The problem with MUHIDINI ISSA MICHUZI

Status
Not open for further replies.

SPOILA

Senior Member
Jun 25, 2007
113
13
Huyu bwana ni mwenzetu na kutokana na nafasi yake katika jamii nilitokea kumheshimu sana. Jana alileta story ya RAFIKI YAKE WA KARIBU bwana JACK PEMBA ambaye kutokana na evidence katika hapo chini MICHUZI BLOG imekuwa kama NOTICE BOARD ya JACK PEMBA na biashara zake za kitapeli
attachment.php



Cha ajabu ni nikuwa leo kaondoa ile story ya UTAPELI WA JACK PEMBA!

sasa nishajua kwa nini hawakumpa kazi kule OFISI KUBWA. Huyu ni rahisi sana kununuliwa AMA KWELI TUMEKWISHA!

MICHUZI
 

Attachments

  • DSC01626.jpg
    DSC01626.jpg
    44 KB · Views: 1,130
Acha hizo Spoila

ninavyofahamu mimi, Ndg Michuzi huwa anai-update blog mara kwa mara kulingana na mapenzi yake, sasa kama wewe uliona imeondolewa ni kiasi tu cha kumuomba airudishe, siku nyingine ukipenda inf. fulani nikiasi tu cha kui-backup bila kusahahu ku-note source yake.
 
Spoila,

Mimi nadhani wewe ndio hujaelewa mchezo huu wa uandishi!...

Majuzi kulikuwa na tuhuma kuwa Jack Pemba ni tapeli na kwamba GSB wameondoa ushirikiano wao na Tanzania..Kila mmoja wetu fell for that!..
Jana huyu huyu mtuhumiwa alikuwa na viongozi wa GSB kila kona wakionyesha ushirikiano wao kana kwamba uvumi wa Jack Pemba na Utapeli ni uongo mtupu!...
sasa ulitaka Michuzi afanye nini kama sio kukupa wewe mtihani!...
Mlisema Jack pemba tapeli na GSB hawatakuja tena TZ mbona wapo?... na mbona wanashirikiana bado na J.pemba!...
Picha zinajieleza zaidi!
 
Mkandara.

Kuna waandishi wa aina nyingi.moja wapo ni waandishi wa mishiko hawa wana toa tu story so long umemcheki. niliwahi kusoma gazeti moja ambapo jana yake mwandishi kaandika negative siku ya pili very positive.

Nampenda sana Mjengwa Majjid ambaye hutuletea picha za wanyonge na halisia kwenye blog yake. kumekuwa na Blog nyingi sana zingine kama ni BIG BROTHERS.
 
Mtalii,

Pamoja na yote ulozungumza kuna tofauti kubwa kati ya Mjengwa na Michuzi. mara nyingi Mjengwa huzungumza mawazo yake yeye mwenyewe ama kuweka story anazikubali yeye!..Yes! ktk kiwango hicho bwana mdogo anajitahidi sana..he is good.

Lakini ukitazama Michuzi huwa anaweka picha zinazojieleza zenyewe bila yeye kutoa mawazo yake. Kitu kimoja anachojaribu sana kufanya ni kukunyanya mitazamo tofauti nasio mapenzi yake kisha kutafuta habari zile yenye kuzua hoja!
hadi sasa hivi hakuna blog inayotembelewa kam ya Michuzi na budi kumpa sifa zake, kwa sababu hakuna ulazima wake kuwa sawa na blogger wengine as long he stays on top.

Mtalii wengi wamesha sema sana kuhusu Michuzi na wengi wamejaa wivu na wapishi wazuri wa wajungu lakini bado hawabadilishi ukweli kuwa Michuzi is very good in what he is doing!..iwe mshiko ama sio kwani hii ni kazi yale inayompa kula.....
 
Kukosa kazi kwa michuzi ofisi kuu si kwa sababu anaweza kununuliwa kirahisi bali hana kimungu mtu cha kumpigia debe. Wengi waliokuwa ofisi hiyo ni watoto wa baba zao ambao wana vimungu mtu vinavyowapigia debe kila kukicha ili waingizwe ofisi hiyo au waendelee kubaki huko. But so far Michuzi is doing very well. Keep it up brother.
 
Chaguo langu kwenye blogu za picha ni haki-hakingowi.blogspot.com.Presentation yake ni bomba kuliko Michuzi.
 
Wenyeji

Mimi bado mchanga. Bado natafakari. I have no comments. Ila tu nijuavyo mimi Michuzi ni mtu makini sana. Hayo mengine siyajui. No research, no right to speak.

By the way Kwani Jack ana tatizo gani? Huyu si yule aliyetaka kuileta Timu ya Vijana UK? Hivi huyu ana uraia wa nchi mbili? Passport ya UK imetundikwa hapa je ile ya bongo anayo? If so, tunataka mambo hadharani sio uwani
 
Katika kujadiliana na wenzangu tumeona kuwa Issa Michuzi anamchezo wa kutopost message za watu kama wanataka ongea ukweli juu ya mambo.

Yeye analeta topic watu wakianza kujibu na kusahishana anaamua kuchuja

kuna moja mwenzangu alisema mtu aliandika maneno mabaya alipocomment kitu basi yeye alipojibu post yake aikuiingia mtanaoni ila ya huyo mtu as ANON zilikuwa zinapita

Pia mie nilitumaga post kucomment juu ya yule baba aliyesema amesafiri atatoa zawadi9UTABIRI WA MECHI YA MPIRA) akirudi bongo hiyo ilikuwa miezi 3-4 imepita kama sio zaidi ila hadi leo kimya, tumejaribu kutuma comments kuuliza vipi Michuzi anaziignore atuzioni mtandaoni... HII NI SABABU MMOJA ALITABIRI SAWA

Je ni nini sasa kama anaweka mambo kwewnye globu yake halafu anashindwa kuridhisha watu na kuturuhusu tuweke comments... si ameifungua kwa nini mengine yanamwingia moyoni???

Conclusion yetu ni kwambaaaaaaaa
Michuzi anapost comments mwenyewe mara nyingi ili kuleta uchangamfu blogini vikimshinda anaanza kuzuia comments za watu.

Pia ana uwezo wa kujua mtu yupo nchi gani etc

Pia Michuzi yupo na serikali umeshagundua huwa asemi kitu kuhusu siasa ya nchi yetu na ubaya wake.. i guess akitaka kujificha anatuma post as anon kuisaidia kujibu ili watu waache kutongea ukweli ambapo hatapost comments zao watu wasome

I hope hii itamfanya abadilike ili wengine wasikimbie blog yake esp katika kuacha kutoa opinion

ametuuzi sana, ndio tabu mfano anatupa ya watanzania wa namna yake

haya ndio maoni yangu, baada ya uchunguzi wa muda. badilika ok

unaonaje weye???????????????????????
 
Just boycott him then.

JF is where it's at,tunamkoma nyani kama kupumua!
 
Carrie, inaonekana imekuuma sana.
Sasa kama unaona ni ishu, ngoja nikupe idea.
Kwenye keyboard yako kuna vi-button viwili. Moja imeandikwa 'fn' (meaning function), na nyingine ni 'prt sc'. Hii ya 'prt sc' iko kwenye vi-button pale juu.

Sasa basi. Wewe kama unaona unazibiwa, basi, andika comment yako unayotaka kuandika,kabla hujatuma/submit, chukua screen grab (yaani bonyeza 'fn' halafu 'prt sc'), Hii ita-grab kinachoonyesha ulichoandika, na muda kwa chini. Ipeleke kwenye 'Paint' programme, paste, crop it, save kama .jpg. Ukisha fanya hivyo, submit. Lazima utapata message kwamba inasubiri moderator aikubali. Take a screen grab of that too.....kwani itaonyesha muda (ambao utakaribiana na screen grab iliyopita).

Unaweza kuwaambia rafiki zako wafanye hivyo hivyo. Hapo mta-build case ya ku-accuse mnazibiwa. Zibandike hizo screen grab hapa tuone.

Kama ni kazi kubwa, basi, endelea kwingine.
 
i agree with wewe uliyepost thread hii na its true as mimi mwenyewe nshawahi once ask about lile shindano la arsenal na man utd nkashangaa kilikua kimya tuu!atleast kama ilikua vipi na ule tapeli wake wangetoa hata taarifa huo ndio ustaarabu na sio kukaa kimya tuu
 
Huyu ni mwandishi wa habari pamoja na kuwa kaajiriwa na gazeti la siri kali, hatakiwi afanye censorship ya mawazo mbali mbali ya Watanzania kwenye blog yake hasa pale anapoanzisha mijadala kuhusiana na mada mbali mbali ndani ya Tanzania. Wengi wanalalamikia hii censorship yake, inabidi ajirekebishe haraka sana vinginevyo ni kuiepuka blog yake kama ukoma.
 
Niliwahi kumtumia Michuzi message privately kumuelezea kero kama hii, ilikua ni ushauri wa bure tu kwamba as long as mtu anatumia lugha ambayo ni appropriate kutoa maoni yake- basi hana budi kupost hiyo comments hata kama hakubaliani nayo- si anaiita blog ya watu?
Nakumbuka wakati Twanga inakuja London aliifagilia Club Afirque kwa sana bila kujua kwamba wabongo wengi ambao wamewahi kwenda mahali hapo walikua hawaridhishwi na standards za jinsi Bw. Jesse anavyoi run club hiyo.I was one of many people who used that opportunity to express their concerns on this club,lakini to my suprise 'hakuirusha'. Nilitoa points za msingi sana kama Health and safety issue, hygiene na security- lakini Bw. Michuzi alidiriki kuziita hizi issue kuwa ni "wivu tu wa wabongo na kutotakiana mema" akisahau kwamba mimi ni mteja na nilikua namtakia mema tu mmiliki wa sehemu hiyo. Binafsi nadhani kama angepost comments zote zilizotolewa angekua amemsaidia sana mshkaji wake Bw. Jesse kwani ingekua ni kama free customer survey(Imagine how much this would have cost him kama angeamua kufanya research),huenda saa hizi angekua ameshabadilisha yale ambayo yanawakera wateja wake. na karne hii kama unafanya Biashara,haswa majuu, inabidi ujitahidi ku operate kulingana na matakwa ya wateja wako na sio unaanzisha Bar mamtoni lakini unairun kwa standard za kibongo.
By the way, ushauri wangu ni kuiboycot hiyo blog, binafsi nimeamua nitakua naangalia picha tu hapo kwa Michuzi(this is what he is good at), siwezi tena toa comments zangu on any issue.
 
Msusieni tu blogu yake iwe ya udaku.Pamoja jamaa ni mserikali lkn hamna haja ya kuchuja maoni yanayojenga.Pamoja yeye ndio mmiliki wake
 
Everyone humu JF knows the man is an idiot ndio maana we spend more time humu kuliko kwa huyo mediocre

Hivi hamjiulizi kwa nini CRDB wameondoa matangazo kwake?
 
Leo ni siku ya tano au sita nashindwa kuingia kwenye blog hiyo. Je, kuna yeyote anayeijua kulikoni?
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom