Madame S
JF-Expert Member
- Mar 4, 2015
- 17,172
- 34,277
SIMULIZI:THE LOST BOYS
MTUNZI: FRANK MASAI
MAWASILIANO:0752353039
SEASON 1.
ALFRED MUSITA.
ANAPENDA kujiita Fred. Jina ambalo kazoeleka kuitwa na rafiki zake pamoja na ndugu zake pia. Ni kijana mwenye asili ya Kiarabu na Kiafrika, yaani Chotara kwa lugha yetu pendwa ya Kiswahili.
Ni kijana mwenye kila sifa ya kuitwa mtanashati na mtu yeyote duniani. Akiwa kavaa kofia au mzula, waweza sema huyu ni muafrika wa kawaida tu!, ila akivua ndiyo utamtambua kuwa ni mchanganyiko hasa kutokana na nywele zake nyingi na zilizojiviringa vizuri kabisa. Kwa kifupi jamaa ni mzuri na mtanashati.
Baba yake ambaye ni maarufu kwa jina la Mzee Musita, ni Mtanzania halisi kabisa kutoka Mbeya. Na mama yake ni mtu wa Iran.
Alfred au Fred, yeye aliamua kuchukua dini ya baba yake ya kikristo kwa sababu muda mwingi aliishi na baba kuliko mama.
Baada ya kumaliza kidato cha nne katika Shule ya Sekondari ya wavulana, Bwiru, Fred alichaguliwa kuendelea na masomo yake ya kidato cha tano na sita Morogoro Sekondari, na alichukua masomo ya biashara kwa sababu ya hamasa aliyokuwa akipewa na baba yake Mzee Musita, ambaye alikuwa ni maarufu sana hapa Tanzania kutokana na biashara mbalimbali alizokuwa anazimiliki.
Alipomaliza kidato cha sita, matokeo yake yalikuja vizuri, hivyo alichaguliwa kuendelea na masomo hayo katika Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam au UDSM kama wengi hapa Tanzania walivyokiita. Na kama alivyokuwa anaota kila siku, aliweza kutimiza ndoto yake kwa kwenda kuchukua masomo ya Uhasibu.
Kwenye maisha yake tofauti na ya shule, Fred alikuwa ni mpole na mtulivu sana. Hakupenda kufuatilia wanawake japo wanawake wengi walimtaka kimapenzi na wengine kuomba japo wawe naye tu!. Naweza kusema ni dini ambayo alikuwa ameiweka kichwani mwake, ndiyo hasa ilimfanya ajiweke mbali na jinsia ya kike.
Aliishi kwa njia ya maneno ya MUNGU. Hata kwa wale wanawake waliokuwa wanamtakia wazi kuwa wanampenda na kumuhitaji, alikuwa anawakatisha tamaa kwa kutumia maneno hayo kutoka kwenye vitabu vitakatifu.
Kuhusu wazazi wake hasa baba yake, alikuwa si tajiri sana wala masikini kupindukia. Biashara alizokuwa anazifanya, zilikuwa zinampa chakula pamoja na makazi mazuri kabisa ya kulala yeye na mwanae yule wa pekee. Kila alichokitaka Fred, alikipata kwa wakati muafaka kama alivyoahidiwa.
Mama yake Fred alisha-talikiana na Mzee Musita hivyo hakuwa mtu wa mara kwa mara kuonana na Fred, na hata wakionana basi ni kwa muda mchache. Hiyo ni kutokana na mme wake mpya kuwa anambana sana pamoja na wivu.
Na sababu kubwa ya Mzee Musita kutalikiana na Mama Fred, ilikuwa ni rangi ya watu hawa wawili, mmoja Mwarabu na mwingine Mnyakyusa halisi, yule mweusi kabisa. Hapo wazazi wa Mama Alfred, waliingilia na kumtaka mtoto wao aolewe na Mwarabu mwenzake, na hicho ndicho kilichotokea.
Ukitoa Mama Fred kuonana na mwanae uso kwa uso ambapo ilikuwa nadra sana. Walikuwa pia wanawasiliana katika mitandao ya kijamii na MMS.
Neno la dini, ndilo lililokuwa kipaji chake huyu bwana mkubwa.
Hiyo ni kwa kifupi kuhusu Alfred Musita.
HASSAN JENGE.
Huyu alipenda kujiita Hans J, lakini wenzake walishambadilisha jina hilo toka akiwa kidato cha pili kwa kumuita Crazy Hans au kwa Kiswahili Kichaa Hans. Hiyo ni kutokana na mambo pamoja na tabia aliyokuwa nayo.
Hans J, yeye alikuwa ni mrefu kiasi, huku mwili wake ukijengwa kwa rangi ya maji ya kunde.
Baba yake, Mzee Jenge, alikuwa ni Mngoni na mama yake alikuwa ni Mchaga. Mchanganyiko huo, ulimfanya Hassan aonekane ni mtanashati kupindukia.Ndiyo maana yake, jamaa alikuwa ni Handsome haswaa.
Kuhusu tabia huyu jamaa, unaweza kusema ni mhuni sana kama ukimuangalia kwa nje tu!. Kila muda nywele zake zilikuwa tim-tim. Na alipenda sana kuvaa suruali za jinzi na kuzipiga mlege mkubwa tu.
Fulana zake mara nyingi zilikuwa ni mitumba tu. Hakuwahi kuingia dukani na kununua shati au nguo yoyote humo.
Licha ya hayo yote, yaani kuvaa kihuni, kutimua nywele, na kuvaa vitu vya mtumba, huyu Hans alikuwa anajipenda sana. Muda wote alionekana msafi wa kila kitu.Hizo nywele japo zilikuwa tim-tim, lakini zilikuwa ni safi na za kung’aa kutokana na mafuta aliyokuwa anayapaka.
Mwili wake uliyojaa kiasi, na mavazi aliyokuwa anayavaa, ndicho hasa kilimfanya huyu jamaa azidi kuteka wanawake wengi pale alipokuwa anasoma na kuishi.
Kidato cha nne, yeye alimalizia Makongo na baadae aliamua kuendelea na kidato cha tano na sita katika shule ya Sekondari Merriwa iliyopo Dodoma. Alipomaliza masomo hayo, alipata alama za juu pia, na kuchaguliwa kwenda kuendelea na masomo yake katika Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam.
Alikuwa ni mtu wa Sayansi, na aliweza sana kuyamudu masomo yake hayo. Mara nyingi alikuwa anafanya mambo ya hatari sana na ya kushtua kwa kutumia hiyo Sayansi yake, na ndio sababu kubwa ya wanafunzi wenzake kumuita Crazy Hans.
Akiwa kidato cha pili katika shule ya Muheza Muslim iliyopo Tanga. Huyu Hans aliwahi kuchukua kemikali na kuzichanganya kwenye chombo kimoja, na baadae alichukua mchanganyiko huo na kuufungia kwenye chupa ya soda. Aliporidhika, akatoka nje na kuitupa chupa ile kwenye eneo lililokuwa halina watu.
Chupa ilipodondoka, eneo lile la shule lilikuwa kama limevamiwa na magaidi kutokana na mlipuko uliotokea pale. Ilikuwa ni mshike-mshike wa kufa mtu pale shuleni, kuanzia waalimu hadi wanafunzi. Na hata Hans alipoitwa kujibu mashitaka, wala hakuwa na wasiwasi.
Pale alipofukuzwa shule kwa kitendo kile, yeye aliona hamna shida. Uwezo waliokuwa nao familia yake, ulimfanya apelekwe Makongo, ambapo kama ukichaa, ndiyo ulimpanda vya kutosha.
Nje ya maisha hayo, Hans J alikuwa ana wadogo zake wawili wa kike ambao wakati yeye anaingia UDSM, wao walikuwa kidato cha nne. Wakati huo, baba yake alikuwa ni daktari bingwa hapa Tanzania na mama yake alikuwa ni Mbunge wa viti maalumu.
Hivyo suala la umasikini kwao, wala halikuwepo kabisa. Walikuwa wanajiweza sana, na hawakupata kichwa, eti kwa kuwa mama na baba matajiri, basi tusisome. Hiyo ilikuwa hamna kwa watoto wa familia ile, walikuwa wanasoma kupita maelezo.
Uso wake mpana na wenye usiriazi kila mara, pamoja na kutokuwa na chunusi wala vidoa, huku ukipendezeshwa na rangi ya maji ya kunde, ndiyo nyenzo kubwa iliyofanya wasichana wengi washindwe kulala bali kumuwaza Hans J.
Jamaa alikuwa anatakwa na wanawake wengi sana, kuanzia kidato cha kwanza hadi cha sita. Lakini hakuwahi kuwa na yeyote kati yao.Alikuwa ni mgumu kupitiliza, yaani alikuwa haelewi ni nini maana ya mapenzi na wala alikuwa hana mpango wa kujua maana yake.
Ukiwatoa mama na wadogo zake, Hans hakuwahi kuwafikiria wanawake wengine wa nje hata mara moja katika kalia yake ya maisha.
Jina lake la Crazy Hans, halikuja hivi-hivi. Licha ya vituko vingi vya kisayansi alivyokuwa anavifanya, lakini pia alikuwa ni bingwa wa kuwaumbua wanawake hadharani hasa wale waliokuwa wanamtaka. Hilo pia,lilichangia jina la ukichaa kuendelea kukua siku hadi siku.
Mabinti wengi walikuwa wanawatumia wadogo wa Hans kumletea ujumbe za mapenzi. Lakini mara nyingi kwa Hans, mjumbe alikuwa anauawa tu!. Hao madogo walikuwa wanachezea sana makwenzi na mateke kama wakithubutu kuleta ujumbe hizo.
Sasa kafaulu kuingia UDSM. Huko msimamo wake utakuwaje? Endelea kusoma tu!
JUNIOR KING NICKSON.
Au King Jr kama alivyojiita kisanii. Huyu yeye alimaliza kidato cha nne katika shule iitwayo Bunazi iliyopo Mwanza. Na baada ya kumaliza na yeye akafanikiwa kuendelea na masomo yake ya kidato cha tano na cha sita katika shule ya Sekondari ya Mwanza, iliyopo huko-huko Mwanza. Yeye alikuwa ni mpenzi wa masomo ya sanaa au arts kwa kiingereza, na aliyafaulu vizuri sana, hivyo naye akachaguliwa kuendelea katika chuo hicho-hicho cha Dar Es Salaam au UDSM.
MTUNZI: FRANK MASAI
MAWASILIANO:0752353039
SEASON 1.
ALFRED MUSITA.
ANAPENDA kujiita Fred. Jina ambalo kazoeleka kuitwa na rafiki zake pamoja na ndugu zake pia. Ni kijana mwenye asili ya Kiarabu na Kiafrika, yaani Chotara kwa lugha yetu pendwa ya Kiswahili.
Ni kijana mwenye kila sifa ya kuitwa mtanashati na mtu yeyote duniani. Akiwa kavaa kofia au mzula, waweza sema huyu ni muafrika wa kawaida tu!, ila akivua ndiyo utamtambua kuwa ni mchanganyiko hasa kutokana na nywele zake nyingi na zilizojiviringa vizuri kabisa. Kwa kifupi jamaa ni mzuri na mtanashati.
Baba yake ambaye ni maarufu kwa jina la Mzee Musita, ni Mtanzania halisi kabisa kutoka Mbeya. Na mama yake ni mtu wa Iran.
Alfred au Fred, yeye aliamua kuchukua dini ya baba yake ya kikristo kwa sababu muda mwingi aliishi na baba kuliko mama.
Baada ya kumaliza kidato cha nne katika Shule ya Sekondari ya wavulana, Bwiru, Fred alichaguliwa kuendelea na masomo yake ya kidato cha tano na sita Morogoro Sekondari, na alichukua masomo ya biashara kwa sababu ya hamasa aliyokuwa akipewa na baba yake Mzee Musita, ambaye alikuwa ni maarufu sana hapa Tanzania kutokana na biashara mbalimbali alizokuwa anazimiliki.
Alipomaliza kidato cha sita, matokeo yake yalikuja vizuri, hivyo alichaguliwa kuendelea na masomo hayo katika Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam au UDSM kama wengi hapa Tanzania walivyokiita. Na kama alivyokuwa anaota kila siku, aliweza kutimiza ndoto yake kwa kwenda kuchukua masomo ya Uhasibu.
Kwenye maisha yake tofauti na ya shule, Fred alikuwa ni mpole na mtulivu sana. Hakupenda kufuatilia wanawake japo wanawake wengi walimtaka kimapenzi na wengine kuomba japo wawe naye tu!. Naweza kusema ni dini ambayo alikuwa ameiweka kichwani mwake, ndiyo hasa ilimfanya ajiweke mbali na jinsia ya kike.
Aliishi kwa njia ya maneno ya MUNGU. Hata kwa wale wanawake waliokuwa wanamtakia wazi kuwa wanampenda na kumuhitaji, alikuwa anawakatisha tamaa kwa kutumia maneno hayo kutoka kwenye vitabu vitakatifu.
Kuhusu wazazi wake hasa baba yake, alikuwa si tajiri sana wala masikini kupindukia. Biashara alizokuwa anazifanya, zilikuwa zinampa chakula pamoja na makazi mazuri kabisa ya kulala yeye na mwanae yule wa pekee. Kila alichokitaka Fred, alikipata kwa wakati muafaka kama alivyoahidiwa.
Mama yake Fred alisha-talikiana na Mzee Musita hivyo hakuwa mtu wa mara kwa mara kuonana na Fred, na hata wakionana basi ni kwa muda mchache. Hiyo ni kutokana na mme wake mpya kuwa anambana sana pamoja na wivu.
Na sababu kubwa ya Mzee Musita kutalikiana na Mama Fred, ilikuwa ni rangi ya watu hawa wawili, mmoja Mwarabu na mwingine Mnyakyusa halisi, yule mweusi kabisa. Hapo wazazi wa Mama Alfred, waliingilia na kumtaka mtoto wao aolewe na Mwarabu mwenzake, na hicho ndicho kilichotokea.
Ukitoa Mama Fred kuonana na mwanae uso kwa uso ambapo ilikuwa nadra sana. Walikuwa pia wanawasiliana katika mitandao ya kijamii na MMS.
Neno la dini, ndilo lililokuwa kipaji chake huyu bwana mkubwa.
Hiyo ni kwa kifupi kuhusu Alfred Musita.
HASSAN JENGE.
Huyu alipenda kujiita Hans J, lakini wenzake walishambadilisha jina hilo toka akiwa kidato cha pili kwa kumuita Crazy Hans au kwa Kiswahili Kichaa Hans. Hiyo ni kutokana na mambo pamoja na tabia aliyokuwa nayo.
Hans J, yeye alikuwa ni mrefu kiasi, huku mwili wake ukijengwa kwa rangi ya maji ya kunde.
Baba yake, Mzee Jenge, alikuwa ni Mngoni na mama yake alikuwa ni Mchaga. Mchanganyiko huo, ulimfanya Hassan aonekane ni mtanashati kupindukia.Ndiyo maana yake, jamaa alikuwa ni Handsome haswaa.
Kuhusu tabia huyu jamaa, unaweza kusema ni mhuni sana kama ukimuangalia kwa nje tu!. Kila muda nywele zake zilikuwa tim-tim. Na alipenda sana kuvaa suruali za jinzi na kuzipiga mlege mkubwa tu.
Fulana zake mara nyingi zilikuwa ni mitumba tu. Hakuwahi kuingia dukani na kununua shati au nguo yoyote humo.
Licha ya hayo yote, yaani kuvaa kihuni, kutimua nywele, na kuvaa vitu vya mtumba, huyu Hans alikuwa anajipenda sana. Muda wote alionekana msafi wa kila kitu.Hizo nywele japo zilikuwa tim-tim, lakini zilikuwa ni safi na za kung’aa kutokana na mafuta aliyokuwa anayapaka.
Mwili wake uliyojaa kiasi, na mavazi aliyokuwa anayavaa, ndicho hasa kilimfanya huyu jamaa azidi kuteka wanawake wengi pale alipokuwa anasoma na kuishi.
Kidato cha nne, yeye alimalizia Makongo na baadae aliamua kuendelea na kidato cha tano na sita katika shule ya Sekondari Merriwa iliyopo Dodoma. Alipomaliza masomo hayo, alipata alama za juu pia, na kuchaguliwa kwenda kuendelea na masomo yake katika Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam.
Alikuwa ni mtu wa Sayansi, na aliweza sana kuyamudu masomo yake hayo. Mara nyingi alikuwa anafanya mambo ya hatari sana na ya kushtua kwa kutumia hiyo Sayansi yake, na ndio sababu kubwa ya wanafunzi wenzake kumuita Crazy Hans.
Akiwa kidato cha pili katika shule ya Muheza Muslim iliyopo Tanga. Huyu Hans aliwahi kuchukua kemikali na kuzichanganya kwenye chombo kimoja, na baadae alichukua mchanganyiko huo na kuufungia kwenye chupa ya soda. Aliporidhika, akatoka nje na kuitupa chupa ile kwenye eneo lililokuwa halina watu.
Chupa ilipodondoka, eneo lile la shule lilikuwa kama limevamiwa na magaidi kutokana na mlipuko uliotokea pale. Ilikuwa ni mshike-mshike wa kufa mtu pale shuleni, kuanzia waalimu hadi wanafunzi. Na hata Hans alipoitwa kujibu mashitaka, wala hakuwa na wasiwasi.
Pale alipofukuzwa shule kwa kitendo kile, yeye aliona hamna shida. Uwezo waliokuwa nao familia yake, ulimfanya apelekwe Makongo, ambapo kama ukichaa, ndiyo ulimpanda vya kutosha.
Nje ya maisha hayo, Hans J alikuwa ana wadogo zake wawili wa kike ambao wakati yeye anaingia UDSM, wao walikuwa kidato cha nne. Wakati huo, baba yake alikuwa ni daktari bingwa hapa Tanzania na mama yake alikuwa ni Mbunge wa viti maalumu.
Hivyo suala la umasikini kwao, wala halikuwepo kabisa. Walikuwa wanajiweza sana, na hawakupata kichwa, eti kwa kuwa mama na baba matajiri, basi tusisome. Hiyo ilikuwa hamna kwa watoto wa familia ile, walikuwa wanasoma kupita maelezo.
Uso wake mpana na wenye usiriazi kila mara, pamoja na kutokuwa na chunusi wala vidoa, huku ukipendezeshwa na rangi ya maji ya kunde, ndiyo nyenzo kubwa iliyofanya wasichana wengi washindwe kulala bali kumuwaza Hans J.
Jamaa alikuwa anatakwa na wanawake wengi sana, kuanzia kidato cha kwanza hadi cha sita. Lakini hakuwahi kuwa na yeyote kati yao.Alikuwa ni mgumu kupitiliza, yaani alikuwa haelewi ni nini maana ya mapenzi na wala alikuwa hana mpango wa kujua maana yake.
Ukiwatoa mama na wadogo zake, Hans hakuwahi kuwafikiria wanawake wengine wa nje hata mara moja katika kalia yake ya maisha.
Jina lake la Crazy Hans, halikuja hivi-hivi. Licha ya vituko vingi vya kisayansi alivyokuwa anavifanya, lakini pia alikuwa ni bingwa wa kuwaumbua wanawake hadharani hasa wale waliokuwa wanamtaka. Hilo pia,lilichangia jina la ukichaa kuendelea kukua siku hadi siku.
Mabinti wengi walikuwa wanawatumia wadogo wa Hans kumletea ujumbe za mapenzi. Lakini mara nyingi kwa Hans, mjumbe alikuwa anauawa tu!. Hao madogo walikuwa wanachezea sana makwenzi na mateke kama wakithubutu kuleta ujumbe hizo.
Sasa kafaulu kuingia UDSM. Huko msimamo wake utakuwaje? Endelea kusoma tu!
JUNIOR KING NICKSON.
Au King Jr kama alivyojiita kisanii. Huyu yeye alimaliza kidato cha nne katika shule iitwayo Bunazi iliyopo Mwanza. Na baada ya kumaliza na yeye akafanikiwa kuendelea na masomo yake ya kidato cha tano na cha sita katika shule ya Sekondari ya Mwanza, iliyopo huko-huko Mwanza. Yeye alikuwa ni mpenzi wa masomo ya sanaa au arts kwa kiingereza, na aliyafaulu vizuri sana, hivyo naye akachaguliwa kuendelea katika chuo hicho-hicho cha Dar Es Salaam au UDSM.