Artificial intelligence
JF-Expert Member
- Jan 28, 2021
- 1,262
- 2,191
Miaka ya nyuma kipindi cha mediaval na reformation of church, kanisa katoliki lilikumbwa na misuko suko mbali mbali iliyolitikisa kanisa kweli kweli. Mojawapo ikiwa ni kuanzishwa kwa kanisa la protestant kutoka kanisakatoliki.
Vugu vugu hilo lilianzishwa na mtaalamu wa theolojia ya dini na Profesa wa chuo kikuu nchini Ujerumani aliyebobea katika maandiko ya dini , hapa namzungmzia Martin Luther.
Kuanzishwa kwa Protestant Church
Protestant ilianzishwa kwa kupinga mamlaka na utawala wa papa juu ya indulgences katika kanisa katoliki.
Indulgences- Katika kipindi hicho 'indulgences' katika kanisa katoliki ilimaanisha kwamba ili kuhungama dhambi na kusemehewa dhambi, kupata baraka wakatoliki walitakiwa kutoa matoleo kama vile pesa na vitu mbali mbali vya thamani au kuchangia pesa kanisa ili waweze kuombewa na kusamehewa dhambi zao.
Wakati wa indulgences ndipo Luther alipata wazo la kupingi mamlaka ya Papa na utaratibu huo wa indulgences ili kujitenge na kanisa katoliki na kuanzisha protestant kama kanisa jipya katika kanisa katoliki. Katika hili Luther alipata uungwaji mkono kutoka kwa baadhi ya wahumini ambao walikuwa hawaridhishwi na namna utaratibu huo wa indulgences ulivyokuwa ukitumika katika kanisa katoliki.
Mnamo tarehe 31 October 1517 Luther alimuandikia barua askofu mkuu wa jimbo la Mainz na Magdeburg nchini Ujerumani Albrecht akipinga vikali shughuli za padri Peter Tetzel na Papa Leo X kuhusu indulgences katika kanisa katoliki ambapo katika kipindi hicho Albrecht na Papa Leo X walikusanya fedha na misaada kupitia indulgences kwa ajili ya ujenzi wa St Peters Basilica. Ni katika tarehe na mwaka huo protestant Church ilianzishwa rasmi chini ya Martin Luther.
Katoliki walichukulia kutoa matoleo ya fedha kupitia indulgences kama kazi nzuri katika utumishi wa Mungu lakini Luther hakukubaliana na hilo kabisa.
Waraka wa Martin Luther
Katika waraka wake 'on the power and efficacy of indulgences ' ambao baadaye ulijulikana kama 'The 95 Theses' aliuambatanisha katika barua yake kwenda kwa Papa Leo X, Luther alisistiza kwamba 'Ni Mungu pekee anayeweza kutoa msamaha wa dhambi na uponyaji wake na msamaha huo hauwezi kupatikana kwa kununua indulgences.
Vile vile Luther akaendelea kusisitiza kwamba nadharia ya kanisa Katoliki kwamba Papa ni mediator kati ya Mungu na Yesu kristu kwa niaba ya mwanadamu siyo kweli na akaenda mbali akisema Yesu pekee ndiye mediator kati ya Mwanadamu na Mungu na hapa ndipo nadharia kuu ya protestant iliposimama. Aliendelea kusisitiza kwamba uponyaji na msamaha wa dhambi unapatikana kwa kuwa na imani katika Yesu kristu tu na siyo kwa kazi za matoleo na misaada katika kanisa Katoliki.
Vugu vugu hilo la kuanzishwa kwa protestant lilipelekea Ulaya kugawanyika katika makundi mawili makuu ya imani ,yaani kaskazini yote ikawa protestant huku ulaya kusini ikabakia kuwa Katoliki. Na nikuanzia hapa protestant ikaenea sehemu mbali mbali duniani kote.
Baada ya kuanzishwa kwa protestant, msingi wa imani kuu yao umebadilika
na nikama vile wamerudi kule kule walipokuwa wakatoliki. Kwa sasa indulgences zimejaa katika protestant kiasi cha kwamba wameweka hadi utaratibu wa sadaka ya kwenda madhabahuni kuwekewa mkono na mchungaji ili kupata baraka zake.
Inamaana ni kama Martin Luther alihitaji na yeye awe anapata hizo indulgences ila kutokana na uzibe akatumia mwanya huo kuanzisha protestant kwa kutumia mapungufu hayo ya kiimani waliyokuwa nayo katoliki.
Swali langu kuu, ambalo ningependa kuwaachia wana jf, protestant wanapinga sana indulgences katika imani lakini kwa nini wanazitumia katika kuendesha kanisa leo?
Namaliza kwa kusema tamaa ya mali ilipelekea kuanzishwa kwa protestant kutoka kanisa katoliki na mafundisho yamebaki yale yale zaidi ya 90%.
Vugu vugu hilo lilianzishwa na mtaalamu wa theolojia ya dini na Profesa wa chuo kikuu nchini Ujerumani aliyebobea katika maandiko ya dini , hapa namzungmzia Martin Luther.
Kuanzishwa kwa Protestant Church
Protestant ilianzishwa kwa kupinga mamlaka na utawala wa papa juu ya indulgences katika kanisa katoliki.
Indulgences- Katika kipindi hicho 'indulgences' katika kanisa katoliki ilimaanisha kwamba ili kuhungama dhambi na kusemehewa dhambi, kupata baraka wakatoliki walitakiwa kutoa matoleo kama vile pesa na vitu mbali mbali vya thamani au kuchangia pesa kanisa ili waweze kuombewa na kusamehewa dhambi zao.
Wakati wa indulgences ndipo Luther alipata wazo la kupingi mamlaka ya Papa na utaratibu huo wa indulgences ili kujitenge na kanisa katoliki na kuanzisha protestant kama kanisa jipya katika kanisa katoliki. Katika hili Luther alipata uungwaji mkono kutoka kwa baadhi ya wahumini ambao walikuwa hawaridhishwi na namna utaratibu huo wa indulgences ulivyokuwa ukitumika katika kanisa katoliki.
Mnamo tarehe 31 October 1517 Luther alimuandikia barua askofu mkuu wa jimbo la Mainz na Magdeburg nchini Ujerumani Albrecht akipinga vikali shughuli za padri Peter Tetzel na Papa Leo X kuhusu indulgences katika kanisa katoliki ambapo katika kipindi hicho Albrecht na Papa Leo X walikusanya fedha na misaada kupitia indulgences kwa ajili ya ujenzi wa St Peters Basilica. Ni katika tarehe na mwaka huo protestant Church ilianzishwa rasmi chini ya Martin Luther.
Katoliki walichukulia kutoa matoleo ya fedha kupitia indulgences kama kazi nzuri katika utumishi wa Mungu lakini Luther hakukubaliana na hilo kabisa.
Waraka wa Martin Luther
Katika waraka wake 'on the power and efficacy of indulgences ' ambao baadaye ulijulikana kama 'The 95 Theses' aliuambatanisha katika barua yake kwenda kwa Papa Leo X, Luther alisistiza kwamba 'Ni Mungu pekee anayeweza kutoa msamaha wa dhambi na uponyaji wake na msamaha huo hauwezi kupatikana kwa kununua indulgences.
Vile vile Luther akaendelea kusisitiza kwamba nadharia ya kanisa Katoliki kwamba Papa ni mediator kati ya Mungu na Yesu kristu kwa niaba ya mwanadamu siyo kweli na akaenda mbali akisema Yesu pekee ndiye mediator kati ya Mwanadamu na Mungu na hapa ndipo nadharia kuu ya protestant iliposimama. Aliendelea kusisitiza kwamba uponyaji na msamaha wa dhambi unapatikana kwa kuwa na imani katika Yesu kristu tu na siyo kwa kazi za matoleo na misaada katika kanisa Katoliki.
Vugu vugu hilo la kuanzishwa kwa protestant lilipelekea Ulaya kugawanyika katika makundi mawili makuu ya imani ,yaani kaskazini yote ikawa protestant huku ulaya kusini ikabakia kuwa Katoliki. Na nikuanzia hapa protestant ikaenea sehemu mbali mbali duniani kote.
Baada ya kuanzishwa kwa protestant, msingi wa imani kuu yao umebadilika
na nikama vile wamerudi kule kule walipokuwa wakatoliki. Kwa sasa indulgences zimejaa katika protestant kiasi cha kwamba wameweka hadi utaratibu wa sadaka ya kwenda madhabahuni kuwekewa mkono na mchungaji ili kupata baraka zake.
Inamaana ni kama Martin Luther alihitaji na yeye awe anapata hizo indulgences ila kutokana na uzibe akatumia mwanya huo kuanzisha protestant kwa kutumia mapungufu hayo ya kiimani waliyokuwa nayo katoliki.
Swali langu kuu, ambalo ningependa kuwaachia wana jf, protestant wanapinga sana indulgences katika imani lakini kwa nini wanazitumia katika kuendesha kanisa leo?
Namaliza kwa kusema tamaa ya mali ilipelekea kuanzishwa kwa protestant kutoka kanisa katoliki na mafundisho yamebaki yale yale zaidi ya 90%.