THE POWER GAME: Ni ukanda upi hapa Tanzania wanaongoza kwa uwezo mkubwa wa kucontroll power?

NetMaster

JF-Expert Member
Sep 12, 2022
1,454
4,853
hj.png


The power Game, Anaeweza kushika madaraka ndie yupo juu zaidi, Mfano kwa Nigeria kanda ya kaskazini wapo nyuma kielimu na kibiashara lakini linapokuja suala la Power wao ndio wameikamta na kuweza kuitumia kuwa juu ya kanda ya kusini mashariki walioshika biashara za nchi na kanda ya kusini magharibi wanaoongoza kwa elimu.

Power game sio kuangalia kwa sasa anaongoza nani, ni kuangalia katika kipindi kirefu ni nani alieweza ku dominate zaidi, Power game haihusiani na maendeleo ya sehemu wanakotoka wenye power, wanakotoka kunaweza kuwa choka mbaya lakini power imewapa ulinzi, connecions na ukwasi wa kutisha ila wanauficha ikiwa ni moja ya mbinu za power game.

Kwangu mimi kwa hapa kwetu naona ni ukanda wa pwani wanajua sana kuucheza huu mchezo kama bao, kanda hii hujumuisha Tanga, Pwani, na Zanzibar .. nguvu yao kuu ni viongozi kuandaa watoto waje kuwa viongozi hapo baadae (suvcesion plan) tofauuti na sehem nyingine mtoto anakazaniwa zaidi aje kuajiriwa ama apewe mtaji, connection wanazijenga kuhakikisha mambo yapo smooth, wanaishi maisha ya kawaida wanayoyapenda watu ilhali wana ukwasi na power kubwa, n.k
 
Kanda ya pwani tuna power kwa vile maneno mengi japo ki elimu tuko nyuma maana ujuaji ni mwingi na elimu ya kukariri hatuwezi ...

Nina ushahidi wa kutosha baadhi ya kanda Kuna wasomi ila hwajiamini kabisa ,mfano wanaohofia na kuwachukia watu wa jamii fulani wakati wao hawana time now.

Binafsi nimekutana wa watu wa kanda kibao kuanzia advance mpaka namaliza chuo nilikuwa na kundi na jamaa kibao maana sikuwa labda kipanga sana ila maneno mengi basi nilikuwa chairman kote huko advance mpaka chuo kila group😂😂😂mpaka nashangaa yaani kwa nn ivyo wapo wengi Wana uwezo na wamesoma shule kali ila hawajiamini ..wananiambia we kijana unafaa sana kuwa kiongozi ...wengine walikuwa wanadhani Mimi ni usalama wa taifa😂😂😂
 
Kwa Nigeria kanda ya kaskazini wapo nyuma sana kielimu na kibiashara lakini linapokuja swala la Power ndio ma master, Power imewafanya wawe juu kuzidi hata kanda ya kusini mashariki walioshika biashara kibao za nchi na kanda ya kusini magharibi wanaoongoza kwa elimu

Kwangu mimika hapa kwetu naona ni wazi kabisa ukanda wa pwani hawana mpinzani, kanda hii hujumuisha Tanga, Pwani, na Zanzibar ..

Kwenye Elimu wapo nyuma kidogo lakini linapokuja swala la Power wana uwezo mkubwa sana...

Kuweka stori iwe fupi hawa ndio wafalme,,, Anaefata labda kanda ya ziwa na kaskazini
Power is evenly distributed in Tanzania. Tanzania haina inclination au kama ipo ni kidogo sana linapokuja swala la power. Mara nyingi tunaitafsiri power kwa kuifungamanisha na wanasiasa lkn kumbuka kuna nguvu nyingine iliyobebwa na wasiokuwa wanasiasa ndani ya mifumo.
Na ndio maana ni rahisi kwa eneo lenye watu wenye nguvu isiyokuwa ya wanasiasa kuendelea na kufaidi matunda ya nchi(national cake) kuliko eneo lenye wanasiasa maarufu.
Wanasiasa ni watu wabinafsi, wachache na wanaodumu kwa muda mchache.
Kuna watu sio wabinafsi, wengi na hudumu kwa miaka 30 hadi 40 kwenye corridors of power. Na hao ndio wanaocommand power.
 
Power is evenly distributed in Tanzania. Tanzania haina inclination au kama ipo ni kidogo sana linapokuja swala la power. Mara nyingi tunaitafsiri power kwa kuifungamanisha na wanasiasa lkn kumbuka kuna nguvu nyingine iliyobebwa na wasiokuwa wanasiasa ndani ya mifumo.
Na ndio maana ni rahisi kwa eneo lenye watu wenye nguvu isiyokuwa ya wanasiasa kuendelea na kufaidi matunda ya nchi(national cake) kuliko eneo lenye wanasiasa maarufu.
Wanasiasa ni watu wabinafsi, wachache na wanaodumu kwa muda mchache.
Kuna watu sio wabinafsi, wengi na hudumu kwa miaka 30 hadi 40 kwenye corridors of power. Na hao ndio wanaocommand power.
Na CCM haina tabia ya kuchagua viongozi bila kuangalia historia, desturi na mahitaji ya kidemografia ya nchi yetu.
 
Elimu, uwezo na uzalendo pekee tu sio vigezo vya kusogea na kudumu kwenye siasa nchi karibu zote duniani hasa zenye demokrasia.

Kusogea kwenye siasa kunataka fitna kwa asilimia kubwa na kama uwezi fitna elewa upo kwenye wrong proffesion au usiwe na ndoto za kufika juu.

Tofauti yetu na nchi zilizoendelea zinawanasiasa ambao kwa asilimia kubwa ni wasomi tena top universities kwa standard zao. Sisi tunawasiasa wengi wenye elimu za kuunga.

Lakini common ground ya siasa zote za nchi zenye demokrasia, makundi hayakwepeki na wenye fitna kubwa ndio mara nyingi utoka kidedea.

Si wazungu hao hao ndio walioanzisha msemo ‘there are no permanent friends in politics, only permanent interest’ ndio tuelewe bila ya fitna, toa political ambitions kwenye maisha yako.
 
Kuna sababu kama mbili za haraka zinazonifanya nione kwanini ukanda wa Pwani unaonekana kunufaika zaidi.

Kwanza, naweza kusema sababu ya kihistoria inachangia zaidi, kwasababu harakati za kudai uhuru mostly zilifanyika ukanda huu, mfano Nyerere alitoka Bara akaja kuongezwa nguvu na waswahili wa Pwani wakafanikisha uhuru kupatikana.

Sababu ya pili ni uwekezaji uliofanywa na viongozi waliotangulia serikalini toka ukanda huu wa Pwani, mfano leo tunaona wameacha watoto wao madarakani ambao wengine tumeanza kusikia nao wanautaka urais Makamba in particular..

Sitashangaa mbele ya safari Ridhiwani Kikwete nae akaanza kuhusishwa na hizo mbio na hata akaja kuwa Rais wa hii nchi, wanajua kutengeneza mtandao ambao tayari una nguvu ya pesa walizopata kupitia madaraka waliyoshika, wanazoweza kuzitumia kuingia ikulu.

Kwangu naona ingeweza kutokea hali ya tofauti na kubadili huu upepo endapo Magufuli angebaki mpaka amalizie muhula wake wa pili, ingependeza tuone angemuachia nani kuja kumrithi.

Kwasababu ndani ya CCM nguvu ya mwenyekiti kuamua amtakaye ni kubwa ndio maana ikasemekana JK aliwahi kuingia na majina yake mfukoni, nae juzi kwenye interview yake na Clouds Media akakiri kufanya hivyo.
 
Huku ni kujifanya unajua Sasa. Au labda hukumuelewa mtoa hoja.
Huoni ndio ubaguzi unaanzia hapo kujiona kuwa akina fulani wao ndio wameumbwa kuwa ivyo. Pia inatakiwa nchi yetu tuione Kama familia yetu sote,wewe ukiwa pm or president sio lazima mie niumie ilhali na wewe Ni sehemu ya familia
 
Back
Top Bottom