Salaam.. Reli ilipong'olewa Kibera, Uganda wakakimbilia Da es Salaam, pamoja na kuwa ni njia ndefu.

Kenya waliofanya Mikutano yao mikubwa mwaka 2015, kama ule wa waJapan TICAD (nadhani inaitwa), walitegemea Magufuli wa wote wa Africa Masharika watakuwepo. Jamaa akamtuma Mama Samia. Wakaanza kulalamika tokea hapo.

Siku zote, inaeleweka, mipango ni kuifanya Nairobi iwe ndio Kitovu (Hub/ Gateway) ya eneo hili. Kiwe kitovu cha biashara, hata zile haramu. "Mabeberu", ndio na mimi ngoja nitumie neno hilo, wako 'bize' sana kuwekeza huko wakilenga kufaidika na ukanda wote huu. Ukiona jamaa wanaporomosha ma-godown na miundo mbinu za 'Logistics', usidhani hawajui wanachofanya.
Ile EPA, si unaikumbuka?..., basi iweke kwenye mipango na anza kuwaza makubwa.

Magufuli, hapana hata Kikwete wote walijihami. Mashirika mengi ya Kimataifa yanaweka ofisi huko, ili waje wafanye kazi hadi huku. Sawa, Mbongo kaweka kodi. Ukija hapa na kufanya kiconsultancy chako siku mbili tatu, lipia kibali na kodi kila unapotaka kuja hapa. Jamaa hawajaacha kulia.

Hivi Paskali, mbona unajifanya msahaulifu hivyo? Hata yule ng'ombe aliyekufa humkumbuki? The Coalision of the Willing. Hiyo ilikuwa ni vita ya wazi iliyolengwa kumtandika Kikwete. Kwa bahati nzuri sana aliipangua na mpango mzima ukasambaratika.

Bandari ya Bagamoyo waliiogopa sana, kwa maana ililenga kuiondoa kabisa Mombasa. Sasa watakuwa wamevuta pumzi.
Ile Barabara ya "kwenda Burundi" tokea Mombasa bila shaka huijui Paskali. Kuna siku waliandika "Wanajenga barabara ya kwenda Burundi.
Habari hiyo ilichapishwa katika kijarida chao cha siku zote 'The East African'. Sasa wanamsherehekea Tshekedi...

Nami ntaandika gazeti kama lako? Hapana...
 
Rwanda secures dry port in Kenya

Duh...!, this is very bad to our SGR, maadam tuliisha sainiana nao mkataba, they have to honor it. Huku kutaka kuunda ka coalition of the willing kangine, it did work well with JK, but it won't work well with JPM, ikibidi, tutawaadabisha, wasituletee mchezo!.

P
 
Wanabodi
Bandari ya Mombasa is very busy kwa sababu ya mizigo ya Uganda, Sudan ya Kusini na Tanzania. Hata kama tutaboresha efficiency ya Bandari ya Dar, mizigo yote ya Tanzania itapitia Dar, hivyo bandari yetu ikifanikiwa kwenye hili, mizigo yote ya DRC, Rwanda na Burundi itapita Dar na kuifanya Dar port kuwa the biggest, the busiest na the most profitable kuliko bandari ya Mombasa, lakini bado haiwezi kushibisha SGR ikajiendesha kwa faida, ndio maana wenye kuona mbali, wakaamua tujenge bandari ya kisasa Bagamoyo, na kuziboresha Bandari za Dar, Tanga na Mtwara na ndipo tutakuwa na mzigo wa kutosha kuishibisha SGR na kuiendesha kwa faida. Lakini wakatokea wenye uoni wa mpaka mwisho tuu wa pua zao, wakaambizana eti bandari ya Bagamoyo atafaidi Mkwere, waka abandon hii project.

Paskali
Wanabodi, Tanzania ni nchi yetu sote, viongozi wetu wana wajibu wa kutusikiliza sisi wananchi wao tunasema nini na kushauri nini, kama ushauri wetu ni mzuri, wauzingatie, kama ni ushauri wa hovyo, wau puuzie.

Ushauri huu ulitolewa miaka 3 iliyopita, ulipuuzwa!. Leo Spika kaenda China, akaonyeshwa na Wachina umuhimu wa bandari ya Bagamoyo, sasa ndio leo, Spika wetu anaongea Bungeni!.


Yaani kuna vitu wakishauri kina yakhe, vina puuziwa, lakini akishauri mchina, ndio Spika anaelewa!.
P
 
Hela hatuna, tusikope sana ili kupunguza kutumia na madeni.

Tabora ni karibu sana na Burundi, Rwanda, DRC, Mwanza na Uganda. Tujenge bandari kavu kuubwa pale Tabora ili watu wa Mwanza, Uganda, Rwanda, Burundi, DRC na Kigoma wachukulie Tabora mizigo yao itakayoletwa na SGR hapo.

Tukipata faida hapo tutaendelea na ujenzi hadi Mwanza, Burundi Rwanda na DRC kama tulivyokuwa tumepanga.

Hii itasaidia kuepuka uharibifu wa barabara kutoka dar hadi Tabora lakini na kupunguza umbali na gharama kwa watu wa DRC, Rwanda, Burundi kufuata bidhaa zao Dsm.
Mkuu kavulata , kwanza asante kwa mawazo yako. Sii wengi humu wanajua how SGR can operate profitably!. Ili SGR iweze kuleta faida ni lazima iwe na kitu kinachoitwa linkages. Mfano hiki kipande cha Dar Moro ambacho kiko tayari, kiteendeshwa kwa hasara muda wote hadi SGR itakapo link na Rwanda, Burundi, Uganda na DRC.

Karibu mitaa hii

Pia kasome
P
 
Wanabodi, Tanzania ni nchi yetu sote, viongozi wetu wana wajibu wa kutusikiliza sisi wananchi wao tunasema nini na kushauri nini, kama ushauri wetu ni mzuri, wauzingatie, kama ni ushauri wa hovyo, wau puuzie.

Ushauri huu ulitolewa miaka 3 iliyopita, ulipuuzwa!. Leo Spika kaenda China, akaonyeshwa na Wachina umuhimu wa bandari ya Bagamoyo, sasa ndio leo, Spika wetu anaongea Bungeni!.


Yaani kuna vitu wakishauri kina yakhe, vina puuziwa, lakini akishauri mchina, ndio Spika anaelewa!.
P

Sad
 
  1. Kutandaza SGR kuelekea mipaka yetu yote ili mizigo ya jirani zetu wote ipite bandari ya DSM.
  2. Kuongeza ndege za ATC hadi ATC i oparate kama Ethiopia Air na SAA.
  3. Kukamilisha Stigler
  4. Kujenga Tanzania ya Viwanda.
  5. Kukamilisha Tanzania kuwa nchi ya Uchumi wa Gesi
  6. Kufikisha Tanzania kwenye kuwa ni nchi ya Uchumi wa Kati
Alhamisi Njema.

Paskali.
Kiukweli kabisa, huyu mtu aliyeifanya kazi hii, akitokea kuja kuchaguliwa kuwa Mwakilishi wa Tanzania ndani ya EALA, you can just imagine atafanya nini!. Kama amaweza kufanya yote haya akiwa just a journalist, akitokea akawa mbumbe wa kitu kama EALA, si Tanzania itapaa?. Au mnasemaje wanabodi?.
P
 
Wanabodi,
Rais Magufuli aliposema vita vya uchumi ni mbaya ni kuliko vita vya kawaida, alikuwa right.

Hili ni bandiko kuhusu vita kubwa, ambayo mimi nimeipa jina la Magufugame vs Musevenyatta.

Magufugame vs Musevenyata ni Vita Kubwa ya Kiuchumi!. Its a Win Lose War!. When One Wins, The Other Lose, No Win Win Situation!.

Paskali.
Hili jina sasa limebadilikablimekuwa SAMIGAME VS MUSERUTO
P
 
Kwenye mambo ya SGR, Watanzania tunapaswa kuambiwa tuu ukweli wa kila kitu!, serikali yetu lazima iwe very transparent see through kwenye kila kitu including mikataba na financial maters kufuatia kuwahi kupigwa huko nyuma kwenye rada, kwenye ndege, kwenye meli na sasa kwenye reli
Maswali haya yajibiwe kikamilifu
Wanabodi,
1. Taarifa ya TRC inasema vichwa vipya na mabehewa mapya, lakini ukweli ni kuwa ni vichwa mitumba na mabehewa mitumba kama ya mwaka '1947'!.

2. Ukiyaangalia kwa ndani, haya mabehewa ni kama yana madirisha only one sided!, hiki ni kuashiria originally haya ni mabehewa ya underground trains na sio ya terestrial train!. Sisi SGR yetu ni terestrial, moja ya faida kubwa kusafiri na treni ni pamoja na kuenjoy kitu kinachoitwa scenery enjoymement, madirisha makubwa both sides abiria kuona nje, hizi behewa za madirisha ya upande mmoja, hebu mfikirie abiria wa Kigoma, seat ya upande usio na dirisha!, kuna tofauti gani na chumba cha jela?.

3. Mkataba ni wa ukarabati na kutiwa nakshi nakshi kwa vichwa na mabehewa mitumba!, na sio kuundwa kwa vichwa na mabehewa mapya!, kwanini Watanzania hatuelezwi ukweli?.
Hakuna ubaya nchi kununua vichwa mitumba na mabehewa mitumba, kitu muhimu ni Watanzania tuelezwe ukweli!.

4. Je, hivyo vichwa viliundwa lini, wapi?, jee originally vimetumika wapi na kwa muda gani kabla sisi hatujauziwa?

5. Mitumba hiyo imenunuliwa kwa bei gani, ikakarabatiwa kwa bei gani, na kusafirishwa kwa gharama gani?

6. Tufanyiwe comparative analysis, kama tungenunua vichwa vipya na mabehewa mapya, tungetumia gharama kiasi gani, compared na kununua vichwa mitumba na mabehewa mitumba, ili tujue tumeokoa fedha kiasi gani kwa kununua mitumba hiyo?

7. Japo gharama za kununua vitu vipya ni juu ila maintance cost ni ndogo, unaweza kununua mitumba kwa bei poa kumbe ni mitumba choka mbaya, hivyo maintenance cost ikawa juu.

8. Sii wengi wanajua kazi ya CAG sio kutoa tuu zile ripoti za hesabu za serikali, CAG ni Mdhibiti na Mkaguzi, ufhibiti unafanywa kabla ya manunuzi, je, kulifanyika tathmini yoyote rail worthness report ya vichwa na mabehewa hayo mitumba kabla hayajanunuliwa?. Then CAG atufanyie value for money audit, msikute mitumba hiyo tumepewa bure, huku watu wakipiga kubwa tunauziwa kwa bei ya mapya!.

9. Ukiingia mkataba wa manunuzi, kwa matengenezo, mzigo ukanunuliwa, delivery ndio ikachelewa, huwezi kuvunja mkataba huo ukabaki salama, hivyo kesi ikifunguliwa, Tanzania tunashindwa hata kabla kesi haijaanza!.

10. Tulivunja mkataba wa Dowans, tulishitakiwa, tukashindwa, tukadaiwa tukasema hatulipi!, watu wakajiapisha "over my dead body", hatulipi!.
ukweli ni kuwa tumelipa kwa siri, Watanzania hatukuambiwa!.

11. Tulipo vunja mkataba wa Dowans, Zitto akashauri tuitaifishe mitambo ile, Wabunge wetu wakagoma kuwa Tanzania hatununui mitambo chakavu, mitambo mitumba!

12 Mitambo ile ikanunuliwa na Simbion, tukaingia nao mkataba ule ule wa Dowans, watu wale wale walio ikataa dowams, ndio hao hao danced to the tune na Hilary Clinton kuzindua Simbion kwa mkataba ule ule tuliovunja!, kwa gharama zile zile!, na capacity charge ile ile!, na tukawalipa!.

13. JPM alipoingia tukavunja mkataba wa Simbion, tukashitakiwa, tukashindwa, JPM akagoma kulipa!, ila baada tuu ya JPM kuitwa kule alipoitwa huku nyuma, sisi sio tuu tumelipa!, bali pia tumeinunua ile mitambo ya Simbion kwa bei ya ajabu!, sasa mitambo ile tuliosema ni chakavu, mtumba, na serikali yetu hatununui, mivitu chakavu, sasa ndio tumeinunua!, sasa mitambo ile ya Simbion ni mitambo yetu, ni mali yetu! na malipo yote yaliisha fanyika chap chap fasta fasta!, bila bajeti yake kuombwa popote!, bila Bunge letu kuijadili, bila CAG kuidhinisha malipo hayo!, na haya yote yamefanyika bila iWatanzania kuambiwa!.

14. NB. Unapohoji vitu kama hivi, huchelewi kunyooshewa vidole vya kukosa uzalendo au kutokuwa na nia njema!, no!, wala sijasema kilichofanyika ni wrong!, no!, ninachosema hapa ni sisi
Watanzania wa sasa ni waelewa, tuwe tuu tunaambiwa ukweli,

15. Kwa vile mambo kama haya kwenye manunuzi makubwa yaliwahi kutokea kule nyuma kwenye ununuzi wa Rada mtumba toka BAE, watu wakaweka cha juu kikubwa tuu, tukalipa fasta!, Mama Mzalendo wa kizungu, Linda Chalkel akabaini, akatupigania tukarudishiwa chenji ya Rada!.

16. Ununuzi wa ndege ya rais Gulf Steeam bei ikapaishwa zaidibya mara tatu!, John Cheyo akaonyesha bei ya kiwandaji watu wakatia pamba masikioni tukalipa fasta!.

17. Kuna vifaa vya kijeshi chakavu tumeuziwa hapa!, tangu vimenunuliwa havijawahi kutumika mpaka leo!. Hivi naomba nisivizungumzie wala msiniulizie!, maana hata sisi waandishi wa habari haturuhusiwi kuzungumzia mambo ya jeshi na usalama wa taifa, ila fedha zilizotumika sio fedha za jeshi au za usalama wa taifa, ni fedha za Watanzania, kuzungumzia vifaa vya jeshi, tuliuziwa nini mitumba ni vifaa vya nini na viko wapi, hii ni no!, hatuzungumzi, lakini tulilipia fedha kiasi gani, ni haki ya Watanzania kujua!.

18. Tukanunua Boti mtumba ya MV Bagamoyo, ikafanya safari moja tuu mahali pa 30 min, ilitumia masaa 3!, Hii pia sasa ni kufaa cha kijeshi!, isizungumzwe!, ila fedha zake ni fedha za Watanzania!.

19. Hivyo kweli hivi vichwa na mabehewa haya, ni bora tukaelezana ukweli tangia mwanzo!.

20. Namalizia kwa msisitizo, hakuna ubaya kutumia vitu used!, tena vingine ni vizuri, imara, bora, madhubuti kuliko hata vipya!, na Watanzania walio wengi, kutokana na low purchasing power due to umasikini uliotopea, wengi wetu affordability yetu ni mitumba kuanzia magar
i, nguo hadi mitambo, hivyo tumezoea, tunachohitaji ni kuambiwa ukweli tuu!,
tutaelewa tuu kuliko...

Wasalaam.
Paskali.
Maswali haya yanahitaji majibu ya kina na sio blah blah!.
Kama mtu kuuliza maswali kama haya, kutapelekea kuhojiwa uzalendo wake, mimi naomba kutumia kinga ya kihabari na kanuni ya kwanza ya mwandishi wa habari no seek the truth, and write nothing but the truth!, kuna kitu ninadhamiria sio tuu kuandika bali kukitengenezea a video documentary ya safari ya SGR ya Tanzania, tulipotoka, tulipo na tunapokwenda, ili huko mbele, likija kujitokeza liji white elephant fulani hivi ambalo sijui kama ni mimi tuu naliona, angalau dhamira yangu isinisute, niliona kabla, nikasema kabla, nikaandaa documentary kabla, nikaonyesha kabla, ili angalau jamii ya Watanzania wajue kuna watu waliona kabla na walisema kabla!.

Na labda kuwasaidia Watanzania wenzangu wasio jua, kwenye ile kashfa ya rada, BAE walikiri kutoa mlungula wa kickbacks, lakini sheria yao inawaruhusu non disclosure ya waliowapa mlungula, ilo usipoteze wateja wapya wapenda mlungula, kibiashara mlungula wa 10% ni halali!, ila ikijulikana kuwa umetoa mlungula, unapaswa ama uwataje uliowapa mlungungula, wakamuliwe wautapike huo mlingula, ama uwahifadhi usiwataje, na badala yake utozwe faini kwa uliowapa mlungula, na kuurejesha ule mlungula, na hicho ndicho kilichofanywa na BAE, kuwahifadhi waliowapa mlungula, na badala yake ikakubali kulipa faini na ndipo tukarejeshewa ile chenji ya rada.

Hii maana yake, kuna viongozi wetu walikula mlungula BAE akawakingia kifua kuwahifadhi kwa kulipia faini na ule mlungula ukarudishwa nchini kama chenji ya rada, endapo BAE wasinge wakingia kifua kuwahifadhi na kuwalinda, amini usiamini, hayo majina ya waliopokea mlungula na kuzihifadhi fedha zao kule Credit Suisse, yangetoka, Watanzania msinge amini macho na masikio yenu!.

Kashfa hii iliobuka kwasababu tuu kulitokea lijinga limoja, mgao wake yeye ukauhifadhi visiwa fulani ambavyo viko chini ya milki ya Uingereza, ndipo Muingereza akabaini, lakini kama wote wange bank Swiss banks, kule fedha zao ni very secure, hata bank manager, hajui majina ya customers na clients ni secret codes tuu zinatembea, hivyo wala kashfa ya rada isinge ibuka!.

Hivyo watu tunaoulizia kuhusu haya mabenewa, naomba mtuelewe ni wazalendo wa kweli wa nchi hii!.

Paskali
 
28 Reactions
Reply
Back
Top Bottom