The saga continue: Dili la kupeleka wagonjwa wa Moyo India

Yo Yo

JF-Expert Member
May 31, 2008
11,217
1,702
WAGONJWA WA KITANZANIA WANAOTIBIWA NARAYANNA HOSPITAL BANGALORE ,INDIA.

Mwezi wa saba mwaka 2008 huu tarehe za 21/22 Watanzania 17 wagonjwa wakiongozana wa wasaidizi wao 11 waliondoka nchini kuelekea nchini india kwa ajili ya kupatiwa matibu ya ugonjwa wa moyo katika hospitali iliyo katika mji wa Bangalore huko India,wagonjwa hao wengi wao wakiwa ni watoto na watu wazima wachache.

Kwa mujibu wa habari zinazofahamika nchini Tanzania wagonjwa hao waliweza kwenda kutibiwa nchini India wa ushirikiano kati ya Regency hospital chini ya Dr Kanabah na Lions club ambaye mwenyekiti wake ni Dr Yusuph Dalali,wagonjwa hao walifika katika hospitali ya Narayanna na kuanza matibabu yao kama kawaida kwani tayari walikuwa wameshafanya malipo yao nchini Tanzania .

Wakati matibabu hayo yakiwa yanaendelea yalijitokeza matatizo ambayo yaliweza kusababisha baadhi ya wagonjwa matibabu yao kusimamishwa kwa muda,hii ikiwa na maana kwamba fedha ambazo narayana hospital ilizipokea kutoka nyumbani Tanzania zilikuwa zinawezesha kutibu wagonjwa wachache kulingana na fedha zenyewe,hali ilipozidi kuwa ngumu ilibidi wagonjwa kutaka kujua ni kiasi gani cha fedha kilitumwa kutoka Tanzania? Na je kiasi hicho kilichotumwa kinaonyesha nani aliyelipa na nani asiye lipa? Jibu la hospitali likawa fedha ni ndogo ,ikabidi baadhi ya wagojwa waweze kutolewa wodini mpaka hapo fedha zitakapotumwa .

Habari zisizo rasmi zinazoendelea nikwamba fedha zimeshatumwa wagonjwa wawili ndio watakao weza kufanyiwa upasuaji siku yeyote kuanzia jumatatu ya 18/08/2008 Bw Robert Kewel na Bw Wilfred Kirika Laizer , mwingine imeonekana hana ugonjwa wa moyo kabisa na wala hana tatizo la aina yeyote kulingana na vipimo vya Narayanna hospital ambaye ni bwana Chacha,na mwingine imeonekana kuwa anatatizo la miguu kujaa maji inabidi kurudi nyumbani ,arudi tena Narayanna hospital baada ya miezi sita bw Athmani Juma Abdallah,kwa mujibu habari zilizopo watoto wawili Abdulkarim Abdul Ipande na Ester Paulo Mwita wao jopo la madaktari limeona itakuwa ni hatari sana kuwaopereti watoto hao kulingana na hali zao,ni bora wakaendelea na dawa tu ,mtoto Abdulkarim Abdul Ipande yeye ni mara yake ya pili kuletwa Narayanna hospital,alishaletwa mwaka 2007 na mwaka huu 2008 kwa mujibu wa habari rasmi ni kwamba wagonjwa wote hao waliongozana na mkuu wao wa msafara Dr Ally Amour kutoka mnazi mmoja hospital Zanzibar ambaye pia ni daktari wa moyo.

Wagonjwa wote kwa pamoja wameshtushwa na habari zilizoandikwa na gazeti la Bangalore India,"Sunday express la jumapili 10/08/2008 ukurusa wa 3"lenye kichwa cha habari kisemacho "17 AFRICANS TREATED IN CITY", kwamba wao ni masikini sana walioshindwa kumudu gharama za matibabu nchini kwao,lions club ya Dar es salaam imegharamia matibabu ,usafiri,malazi,na matumizi mengine katika muda wote wa matibabu yao,wakizungumza kwa uchungu mbele ya wanafunzi wa kitanzania wanaosoma Bangalore University,India ambao waliwatembelea tarehe 15/08/2008 siku ya ijumaa majira ya jioni kwa ajili ya kuwapa pole,wagonjwa hao wamesikitishwa na hilo kwani wao wamejilipia usafiri wenyewe kuja na kurudi ,malazi wanajilipia wenyewe katika hostel wanazo kaa za na pia wanapika wenyewe , Shantinikethan hostel boomasandra area , wamejinunulia masafuria,sahani ,vikombe na vyakula kama mchele,maharage,kuku kwa ajili hiyo , hii ni kutokana kushindwa kumudu vyakula vya kihindi kutonakana na pilipili,sehemu za malazi zenyewe zinaonekana kuna kunguni,chawa na pia hazina mpangilo mzuri wa uwekaji wa vitu ,kwani hakuna makabati hata ya kuwekea nguo na baadhi ya vitu vidogo vidogo,baadhi ya wagonjwa wameshindwa kukaa katika hostel hiyo na kuamua kutafuta nyingine ambayo ni nzuri inajulikana kwa jina la online suite Boomasandra area ,kwani wanapata chakula kizuri,na vyumba vina Tv na simu kwa ajili ya mawasiliano,kwa mujibu wa wagonjwa hostel zote hizo ziko karibu.

Wagonjwa wamelalama pia inakuaje wanaambiwa wamelipiwa matibabu,na kwamba hata wao wenyewe waliambiwa wachangine kiasi Fulani cha fedha? Kulingana na uwezo wa mgojwa aliokuwa nao? Na pia wameshtushwa sana na wao kutopewa risiti wakati wa malipo na kudai kuwa malipo waliyafanya kwa mwenyekiti wa lions club bw yusuph Dalali , Gents corner DTV round about ambako ndio duka lake la nguo/vitambaa lipo,na pia wameshtushwa na uwepo wao Bangalore India ,bila ya ubalozi wao wa Tanzania New Delhi kufaham? Na je kama mabomu yaliyojitokeza maeneo ya madiwala market ,ambapo ni umbali wa kilomita 17 kutoka eneo walipo yangeweza kutokea eneo la hospitali ingekuwaje?

Baadhi ya wagonjwa wamshtushwa pia kutokumjua mkuu wao wa msafara Dr Ally mapema ,kwani wameanza kumjulia Nairobi wakati wakibadilisha ndege ya Kenya air ways ya kwenda Bombay,na wengine kumjua kwamba yeye ndio mkuu wa msafara walipofika Narayana hospital,India.

Wagonjwa hao wamewashukuru wanafunzi wa Kitanzania wanaosoma Bangalore University,India waliotembelea katika hostel wanazo kaa na kujionea hali ilivyo na pia kuwasaidia kutambulika ubalozi wa Tanzania New Delhi India.

Kwa mujibu wa vyanzo vya habari mbalimbali ni kuwa wagonjwa hao wanategemea kuwasili nyumbani Tanzania siku ya jumatano saa tisa mchana wakitokea Bombay India kupitia Nairobi ,kwa shirika la ndege ya Kenya airways.

Maoni yangu:
Kazi kweli kweli......malipo yamefanywa dukani kwa mdosi tena bila risiti,malazi walioandaliwa machafu kiasi kwamba wangepata maambukizo mengine ya magonjwa,fedha wamelipa huduma hawajapata(zimeliwa?)........ni ufisadi juu ya ufisadi sasa tutaanza kuona umuhimu wa THI......

Source:http://kamerayangu.blogspot.com/ huyu kijana yuko nchini India kwa hiyo kaandika aliyoyaona.
 
Last edited:
mwanzo wa ngoma ni lelemama! ni rahisi kuiba wenyewe wakiwa mbali; tumeshasema na tunarudia tena kukataliwa na kuwekewa vikwazo vya THI vinahusiana moja kwa moja na safari za kutengeneza per diem za India.... yangu macho, nimepiga kelele wananiona mpinzani!! haya Tanzania wanao wanasaliti hadi wagonjwa!

Yoyo I hope that is story is not true kuwa imetiwa chumvi nyingi.. tusubiri tuone.
 
Jamaa wamezidi sana mpaka wagonjwa wanafukuzwa wodini na hela zao wamekwisha lipa? inatia hasira sana.....ukiangalia kuna bonge la usanii unaogubika suala zima la kupeleka wagonjwa India...
 
Jambo la kutisha sana ni kuwa Waziri muhusika anasimama tena bila woga na kusema eti maamuzi ya kuwatoa wale wagonjwa pale THI ni sahihi kabisa wakafie mbele.
Na ajabu kubwa zaidi hata Ikulu inaridhia wakafie mbele ili Deal za watu ziendelee. Ama kweli tumekwisha! Kama sio mahakama ya Rufani hali ingekuwaje kwa wale wagonjwa ambao NSSF na serikali hii hii tunayoita yetu walitaka kuwasomba kama wanavyo peleka ma buldozer kubomoabomoa?
 
Mh, hili la watu kupigwa mabao India halijaanza leo wakuu. Maswali ni mengi sana lakini bahati nzuri au mbaya majibu tunayo na yametuzunguka..... Je wahusika ina maana hajatosheka? Lions Club, Wizara husika etc etc etc, jamani haijatosha tuuu?? Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni japo imechelewa!

Kama walivyosema wenzangu, na kichwa habari pia kimesema "The saga continues......"

Tusubiri kama MMK alivyosema, kwenye posti yake hapo juu mmstari wa mwisho.... Ha aha aaaaaa

Mungu Ibariki Tanzania, Mungu tubariki waTanzania!!!
 
Mh, hili la watu kupigwa mabao India halijaanza leo wakuu. Maswali ni mengi sana lakini bahati nzuri au mbaya majibu tunayo na yametuzunguka..... Je wahusika ina maana hajatosheka? Lions Club, Wizara husika etc etc etc, jamani haijatosha tuuu?? Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni japo imechelewa!

Kama walivyosema wenzangu, na kichwa habari pia kimesema "The saga continues......"

Tusubiri kama MMK alivyosema, kwenye posti yake hapo juu mmstari wa mwisho.... Ha aha aaaaaa

Mungu Ibariki Tanzania, Mungu tubariki waTanzania!!!
Hao ndio wasanii wa kutupwa.....mimi kitu chochote akiwepo muhindi sina imani nacho.....Wizara wanajua na bado wanabariki wagonjwa wapelekwe kule....imagine eti hata ubalozi wetu New Delhi walikuwa hawajui issue hii,ina maana wanajiendea endea tu.....au hizi dili wanapanga nje ya ofisi....yes yawezekana kama malipo yanafanywa dukani kwa mdosi na lisiti hupewi nini kinategemewa hapo
 
Wa-Tanzania bwana, kweli tulikuwa tumelala kwa muda mrefu sana, hizi deal za kwenda India kwa wagonjwa hazikuanza leo, ninawajua mpaka wanasiasa flani maarufu sana sasa hivi walionufaika na hizi deal,

Pale mjini kulikuwa na watu flani ambao walikuwa wame-specialize na kutengeneza documents za magirini, baadaye wanawauzia vibopa flani, ambao huenda Wizara ya Afya kuomba karatasi ya kupata kibali BOT, baadaye nina mshikaji wangu wa karibu sana aliyekuwa ame-specialize na kwenda front line, yaani pale BOT Foreign Branch kuchukua TC, wakati hakukuwa na mgonjwa yoyote, na hawa vibopa walikuwa wakimkatia karibu robo ya zile TC, huyu jamaa alikuwa na kaka mzito sana huko ndani kwa hiyo hakukuwepo mtu wa kumgusa!

Angalau siku hizi na wagonjwa wapo, then hawakuwepo kabisa na jamaa wametajirika sana na hii deal na sasa wana kinga za uanasiasa, wakuu ufisadi ulianza siku nyingi sana haya ya sasa ni marudio tu, kwa mwananchi yoyote aliyefanya kazi kazi BOT in the 80s, lazima awe anajua kuhusu hii deal na waliokuwa wanahusika, unajua ufisadi ukifikia mahali mpaka tunaanza kuwatumia wagonjwa, sasa tunaelekea kulana wenyewe kwa wenyewe kama wanyama!
 
Jamaa kama yuko India mwambie apige picha hizo sehemu wanazokaa, na pia hata picha ya hilo gazeti, hata kama limeandikwa kihindi najua kuna watu watatafsiri au watu wanaojua watu huko Bangalore.
 
mwanzo wa ngoma ni lelemama! ni rahisi kuiba wenyewe wakiwa mbali; tumeshasema na tunarudia tena kukataliwa na kuwekewa vikwazo vya THI vinahusiana moja kwa moja na safari za kutengeneza per diem za India.... yangu macho, nimepiga kelele wananiona mpinzani!! haya Tanzania wanao wanasaliti hadi wagonjwa!

Yoyo I hope that is story is not true kuwa imetiwa chumvi nyingi.. tusubiri tuone.

Mwanakijiji,

Niliwahi kuongelea hili humu JF wakati wa mchango wangu kwenye hoja ya THI lakini wengi wenu mlipuuzia lakini ukweli ni huu;

Mradi wa kupeleka wagonjwa wa moyo India ulibuniwa zamani kwa ushirikiano kati ya wizara ya afya, wizara ya fedha na Lions Club kwa lengo la kujipatia fedha kupitia migongo ya wagonjwa wa moyo. Fedha zinazoidhinishwa kugharamia matibabu, usafiri na malazi kwa wagonjwa hutolewa na serikali lakini mgonjwa huishia kuombwa achangie na hata per diem yao hawaioni. Wakati huo huo Lions Club Dar hupata sifa huko nje kuwa wao ndio wamegharamia na hivyo kupokea pesa zaidi kutoka kwa wafadhili wao.

Hivyo hizo fedha za kigeni huishia mifukoni mwa wahusika katika hizo wizara na wajanja wa Lions Club. Wagonjwa wenyewe huishia kwenye hospitali za bei ndogo na kwenye makazi ya chini kama hayo. Ndiyo maana Taasisi kama THI imepigwa vita kama tulivyoshuhudia humu JF. Nachukua nafasi kuwaomba wazalendo wenye taarifa sahihi za fedha zinazoidhinishwa wizarani watutolee data lakini najua kuna fungu maalumu huwa linatengwa mwaka hadi mwaka.
 
Dili la kupeleka wagonjwa india ni la wahindi wakihonga wataalamu wa wizara ya afya. wahindi hawa wanafanya kila hila kuuwa uwazishwaji wa kitengo cha magonjwa ya moyo muhimbili kwa miaka mingi sana. wanaongozwa na dr. kaushik wa hindumandal, kanabar regency na baadhi ya magabachori wanaojiita lion club. niliwahi kumweleza DR. masau alipofika tanzania kwamba wenzake matibabu ni dili sio huduma hivyo kamwe hawatamwacha ashamiri.
Swali zuri je ni watanzania wangapi wanauwezo wa kwenda india na kukaa kwenye hivyo vijumba wakitibiwa, je serikali haioni imeamua kutoa hukumu ya kifo. Je niwagonjwa wangapi wanaoachwa au kufa kwa kukosa huduma. Kwanini serikali isitoe ushirikiano na wataalamu wetu kwa manufaa ya watanzania masikini. viongozi wetu sio tu ni mazumbukuku bali ni mahayawani wa kutupa.

Huduma za afya tanzania ni za kutisha , wahindi wameitawala nchi mpaka kwenye afya zetu. waliwahi kuleta wahindi wenzao kwenye hospitali zao kama TMJ na Aga khan wakauwa watu wakati wa operation zikafunikwa kwani wahindi hao walikuwa sio madaktari.
Serikali ikioza matunda mabovu twala sisi.
 
Ndugu Yo Yo
Asante kwa kutuletea huu mkasa. Nikiwa kama daktari niliyekula kiapo, nisingependelea kuona majina ya wagonjwa na ugonjwa wao ukiandikwa wazi, hii inaondoa usiri amabo ni haki ya wagonjwa. Ingekuwaje kama wewe ungeandikwa kuwa una kaswende kwenye gazeti linalosomwa dunia nzima. Naomba tafadhali anayesimamia JF aondoe hii habari au afute majina ya wagonjwa. La sivyo nitaomba wagonjwa waliotajwa majina wafungue kesi.
Willy
 
Willy source ya habari imeshatajwa, unaweza ukasoma vizuri hii thread na kupata hiyo source. by the way umesahau kuweka Dr. kwenye Willy.
 
Willy source ya habari imeshatajwa, unaweza ukasoma vizuri hii thread na kupata hiyo source. by the way umesahau kuweka Dr. kwenye Willy.
Lusajo, Doctor kasahau kuweka huo utambulisho kwa sababu anawapenda sana wagonjwa wake ndio maana kasema atawashauri wafungue mashtaka, tehe! tehe! tehe!
 
ufisadi unaofanyika kwa wagonjwa india, hakuna anaependa..and those responsible wachukulie hatua KALI...na pia ufisadi anaofanya Dr. Masau wa kutolipa deni pia si lenye kufurahisha...

Kipindi cha Miaka 2 kutolipa rent nacho ni kikubwa....Wakati wengine wanatakiwa kulipa rent ya Mwaka au Miezi...Dr. Masau kafanyiwa Ihsani ya Hali ya Juu ya kuanza kazi with zero rent...Hapa tusijustify ufisadi wa sehem moja kwa mwingine...
 
Ndugu Yo Yo
Asante kwa kutuletea huu mkasa. Nikiwa kama daktari niliyekula kiapo, nisingependelea kuona majina ya wagonjwa na ugonjwa wao ukiandikwa wazi, hii inaondoa usiri amabo ni haki ya wagonjwa. Ingekuwaje kama wewe ungeandikwa kuwa una kaswende kwenye gazeti linalosomwa dunia nzima. Naomba tafadhali anayesimamia JF aondoe hii habari au afute majina ya wagonjwa. La sivyo nitaomba wagonjwa waliotajwa majina wafungue kesi.
Willy



Willy,Utafanya la maana sana kuwaomba hao wagonjwa wafungue kesi,maana nasi tusiojua nini kinaendelea katika hiyo taaluma yenu na wizara zote husika tutapata mwanga wa kujua nini kinaendelea,Binafsi naona bora hao wagonjwa wamelalamika maana wanahitaji msaada.Lah !kama kweli ni Dr ,basi wasaidie kwanza ushauri wa jinsi ya kupata matibabu ,mungu mwema wakishamaliza hilo la ugonjwa ndio uanze hilo la kufungua kesi.
 
Ndugu Yo Yo
Asante kwa kutuletea huu mkasa. Nikiwa kama daktari niliyekula kiapo, nisingependelea kuona majina ya wagonjwa na ugonjwa wao ukiandikwa wazi, hii inaondoa usiri amabo ni haki ya wagonjwa. Ingekuwaje kama wewe ungeandikwa kuwa una kaswende kwenye gazeti linalosomwa dunia nzima. Naomba tafadhali anayesimamia JF aondoe hii habari au afute majina ya wagonjwa. La sivyo nitaomba wagonjwa waliotajwa majina wafungue kesi.
Willy
Karibu JF Dr Willy.....kumbuka kuwa mtoajai wa habari hii kwa maandishi yake alikuwa na wagonjwa hawa hospitalini so nafikiri aliwauliza majina ili awe na uhakika na habari atakayoandika.....je angeulizwa majina ya wagonjwa ni akina nani si angeonekana mzushi....after all nina imani si mwanataaluma wa udaktari....lakini jana nimesikia Joddy wa BB UK akitangazwa kama ana kansa...

Hilo la kuwashitaki unaonaje kama wagonjwa wakaanza na hao wasanii waliokuwa pesa yao mpaka magazeti ya kule India kuwaandika kama omba omba.....

Wewe kama Dr Willy......hili suala unalionaje la kupekea wagonjwa nje kiusanii? tuachie mbali taaluma ya kutaja majina..
 
Wajameni hii taarifa imenigusa. Utakumbuka nilichangia sana ile saga ya THI ila sijui kama mchango wangu ulisomwa na wengi maana huwa nashagaa reply zangu au michango huwa siioni nikishapost. Huenda moderator ana edit lakini huwa naamini naandika ya msingi sana. Nakuomba moderator uwe unaweka mchango wangu wanajamii wauone. June 25-7th July 2005 nilimpeleka mwanangu India through Regency -Lions Club. Alikuja Dr. mmoja toka Narayana hospital kucheck watoto wenye matatizo ya moyo kwa lengo la kuwasaidia bure upasuaji Narayana Hospital. Mwanangu alionekana serious na alitakiwa apelekwe ila mizwengwe ikaanza pale Regency walitaka wapeleke watu wao. Nilipigana kufa na kupona ikabidi tajiri mmoja mhindi alikuwa anafahamiana na mume wangu na pengine ni mchangiaji wa Lions Club akatusaidia tukapata chance ya kwenda Narayana. Hata hivyo, tulilazimishwa na Dr. Kanabar mwenyewwe tulipie usafiri return ticket na malazi Narayana. tulijitahidi tukapata pesa ila kama alivyosema mwenzetu tulilazimishwa kwenda kununua ticket kwa agent wa Regency. Tulipofika India tulikuwa na Dr. Mhindi mkuu wa msafara ambaye suprisingly THI wanamtumia kuwafanyia vipimo vya moyo (visiting consultant) wakati ameajiriwa na regency. Kitendawili hicho. Tulipokuwa India wagonjwa waligawiwa dola 200 za kujikimu. Kwa kuwa mimi ni msomi na mdadisi niliweza kuona documents za malipo za wagonjwa na kuwa wote walikuwa full paid including mimi niliyetakiwa kuchangia. Moyo uliniiuma sana. Na kila mzazi niliyeongea naye mwenye mtoto mgonjwa alisema alilipa chchote kidogo kupata nafasi ile. Ni wachache tu walikuwa wamepata chance bila kutoa chochote. Nimesema wahindi serikali imewakumbatia sana na kwa sababu wanaweza ku finanance uchaguzi wa sisiemu na wananchi tunadharaulika.

Huyo JK wa kasi mpya, nguvu mpya na ari mpya amelenga wapi wakati well being ya watanzania inadidimia. Huo MKUKUTA ni wimbo wa taifa usio na washangiliaji.

Kuhusu kulala ni hostel hakuna hata kabati. mnabwaga chumbani kama mende. Usafi India ni ndoto,, kunguni kila kona. Chakula hutii mdomoni. Niliteseka sikula nilirudi nyumbani sitamaniki ila tu nikafurahi mwanangu alifanyiwa operation na amepona kabisa. Tufanye maandamano tulaani kuitesa THI. Nawasilisha wakuu.
 
Wajameni hii taarifa imenigusa. Utakumbuka nilichangia sana ile saga ya THI ila sijui kama mchango wangu ulisomwa na wengi maana huwa nashagaa reply zangu au michango huwa siioni nikishapost. Huenda moderator ana edit lakini huwa naamini naandika ya msingi sana. Nakuomba moderator uwe unaweka mchango wangu wanajamii wauone. June 25-7th July 2005 nilimpeleka mwanangu India through Regency -Lions Club. Alikuja Dr. mmoja toka Narayana hospital kucheck watoto wenye matatizo ya moyo kwa lengo la kuwasaidia bure upasuaji Narayana Hospital. Mwanangu alionekana serious na alitakiwa apelekwe ila mizwengwe ikaanza pale Regency walitaka wapeleke watu wao. Nilipigana kufa na kupona ikabidi tajiri mmoja mhindi alikuwa anafahamiana na mume wangu na pengine ni mchangiaji wa Lions Club akatusaidia tukapata chance ya kwenda Narayana. Hata hivyo, tulilazimishwa na Dr. Kanabar mwenyewwe tulipie usafiri return ticket na malazi Narayana. tulijitahidi tukapata pesa ila kama alivyosema mwenzetu tulilazimishwa kwenda kununua ticket kwa agent wa Regency. Tulipofika India tulikuwa na Dr. Mhindi mkuu wa msafara ambaye suprisingly THI wanamtumia kuwafanyia vipimo vya moyo (visiting consultant) wakati ameajiriwa na regency. Kitendawili hicho. Tulipokuwa India wagonjwa waligawiwa dola 200 za kujikimu. Kwa kuwa mimi ni msomi na mdadisi niliweza kuona documents za malipo za wagonjwa na kuwa wote walikuwa full paid including mimi niliyetakiwa kuchangia. Moyo uliniiuma sana. Na kila mzazi niliyeongea naye mwenye mtoto mgonjwa alisema alilipa chchote kidogo kupata nafasi ile. Ni wachache tu walikuwa wamepata chance bila kutoa chochote. Nimesema wahindi serikali imewakumbatia sana na kwa sababu wanaweza ku finanance uchaguzi wa sisiemu na wananchi tunadharaulika.

Huyo JK wa kasi mpya, nguvu mpya na ari mpya amelenga wapi wakati well being ya watanzania inadidimia. Huo MKUKUTA ni wimbo wa taifa usio na washangiliaji.

Kuhusu kulala ni hostel hakuna hata kabati. mnabwaga chumbani kama mende. Usafi India ni ndoto,, kunguni kila kona. Chakula hutii mdomoni. Niliteseka sikula nilirudi nyumbani sitamaniki ila tu nikafurahi mwanangu alifanyiwa operation na amepona kabisa. Tufanye maandamano tulaani kuitesa THI. Nawasilisha wakuu.
Pole sana dada maane......lol inaleta hasira sana ati yaani mgonjwa analipiwa kila kitu alafu jamaa wanaomba rushwa mgonjwa anatoa na bado hapati malazi mazuri kama hawa wenzetu......hivi JK mambo kama haya ina maana hayaoni ila ya mamiss yanaonekana.....afya ndio msingi wa uchumi kama huna afya bora hizo pro[aganda zake za kasi na vijitu gani haziwezi kufanikiwa.......kama afya ya wapiga kura wake inachezewa namna hii tunakwenda wapi?

Imekuwa vizuri wewe umefika kwenye hospitali hio ya Narayana wengine walitaka ushahidi wa hili.....raisi Jk ni wakati wako sasa utu tu miaka tuwili tulitobaki uwe mcha Mungu basi...
 
ufisadi unaofanyika kwa wagonjwa india, hakuna anaependa..and those responsible wachukulie hatua KALI...na pia ufisadi anaofanya Dr. Masau wa kutolipa deni pia si lenye kufurahisha...

Kipindi cha Miaka 2 kutolipa rent nacho ni kikubwa....Wakati wengine wanatakiwa kulipa rent ya Mwaka au Miezi...Dr. Masau kafanyiwa Ihsani ya Hali ya Juu ya kuanza kazi with zero rent...Hapa tusijustify ufisadi wa sehem moja kwa mwingine...


Chuma kuna kesi mahakamani, kesi ambayo Mahakama ya Rufaa inasema isikilizwe kwanza; kwanini hutaki kuacha sheria ifuatwe? Kwa vile mtu anadaiwa au hataki kulipa haina maana hana haki ya kusikilizwa sababu yake. Ndio maana tuna mahakama. Au unataka alipe tu kwa vile anadaiwa na asipate nafasi ya kusikilizwa mahakamani? Yaani mtu akikudai na unajua kuwa kuna vitu ameongeza au hasemi kweli usiende mahakamani wewe lipa tu yaishe? Hatuishi kwenye utawala wa kiimla, tuna mahakama.

Na sitoshangaa when everything is said and done, NSSF wataoneshwa makosa yao na watatakiwa kufanya matengenezo na vipengele vya mkataba vya kinyonyaji na kikandamizaji vitaoneshwa si halali.

Kama vile NSSF walivyooneshwa kuwa ni wababe, walijipa mamlaka ya kujitungia sheria yao na kwenda kutishia kuwaondoa wagonjwa hospitali bila amri halali ya mahakama ndivyo hivyo hivyo wataooneshwa Dr. Dau na wenzake kuwa wameionea taasisi hiyo kwa na haki Dr. Masau hatakiwi kulipa na NSSF itatakiwa ilipe kwa usumbufu mkubwa kwa hospitali, wagonjwa na kukosesha mapato taasisi hiyo.

Huoni haja ya kusubiri kesi ya msingi mahakamani kumalizia? au wewe unataka walipe tu na kesi iliyopo isiendelee?
 
ufisadi unaofanyika kwa wagonjwa india, hakuna anaependa..and those responsible wachukulie hatua KALI...na pia ufisadi anaofanya Dr. Masau wa kutolipa deni pia si lenye kufurahisha...

Kipindi cha Miaka 2 kutolipa rent nacho ni kikubwa....Wakati wengine wanatakiwa kulipa rent ya Mwaka au Miezi...Dr. Masau kafanyiwa Ihsani ya Hali ya Juu ya kuanza kazi with zero rent...Hapa tusijustify ufisadi wa sehem moja kwa mwingine...

Chuma

What crap.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom