The Richest Man In Africa: Kila Utajiri una Ukafiri nyuma yake

View attachment 815761
me namaswali kdogo ukimaliza historia utanijibu ila wakati haya yanatokea ulikuwa wap?,kama uliadisiwa hauoni kuna makusudi zinafanywa kuchafua watu na nchi za watu?,na kama ulikuwa kwenye tukio hatuwezi kuzani we ni mmoja wa waarifu mliomuua uyo mnadhimu wa jeshi?,yangu ni ayo tu

The Richest Man in Africa: Nyuma ya kila utajiri kuna ukafiri



SEHEMU YA KWANZA


Wanasema ukosefu wa rasilimali unakufanya uchakate ubongo zaidi. Hii yaweza kuwa kweli katika ngazi ya mtu binafsi na hata taifa kwa ujumla. Unaweza kujipima binafsi namna ambavyo ukiwa 'umechacha' mbongo yako inavyochakata mawazo ili uweze kupata kile ambacho unakihitaji. Vivyo hivyo katika ngazi ya taifa, ukosefu wa rasilimali unaweza kufanya taifa kuwa na mipango madhubuti zaidi na hari zaidi ya kujipatia maendeleo. Mfano mzuri wa kuthibitisha hili ni nchi kama Singapore. Kanchi kadogo kabisa ambacho hakajajaaliwa rasilimali yeoyote, yamenyimwa mpaka ardhi na inawabidi 'kutengeneza' ardhi kutoka baharini kwa ajili ya matumizi yao. Singapore ambayo haina hata maji 'matamu' yasiyo na chumvi kutosheleza mahitaji ya wananchi hivyo inawapasa kununua maji kwa mabilioni ya lita kwa mwaka kutoka nchi jirani ya Malaysia ambapo wameunga bomba la kipenyo kikubwa kuingiza maji nchini mwao. Lakini ni ajabu kwamba nchi hii imeweza kujiletea maendeleo makubwa mno kufikia kiwango cha pato lake la taifa la mwaka kukaribia kabisa pato la nchi zote za kiafrika zilizopo kusini mwa jangwa la Sahara.

Ni ajabu, lakini ndio uhalisia. Ndio kusema kwamba hoja ya kwamba ukosefu wa rasilimali unafanya bongo kuchakata zaidi inapata mashiko madhubuti kabisa. Na pengine kujaaliwa rasilimali lukuki kunaweza kuwa chanzo cha kudumaza hari ya kujiletea maendeleo.

Ndipo hapa inanifanya niifikirie nchi ya Rwanda… japokuwa wamejaliwa rasilimali japo kidogo lakini huwezi kulinganisha na rasilimali ambazo majirani zao wamejaaliwa. Kila upande wamezungukwa na jirani aliyejaaliwa rasilimali za kufuru, magharibu kwao kuna nchi ya Congo, DRC moja ya nchi yenye utajiri mkubwa zaidi wa madini duniani. Mashariki kwao kuna Uganda ambao wana rasilimali lukuki kuanzia ziwa viktoria mpaka mafuta ardhini, na kusini mashariki kuna Tanzania ambao ndio hatuna haja ya kusema… tumejaaliwa kila aina ya rasilimali kuanzia madini, ardhi kubwa yenye kulimika, mbuga na wanyama wake, gesi asilia, bahari (bandari), na kadhalika na kadhalika.
Mbaya zaidi Rwanda hiyo hiyo ambayo imenyimwa rasilimali za kutosha tofauti na majirani zake bado wakapata mkosi wa mapigano ya kikabila yaliyodumu kwa zaidi ya miongo minne.
Licha ya yote haya leo hii Rwanda imeibuka kuwa mfano wa kuigwa katika nchi zote hizi za ukanda wa afrika mashariki na kati. Rwanda imegeuka nchi ambayo tunajisikia wivu tukitamani kuwa kama wao na hata kufikia hatua ya kujipendekeza tukidhani labda tunaweza kudurufu mipango na mikakati yao.

Japokuwa hatuwezi kusema maendeleo ya nchi fulani yamesababishwa na mtu mmoja pekee lakini hatuwezi kufumba macho na kukiri kwamba Paul Kagame ameibeba Rwanda mabegani mwake na kuifikisha hapa ilipo leo hii. Na si tu kwamba Kagame ameweza kuivusha Rwanda kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine bali pia Kagame ameibuka kuwa ndiye mtu mwenye ushawishi zaidi katika ukanda huu wa Afrika Mashariki na kati. Na si ushawishi tu pekee bali pia kupitia makala hii natamani kujenga hoja juu ya ushawishu huu alionao katika nchi zote za Afrika Mashariki na kati kunavyomfanya kuweka kiwango kikubwa cha rasilimali za nchi hizo mikononi mwake na hivyo kumfanya kuwa mtu tajiri zaidi barani Afrika.

Lakini ni muhimu kufahamu gharama ya kuupata utajiri, gharama ya kuweza kuwa na ushawishi mkubwa kiasi hiki. Yako mambo mengi sana ambayo yanatokea nyuma ya pazia. Mambo ya kuogofya, mambo ambayo hayawezi kusemwa hadharani.

Ni matumaini yangu kwamba tutaachwa tujadili makala hii kwa uhuru bila kuingiliwa na mtu au taasisi yoyote na labda tunaweza kuamsha hari za vijana wetu kuitaka kuijua nchi yao kiundani na hivyo walau tukawa tumetoa mchango wetu kwa kizazi kijacho kuwa na dira ya kuwawezesha kufika pale ambako sisi tumeshindwa kuifikisha nchi yetu.

Naomba nifungue rasmi mjadala…

View attachment 815763
Kamanda Anselme Masasy Nindaga

Mahali fulani Msituni karibu na Mji wa Lubumbashi, DRC - November, 2000


Japokuwa ilikuwa ni mchana lakini kwa namna ambavyo miti ilikuwa imeshonana ilifanya kuwe na hali fulani ya giza giza. Sehemu hii ambayo walikuwepo walau kidogo ilikuwa imefyekwa na kukatwa miti. Ilionekana dhahiri kwamba eneo hilo limewahi kutumika kuhifadhi wanajeshi kwa muda fulani au kuliwahi kuwepo na kambi ya dharura ya kijeshi. Mabaki ya magari mabovu ya kijeshi yalikuwa yametapaka hapa na pale. Upande mwingine kulikuwa na mabaki ya kifaru cha kivita ambacho nacho kilikuwa kimeota kutu tayari kutokana na kutelekezwa kwa muda mrefu. Lakini jambo la kuogofya zaidi mahala hapa ilikuwa ni maiti za binadamu ambazo zilikuwa zimetapakaa. Kwa haraka haraka kulikuwa na karibia maiti kama nane hivi katika upeo wa macho yao ambazo zilikuwa zimetapakaa mahala hapa.

Japokuwa wote wawili walikuwa wanajeshi hodari lakini kama ilivyo kwa binadamu wengine wote walikuwa wanavuja jasho wakihofia juu ya kifo ambacho kilikuwa kinawanyemelea mbele yao. Walikuwa na hisia kwamba ndani ya muda mchache ujao miili yao nayo inaweza kuwa imelala mahali hapa bila uhai kama maiti wanazoziona mbele yao. Kila dalili ya kwamba muda wa wao kuuwawa ilikuwa dhahiri kabisa umekaribua. Walikuwa wanawaona watekaji wao wawili wakiwa wanachimba shimo kama umbali wa mita tano tu kutoka pale walipo. Watekaji wao wengine wapatao sita walikuwa wamewazunguka na mitutu mikononi wakiwa kama kuna kitu fulani hivi wanasubiria.
Vichwani mwao walihisi kabisa kwamba lilikuwa linasubiriwa shimo limalizwe kuchimbwa ndipo wauwawe.

Mateka hawa walikuwa ni maswahiba wawili, ambao siku chache tu nyuma walikuwa ni moja ya watu wenye ushawishi mkubwa zaidi nchini Kongo. Wa kwanza alikuwa ni Kamanda Anselme Masasu Nindaga, ambaye mpaka wiki moja tu iliyopita alikuwa ni mnadhimu mkuu wa Jeshi la Kongo na wa pili alikuwa ni msaidizi wake wa kikazi na swahiba wake mkubwa Antoine Ngalamulume. Wote wawili walikuwa wamepigishwa magoti chini na kufungwa mikono kwa nyuma.

Dakika chache baadae walisikia mlio wa gari zikiwa zinakuja hapo walipo. Ziliwasili gari tatu za kijeshi ambazo ziliwasili zikiwa na watu karibia sita walioshuka kutoka ndani ya kila gari. Baada ya kushuka tu kutoka kwenye gari, wanajeshi kadhaa kati ya wale waliowasili walishusha maturubai kutoka kwenye gari na haraka haraka likatengenezwa hema mahala pale. Vikashushwa pia viti vitatu na meza na kisha wanajeshi watatu wenye vyeo vikubwa kuzidi wale wengine wote wakaketi kwenye vile viti.

Kamanda Masasu na mwezie walielewa ni nini kilikuwa kinafanyika hapa. Wale watu watatu walikuwa ni majaji wa mahakama ya kijeshi na kinachotaka kufanyika hapa ni kuendesha kesi kijeshi dhidi yao.

Hawakukosea, dakika chache tu baada ya mabwana wale kuketi "mahakama" ilianza.
Baada ya kuzungumza maneno kadhaa ya kiprotokali hatimaye "Jaji" akasoma mashataka. Ajabu ni kwamba mashataka haya alisomewa Kamanda Masasu pekee.

"Anselme Masasu Nindaga, unashitakiwa kwa kosa la uhaini wa kupanga njama kumpindua Rais na Amiri jeshi mkuu Mheshimiwa Laurent Desire Kabila… je, una lolote la kuieleza mahakama?" Jaji wa kijeshi, mtu mzima wa makamo ya kama miaka hamsini na sita hivi alisoma mashtaka na kisha kumuangalia Kamanda Masasu.

Kamanda Masasu licha ya mwili wake kuwa umedhohofu mno kutokana na mateso aliyopitia kwa muda wa wiki nzima lakini aliweza kutabasamu. Alitabasamu na kisha kutazama chini. Akatoa tena kicheko hafifu na kisha kuinua uso kuwatazama wale "majaji".

View attachment 815778
Mzee Laurent Kabila

"Mnatoa wapi uthubutu ya kuhoji utiifu wangu kwa Mzee Kabila?" Masasu aliongea huku anawatazama kwa hasira. "Mzee Kabila ni kama baba yangu mzazi na hakuna yeyote kati yenu hapa mwenye uwezo wa kuhoji utiifu wangu kwake. Kabila yuko madarakani leo hii kwa sababu nimeruhusu awe madarakani. Hakuna yeyote kati yenu hapa mwenye uwezo wa kuhoji utiifu wangu kwake."

Ulipita ukimya wa dakika kadhaa bila yeyote yule kusema neno.

"Una chochote cha kujitetea?" Jaji alimuuliza Masasu.

"Kama kuna tofauti kati yangu na Mzee Kabila tutazimaliza kati ya mimi na kabila. Hakuna yeyote kati yenu anayeweza kuingilia chochote kati yangu na Mzee. Tofauti zangu na kabila haziwahusu!!"

Ukapita yena ukimya mwingine. Ukimya mkubwa zaidi.

"Kamanda Masasu una chochote cha kujitetea?" Jaji akauliza tena.

Masasu alikaa kimya bila hata kuwatazama.

Wale "majaji" wakanong'onezana kitu kwa muda wa kama dakika mbili hivi kisha mmoja wao akaongea.

"Anselme Masasu Nindaga, mahakama hii imekukuta na hatia kwa kosa la uhaini wa kupanga njama kumpindua Mzee Laurent Desire Kabila, Rais wa nchi na amiri jeshi mkuu. Mahakama hii inakuhukumu kifo.!" Jaji aliongea bila kumtazama Masasu.

Baada ya kumaliza kusoma 'hukumu' hiyo walibeba makabrasha yao, lile hema likaondolewa wote wakakwea tena kwenye magari waliyokuja nayo na kuondoka wakiwaacha pale msituni na wale watu ambao walikuwa na kina Masasu tangu awali.
Kama dakika kumi tu baada ya wale waliokuja kusoma kesi kuondoka, waliobakia pale walimtutusa mzobe mzobe Kamanda Masasu mpaka mahala pale ambako wamechimba shimo na kumpigisha magoti Masasu akiwa amefungwa mikono yake kwa nyuma.

Hawakupoteza muda, mmoja wa wale watu wa 'kikosi hiki maalumu' akasimama nyuma ya masasu na kuinua bunduki yake kuelekea kichogoni mwa Masasu.

"BAAAAANNNGGG..!!"

Risasi ilifyatuliwa kichwani mwa Masasu na kumfanya adondoke kama gunia ndani ya shimo lililo mbele yake?

Msaidizi wake Antoine Ngalamulume ambaye alikuwa anashuhudia yote haya jasho lilimtoka asiamani kile ambacho alikuwa anakiona mbele yake. Hakuamini machi yake kama ule ndio ulikuwa mwisho wa Komredi Masasu, moja ya watu wakwanza kabisa kumuunga mkono Laurent Kabila katika vita yake ya kumuondoa Mobuttu Seseseko. Mtu ambaye alitembea kwa miguu umbali wa maili elfu mbili kutoka mashariki mwa Kongo mpakani na Rwanda alikokuwa na vikosi vyake mpaka kuingia Kinshasa kumng'oa Mobuttu. Mtu mwenye kuaminiwa zaidi na kupenda na wanajeshi wote wa Kongo. Mtu ambaye walikuwa wanamuusudu kwa mioyo yao yote. Ngalamulume hakutaka kuamini macho yake kwamba komredi mwenzake ndio alikuwa anafukiwa ardhini namna hii kama mnyama.

Alikuwa haamini macho yake, akabakia tu kujiuliza kichwani ni 'shetani' gani amemkubwa Mzew Kabila mpaka kufanya unayama wa namna hii kwa mtu aliyenza naye tangu sufuri.




Siku fulani, katikati ya Mji wa Kinshasa, DRC

Katika nyumba hii ya ghorofa moja katikati kabisa ya mji wa Kinshasa sehemu yenye mandhari ya kufanana kabisa na sehemu kama Kariakoo kwa hapa nchini kwetu, kulikuwa na kikao kizito kikiendelea kati ya bwana mmoja muarabu aitwaye Bilal Heritier raia wa Lebanoni. Kikao hiki kilihusisha watu watatu… yeye Heritier, 'mwakikishi kutoka Rwanda' na mtu wa tatu alikuwa ni mtu anayeitwa George Mirindi.
Mwakilishi huyu wa kiongozi mkubwa kutoka Rwanda nisimtaje jina kwa sasa wala kiongozi aliyekuwa anamuwakilisha ili nisiondoe uhundo wa makala hii… labda nieleze tu hao wenzake wawili, Bilal Heritier alikuwa ni mfanyabiashara mkubwa wa madini ya almasi na ajabu ni kwamba mtu wa pili yaani George Mirindi alikuwa ni mmoja wa walinzi wakuu wa Rais Laurent Kabaila.

View attachment 815779
Kanali Sue Ann Sundusky enzi za usichana wake

View attachment 815780

View attachment 815781
Kanali Sue Ann Sundusky


Kikao hiki kilikuwa ni cha siri mno kutokana na uzito wa masuala ambayo yalikuwa yanajadiliwa.

Kikao hiki haswa kilikuwa kimeitishwa na mtu ambaye mwenyewe hakuwepo kwenye kikao. Kikao kiliitishwa na Kanali Bi. Sue Ann Sanduski, mwakilishi wa masuala ya kijeshi katika ubalozi wa Marekani nchini Kongo. Waliopo hapa walikuwa wanapaswa kujadili na kisha kumpa mrejesho Bi. Sanduski.

Suala lenyewe lilikuwa kwamba, mabadiliko makubwa sana yalikuwa yanafanyika na Mzee Kabila. Awali Heritier katika biashara yake ya almasi alikuwa 'anadili' moja kwa moja na Mzee Kabila. Alikuwa anafika ikulu ambayo kabila mwenyewe aliibatiza jina la 'White House' na kisha anasindikizwa na walinzi wa kabila mpaka ndani ambako walikuwa wanajadili ana kwa ana na Mzee Kabisa kuhusu masuala hayo ya biashara ya almasi.

Lakini katika wiki za hivi karibuni Heritier amenyimwa kabisa kuoanana na Mzee Kabila. Kabila hataki kuonana nae na pia amemuwekea ugumu mkubwa kwenye ufanyaji wa biashara yake hiyo ya alamasi. Suala hili lilimshitua kila mtu kutokana na ukweli kwamba Mzee Kabila alikuwa anategemea hela za almasi kuendesha nchi na hasa hasa kuendesha jeshi. Kwa hiyo kama Mzee Kabila alikuwa anakataa kuonana na Heritier maana yake ni kwamba anapanga mipango mingine juu ya biashara hiyo.
Ndio hapa George Mirindi mmoja ya walinzi wakuu wa Mzee Kabila ambaye miezi kadhaa nyuma alikuwa 'recruited' na CIA aliitwa aeleze kama kuna chochote ambacho anakijua juu ya mabadiliko haya ya kutia mashaka.

Mirindi akawaleza kile ambacho alikuwa anakijua. Kwamba, kuna uwezekano Mzee Kabila ameshitukia 'mipango yao'. Kwa sababu kwa siku kadhaa amekuwa anakutana na wawakilishi wa nchi ya Israel pamoja na kampuni inayoitwa IDI Congo kutoka Israel inayojihusisha na masuala ya madini. George Mirindi aliwaeleza kwamba siku si nyingi Mzee Kabila atasiani makubaliano na IDI Congo na kuwapa 'monopoly' ya biashara ya almasi nchini Congo. Kwamba kampuni hiyo ndio itakuwa pekee yenye kuruhusiwa kujihusisha na biashara ya almasi nchini Congo. Mkataba huo utakuwa wa miaka mitatu na IDI Congo watalipa kiasi cha Dola Milioni 20 kwa serikali ya Congo na kutakuwa na uwezekano wa kuongeza mkataba baada ya miaka mitatu.

George Mirindi akaendelea kuwaeleza kwamba kama sehemu ya mkataba pia nchi ya Israel itatoa mafunzo kwa kikosi maalumu cha Intelijensia ya jeshi ambacho kitaanzishwa na kazi ya kikosi hicho itakuwa ni kupambana na "mapandikizi" ndani ya jeshi la Kongo.

Hii ilikuwa ni habari mbaya kweli kweli kwa kila mtu katika kikao hicho… ilikuwa ni habari mbaya kwa Bilal Heritier, ilikuwa habari mbaya zaidi kwa Rwanda na ilikuwa habari mbaya kwa Bi. Sunduski.

Swali ni je, wafanye nini kuepuka kile ambacho kilikuwa kinakuja mbele yao?



Stay here…


Habibu B. Anga 'The Bold' - 0718 096 811
To Infinity and Beyond
 
IMG-20180529-WA0029.jpg



The Richest Man in Africa: Kila utajiri una ukafiri nyuma yake







SEHEMU YA PILI





Katika sehemu ya kwanza ya mfululizo wa makala hii nilieleza juu ya kifo cha kamanda Anselme Masasu aiyehukumiwa na kupigwa risasi mbele ya rafiki yake na msaidizi wake Antoine Ngalamulume msituni karibu na mji wa Lubumbashi. Pia nilieleza juu ya kikao cha siri kilichofanyika katikati ya jiji la Kinshasa kati ya raia a Lebanoni na mfanyabiashara maarufu wa almasi Bwana Bilal Hritier aliyekutana na mwakilishi wa ‘kigogo’ kutoka Rwanda na George Mirindi ambaye alikuwa ni moja kati walinzi wakuu wa Rais Laurent Kabila. Kisha nikaeleza juu ya mabadiliko ya biashara ya madini ambayo Rais Kabila alikuwa anayafanya kutoka kuwa na ‘deal’ ya moja kwa moja na Heritier mpaka kuwapa kampuni ya kiisrael iitwayo IDI Congo ‘monopoly’ ya biashara ya almasi ndani ya nchi ya Congo. Lakini pia nilieleza juu ya mipango ya Rais Laurent Kabila kwa kushrikiana na Israel kutaka kutengeneza kitengo maalumu cha intelijensia ndani ya jeshi la Congo ili kubaini mapandikizi na wasaliti wote ndani ya jeshi.



Katika sehemu hii ya pili pia nitaeleza mfululizo wa tukio lingine muhimu ambalo lilitokea na tutalitumia kama rejea huko mbele kadiri hii makala inavyoendelea.



Tuendelee…





Kuna suala moja adhimu sana kuhusu saikolojia ya viumbe wote hasa wa asili ya wanyama akiwemo binadamu. Kwa mfano, licha ya ukali na ukatili wake wote, ukiweza kumchukkua simba angali bado mtoto na kumlea, pindi atakapokuwa mkubwa atakuwa tishio na uwezo wa kudhuru watu wote isipokuwa wewe ambaye umelea. Saikolojia ya wanyama wote ina ombwe la kiu ya mafungamano ya kudumu na kiu ya utii kwa wale ambao wamekuwa nasi tangu siku ya kwanza. Ombwe hili la kiu ya utii na mafungamano kama ambavyo ilivyo katika saikolojia ya wanyama wengine ndivyo vivyo hivyo pia ilivyo katika saikolojia ya binadamu. Kwa namna yeyote ile tunajitahidi mno kuwa na utii na kufungamano na wale ambao wametukuza na kuwa nasi tangu siku ya kwanza au tulipokuwa kwenye hali ya utete.

Nimeanza mjadala wangu kwa kusema hili ili kujenga msingi wa kile ambacho nataka kukieleza katika sehemu hii ya pili.





Wanasema kwamba madaraka yanalevya na yanaweza kukufanya usisfikiri sawa sawa na kuhisi kwamba unaweza kufanya lolote na yeyote yule asikuguse. Ulevi huu wa madaraka unaweza kukufanya hata ukajisahu na kuvuka mpaka wa kupuuza mafungamano na utii watu walionao kwa mtu ambaye unaunda naye uadui.

Kifo cha kamanda Masasu kilikuwa kama mwiba kwenye serikali ya Rais Kabila. Sijui kama Kabila mwenyewe hakulifikiria hili kabla au labda hakudhani kama litakuja kuzua kizungumkuti ambacho alikuwa anapambana nacho wakati huo.



Uvumi juu ya kuwawa kwa Kamanda Masasu kulizua taharuki kubwa na sintofahamu ndani ya jeshi la Congo. Masasu alikuwa ni kipenzi cha wanajeshi wengi na wengi walikuwa na utii na mafungamano naye wakumuona kama ‘mlezi’ wao.

IMG-20180610-WA0043.jpg

Kamanda Anselme Masasu


Wanajeshi wengi ambao walishiriki katika mapigano ya kumng’oa Mobuttu na kumuingiza madarakani Kabila walikuwa ni ‘vijana’ wa Masasu.



Kumbukumbu zinaonyesha kwamba Kamanda Masasu hakuwahi kupata mafunzo rasmi ya kijeshi katika maisha yake bali akiwa mtoto alichukuliwa na waasi nchini Rwanda na kufanywa mpiganaji wa msituni. Baadae akiwa kijana wa miaka ishirini na sita hivi alianzisha kikundi chake cha wapiganaji na wanajeshi wake wote walikuwa ni watoto. Baadae kikundi hiki kilikuwa kikubwa kwa idadi ya mamia na ndipo hapa ambapo alikipa jina la Revolutionary Movement for Liberation of Zaire. Mbele kidogo katika muendelezo wa makala hii nitaeleza juu ya uhusika wa ‘kigogo’ wa Rwanda katika kuunda kikundi hiki cha Kamanda Masasu kwa lengo la kwenda kuvuna rasilimali za nchi ya Congo. Katikati ya miaka ya tisini kikundi hiki cha Kamanda masasu kiliunganisha nguvu na kikundi cha waasi wa Kabila na kufanikiwa kumng’oa madarakani Dikteta Mobutu Sese seko. Kwa hiyo kwa maneno mengine Rais Kabila aliingia madarakani kwa mgongo na nguvu ya wanajeshi watoto wa Kamanada Masasu. Ndio maana siku ile msituni alipotakiwa kujitetea juu ya kupanga njama za kumpindua Rais Kabila, Masasu alikuwa na kiburi cha kutamba kwamba ‘Kabila yuko Madarakani kwa sababu yeye ameruhusu awe madarakani’. Jambo la kusikitisha zaidi hata walinzi wakuu wa kijeshi wa Rais na wanausalama walikuwa ni ‘vijana wa masasu’ ambao chimbuko lao ni kwenye kile kikundi cha wanajeshi watoto wa kamanda masasu waliotoka naye mpakani Rwanda.

Nitaeleza pia kwa undani chanzo hasa cha mgororo wa Kabila na Masasu, lakini kwa ufupi tu ni kwamba ilifikia muda Rais Kabila alianza kumuona Masasu kama tishio kwa utawala wake. Kukubalika na umaarufu wa Kamanda Masasu kwa jeshi ulikuwa ni mkubwa kufikia hatua kwamba alimzidi hata Rais kwa umaarufu na kukubalika ndani ya jeshi. Ndio maana Rais Kabila alihisi suluhisho la kuondoa tishio hili ni kumuondoa Masasu duniani.



Taarifa za kuuwawa kwa Kamanda Masasu zilianza kusambaa mwishoni mwa mwaka 2000 mwezi Desemba. Katika jeshi kulikuwa na taharuki kubwa watu kutaka kujua kama ilikuwa ni taarifa ya kweli ama la.

Serikali ya Kabila baada ya kugundua kuwa wamefanya kosa kubwa kumuua Masasu kutokana na utii wa wanajeshi wengi walionao kwa Masasu kutokana na mafungamano yao naye kwani ni kama aliwalea kutokea utoto wao alipowaingiza kwenye kikundi chake, ilibidi serikali kutumia nguvu kubwa kukanusha kuwa Masasu ameuwawa.

Kumbukumbu nzuri ni mkutano wa waandishi wa habari uliofanywa na Mandhimu mpya wa jeshi Generali Sylvestre Luetcha akiwa ameongozana na Generali Francois Olenga walikanusha vikali kabisa kwamba masasu hajauwawa bali anashikiliwa na serikali katkka jela ya siri kutokana na kosa la uhaini. Baada ya taarifa hii kueneo watu wengi walilipukwa kwa hasira wakitaka basi angalau Kamanda Masasu aonyeshwe kwa wanahabari, na ndipo hapa Genereali Francois Olenga alitoa jibu maarufu sana ambalo alinukuliwa akisema “Wahalifu wanaotishia usalama wa nchi hawapaswi kufanywa maonyesho”.



Licha ya serikali ya Kabila kujitutumua mno kuaminisha umma na wanajeshi kwamba Kamanda Masasu yuko hai lakini uhalisia ni kwamba hofu na hasira ilizidi kuwa kubwa miongoni mwa wanajeshi ambao walimuona Masasu kama ‘Baba yao’.

IMG-20180610-WA0044.jpg


IMG-20180610-WA0044.jpg

Huyu mwanajeshi aliyezungushiwa mng'ao wa duara ambaye alikuwa ni moja ya walinzi wakuu wa Rais Kabila alikuwa ni moja ya vijana waliolelewa na Kamanda Masasu katika kikundi chake cha wanajeshi watoto wa msituni.


Katika tukio muhimu zaidi ambalo tutalitazama kwa undani zaidi kadiri ambavyo tunaendelea na makala hii basi ni tukio la siku ya tarehe 16 mwezi January mwaka 2001.

Ilikuwa ni siku tulivu, siku ya kazi ndani ya mji wa Kinashasa kama siku nyingine zote. Rais Laurent Desire Kabila alikuwa ofisini mwake katika katika makazi ya Rais ambayo mwenyewe alikuwa ameyapa jina la “Palais de Marbre” (Marble Palace). Yeye pamoja na msaidizi wake maalumu aliyeitwa Emile Mota walikuwa wanajiandaa kwa ajili ya mkutano wa nchi zinazozungumza lugha ya kifaransa ambao ulikuwa unafanyika siku chache kutoka siku hiyo. Katika chumba cha pili kulikuwa na Bw. Leonard Mashako Mamba ambaye alikuwa ni Waziri wa Afya wa Congo kipindi hicho naye akisaidia maandalizi ya mkutano huo.

Ofisi ya Mzee Kabila katikati ilikuwa na meza kubwa ndefu hivi ya duara kama ya mikutano alafu pembeni kabisa mwa ofisi hii ndio kulikuwa na meza na kiti cha ofisi cha Mzee kabila mwenyewe. Meza ile kubwa ya duara katikati ya chumba cha ofisi ilikuwa inazungukwa na viti vitatu vya sofa kila upande. Siku ya leo kiti kimoja kilikuwa kimekaliwa na Rais Kabila na kiti kingine kile cha pili kilikuwa kimekaliwa na msaidizi wake Emile Mota.



Ofisi hii ilikuwa na mlango mkubwa wa kawaida mbele yake lakini pia kwenye upande mmoja wa chumba cha ofisi kulikuwa na ‘private entrance’ ambayo ilikuwa inatumiwa na Mzee kabila mwenyewe na watu wachache maalumu. Mzee Kabila na msaidizi wake Emile mota wakiwawanaendelea kupitia hotuba yake alisikia mlango wake ule maalumu ukifunguliwa. Mlangoni pale alisimama moja ya walinzi wake wakuu aliyeitwa Rashidi. Alipiga saluti na kisha kusimama kwa ukakamavu akiashiria kusubiri ruhusa aingie ndani. Mzee kabila kwa tabasamu kabisa alimkaribisha Rashidi aingie ofisini.

Kwa mujibu wa ushahidi ambao umetolewa na Emile Mota, Rashidi alipoingia ndani ya ofisi ya Mzee Kabila hakusema neno lolote lile, alichomoa bastola kutoka kiunoni mwake na kumtandika Mzee Kabila risasi ya kwanza ambayo ilimpata kifuani. Risasi hiyo ilimfanya Mzee kabila kudondoka chini pamoja na kiti ambacho alikuwa amekalia. Akiwa anatapa tapa pale chini RAshidi alimuongeza Risasi nyingine mbili ambazo zilimpata tumboni.



Ni ajabu sana, nasisitiza… ajabu sana, Rashidi hakumdhuru Emile Mota ambaye alikuwa amekaa pale pembeni ya Mzee Kabila. Badala yake Rashidi alitupa bastola chini na kisha kuanza kukimbia kutoka kwenye chumba cha ofisi. Rashidi akiwa anakimbia kutoka ofisini alipofika mlangoni alikutana na Leonard Mamba ambaye alikuwa kwenye chumba cha pili na alikuwa anakuja ofisini kwa Kabila aliposikia milio ya risasi. Emile Mota alikuwa anamkimbiza Rashidi kwa nyuma huku akipiga kelele kwa lugha ya Kiswahili, “..amepiga mzee masasi… amepiga mzee masasi (risasi).!”



Baada ya kusikia kelele hizi, moja ya walinzi wa Ikulu aliyeitwa Chiribangura baada ya kumuona Rashidi akikimbia kutoka kwenye ofisi ya Rais, alimfyamtulia risasi Rashidi ambaye ilimpta mguuni na kumfanya apoteze fahamu papo hapo.



Msaidiki mkuu wa kijeshi wa Mze Kabila ambaye pia alikuwa ni binamu yake, Kanali Eddy Kapend mbaye alikuwa eneo la Ikulu aliwasili mara moja kwenye eneo ambalo Rashidi alikuwa amepigwa risasi na Chiribangula. Kanali Kapend aliwasili akiwa ameshikilia bastola aina ya Kalashnikov mkononi. Chiribangula alipomtazama tu Kapend usoni alihisi kile ambacho alikuwa anataka kukifanya na alijitahidi kweli kweli kumsihi asifanye kile ambacho alikuwa anataka kukifanya… alimsihi asimuue Rashidi bali wasubiri azinduke na waanze kumuhoji kwa nini amempiga risasi mzee Kabila. Lakini Kapend hakutaka kumsikiliza Chiribangula, alimfyatulia Risasi kadhaa Rashidi na kumuua pale pale.



Jambo ambalo wakati ule hata serikali ya Congo wenyewe hawakulifahamu ni kwamba nje ya ukuta wa uzio wa Ikulu kulikuwa na gari ambayo ndani yake alikuwemo George Mirindi, moja ya wanausalama ambaye alikuwa ni mlinzi wa Rais. Mpango ulikuwa kwamba Rashidi akishampigarisasi Mzee kabila akimbie na kuruka ukuta na akifika nje George Mirindi ampakie kwenye gari na kutokomea pamoja.

Lakini baada ya Mirindi kuona Rashidi hatokei na milio ya risasi inaendelea kuunguruma ndani ya Ikulu alielewa kwamba mpango wao umeenda mrama. Kwa hiyo akang’oa gari na kutokomea katikati ya jiji la Kinshasa.

kama tujuavyo namna ambavyo habari mbaya inasambaa kwa kasi, kukaanza uvumi ndani ya jeshi kwamba Rais Kabila ameuwawa.
Kanali Eddy Kapend, yule binamu wa Mzee Kabila aliyempiga risasi na kumuua Rashidi, kinyume kabisa na protokali alichukua simu na kuanza kuwapigia simu wakuu wote wa vikosi vya jeshi maeneo yote ya Congo kuwaeleza kwamba Mzee Kabila amepata ‘ajali’ ndogo lakini ni mzima na hivyo wanatakiwa wadhibiti wanajeshi wao kusije kuzuka taharuki ndani ya jeshi ambayo inaweza kutishia usalama wa nchi. Japokuwa Kapend alikuwa na cheo kidogo kijeshi kulinganisha na wale wakuu wa vikosi ambao alikuwa anawapa amri, lakini wakuu wale wa vikosi vya jeshi walitii kwa sababu Mzee Kabila kwa muda mrefu alikuwa anapenda kumtumia Kapend kutoa maagizo kwa viongozi wa kijeshi. Kwa hiyo wakuu wale wa vikosi vya jeshi walitii maagizo ya Kapend kana kwamba yanatoka kwa Mzee Kabila, Amiri Jeshi wao mkuu.
Kapend hakuishia hapo tu, bali pia kinyume na protokali ya nchi alikwenda mpaka kwenye kituo cha televisheni cha Taifa na kutoa hotuba ya moja kwa moja kwa taifa kuwaeleza kwamba ni kweli Mzee Kabila amepatwa na ‘ajali’ ndogo hapo Ikulu lakini ni mzima hivyo wananchi wanapaswa kuwa watulivu na kusubiri taarifa zaidi zitawajia juu ya afya ya Mzee Kabila.


Lakini ukweli ni kwamba Mzee Kabila alifariki pale pale alipopigwa risasi.

Japokuwa hali ya dharura haikutangazwa moja kwa moja, lakini jeshi liliwekwa kwenye utayari wa hali ya juu huku anga la nchi hiyo likifungwa na hata wanajeshi na watu wa usalama wakiranda randa kwenye mitaa ya Kinshasa.

Kwa hiyo ili kuhalalisha kile ambacho walikuwa wanawaambia wanachi, kwamba Mzee Kabila ni mzima japo amepata ‘ajali’ ndogo… ilibidi mwili wa Kabila usafirishwe mara moja kwa ndege kutoka Congo kwenda Zimbabwe kwa ajili ya “matibabu”.

Wakati ‘maigizo’ hayo yakiendelea, viongozi wakuu wa jeshi na ‘wazee’ walituma taarifa kwenda Lubumbashi ambako mtoto wa Mzee Kabila, Joseph Kabila alikuwepo kwa ajili ya kazi maalumu ya kijeshi. Joseph Kabila alitakiwa kufika Kinshasa mara moja kwa ajili ya suala maalumu ambalo ‘wazee’ hao na viongozi wa kijeshi walidai kwamba Mzee Kabila alikisema kabla ya ‘ajali’ aliyoipata.


IMG-20180611-WA0025.jpg

Rashidi Muzele

IMG-20180611-WA0026.jpg

IMG-20180611-WA0027.jpg

Kanali Eddy Kapend




Itaendelea…

The Bold - 0718 096 811
To Infinity and Beyond
 

Attachments

  • IMG-20180614-WA0024.jpg
    IMG-20180614-WA0024.jpg
    18.6 KB · Views: 282
SEHEMU YA PILI


Nifah Divine... glory to yhwh BansenBurner Alisen Papushikashi Magazine Fire miss chagga SANCTUS ANACLETUS mngony Excel Mussolin5 Jimena Inferiority Complex gwijimimi wambura marwa Hoshea shareef conscious wambeke The Boss Deejay nasmile gkileo Juma chief Mangi flani hivi Ngongo makaveli10 KENZY kadada wa pili Root aretasludovick jonnie_vincy Clkey KAFA.cOm mbewe makedonia Afande Nyati peterchoka Leonard Robert Nchi Kavu STUNTER Chrizo jully Van persie Khalidoun Tetramelyz punje haradari Mazigazi @Alybaba babu na mjukuu platozoom jimmyfoxxgongo Nicodemas Tambo Mwikozi Ls man Heaven Sent sifongo Infantry Soldier haa mym 20acres MTS MarkHilary compos Tembo2 Erick the future nancy1983 Bulah binsaad Fazzaly the wolf everhurt Melvine Mgibeon kijana wa leo samsun Coolant Jagood pacesetter apologize payton George Betram kisengeli Kiranga Jiwe Linaloishi Madame B jay john Guasa Amboni Dinazarde Analyse Diva Beyonce snowhite Mmanu Expected Value onechromosome Missy rose Innocenthezron Immortal_MH Ficus sunola Robot la Matope mamaafacebook II JEKI likikima Compact scorpio me G'taxi YNWA adna yuzo ntamaholo Otorong'ong'o naan ngik-kundie kandukamo1 AFRICA101 mwalidebe Kobe Blaki Womani kalendi savius The Great Emanuel r2ga Ntaluke.N. Transcend Msemachochote Mchumiajuone mwampepec MTOTO WA KUKU Fukara proto cute kawombe zinginary MLALUKO JR Vupu barafu BlackPanther Ntuzu Matola impongo ntamaholo Mkoroshokigoli Deadbody KING easy mahoza Msolo kkenzki deborah1 KIDUDU buffalo44 winlicious riziki Allys MUHUNZI Moses2015 nacktary Liuumi dochivele Renzo @barbers hmjamii mbere TATIANA famicho LUCKDUBE mwanadome Straton memphis ghazar Graph Theory Honey Faith Shunie Slave ddcmanesto zinginary pacesetter Nkanaga KOMUGISHA mikatabafeki johnsonmgaya lee empire wigo MJINI CHAI Asprin mtzmweusi Erasto kalinga Chrizo kichakaa man LULU bike FORTALEZA poleni shibumi ZE DONE umande Edger Sr sir joshua sammoo Roram Password Bavaria hambiliki mwanangu Asili100 Evarist Massawe nice1 Jumong S Rogie 1babake nasreen uberito baest dustless Kilemachocho Tumosa mtembea kwa miguu Debbs Joe scorpnose musacha shibumi seeker of knowledge Simuchi Veni Vidi Vici TUJITEGEMEE abuu garcia Hon Nkundwe Festo Festo marion09 mike2k The dream bro kay vandelintz kirikou1 POINT LOAD lusaka city Dirham Rodcones bato MANCNOO multiphill90 GEORGE Dalali mwanamalundi90 MwaFreeca Roram Ta-kibombo troublemaker mambo KOMUGISHA calabocatz Papaa Azonto Msemachochote Mdomo bakuli tizo1 option dikembe iL Buono fakalava ABDUL KAREEM @Gobe Justine Marack Goodluck Mchika MR UNINFORMED darcity nkasoukumu nG'aMBu thatonegAl kabanga MPARE KIBOGOYO Edward Sambai Rassa mnonje srinavas last king of uscoch proto cute Kennedy krava Rais2020 kbosho Mzee wa BsN sam2000 fuma 999 Bableee dawa yenu The Certified DON SINYORI mij addenbwii ONTARIO Kobe The Vein Mondray jaxonjaxon successor mzee wa liver sawariya Sitaki ukuda Domhome Mpatanishi MKANDAHARI mtugani wa wapi huyo wealthier cluecell Toyota escudo mgumu2 troublemaker Linamo shedede kamtu33 SteveMollel ngushi Donald stewart Mshuza2 Glycel mnonje Ochuanilove SingleFather Santi DEOD 360 ngushi anatory antony ukhuty chris van chicha auxillius Goma Son Hubeb pes KING DUBU VILLAIN mwayena donbeny Aleppo JipuKubwa shoo61 BOMBAY John mungo Nyakageni bato Dogo 1 sufra chamlungu painscott wegman Bravo Engliash MOSELBAY wa stendi FaizaFoxy bigmind cadabraa Internal Kelvin mwalukas mnonje Kelvin X Somoche Wgr30 Miiku Poise Jabman kalamuyamwalimu BOMBAY the say juxhb witnessj Gide MK Mmanyema mgogoone Mnongane Mandingo koncho77 afsa ngaboru Paradoxer Heavy Metal KIMBURU 06 Raaj kichekoh ngumba njeche kikale DullahTza Goodluck Mshana julius Darcy Denis Kasekenya mashonga kitalembwa Khaleed Shaban middle east SirChief jiwe jeusi Mkambarani mansakankanmusa gambada ynwa ney kush mossad 03 white wizard xtaper Mzigua90 Ollachuga Oc Gidbang Mateja M.G Yango jipu abaa4all DIBAJI Agenda1 Grahnman The MaskmaN Slim5 Xubzero agprogrammer JoJiPoJi Architectus blance86 Mamtolo monde arabe Ngao Ya Imani stardust JK naiman64 Dharra seledunga ABB SHAMMA Richard Waziri wa Kaskazini Mwinjuma1 Kanungila Karim baracuda Mwamba028 besaro Pyepyepye Bilionea Asigwa ibn Kiti Chema Tugas Royal Warrior mederii mmangO manzi james LIKUD adrenaline Royal Son Mhadzabe
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom