Emc2
JF-Expert Member
- Sep 26, 2011
- 16,808
- 16,831
Nawasalimia ndugu zangu, poleni na majukumu ya kila siku.
Utangulizi
Leo nitaanza kuelezea jambo la namba. Namba ambayo nitaielezea leo ni namba 8. Nitaeleza jumbe mbalimbali na siri iliyopo kwenye namba 8.
Katika thread hii nitaelezea namba hii katika nyanja mbalimbali.
1. Kiimani, 2. Kitamaduni, 3. Kimazingira, 4.Kiroho, 5.Kisayansi,na 6. Kihesabu.
Kwenye imani nitaongelea dini na madhehebu mbalimbali kuhus hii namba.
Kwanza kabisa tukianza kuongelea namba 8 tunaongelea namba inayofuata baada ya namba 7 tukitumia (decimal numbers) namba zinazoanzia 0 - 9.
Kwa kifupi tu; kuna aina nyingi za mfumo wa namba:-
1. Binary Number (0 -1)
2. Octa decimal (0 - 7) base 8
3. Decimal Number (0 -9) base 10
4. Hexadecimal Number (0 - F) base 16
Sasa base tukitaka kuandika namba 8 kwa mfumo wa binary itakuwa ni: 8 base 10 = 00001000 base 2
Ngoja nisiwachanganye sana. Katika maelezo yangu nitajikita sana kuongelea namba za base 10.
Sasa basi katika thread hii nitakuwa naelezea hatua kwa hatua huku wachangiaji wengine wakichangia.
Hata hivyo tunatakiwa kujua maisha yetu yamefungiwa kwenye siri ya namba na siri hiyo ipo katika mahesabu. Sasa basi utakapo kosea mahesabu tayari jibu utakalolipata siyo sahihi.
Sasa basi nitaanza kuongelea namba 8 hatua kwa hatua huenda baada ya somo hili baadhi yetu tutaanza kuelewa kusoma nyakati na kujua wakati ni wa kufanya nini.
Katika huu mfumo wa namba hususani namba 8 tutatumia Gematria method na Numerology katika mambo yetu. Ikumbukwe kwamba katika baadhi ya tamaduni majina, slogan na companies zinakuwa encoded kwenye namba na hivyo kuleta impact kubwa katika physical world.
Sitaki niwachoshe huu ni utangulizi tu ngoja kila mmoja aanze kutafakari kabla sijaendelea zaidi.