The road towards 2010 Elections

Kati ya hawa nani atafaa kutuongoza 2010-2015?

  • Edward Lowassa

    Votes: 0 0.0%
  • Dr. Slaa

    Votes: 7 38.9%
  • Prof. Lipumba

    Votes: 0 0.0%
  • Mizengo Pinda

    Votes: 5 27.8%
  • Samwel Sitta

    Votes: 0 0.0%
  • Jakaya Kikwete

    Votes: 2 11.1%
  • Mark Mwandosya

    Votes: 2 11.1%
  • Harisson Mwakyembe

    Votes: 2 11.1%
  • None of The above

    Votes: 0 0.0%

  • Total voters
    18
  • Poll closed .
Ni kweli Kalamu mpaka sasa wanaopinga pendekezo hili hawajatoa jina mbadala kwa hiyo kuonyesha dhahiri kwamba Dr. Slaa anakubalika na wengi au hakuna majina mengine yanayoonekana yanafaa kumzidi yeye. Kuna umuhimu mkubwa wa katiba yetu kubadilishwa ili kukidhi haja ya mfumo wa vyama vingi na kuongeza uwazi zaidi katika kuwachunguza au kuwashitaki viongozi mbalimbali ambao watatuhumiwa kuwa mabadhirifu wa mali za umma. Ukiangalia kwa undani zaidi utaona mtu ambaye kwa kiasi kikubwa amechangia katika kuifahamisha jamii ya CCM kuhusiana na Ufisadi unaofanywa na viongozi wa Serikali kutoka CCM ni Dr. Wilbroad Slaa.

Kwa hiyo hii ndiyo sifa pekee inayomfanya aonekane anafaa kwa uraisi 2010? Je, historia ya utendaji wake wa kazi na mafanikio vipi, kuna mtu anayeijua? Pia na historia ya mahusiano yake na watu mbalimbali, kuna yeyote anayeijua?
 
Kwa hiyo hii ndiyo sifa pekee inayomfanya aonekane anafaa kwa uraisi 2010? Je, historia ya utendaji wake wa kazi na mafanikio vipi, kuna mtu anayeijua? Pia na historia ya mahusiano yake na watu mbalimbali, kuna yeyote anayeijua?


Haya ndio tunayotaka kuyajua kwa uhakika; sio kwa Dr. Slaa tu, bali na hao wengine wote watakaojitokeza kugombea urais katika uchaguzi ujao.

Ni muhimu kabisa sasa, waTanzania tuwe na tabia ya kuwahoji watu wanaowania uongozi kabla hatujawachagua katika nafasi za kutuongoza.

Utamwajiri vipi mtu hata bila ya kumsaili? Akina Hillary na Obama tumeona wanavyohenya katika 'interview', kwa nini wa kwetu wawe tunawaajili chee tu?
 
Yes Slaa for Presidency na anafaa kabisa kwenye hilo. Slaa ni kiongozi ambaye kwa uzalendo wake ameweza kufichua maovu mbalimbali yanayofanywa na Majambazi wa CCM.Nilishasema huko nyuma CCM ni chama kinachonuka uvundo wa RUSHWA. Hell NO to CCM, CHAMA CHA MAJAMBAZI.

Mazee GQ,

naona umekata tamaa kabisa na CCM kama mimi hapa!
 
Mazee GQ,

naona umekata tamaa kabisa na CCM kama mimi hapa!

Kukata tamaa ni understatement, CCM mimi si tu kwamba nimeichoka bali ingekuwa ni ridhaa yangu ningefurahi kuona kinafutwa au kuvunjwa na kuundwa upya.

CCM inanuka zaidi ya harufu ya kinyesi au mzoga uliooza wenye kutoa harufu kali na haifai kabisa kuiongoza nchi yetu. Kama ni kweli sote tunataka mabadiliko ya kweli nchini mwetu basi hatuna budi kuhakikisha CCM inang'oka katika kazi zote za uongozi. CCM Stinks.

Nyani,
Hizo ni kati ya sifa ambazo wengi tunazifahamu kuhusiana na Dr. Slaa lakini nadhani ingekuwa vizuri wengine wanaomjua vizuri katika utendaji wake waweke wazi hapa ili sote tuzidi kumjua.

Kitu alichokifanya Dr. Slaa cha kuibua maovu ya viongozi mbalimbali hakuna kiongozi wa CCM ambaye alishathubutu kukifanya na hii inamfanya wengi wetu tumuone kama Mkombozi.

Sera za CCM ni kuficha maovu, kulindana na kusaidia kuwezesha Ufisadi ufanikiwe. MAFISADI wote ambao wamejiuzulu serikalini mpaka leo hii wapo ndani ya CCM bila ya hata kuchukuliwa hatua zozote. CCM kweli ni Chama Cha Mafisadi na Majambazi.
 
Kukata tamaa ni understatement, CCM mimi si tu kwamba nimeichoka bali ingekuwa ni ridhaa yangu ningefurahi kuona kinafutwa au kuvunjwa na kuundwa upya. CCM inanuka zaidi ya harufu ya kinyesi au mzoga uliooza wenye kutoa harufu kali na haifai kabisa kuiongoza nchi yetu. Kama ni kweli sote tunataka mabadiliko ya kweli nchini mwetu basi hatuna budi kuhakikisha CCM inang'oka katika kazi zote za uongozi. CCM Stinks.

Nyani,
Hizo ni kati ya sifa ambazo wengi tunazifahamu kuhusiana na Dr. Slaa lakini nadhani ingekuwa vizuri wengine wanaomjua vizuri katika utendaji wake waweke wazi hapa ili sote tuzidi kumjua. Kitu alichokifanya Dr. Slaa cha kuibua maovu ya viongozi mbalimbali hakuna kiongozi wa CCM ambaye alishathubutu kukifanya na hii inamfanya wengi wetu tumuone kama Mkombozi. Sera za CCM ni kuficha maovu, kulindana na kusaidia kuwezesha Ufisadi ufanikiwe. MAFISADI wote ambao wamejiuzulu serikalini mpaka leo hii wapo ndani ya CCM bila ya hata kuchukuliwa hatua zozote. CCM kweli ni Chama Cha Mafisadi na Majambazi.

Mimi nakuunga mkono hapa Geeque kwa ulichofanya hapa. Umeweka hoja na pendekezo lako kwa yule unayemuona kuwa anafaa kusaidia watanzania kutoka kwenye makucha ya kifisadi ya ccm.

Kama kawaida ya JF, hoja za kuunga mkono au kupinga zitawekwa hapa ili kujadiliwa na membaz. So far sijaona hoja za kupinga kwa nini Slaa asiwe presidaa. Hata hivyo maswali pia ya kina kumhusu itabidi yaulizwe. Mwishoni watanzania inabidi wapate the best president ambaye atapitia scrutiny ya kutosha.

Asante sana kwa hii thread!
 
Tatizo la watz wanachagua chama na si mtu, Mrema enzi zile he had a proven record kwa utendaji wake akagombea matokeo yake hawakumpa kura za kumuwezesha kuingia ikulu.

Watz bado hawajaamka tshirt, kofia na wekundu tayari wanapagawa bila kujua ivyo vyote vitawatokea puani
 
Muda wa Slaa kugombea urais bado,akipewa urais sawa na wabunge atawapata wapi jamani? Tusimhadae mpiganaji wetu.

Lakini kwa ushauri wangu 2010 Mbowe akae pembeni Slaa akiwakilishe chama ktk nafasi ya urais. Hata kama hataupata urais.
 
Mimi nakuunga mkono hapa Geeque kwa ulichofanya hapa. Umeweka hoja na pendekezo lako kwa yule unayemuona kuwa anafaa kusaidia watanzania kutoka kwenye makucha ya kifisadi ya ccm.

Kama kawaida ya JF, hoja za kuunga mkono au kupinga zitawekwa hapa ili kujadiliwa na membaz. So far sijaona hoja za kupinga kwa nini Slaa asiwe presidaa. Hata hivyo maswali pia ya kina kumhusu itabidi yaulizwe. Mwishoni watanzania inabidi wapate the best president ambaye atapitia scrutiny ya kutosha.

Asante sana kwa hii thread!

Mimi napingana na hilo wazo la kumpendekeza Dr. Slaa kuwa mgombea uraisi. Ku-focus kwenye uraisi pekee ni moja ya sababu kubwa ya wapinzani kushindwa kwenye kila uchaguzi. Ufumbuzi wa matatizo ya mtanzania hautatokana na upinzani kuingia ikulu, bali kwa kubadilisha mfumo mzima wa kiutawala. Ni vema tukaelewa yafuatayo;
  1. Nchi haijengwi na mtu mmoja na ndio maana Nyerere yalimshinda. Kwa hiyo kama mfumo wa kiutawala hautabadilishwa na kuondoa madaraka makubwa aliyonayo raisi na serikali yake hivi sasa, na kuyahamishia bungeni, mahakamani na kwa wananchi, yeyote yule atakayeingia anaweza akaifuja nchi bila kipingamizi.
  2. Hadi hivi sasa hakuna dalili zozote zinazoonyesha uwezekano wa CCM kushindwa kwenye kinyang'anyiro cha uraisi 2010, hata baada ya kulipuliwa kwa mafisadi wote wakiwa wanaCCM. Uchaguzi wa hivi karibuni Kiteto inatoa picha ya ugumu uliopo.
  3. Mgawanyiko na tamaa katika kambi ya upinzani ni kikwazo kikubwa sana kwao kupata ushindi. Hata kama Nyerere angefufuka na kuwa mgombea wa chama kimojawapo cha upinzani, bado ingekuwa vigumu kwao kuunganisha nguvu zao kuing'oa CCM.
  4. Uongozi mbovu ndani ya vyama vya upinzani nao ni kikwazo kikubwa katika kuwavutia wasomi na wafanyabiashara wengi ambao wanakerwa na CCM. Ni muhimu kutatua masuala kama ya udini, ukabila na umungu-mtu ndani ya vyama ili kuondoa hali ya hivi vyama kuwa na ushabiki wa kimajimbo na wenye upeo mwembamba.
  5. Nyerere alisema upinzani wa kiukweli TZ utatoka ndani ya CCM, na mimi nakubaliana naye kabisaa hata baada ya kufariki. Hili litawezekana kwa CCM wenyewe kupingana au kwa wapinzani kuwa na vyama ambavyo vitawavutia walioCCM kuhamia kwao. Hivi sasa la awali la CCM kupingana linakaribia linalohitajika ni kwa wapinzani kuunda mazingira yatakayoweza kuwavutia wanaCCM kuhamia kwao.
  6. Msisitizo kwa upinzani uwe katika kuandaa wabunge wengi iwezekanavyo. Na hii ndio sababu kubwa ya kupinga kumuingiza Dr. Slaa kwenye kinyang'anyiro cha uraisi. Uwezekano wa yeye kushinda ubunge ni mkubwa kuliko uraisi na isingekuwa vema akakosekana kwenye ulingo wa kisiasa kwa miaka 5, kama ilivyokuwa kwa Mrema, na kushindwa kufanya yale tuliyoona anaweza kuyafanya akiwa bungeni. Kila mpinzani aliye na uwezo wa kushinda ubunge, aanze kujengwa hivi sasa kwenye majimbo yao ili agombee ubunge na kuimarisha upinzani bungeni.
  7. Upinzani wapunguze hili la ku-focus zaidi kwenye uraisi, na kutumia rasilimali zao kwenye ubunge. Kwa mfano CHADEMA walitumia zaidi ya TShs 220millioni (30% ya pesa waliyokuwa nayo) kwenye kukodisha helicopter tu. Lakini jumla ya pesa yote walizowapa wagombea wa ubunge wao ilikuwa ni TShs. 59 millioni tu (8% tu). Kama wangewekeza zaidi kwenye wabunge labda watu kama Bob Makani wangekuwa wabunge hivi sasa.
Changamoto langu kwa vyama vya upinzani ni kuungana na kuwekeza zaidi kwenye ubunge maana kwa hali ilivyo hivi sasa, sio rahisi kuing'oa CCM in 2010.
 
Mimi napingana na hilo wazo la kumpendekeza Dr. Slaa kuwa mgombea uraisi. Ku-focus kwenye uraisi pekee ni moja ya sababu kubwa ya wapinzani kushindwa kwenye kila uchaguzi. Ufumbuzi wa matatizo ya mtanzania hautatokana na upinzani kuingia ikulu, bali kwa kubadilisha mfumo mzima wa kiutawala. Ni vema tukaelewa yafuatayo;

Ufumbuzi wa matatizo ya watanzania ni kubadilisha mfumo mzima wa utawala ikiwemo uraisi wa Tanzania toka kwa mafisadi na wezi wa ccm kwenda kwa upinzani.

Katika hili naona umeeleza vizuri zaidi ya udaku huo mwingine ulioweka kuhusu matumizi ya Chadema kwenye uchaguzi mkuu.
 
Mimi napingana na hilo wazo la kumpendekeza Dr. Slaa kuwa mgombea uraisi. Ku-focus kwenye uraisi pekee ni moja ya sababu kubwa ya wapinzani kushindwa kwenye kila uchaguzi. Ufumbuzi wa matatizo ya mtanzania hautatokana na upinzani kuingia ikulu, bali kwa kubadilisha mfumo mzima wa kiutawala. Ni vema tukaelewa yafuatayo;
]

Contradiction!

Huwezi kubadili mfumo mzima wa utawala kama hutabadili institution ya urais ambayo inateua mawaziri, wakurugenzi, mabalozi, wakuu wa wilaya nk. Hivyo wapinzani lazima walenge pia kumwondoa Kikwete 2010 na CCM.

Asha
 
[*]Nchi haijengwi na mtu mmoja na ndio maana Nyerere yalimshinda. Kwa hiyo kama mfumo wa kiutawala hautabadilishwa na kuondoa madaraka makubwa aliyonayo raisi na serikali yake hivi sasa, na kuyahamishia bungeni, mahakamani na kwa wananchi, yeyote yule atakayeingia anaweza akaifuja nchi bila kipingamizi.
]


Tofauti ya kuwa na mtu mmoja mzuri inaonekana bayana ukimlinganisha Nyerere na Kikwete. Rais ana mamlaka makubwa ya utuezi na utendaji. Ukiwa na Rais msanii kama Kikwete utakuwa na Mawaziri kama Chenge, Mramba, Lowassa na wenzake lakini ukichagua Rais bora utapata safu nzuri ya uongozi

Asha
 

[*]Hadi hivi sasa hakuna dalili zozote zinazoonyesha uwezekano wa CCM kushindwa kwenye kinyang'anyiro cha uraisi 2010, hata baada ya kulipuliwa kwa mafisadi wote wakiwa wanaCCM. Uchaguzi wa hivi karibuni Kiteto inatoa picha ya ugumu uliopo.
[*]Mgawanyiko na tamaa katika kambi ya upinzani ni kikwazo kikubwa sana kwao kupata ushindi. ]


Unajichanganya!

Kama unasema wapinzani hawatashinda urais 2010 kwa kuwa wameshindwa Ubunge Kiteto kwanini unawashauri tena kwamba ni vyema wakagombea Ubunge? Kwanini ushiwashauri wajenge mazingira ya kushinda vyote ama kutoshiriki uchaguzi kabisa? Au unataka kuhamamisha attention yao kwa Kikwete?

Mgawanyo wa upinzani umeouna wapi wakati sasa wana ushirikiano na wamekuwa wakisimamisha mgombea mmoja katika hizi chaguzi za hivi karibuni? Kipimo chako cha mgawanyiko huo ni kipi wakati wapinzani wanashirikaina katika mambo mbalimbali?

Asha
 
[]
[*]Uongozi mbovu ndani ya vyama vya upinzani nao ni kikwazo kikubwa katika kuwavutia wasomi na wafanyabiashara wengi ambao wanakerwa na CCM. Ni muhimu kutatua masuala kama ya udini, ukabila na umungu-mtu ndani ya vyama ili kuondoa hali ya hivi vyama kuwa na ushabiki wa kimajimbo na wenye upeo mwembamba.
]

Acha generalization wewe?

Uongozi mbovu upi? Wa Katibu Mkuu Dr Slaa wa CHADEMA au Mwenyekiti Lipumba wa CUF?. Wasomi na wafanyabiashara hawaachi kujiunga na upinzani kwa kuwa kuna uongozi mbovu bali ni hofu tu ya kulinda maslahi yao. Mbona Msomi Prof Baregu amejiunga CHADEMA? Au mfanyabiashara Ndesamburo mbona anafanya vizuri tu katika siasa za upinzani.

Ushabiki wa kimajimbo gani huo ulioko kwenye vyama?

Mi naona wewe kazi yako ni kupandikiza hofu tu kwa wananchi ili waogope kujiunga na upinzani.

Asha
 
Unajichanganya!

Kama unasema wapinzani hawatashinda urais 2010 kwa kuwa wameshindwa Ubunge Kiteto kwanini unawashauri tena kwamba ni vyema wakagombea Ubunge? Kwanini ushiwashauri wajenge mazingira ya kushinda vyote ama kutoshiriki uchaguzi kabisa? Au unataka kuhamamisha attention yao kwa Kikwete?

Mgawanyo wa upinzani umeouna wapi wakati sasa wana ushirikiano na wamekuwa wakisimamisha mgombea mmoja katika hizi chaguzi za hivi karibuni? Kipimo chako cha mgawanyiko huo ni kipi wakati wapinzani wanashirikaina katika mambo mbalimbali?

Asha

Huyu hana lolote zaidi ya chuki zake na propaganda zake za kikabila. Mpe shule dada Asha kwani mimi nimekamata popcorn zangu tayari kabisa kwa shule ya kutosha hapa.
 
Ufumbuzi wa matatizo ya watanzania ni kubadilisha mfumo mzima wa utawala ikiwemo uraisi wa Tanzania toka kwa mafisadi na wezi wa ccm kwenda kwa upinzani. Katika hili naona umeeleza vizuri zaidi ya udaku huo mwingine ulioweka kuhusu matumizi ya Chadema kwenye uchaguzi mkuu.

Nimeweka kwenye posting yangu points kama 7 hivi. Ningefurahi sana kama utajibu hoja kwa hoja. Matumizi ya CHADEMA nenda kwenye site yao http://www.chadema.net/uchaguzi/gharama.php
utapata jibu. Hili ni muhimu sana kwa mafanikio ya vyama kwenye chaguzi.
 
[[*]Nyerere alisema upinzani wa kiukweli TZ utatoka ndani ya CCM, na mimi nakubaliana naye kabisaa hata baada ya kufariki. Hili litawezekana kwa CCM wenyewe kupingana au kwa wapinzani kuwa na vyama ambavyo vitawavutia walioCCM kuhamia kwao. Hivi sasa la awali la CCM kupingana linakaribia linalohitajika ni kwa wapinzani kuunda mazingira yatakayoweza kuwavutia wanaCCM kuhamia kwao.
[*][]

Dr Slaa alitoka CCM; kama assumpition yako juu ya kauli ya Nyerere ni sahihi kwanini bado unampinga Dr Slaa kuwa hafai? Mbona wanaCCM wanahamia tu? umewaona wakina Pesha, Balozi Ngaiza etc

Asha
 
Nimeweka kwenye posting yangu points kama 7 hivi. Ningefurahi sana kama utajibu hoja kwa hoja. Matumizi ya CHADEMA nenda kwenye site yao http://www.chadema.net/uchaguzi/gharama.php
utapata jibu. Hili ni muhimu sana kwa mafanikio ya vyama kwenye chaguzi.

Wewe achana na rants za chuki za kikabila. Zaidi huna jipya maana imejulikana muda mwingi hapa kuwa ni CHADEMA peke yao wenye taarifa za matumizi yao kwenye mtandao.

Next....
 
.
[*]Upinzani wapunguze hili la ku-focus zaidi kwenye uraisi, na kutumia rasilimali zao kwenye ubunge. Kwa mfano CHADEMA walitumia zaidi ya TShs 220millioni (30% ya pesa waliyokuwa nayo) kwenye kukodisha helicopter tu. Lakini jumla ya pesa yote walizowapa wagombea wa ubunge wao ilikuwa ni TShs. 59 millioni tu (8% tu). Kama wangewekeza zaidi kwenye wabunge labda watu kama Bob Makani wangekuwa wabunge hivi sasa.[/LIST]Changamoto langu kwa vyama vya upinzani ni kuungana na kuwekeza zaidi kwenye ubunge maana kwa hali ilivyo hivi sasa, hakuna atakayemng'oa CCM in 2010.

We kweli kubwa jinga!

1. Kwani hiyo helikopta ilikuwa inafanya kampeni Kenya? Si ilikuwa inapita maeneo ya wagombea ubunge na udiwani ikiwa imembeba mgombea Urais na Mgombea ubunge wa eneo husika kupiga kampeni? Sasa maanake ni kwamba hizo milioni 200 za helikopta zimetumika pia na wagombea ubunge kwa kuwa walipanda helikopta kwenda kwa wapiga kura wao. Zitto na Mnyika si waliwahi kusema kuwa walitumia helikopta ilipokwenda kwenye majimbo yao?

2. Hebu tumia akili, hizo milioni 59 walizopewa wagombea ubunge ni zile walizopewa fedha taslimu. Hizo milioni 500 zingine hazikutumiwa na mgombea urais binafsi. Utaona humu kulikuwa na fedha za mafunzo ya wagombea ubunge, kutengeneza vifaa vya kampeni na kufanya kampeni za vyombo vya habari nk. Vyote hivi vingine vilikuwa vinatumiwa na wagombea ubunge wenyewe moja kwa moja na vingine vililenga kujenga taswira ya CHADEMA. Na ukijenga taswira ya CHADEMA unawasaidia pia wagombea ubunge katika maeneo yao.

Sasa nieleze, kati ya hizo milioni 700 CHADEMA ilizotumia kwenye kampeni zake, ni zipi ambazo Freeman Mbowe kama mgombea urais alitumia mwenyewe; ni zipi hazikutumika katika majimbo. Kwani mgombea urais alifanya kampeni zake katika sayari ya Mars? Kazi yake si ilikuwa kuzunguka nchi nzima kuwanadi wagombea wake? Hebu acha kuwakatisha tamaa watanzania kuunga mkono upinzani.

Ni kweli ni muhimu kuweka mkazo kwenye ubunge, lakini si kwa unavyoonyesha wewe. Wewe hukosoi kwa kujenga, unabwabwaja kwa lengo la kuchafua.

Au ndio maana ya kubwa jinga? Hivi kwani nini umechagua jina hilo?

Asha
 
We kweli kubwa jinga!

1. Kwani hiyo helikopta ilikuwa inafanya kampeni Kenya? Si ilikuwa inapita maeneo ya wagombea ubunge na udiwani ikiwa imembeba mgombea Urais na Mgombea ubunge wa eneo husika kupiga kampeni? Sasa maanake ni kwamba hizo milioni 200 za helikopta zimetumika pia na wagombea ubunge kwa kuwa walipanda helikopta kwenda kwa wapiga kura wao. Zitto na Mnyika si waliwahi kusema kuwa walitumia helikopta ilipokwenda kwenye majimbo yao?

2. Hebu tumia akili, hizo milioni 59 walizopewa wagombea ubunge ni zile walizopewa fedha taslimu. Hizo milioni 500 zingine hazikutumiwa na mgombea urais binafsi. Utaona humu kulikuwa na fedha za mafunzo ya wagombea ubunge, kutengeneza vifaa vya kampeni na kufanya kampeni za vyombo vya habari nk. Vyote hivi vingine vilikuwa vinatumiwa na wagombea ubunge wenyewe moja kwa moja na vingine vililenga kujenga taswira ya CHADEMA. Na ukijenga taswira ya CHADEMA unawasaidia pia wagombea ubunge katika maeneo yao.

Sasa nieleze, kati ya hizo milioni 700 CHADEMA ilizotumia kwenye kampeni zake, ni zipi ambazo Freeman Mbowe kama mgombea urais alitumia mwenyewe; ni zipi hazikutumika katika majimbo. Kwani mgombea urais alifanya kampeni zake katika sayari ya Mars? Kazi yake si ilikuwa kuzunguka nchi nzima kuwanadi wagombea wake? Hebu acha kuwakatisha tamaa watanzania kuunga mkono upinzani.

Ni kweli ni muhimu kuweka mkazo kwenye ubunge, lakini si kwa unavyoonyesha wewe. Wewe hukosoi kwa kujenga, unabwabwaja kwa lengo la kuchafua.

Au ndio maana ya kubwa jinga? Hivi kwani nini umechagua jina hilo?

Asha

Dada Asha,

Huyu hawezi kukuelewa maana hili somo limetolewa hapa mara kwa mara ila chuki zake na mitizamo yake ya kikabila vinamfanya asione haya yote!
 
Wewe achana na rants za chuki za kikabila. Zaidi huna jipya maana imejulikana muda mwingi hapa kuwa ni CHADEMA peke yao wenye taarifa za matumizi yao kwenye mtandao.

Next....

Mimi nashusha mavitus tu. Hayo ya chuki na ukabila unayaleta wewe na nitawaachia wasomaji wengine wenye fikira nzuri wa-tu-judge. Wakishasoma na ku-comment then nitajibu hoja including za bibie Asha. Naipost tena hoja yangu kwa manufaa ya wasomaji.




Mimi napingana na hilo wazo la kumpendekeza Dr. Slaa kuwa mgombea uraisi. Ku-focus kwenye uraisi pekee ni moja ya sababu kubwa ya wapinzani kushindwa kwenye kila uchaguzi. Ufumbuzi wa matatizo ya mtanzania hautatokana na upinzani kuingia ikulu, bali kwa kubadilisha mfumo mzima wa kiutawala. Ni vema tukaelewa yafuatayo;
  1. Nchi haijengwi na mtu mmoja na ndio maana Nyerere yalimshinda. Kwa hiyo kama mfumo wa kiutawala hautabadilishwa na kuondoa madaraka makubwa aliyonayo raisi na serikali yake hivi sasa, na kuyahamishia bungeni, mahakamani na kwa wananchi, yeyote yule atakayeingia anaweza akaifuja nchi bila kipingamizi.
  2. Hadi hivi sasa hakuna dalili zozote zinazoonyesha uwezekano wa CCM kushindwa kwenye kinyang'anyiro cha uraisi 2010, hata baada ya kulipuliwa kwa mafisadi wote wakiwa wanaCCM. Uchaguzi wa hivi karibuni Kiteto inatoa picha ya ugumu uliopo.
  3. Mgawanyiko na tamaa katika kambi ya upinzani ni kikwazo kikubwa sana kwao kupata ushindi. Hata kama Nyerere angefufuka na kuwa mgombea wa chama kimojawapo cha upinzani, bado ingekuwa vigumu kwao kuunganisha nguvu zao kuing'oa CCM.
  4. Uongozi mbovu ndani ya vyama vya upinzani nao ni kikwazo kikubwa katika kuwavutia wasomi na wafanyabiashara wengi ambao wanakerwa na CCM. Ni muhimu kutatua masuala kama ya udini, ukabila na umungu-mtu ndani ya vyama ili kuondoa hali ya hivi vyama kuwa na ushabiki wa kimajimbo na wenye upeo mwembamba.
  5. Nyerere alisema upinzani wa kiukweli TZ utatoka ndani ya CCM, na mimi nakubaliana naye kabisaa hata baada ya kufariki. Hili litawezekana kwa CCM wenyewe kupingana au kwa wapinzani kuwa na vyama ambavyo vitawavutia walioCCM kuhamia kwao. Hivi sasa la awali la CCM kupingana linakaribia linalohitajika ni kwa wapinzani kuunda mazingira yatakayoweza kuwavutia wanaCCM kuhamia kwao.
  6. Msisitizo kwa upinzani uwe katika kuandaa wabunge wengi iwezekanavyo. Na hii ndio sababu kubwa ya kupinga kumuingiza Dr. Slaa kwenye kinyang'anyiro cha uraisi. Uwezekano wa yeye kushinda ubunge ni mkubwa kuliko uraisi na isingekuwa vema akakosekana kwenye ulingo wa kisiasa kwa miaka 5, kama ilivyokuwa kwa Mrema, na kushindwa kufanya yale tuliyoona anaweza kuyafanya akiwa bungeni. Kila mpinzani aliye na uwezo wa kushinda ubunge, aanze kujengwa hivi sasa kwenye majimbo yao ili agombee ubunge na kuimarisha upinzani bungeni.
  7. Upinzani wapunguze hili la ku-focus zaidi kwenye uraisi, na kutumia rasilimali zao kwenye ubunge. Kwa mfano CHADEMA walitumia zaidi ya TShs 220millioni (30% ya pesa waliyokuwa nayo) kwenye kukodisha helicopter tu. Lakini jumla ya pesa yote walizowapa wagombea wa ubunge wao ilikuwa ni TShs. 59 millioni tu (8% tu). Kama wangewekeza zaidi kwenye wabunge labda watu kama Bob Makani wangekuwa wabunge hivi sasa.
Changamoto langu kwa vyama vya upinzani ni kuungana na kuwekeza zaidi kwenye ubunge maana kwa hali ilivyo hivi sasa, hakuna atakayemng'oa CCM in 2010.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom