Mr Acky
JF-Expert Member
- Nov 24, 2019
- 234
- 313
- Thread starter
- #21
The Hidden Truth ( Ukweli Uliofichika)
MTUNZI : Akida Siri Rambao
Contact : 0658328596
Email: akidasiri@gmail.com
Sehemu 1 (D) : Msasani, Kinondoni -Dar es Saalam
Ilipoishia....
Ghorofani Winifrida wazo la kujiua bado lilikuwa limeutawala mwili, akili na nafsi “qataa” huo ndio mlio pekee uliosikika
masikioni akatulia sekunde kadhaa kusikilizia maumivu ya risasi itakayopenya katika kichwa na kuvuruga ubongo....
Endeleaa....
cha kushangaza hapakuonekana kutoka kwa risasi alistaajabishwa inawezekanaje bastola isiwe na risasi aliiangusha bastola chini kwa kuwa haikuwa na msaada
kwake. Wini alibaki kasimama huku akiwaza na kuwazua njia nyingine maana alidhamiria haswa kuutoa uhai wake mara akagutuka katoka mbio na kufungua mlango akashuka ngazi moja kwa moja hadi jikoni sura imemvimba kwa kulia kwa
uchungu “Heee muone wifi kachukia…” Eva alimshtua dada ake kumuonesha kwa kidole “Khaa! hahahaa sasa tusiseme
ukweli aende zake uko” Ester aliongea kwa sauti na kuendelea kurusha roho, Winifrida muda wote akibumburusha droo akifunga na kufungua Fatuma alibaki kaduwaa tu asijue la kufanya mara Wini akatabasamu akautoa mkono katika droo moja ukiwa na kisu kikubwa, “Haa dada Wini” Fatuma aliacha mwiko katika sufuria na kumrukia Winifrida kumzuia kabla hajakisimika kisu tumboni “Niache Fatuma nasema niache”
Wini alipaza sauti iliyochanganyika na hasira “Nasema niache hunielewi” sauti ya Wini ilisikika tena “Jam… jamani dada
anajiua”. Upande wa sebuleni, “Dada unasikia huko Fatumaanahitaji msaada” Eva alimtumbulia macho dada yake akiwa
na macho ya wasiwasi “We usifanye mchezo na kifo anatuchezea tu achana nae” Ester alijibu na kujikalisha
kwenye sofa huku akiongeza sauti ya kwenye redio huku akiutikisa mwili wake mnene kufatisha miondoko, kelele za
pukurushani ziliendelea jikoni huku Fatuma akihitaji msaada, Fatuma hakumpa nafasi hata kidogo aliendelea kuminyana ili
kukitoa kisu mikononi mwa Wini, kwa bahati mbaya Fatuma akashika makali na Winifrida akiwa na mpini ile kujaribu
kuvuta loo! Kisu kikapita katika kiganja cha fatuma na kula nyama damu ikaanza kumwagika Fatuma kwa maumivu
akiwa kashikilia mkono wake asiamini macho yake damuyakimvuja akabaki kupiga mayowe ya maumivu. Winifrida
akabaki kaduwaa macho yamemtoka akaanza kuyumba akayumba mwisho akadondoka mzima mzima “puuh” “Jamani dadaaaaa” Fatuma akapiga ukelele mkali akisogelea mwili wa
Winifrida, “Kuna nini …Mungu wangu…mafuta ya taa yako wapi” Ester aliongea huku kamshika bega Fatuma macho
yamemtoka, Fatuma alimuonesha tu kwa kidole hakuweza kutokana na uchungu aliokuwa nao, licha ya kuwa alikatwa na kisu na kupatiwa maumivu makali lakini alibaki kuwaza usalama wa mwajiri wake pale chini ambae alionekana kupoteza fahamu, Ester na Eva walishirikiana kwa pamoja kumpa huduma ya kwanza Fatuma na kisha wakamgeukia
Wini aliyekuwa amepoteza fahamu kumjulia hali yake kwa kumpepea na kumkanda na kitambaa cha maji ya vuguvugu mpaka alipo pata fahamu.
Baada ya fahamu kumrudia, Wini alijiswaga swaga mpaka ukutani na kukaa kitako sakafuni akawatazama mawifi zake waliokuwa wamesimama na Fatuma wakimtazama yeye, akawaangalia kwa hasira kwa muda kisha ghafla akanyanyuka na kutoka kwa kasi kuelekea ghorofani kama kishada, na kuwaacha alama za mishangao nyuma yake.
“Wewe sikiliza akirudi bosi wako ole wako unyanyue mdomo wako umenielewa?” Ester aliongea akimtazama Fatuma kwa
jicho la ole wako akimaanisha.
Fatuma alikuwa kajiinamia tu
dhahiri macho yakionesha kutoridhishwa na hali ilivyo akionekana akitamani kufanya kitu kama angepata fulsa.
Winfrida alifanikiwa kuingia chumbani akaufunga mlango.Nje ya nyumba, Jumaa akiwa kajibanza kwenye ukuta kwa
tahadhari simu sikioni akisikiliza upande wa pili, “Ndio madam Moo nimeelewa na nimejaribu kumpigia sana lakini
hapokei…ndio hakuna walinzi zaidi yangu hapa nahofia usalama maana hawaonekani kuwa ni watu wazuri kabisa” Jumaa akajipinda na kuchungulia sebuleni kisha akajirudisha alipokuwa “Sawa sitawaruhusu waondoke” Juma aliongea na kuchungulia tena “…najua, nipe muda ndio kwanza nina siku moja hapa…haina shida haitakuwa rahisi nakuhakikishiamadam nitafanya kwa moyo mmoja mpaka nikamilishe”
Jumaa aliiongea kisha akajichekesha simu bado ikiwa sikioni “Aaah acha tu ilikuwa bahati tu kama ingeshindikana
ningekuwa hata daktari wa familia nisingekubali kirahisi kukosa kazi hapa…naelewa naelelewa nitajitahdi kucontrol
hasira zangu.” Jumaa alitabasamu huku akikuna pua yake“…sawa ngoja niendeleee kumtafuta sawa nitaripoti kwako kila siku” Jumaa akakata simu.
Chelsea Hotel, Mtaa wa uhuru Ilala -Dar es Salaam.
Gari aina ya Subaru Impreza nyekundu iliingia kwa maringo na kusimama katika sehemu ya maegesho, dakika moja tu
ilipita kisha Richard akatoka ndani ya gari na kusimama kwa sekunde na kuitoa miwani yake myeusi toka katika mfuko wa
shati na kuivaa kisha akanyanyua kichwa kutazama urefu wa jengo lililojengwa kwa aina yake na kuelekea eneo la mapokezi. “Ooh mheshimiwa karibu sana…mbona upo mwenyewe nasio kawaida yako” Richard akapokea mkono wa salamu na karibisho katika ukumbi wa mikutano “Ahsante waziri kwanza bila shaka taarifa ya kuchelewa kufika uliipata mapema” aliongea Richard huku bado akiwa kaushikilia mkono wa Waziri “Ndio niliipata” alijibu Waziri na kutabasamu “Basi vizuri…Pili, nafikiri kila kitu nilishakisema kwenye vyombo vya habari kuwa nahitaji kuwa huru na kuwamtu wa kawaida kama zamani sitaki kuongeza maadui na nilionao napenda waache kunichukia na wanione kuwa mimi
si mbaya wao hivyo tu” aliongea Richard kwa kujiamini, waziri akamtazama Richard kwa sekunde kadhaa kisha akaongea “Ni kweli ulisemalo watu kama sisi tunaojihusisha na mambo ya siasa tuna maadui wengi na huwezi mjua yupi ni
yupi unaweza shangaa kisu cha tumbo au bastola ya kichwa bila kutegemea na ukashindwa jua ni nani anaye husika” kisha akatabasamu “Skia waziri kiukweli siasa imenigawa mimi na watu wangu wa karibu hasa mke wangu na hata watu
waliokuwa wananifahamu kama ujuavyo roho yangu ya kutoa lakini imekuwa nikifanya inaonekana naifanyia chama tawala ikanipelekea kuweka migawanyo ya imani juu yangu sijapenda japo wewe hujui yaliyojiri lakini amini hivyo
tafadhari” alimaliza kuongea mheshimiwa Richard na kumuacha mdomo wazi waziri huyo wa elimu bwana Mwijaku Mwasenga “Nimekuelewa vizuri kijana naomba tuanze kikao chetu tafadhari”. Majadiliano yakaanza, nusu saa ikaenda lisaa likapotea “Nashukuru sana Mheshimiwa kwa mara ya kwanza nimeona uwezo wako ambao nilikuwa tu nausikia toka midomoni mwa watu waliowahi kushiriki nawe mambo
kadhaa ya kimaendeleo wakidai una kila sifa nzuri ya kuvutia, hebu niache nikuombe kitu kijana wangu kama hutojali” aliongea Waziri huyo kwa kunong’ona, “Sema tu mzee wangu
kama nitalimudu nitafanya kama sitalimudu itakuwa bahati mbaya kwako” aliongea Richard huku akiachia tabasamu
jembamba akiuvuta mguu wake na kukunja nne. “Unaonaje kama utakuwa mtu Fulani uliyeteuliwa ukasimamia taasisi Fulani nchini ninauwezo wa kumshawishi Mheshimiwa Rais,
kwa sababu nakuona una kila kitu muhimu katika maisha haya una mali za kutosha, elimu, akili, maarifa, busara, unapendwa na watu, una huruma, una moyo wa kutoa,
muungwana…” aliongea Waziri huku Richard akionekana kubadilika akajikuta akikosa raha “Mzee wangu nasikitika kukuona kuwa hujanielewa inatosha sitakuwa tayari” aliongea kwa sauti ya kunyongea sana kisha akasimama
nakuaga huyo akashika njia. ‘Nina kila kitu lakini sina mtoto’ alijisemea nafsini huku akipiga hatua fupi fupi ‘Aisee waziri
kama umetumwa kunichunguza basi huna cha kukipata’ akaingiza mkono mmoja katika mfuko wa suruali na kutoa
simu yake ndogo “Ujumbe…missed call shenzi nimezikosa” alijisemea huku akisogeza mguu wake kwa hatua moja fupimara akasimama sura ikakunjamana ikiambatana na mshangao “Haiwezekani” Haraka haraka akaingia kwenye lift
na kushuka, dakika mbili tu zilimtosha kuwa chini ya ghorofa akakazana kuifata gari yake huku watu kadhaa wakimtazama namna alivyokuwa kawaida bila makuu. “Halow natoka hapa
usalama wangu upo sawa? vizuri naelekea nyumbani kuna tatizo naomba baadhi yenu mumfatilie Waziri Mwijaku kwa
karibu zaidi” aliongea huku akikikandamiza kitu sikioni.
Haraka alizungusha funguo akavuta mafuta na kubadili gia mkuku mkuku akatoka eneo hilo. “Haloow mheshimiwa raisnimejaribu kumshawishi kadri nilivyoweza lakini inaonekana bwana huyu amenuia kabisa na kwa taarifa nilizozipata amefukuza walinzi wote nyumbani kwake na kuwapunguza
baadhi ya wafanyakazi wa ndani… “ndio mheshimiwa lakini anaonekana mara zote ni mtu anaejiamini lakini ni kama ana
wasiwasi kama sio hofu” aliongea waziri Mwijaku huku akichukua glasi ya maji mezani “Yaah hata mimi naamini hilo
kuna mtu atakuwa ameamua kufanya kazi naye kwa siri si bure…ngoja nitatuma vijana wangu wamfatilie taratibu
mheshimiwa huenda tukajua sababu iliyomvunja nguvu” waziri Mwijaku akatoa simu sikioni na kushusha pumzi nzito
huku akiwatazama vijana wake.
Msasani, Kinondoni-Dar es Salaam
“Brhiiiiiiik” matairi ya gari yalisuguliwa katika rami kwa breki kali karibu kabisa na geti. Geti likafunguliwa kuipisha gari
kuingia, “Inamaana wapo hapa muda mrefu” aliongea akimuacha Juma kwa nyuma na kuelekea mlangoni, “Mbona
mnakuja bila taarifa” maneno yalimtoka mheshimiwa huku akihema na kurudishia mlango kwa kuubamiza akawatazama
dada zake ambao waliishia kuinamisha vichwa vyao. Sura ya Richard ikaendelea kujawa na hofu zaidi, akaamua kutoka
eneo alilokuwepo na kuzikabili ngazi kupandisha ghorofani kiasi cha kuwafanya dada zake kusimama huku
wakitazamana.
Miguu ikaanza kuwa mizito nguvu zikiendelea kumuisha “Ooh nimechelewa kukuokoa mke wangu tafadhari
kuwa salama” alijikuta akijiongelea mwenyewe huku machozi yakimtoka akiendelea kupanda.Hamadi alipofungua mlango tu mwili ulianza kumzizima
hakuamini macho yake hakuamini alichokiona akayafumba macho yake na kuyafumbua loo! alipoona si utani uchungu ulimzidi kutawala moyo wake mdomo ukaanza kutetemeka
machozi nayo yakaanza kumtiririka kama maji mlimani “Mmmmh mmmmh…. mke wanguuuuuu” kwikwi haswa ilikaa
koooni maneno hayakumalizwa kinywani mwake. Mwili wa Winifrida sakafuni haukujigeuza wala kutikisika tangu
ulipotulia, Richard alianza kupiga hatua za taratibu mfano wa mtoto anae anza kujifunza kutembea akijihimu huku akipepesuka mpaka karibu yake. Kilichommaliza zaidi nguvu na kumfanya ashuke taratibu sakafuni ni pale macho yake yalipokutana na bastora iliyokaa karibu na mwili wa mkewe. Richard alikuwa kama zuzu aliangazaangaza kukitazama chumba ambacho kilikuwa vululu vitu vimetapakaa pahala
pote pa chumba alijisogeza na kuegemea kitanda alipo tazama mkono wake wa kuume akaona kifuko kidogo cha dawa
alikitazama na kukitambua alijiinamia kisha akanyanyua kichwa na kuizungusha shingo pahala pengine na mwishowe
macho yakaishia katika kitanda ambapo napo hapakuwa Patupu alikiona kikaratasi chenye maandishi juu ya godoro.
Richard bado na muonekano wa kama zuzu kamasi zikimtokapuani alijitahidi kusimama akapiga hatua moja ya pili akiruka damu damu ambazo zilikuwa zina vuja toka kichwani mwa Winifrida, alisogea na kukaa katika kona ya kitanda. Richardakakichukua kipande cha karatasi na kuanza kukisoma. “Mke wangu… mke wangu jamani” aliyaongea maneno hayo baada ya kusoma ujumbe alioukuta. Kijana wa watu akajikalisha sakafuni taratibu akamtazama mkewe kwa jicho la huzuni kumbukumbu mbalimbali zikamtembelea na kumuumiza sana
moyo wake loo alijiona mkiwa kweli kweli hasa tabasamu zuri la mkewe lilimmaliza nguvu, aliwaza mengi sana na
kukumbuka kauli mbalimbali za mkewe kipindi kile walipo toka Hospitali.
Mawazo yalipofika tamati alijipangusa machozi akajiburuza hadi karibu na bastora akaikagua kisha akajisimamisha kiuchovu na kulisogelea kabati la nguo
alinyanyua mkono wake na kupapasa mpaka alipopata alichokitaka akaacha, mkononi alikuwa kashikilia risasi moja
akajisogeza hadi kwenye mwili wa mkewe akajikalisha na kutulia akaiweka risasi katika chemba na kuipachika kichwani
tayari kwa kufyatua. Richard wala hakuwa na wazo lingine zaidi ya kujiua hakuwaza kumtikisa mkewe hakuwaza
kumpeleka hospitali hakuwaza kubahatisha kuokoa maisha ya
mkewe kwa sababu aliamini asilimia mia kuwa mkewe ni marehemu hivyo hakuwa na mpango tofauti zaidi ya kujiua.
Baada ya kuweka vizuri akafumba macho huku mkono mmoja ukiwa begani mwa mkewe, “Mke wangu ngoja tu nikufate
maana nikibaki nitakuwa nimevunja ahadi yangu” alipo kuwa anaendeleaa kulia kwa uchungu na kujiongelesha mwenyewe
mwili wa Wini ukaanza kutikisika, Richard wa watu alibaki akitazama kwa mshangao akiwa na hali ya furaha akatulia
kumuangalia mkewe vizuri, Wini akajigeuza tena hukukujinyoosha huku akiyafumbua macho yake. Richard akamvamia mkewe na kuanza kumtingisha na kumuita kwa
jina huku akimgusa mapigo ya moyo “…Ooh asante Mungu mke wangu hujafa?!!” Richard akaitupa bastola ukutani na
kumnyanyua mkewe kumkalisha kitako huku akiwa anahema hovyo hovyo akimuita mfululizo “Mke wangu …mke
wangu…jamani mke wangu… ooh jamani mke wangu”. Richard alimkumbatia kwa furaha mkewe, Wini yeye alibaki
kumtazama tu usoni mumewe bado akiwa na wenge la kuponyoka na kifo alionekana kama mtu asiyejielewa alibaki
kumtazama tu usoni. “Mke wangu sina thibitisho la kunipendainatosha usifanye hivi tena tafadhari, najua mwenyezi Mungu amenipendelea sana kunirudishia furaha yangu naahidi kuto rudia kosa mke wangu sito kuacha ata nzi akukere sitakaa mbali nawe tena” Richard alimkumbatia zaidi mkewe na
kumpiga mabusu mfululizo ya kichwa huku Wini akionekana kutulia akaiweka risasi katika chemba na kuipachika kichwani
tayari kwa kufyatua. Richard wala hakuwa na wazo lingine zaidi ya kujiua hakuwaza kumtikisa mkewe hakuwaza kumpeleka hospitali hakuwaza kubahatisha kuokoa maisha yamkewe kwa sababu aliamini asilimia mia kuwa mkewe ni marehemu hivyo hakuwa na mpango tofauti zaidi ya kujiua.
Baada ya kuweka vizuri akafumba macho huku mkono mmoja ukiwa begani mwa mkewe, “Mke wangu ngoja tu nikufate
maana nikibaki nitakuwa nimevunja ahadi yangu” alipo kuwa anaendeleaa kulia kwa uchungu na kujiongelesha mwenyewe
mwili wa Wini ukaanza kutikisika, Richard wa watu alibaki akitazama kwa mshangao akiwa na hali ya furaha akatulia
kumuangalia mkewe vizuri, Wini akajigeuza tena hukukujinyoosha huku akiyafumbua macho yake. Richard akamvamia mkewe na kuanza kumtingisha na kumuita kwa
jina huku akimgusa mapigo ya moyo “…Ooh asante Mungu mke wangu hujafa?!!” Richard akaitupa bastola ukutani na
kumnyanyua mkewe kumkalisha kitako huku akiwa anahema hovyo hovyo akimuita mfululizo “Mke wangu …mke
wangu…jamani mke wangu… ooh jamani mke wangu”. Richard alimkumbatia kwa furaha mkewe, Wini yeye alibaki
kumtazama tu usoni mumewe bado akiwa na wenge la kuponyoka na kifo alionekana kama mtu asiyejielewa alibaki kumtazama tu usoni. “Mke wangu sina thibitisho la kunipendainatosha usifanye hivi tena tafadhari, najua mwenyezi Mungu
amenipendelea sana kunirudishia furaha yangu naahidi kuto rudia kosa mke wangu sito kuacha ata nzi akukere sitakaa
mbali nawe tena” Richard alimkumbatia zaidi mkewe na kumpiga mabusu mfululizo ya kichwa huku Wini akionekana kwenye sofa maana alipigwa la kushtukiza alitulia kajishika shavu akiugulia maumivu makali. “Mpumbavu wewe usiongee
upuuzi mbele yangu shwaini” alifoka Richard huku akimuangalia Eva kwa jicho lenye hasira sana. “Sikiliza Richard najua unaongea kwa kujiamini sana kwa kuwa tupo kwako, lakini tambua kuwa sisi ndugu zako tunakupenda sana halafu kingine kaa ukijua kuwa unapoteza muda bure na huyo mwanamke” Ester aliingilia kuongea kwa utulivu sana na sio kwa kupayuka kila mtu pale sebureni aliweza kusikia vizuri hapakuhitajika kurudiwa, yalikuwa ni maneno mazito kwa
kijana Rich yalitibua tibua chungu ya moyo akashindwa kujizuia alijikuta anapayuka kwa nguvu “Nasema ondokeni
nyumbani kwangu sasa hivi” “Hatuondoki lolote fanya mpaka utuelewe” Ester nae aliongea kwa jazba tena kwa kujiamini,
Richard aliona anapotezewa muda aliamua kuchukua simu mfukoni mwa suruali yake na kutafuta namba na kupiga, dada zake walibaki wakimtazama tu. “Hallow…yes afande maunaomba mje nyumbani kwangu kuna uvamizi hapa… okay sawa” Richard alitoka eneo hilo na kusogea pahala ambapo meza ya chakula ilikuwepo na ndipo mkewe alikuwa
amejituliza akishuhudia malumbano yanayo sababishwa na yeye. ‘Roho inaniuma sana matatizo yangu leo yana
wapelekea ndugu kugombana’ Winifrida alijisemea nafsini.
Richard alisogea na akaanza kupakuwa chakula na kumnawisha mkewe na kuanza kula huku akimlisha na mkewe kwa tabu tabu. Ndugu wakabaki wakitazama tu kwa mishangao.
Chakula hakikuisha kwenye sahani nje kulisikika honi kali, Juma akiwa hana hili wala lile alitazama katika ukuta kupitia kifaa maalumu “Hee magwanda tena” aliongea na kuchapuka kutoka mbio “Jamani polisi wamekuja…” kauli hiyo ndo ya kwanza kumtoka baada ya kufungua mlango na kuingia ndani huku akihema bila mpangilio macho yakimtoka na kushangaa shangaa “Waruhusu waingie tu” aliongea Richard akiwa hana
wasiwasi kabisa, dada zake walibaki wakitazamana kwa mshangao. Jumaa huyo akatoka, punde Juma na maaskari
watatu wakawa wapo ndani ya nyumba ya Richard “Karibuni sana maafisa nawaomba mnitolee hao watu kwa sababu wanatishia usalama wa familia yangu na muwaambie wasije
wakakanyaga tena hapa ni hilo tu wala msiwapelekerumande” Richard aliongea huku akionesha kidole kwa dada
zake “Jamani Richard wewe wakutuitia polisi leo ama kweli dunia hadaa walimwengu shujaa, wewe niliyekuachia ziwa wewe ukanyonya unanitoa kwako kwa kutumia polisi?” Ester aliongea kwa uchungu mkubwa huku machozi yakimlenga, dada huyu yeye hakuamini kama kweli ndugu yake atafikia
hatua hiyo sasa ndipo alipo amini kuwa basi nia yake imefeli, aligeuza sura akamtazama wifi yake kwa jicho la hasira sana akarudisha uso kwa ndugu yake Eva, “Mdogo wangu naona umejionea amechagua penzi na ndugu kawaacha basi kuanzia sasa sisi sio ndugu zake” Eva alitingisha kichwa huku jicho la chuki likiwa kwa wifi yake, polisi hawakuacha ngonjera ziendelee waliwasogelea na kuwaamuru watoke na wao wakatii. “Tafadhari naomba muhakikishe habari hizi haziwafikii waandishi wa habari kwa gharama zozote…mnajua wazi watu wananiwinda kuchafua sifa yangu…vizuri” Richard alimaliza kuongea akakata simu huku akirudishia pazia alilokuwa amelipenyua.“Mke wangu pole, hakuna atakae kuja kututenganisha zaidi ya
Mungu na wala sio watu, sipo tayari kukukosa kabisa” aliongea Mheshimiwa huku akimvutia mkewe kifuani hii
baada ya kukaa sofani. “Haa Fatuma …” Wini akatahamaki na kujinasua kifuani akanyanyuka na kumfata Fatuma ambaye
alionekana kujiegemeza ukutani akitabasamu huku ameushika mkono wake uliojeruhiwa akamkumbatia “Pole
jamani pole mdogo wangu” aliongea Winifrida huku akimshika bega Fatuma na kumvutia kifuani “Hamna dada
usiwe na hofu kikubwa wewe ni mzima ndio jambo la kushukuru” Fatuma aliongea huku kichwa kikiwa begani mwa
Wini, Richard alikuwa hajaelewa kitu hivyo alibaki kuwatazama tu kwa furaha. Wini alijinasua katika kifua cha Fatuma na kumuangalia mumewe, “Mume wangu Fatuma alikuwa ananizuia nisijiumize pindi nilipokuwa nampokonya kisu nikamjeruhi katika kiganja chake inaniuma sana” Richard ndipo akazibuka masikio nakushangaa akanyanyuka kujionea
“Asante sana Fatuma kwa moyo wako haya jiandae basi nikupeleke hospitali ukatazamwe majeraha” “Sawa kaka
ngoja nimuwekee chakula Jumaa aje kula bado hajakula nilisahau kumuita” “Ooh hapana nitafanya na uende Hospitali
mpendwa” alidakia Winifrida.Tatizo la mtoto katika nyumba ya mheshimiwa Richardlilianza kuzoeleka, lakini haikuwa rahisi katika moyo wa Winifrida liliendelea kuishi na kuitafuna subira na imani yake
iliyobakia ndani ya moyo wake. Winifrida aliendelea kucheka, kufurahi, kula na kuendelea na shughuli zake za kila siku
lakini yote yalikuwa ni maigizo. Usiku mmoja, Winifrida akiwa kajilaza macho juu, alijigeuza na kumuangalia mumewe aliyekuwa mbali kwa usingizi akamtazama jinsi alivyo “Wewe ni Handsome sana mume wangu ukilala hata ukiamka” alijiongelea Winifrida na kutabasamu akaanza kumshika shika mashavu mumewe na lips, alifanya hivyo mpaka Richard alipofumbua macho na
kumtazama “Vipi mke wangu mbona hulali” aliongea bwana Richard kwa sauti ya kichovu chovu, Winifrida alichukua
muda wa takribani dakika tatu akimuangalia tu ndipo alipoamua kusema “Mume wangu najua hupendi kuniona
naongelea tatizo hili ila mimi nimepata njia” “Umepata njia” Richard usingizi ulimpaa macho yakamtoka na akajinyanyua kukaa kitako, “Njia gani mke wangu” Wini nae alifata kwa kunyanyuka na kukaa kitako, “Sio njia nzuri sana…ni kuwa mume wangu, mi naomba utafute mwanamke mwingine uzae nae mi uniache…” kabla haja malizia, Richard alishtushwa sana, hali yake ilianza kubadilika moyo ulimbana pumzi
zikaanza kutoka kwa tabu, akaanza kutweta akikohoa hovyo huku mkono ukiwa katika koo lake kama mtu aliyebanwa kwa loba kooni. Wini alishtuka na kuogopa sana akaanza kumpiga
piga mgongoni kumtuliza lakini wapi akachukua nguo na kuanza kumpepea huku akilalamika “Mume wangu unanini…
jamani mume wanguu” mwisho hali ikaanza kupungua huku Richard macho yakiwa mekundu yamemtoka na machozi
yakimteremka, Wini alimsogeza na kumkumbatia “Basi mume wangu sitataka kukuacha tena sitarudia nakupenda mume wangu, sitasema tena nilichokisema basi tujaribu kumuhasili
mtoto” Richard akiwa kakiweka kichwa kwenye mapaja ya mkewe alisikia lakini uwezo wa kujibu hakuwa nao kwa taabani aliyokuwa nayo, ama kweli mapenzi ni uchawi wa ajabu.
Siku nazo zikaanza kusonga zikienda mbio mbio kama zinakimbizwa, watu mbali mbali wakaanza kumshauri Winifrida kuhusu kuingia katika masuala ya waganga wa jadi kujaribu bahati yake maana wengi hubahatika waliongea kwa
majivuno. Maneno mengi aliambiwa yeye aliishia kuwajibukuwa atafikiria, upande wa mumewe nae mambo yalikuwa
sawa tu na kwa mkewe marafiki na jamaa wengine walimshauri kuhusu kutafuta waganga nae aliwajibu atafikiria.
Kadri siku zilivyokwenda na wao walianza kulewa na maneno ya watu imani ikawatoka na kuanza kuamini mambo ya
waganga wa jadi na sio Mungu tena kama awali. Hatua ya kwanza ilikuwa ni kuwatembelea hao waganga waliokuwa
wanasifika tena bila kukata tamaa, walichanjwa chale wakalishwa madawa ya kila namna wakapewa masharti ya
namna tofauti kulala chini, kuoga na nguo, kwenda kutupa vitu makaburini na mambo mengine ya ajabu kibao kama kawaida ya waganga wengi walivyo. Marafiki na jamaa zao baada ya kuona hakuna mfanikio wala mabadiliko yoyote ndipo wakayaweka wazi midomoni kuwa Winifrida atakuwa
ni tasa kabisa hakuna la ziada. Kama ilivyo marafiki si wakufanana wapo wazuri na wabaya, kati yao kuna waliojikuta wakimkosea sana Richard kwa kuthubutu
kumshawishi amsaliti mkewe na kuzaa nje ya nyumba yake kisiri ili tu awe na mbegu ambayo itakuja kurithi mali zake, jambo hilo lilipelekea kutofautiana baina yake na hao marafiki na hata kuvunja mahusiano kabisa. Richard alikuwa mkali sana hakuwa tayari. Richard na Winifrida walikaa wakachambua wakawaza mioyo yao nayo ilianza kubadilika taratibu na kuanza kusalimu amri kukubali hali halisi kuwa mtoto ni zawadi na hupewa yoyote endapo mwenyezi Mungu akipenda na sio kuwa inatoka kwa binadamu wenzao,
walitubu kwa tabia mbaya walioyoifanya kwa kumkosea mola wao na kuanza maisha mapya.“Ni balaa zito! Tumemuona Bwana Fanuel Mkwasi akiwa makaburini dhahiri ni mtu mwenye uchungu na familia yake aliyoipoteza, alimvamia Mzee
Ishengoma akihitaji ukweli kuhusu familia yake lakini aliukosa na kuishia kumuua huku akibaki na kiapo cha sehemu ya ukweli uliobaki. MheshimiwaRichard nae alifanikiwa kushinda kesi dhidi ya washindani wake bila kutegemea huku akipewa taarifa na wakili wake kuhusu kufojiwa kwa ushahidi na kuhitajika kukutana na mheshimiwa raisi haraka, lakini hatujajua walikutana au hawakukutana na kama walikutana waliongea nini! Miaka mitano ikapita, Winifrida mke wa Richard anaonekana kuwa na kitu kinachomnyima raha kwa miaka mingi hadi kufikia kukumbuka namna ndoa yao ilivyofungwa bila kubainisha, na mwisho wa siku alimshawishi mumewe kuishi maisha ya kawaida na kuyatupilia mbali maisha ya Siasa, je! kwanini? Waliwapunguza walinzi na wafanyakazi na kumuajiri mlinzi mmoja ambaye hatukujua alimtolea wapi, lakini alionekana mheshimiwa Richard kuwa na
walinzi wa siri wakimlinda kila aendapo bila mkewe kujua. Mgongoni mwa
mheshimiwa Richard anaonekana akifatiliwa na watu wa Raisi kwa siri kupitia waziri Mwijaku aliyetumwa kumshawishi bila mafanikio pamoja na Kijana aliyemuamini na kumuajili kuwa mlinzi wa nyumba yao naye kuoneakana
kuwa na kazi ya ziada tofauti na ulinzi. Huzuni ya kukosa mtoto ilimtawala
Richard na mkewe na kuamua kufanya matibabu wanaligundua tatizo na
kuamua kuishi nalo lakini changamoto nyingi zakuingiliwa na ndugu, jamaa
na marafiki hazikukoma kuwaandama. Je! Kijana Jumaa anampango gani na
familia ya Richard na aliwezaje kuishi humo? Je! wanandoa hao wataweza
kuvumiliana kwa hali hiyo ya kukosa mtoto na kudumisha mapenzi yao? Je!
Fanuel Mkwasi atawezakufanikisha ataweza upata ukweli anao utafuta?”
Itaendeleaaaa....
Mijadara inaruhusiwa
MTUNZI : Akida Siri Rambao
Contact : 0658328596
Email: akidasiri@gmail.com
Sehemu 1 (D) : Msasani, Kinondoni -Dar es Saalam
Ilipoishia....
Ghorofani Winifrida wazo la kujiua bado lilikuwa limeutawala mwili, akili na nafsi “qataa” huo ndio mlio pekee uliosikika
masikioni akatulia sekunde kadhaa kusikilizia maumivu ya risasi itakayopenya katika kichwa na kuvuruga ubongo....
Endeleaa....
cha kushangaza hapakuonekana kutoka kwa risasi alistaajabishwa inawezekanaje bastola isiwe na risasi aliiangusha bastola chini kwa kuwa haikuwa na msaada
kwake. Wini alibaki kasimama huku akiwaza na kuwazua njia nyingine maana alidhamiria haswa kuutoa uhai wake mara akagutuka katoka mbio na kufungua mlango akashuka ngazi moja kwa moja hadi jikoni sura imemvimba kwa kulia kwa
uchungu “Heee muone wifi kachukia…” Eva alimshtua dada ake kumuonesha kwa kidole “Khaa! hahahaa sasa tusiseme
ukweli aende zake uko” Ester aliongea kwa sauti na kuendelea kurusha roho, Winifrida muda wote akibumburusha droo akifunga na kufungua Fatuma alibaki kaduwaa tu asijue la kufanya mara Wini akatabasamu akautoa mkono katika droo moja ukiwa na kisu kikubwa, “Haa dada Wini” Fatuma aliacha mwiko katika sufuria na kumrukia Winifrida kumzuia kabla hajakisimika kisu tumboni “Niache Fatuma nasema niache”
Wini alipaza sauti iliyochanganyika na hasira “Nasema niache hunielewi” sauti ya Wini ilisikika tena “Jam… jamani dada
anajiua”. Upande wa sebuleni, “Dada unasikia huko Fatumaanahitaji msaada” Eva alimtumbulia macho dada yake akiwa
na macho ya wasiwasi “We usifanye mchezo na kifo anatuchezea tu achana nae” Ester alijibu na kujikalisha
kwenye sofa huku akiongeza sauti ya kwenye redio huku akiutikisa mwili wake mnene kufatisha miondoko, kelele za
pukurushani ziliendelea jikoni huku Fatuma akihitaji msaada, Fatuma hakumpa nafasi hata kidogo aliendelea kuminyana ili
kukitoa kisu mikononi mwa Wini, kwa bahati mbaya Fatuma akashika makali na Winifrida akiwa na mpini ile kujaribu
kuvuta loo! Kisu kikapita katika kiganja cha fatuma na kula nyama damu ikaanza kumwagika Fatuma kwa maumivu
akiwa kashikilia mkono wake asiamini macho yake damuyakimvuja akabaki kupiga mayowe ya maumivu. Winifrida
akabaki kaduwaa macho yamemtoka akaanza kuyumba akayumba mwisho akadondoka mzima mzima “puuh” “Jamani dadaaaaa” Fatuma akapiga ukelele mkali akisogelea mwili wa
Winifrida, “Kuna nini …Mungu wangu…mafuta ya taa yako wapi” Ester aliongea huku kamshika bega Fatuma macho
yamemtoka, Fatuma alimuonesha tu kwa kidole hakuweza kutokana na uchungu aliokuwa nao, licha ya kuwa alikatwa na kisu na kupatiwa maumivu makali lakini alibaki kuwaza usalama wa mwajiri wake pale chini ambae alionekana kupoteza fahamu, Ester na Eva walishirikiana kwa pamoja kumpa huduma ya kwanza Fatuma na kisha wakamgeukia
Wini aliyekuwa amepoteza fahamu kumjulia hali yake kwa kumpepea na kumkanda na kitambaa cha maji ya vuguvugu mpaka alipo pata fahamu.
Baada ya fahamu kumrudia, Wini alijiswaga swaga mpaka ukutani na kukaa kitako sakafuni akawatazama mawifi zake waliokuwa wamesimama na Fatuma wakimtazama yeye, akawaangalia kwa hasira kwa muda kisha ghafla akanyanyuka na kutoka kwa kasi kuelekea ghorofani kama kishada, na kuwaacha alama za mishangao nyuma yake.
“Wewe sikiliza akirudi bosi wako ole wako unyanyue mdomo wako umenielewa?” Ester aliongea akimtazama Fatuma kwa
jicho la ole wako akimaanisha.
Fatuma alikuwa kajiinamia tu
dhahiri macho yakionesha kutoridhishwa na hali ilivyo akionekana akitamani kufanya kitu kama angepata fulsa.
Winfrida alifanikiwa kuingia chumbani akaufunga mlango.Nje ya nyumba, Jumaa akiwa kajibanza kwenye ukuta kwa
tahadhari simu sikioni akisikiliza upande wa pili, “Ndio madam Moo nimeelewa na nimejaribu kumpigia sana lakini
hapokei…ndio hakuna walinzi zaidi yangu hapa nahofia usalama maana hawaonekani kuwa ni watu wazuri kabisa” Jumaa akajipinda na kuchungulia sebuleni kisha akajirudisha alipokuwa “Sawa sitawaruhusu waondoke” Juma aliongea na kuchungulia tena “…najua, nipe muda ndio kwanza nina siku moja hapa…haina shida haitakuwa rahisi nakuhakikishiamadam nitafanya kwa moyo mmoja mpaka nikamilishe”
Jumaa aliiongea kisha akajichekesha simu bado ikiwa sikioni “Aaah acha tu ilikuwa bahati tu kama ingeshindikana
ningekuwa hata daktari wa familia nisingekubali kirahisi kukosa kazi hapa…naelewa naelelewa nitajitahdi kucontrol
hasira zangu.” Jumaa alitabasamu huku akikuna pua yake“…sawa ngoja niendeleee kumtafuta sawa nitaripoti kwako kila siku” Jumaa akakata simu.
Chelsea Hotel, Mtaa wa uhuru Ilala -Dar es Salaam.
Gari aina ya Subaru Impreza nyekundu iliingia kwa maringo na kusimama katika sehemu ya maegesho, dakika moja tu
ilipita kisha Richard akatoka ndani ya gari na kusimama kwa sekunde na kuitoa miwani yake myeusi toka katika mfuko wa
shati na kuivaa kisha akanyanyua kichwa kutazama urefu wa jengo lililojengwa kwa aina yake na kuelekea eneo la mapokezi. “Ooh mheshimiwa karibu sana…mbona upo mwenyewe nasio kawaida yako” Richard akapokea mkono wa salamu na karibisho katika ukumbi wa mikutano “Ahsante waziri kwanza bila shaka taarifa ya kuchelewa kufika uliipata mapema” aliongea Richard huku bado akiwa kaushikilia mkono wa Waziri “Ndio niliipata” alijibu Waziri na kutabasamu “Basi vizuri…Pili, nafikiri kila kitu nilishakisema kwenye vyombo vya habari kuwa nahitaji kuwa huru na kuwamtu wa kawaida kama zamani sitaki kuongeza maadui na nilionao napenda waache kunichukia na wanione kuwa mimi
si mbaya wao hivyo tu” aliongea Richard kwa kujiamini, waziri akamtazama Richard kwa sekunde kadhaa kisha akaongea “Ni kweli ulisemalo watu kama sisi tunaojihusisha na mambo ya siasa tuna maadui wengi na huwezi mjua yupi ni
yupi unaweza shangaa kisu cha tumbo au bastola ya kichwa bila kutegemea na ukashindwa jua ni nani anaye husika” kisha akatabasamu “Skia waziri kiukweli siasa imenigawa mimi na watu wangu wa karibu hasa mke wangu na hata watu
waliokuwa wananifahamu kama ujuavyo roho yangu ya kutoa lakini imekuwa nikifanya inaonekana naifanyia chama tawala ikanipelekea kuweka migawanyo ya imani juu yangu sijapenda japo wewe hujui yaliyojiri lakini amini hivyo
tafadhari” alimaliza kuongea mheshimiwa Richard na kumuacha mdomo wazi waziri huyo wa elimu bwana Mwijaku Mwasenga “Nimekuelewa vizuri kijana naomba tuanze kikao chetu tafadhari”. Majadiliano yakaanza, nusu saa ikaenda lisaa likapotea “Nashukuru sana Mheshimiwa kwa mara ya kwanza nimeona uwezo wako ambao nilikuwa tu nausikia toka midomoni mwa watu waliowahi kushiriki nawe mambo
kadhaa ya kimaendeleo wakidai una kila sifa nzuri ya kuvutia, hebu niache nikuombe kitu kijana wangu kama hutojali” aliongea Waziri huyo kwa kunong’ona, “Sema tu mzee wangu
kama nitalimudu nitafanya kama sitalimudu itakuwa bahati mbaya kwako” aliongea Richard huku akiachia tabasamu
jembamba akiuvuta mguu wake na kukunja nne. “Unaonaje kama utakuwa mtu Fulani uliyeteuliwa ukasimamia taasisi Fulani nchini ninauwezo wa kumshawishi Mheshimiwa Rais,
kwa sababu nakuona una kila kitu muhimu katika maisha haya una mali za kutosha, elimu, akili, maarifa, busara, unapendwa na watu, una huruma, una moyo wa kutoa,
muungwana…” aliongea Waziri huku Richard akionekana kubadilika akajikuta akikosa raha “Mzee wangu nasikitika kukuona kuwa hujanielewa inatosha sitakuwa tayari” aliongea kwa sauti ya kunyongea sana kisha akasimama
nakuaga huyo akashika njia. ‘Nina kila kitu lakini sina mtoto’ alijisemea nafsini huku akipiga hatua fupi fupi ‘Aisee waziri
kama umetumwa kunichunguza basi huna cha kukipata’ akaingiza mkono mmoja katika mfuko wa suruali na kutoa
simu yake ndogo “Ujumbe…missed call shenzi nimezikosa” alijisemea huku akisogeza mguu wake kwa hatua moja fupimara akasimama sura ikakunjamana ikiambatana na mshangao “Haiwezekani” Haraka haraka akaingia kwenye lift
na kushuka, dakika mbili tu zilimtosha kuwa chini ya ghorofa akakazana kuifata gari yake huku watu kadhaa wakimtazama namna alivyokuwa kawaida bila makuu. “Halow natoka hapa
usalama wangu upo sawa? vizuri naelekea nyumbani kuna tatizo naomba baadhi yenu mumfatilie Waziri Mwijaku kwa
karibu zaidi” aliongea huku akikikandamiza kitu sikioni.
Haraka alizungusha funguo akavuta mafuta na kubadili gia mkuku mkuku akatoka eneo hilo. “Haloow mheshimiwa raisnimejaribu kumshawishi kadri nilivyoweza lakini inaonekana bwana huyu amenuia kabisa na kwa taarifa nilizozipata amefukuza walinzi wote nyumbani kwake na kuwapunguza
baadhi ya wafanyakazi wa ndani… “ndio mheshimiwa lakini anaonekana mara zote ni mtu anaejiamini lakini ni kama ana
wasiwasi kama sio hofu” aliongea waziri Mwijaku huku akichukua glasi ya maji mezani “Yaah hata mimi naamini hilo
kuna mtu atakuwa ameamua kufanya kazi naye kwa siri si bure…ngoja nitatuma vijana wangu wamfatilie taratibu
mheshimiwa huenda tukajua sababu iliyomvunja nguvu” waziri Mwijaku akatoa simu sikioni na kushusha pumzi nzito
huku akiwatazama vijana wake.
Msasani, Kinondoni-Dar es Salaam
“Brhiiiiiiik” matairi ya gari yalisuguliwa katika rami kwa breki kali karibu kabisa na geti. Geti likafunguliwa kuipisha gari
kuingia, “Inamaana wapo hapa muda mrefu” aliongea akimuacha Juma kwa nyuma na kuelekea mlangoni, “Mbona
mnakuja bila taarifa” maneno yalimtoka mheshimiwa huku akihema na kurudishia mlango kwa kuubamiza akawatazama
dada zake ambao waliishia kuinamisha vichwa vyao. Sura ya Richard ikaendelea kujawa na hofu zaidi, akaamua kutoka
eneo alilokuwepo na kuzikabili ngazi kupandisha ghorofani kiasi cha kuwafanya dada zake kusimama huku
wakitazamana.
Miguu ikaanza kuwa mizito nguvu zikiendelea kumuisha “Ooh nimechelewa kukuokoa mke wangu tafadhari
kuwa salama” alijikuta akijiongelea mwenyewe huku machozi yakimtoka akiendelea kupanda.Hamadi alipofungua mlango tu mwili ulianza kumzizima
hakuamini macho yake hakuamini alichokiona akayafumba macho yake na kuyafumbua loo! alipoona si utani uchungu ulimzidi kutawala moyo wake mdomo ukaanza kutetemeka
machozi nayo yakaanza kumtiririka kama maji mlimani “Mmmmh mmmmh…. mke wanguuuuuu” kwikwi haswa ilikaa
koooni maneno hayakumalizwa kinywani mwake. Mwili wa Winifrida sakafuni haukujigeuza wala kutikisika tangu
ulipotulia, Richard alianza kupiga hatua za taratibu mfano wa mtoto anae anza kujifunza kutembea akijihimu huku akipepesuka mpaka karibu yake. Kilichommaliza zaidi nguvu na kumfanya ashuke taratibu sakafuni ni pale macho yake yalipokutana na bastora iliyokaa karibu na mwili wa mkewe. Richard alikuwa kama zuzu aliangazaangaza kukitazama chumba ambacho kilikuwa vululu vitu vimetapakaa pahala
pote pa chumba alijisogeza na kuegemea kitanda alipo tazama mkono wake wa kuume akaona kifuko kidogo cha dawa
alikitazama na kukitambua alijiinamia kisha akanyanyua kichwa na kuizungusha shingo pahala pengine na mwishowe
macho yakaishia katika kitanda ambapo napo hapakuwa Patupu alikiona kikaratasi chenye maandishi juu ya godoro.
Richard bado na muonekano wa kama zuzu kamasi zikimtokapuani alijitahidi kusimama akapiga hatua moja ya pili akiruka damu damu ambazo zilikuwa zina vuja toka kichwani mwa Winifrida, alisogea na kukaa katika kona ya kitanda. Richardakakichukua kipande cha karatasi na kuanza kukisoma. “Mke wangu… mke wangu jamani” aliyaongea maneno hayo baada ya kusoma ujumbe alioukuta. Kijana wa watu akajikalisha sakafuni taratibu akamtazama mkewe kwa jicho la huzuni kumbukumbu mbalimbali zikamtembelea na kumuumiza sana
moyo wake loo alijiona mkiwa kweli kweli hasa tabasamu zuri la mkewe lilimmaliza nguvu, aliwaza mengi sana na
kukumbuka kauli mbalimbali za mkewe kipindi kile walipo toka Hospitali.
Mawazo yalipofika tamati alijipangusa machozi akajiburuza hadi karibu na bastora akaikagua kisha akajisimamisha kiuchovu na kulisogelea kabati la nguo
alinyanyua mkono wake na kupapasa mpaka alipopata alichokitaka akaacha, mkononi alikuwa kashikilia risasi moja
akajisogeza hadi kwenye mwili wa mkewe akajikalisha na kutulia akaiweka risasi katika chemba na kuipachika kichwani
tayari kwa kufyatua. Richard wala hakuwa na wazo lingine zaidi ya kujiua hakuwaza kumtikisa mkewe hakuwaza
kumpeleka hospitali hakuwaza kubahatisha kuokoa maisha ya
mkewe kwa sababu aliamini asilimia mia kuwa mkewe ni marehemu hivyo hakuwa na mpango tofauti zaidi ya kujiua.
Baada ya kuweka vizuri akafumba macho huku mkono mmoja ukiwa begani mwa mkewe, “Mke wangu ngoja tu nikufate
maana nikibaki nitakuwa nimevunja ahadi yangu” alipo kuwa anaendeleaa kulia kwa uchungu na kujiongelesha mwenyewe
mwili wa Wini ukaanza kutikisika, Richard wa watu alibaki akitazama kwa mshangao akiwa na hali ya furaha akatulia
kumuangalia mkewe vizuri, Wini akajigeuza tena hukukujinyoosha huku akiyafumbua macho yake. Richard akamvamia mkewe na kuanza kumtingisha na kumuita kwa
jina huku akimgusa mapigo ya moyo “…Ooh asante Mungu mke wangu hujafa?!!” Richard akaitupa bastola ukutani na
kumnyanyua mkewe kumkalisha kitako huku akiwa anahema hovyo hovyo akimuita mfululizo “Mke wangu …mke
wangu…jamani mke wangu… ooh jamani mke wangu”. Richard alimkumbatia kwa furaha mkewe, Wini yeye alibaki
kumtazama tu usoni mumewe bado akiwa na wenge la kuponyoka na kifo alionekana kama mtu asiyejielewa alibaki
kumtazama tu usoni. “Mke wangu sina thibitisho la kunipendainatosha usifanye hivi tena tafadhari, najua mwenyezi Mungu amenipendelea sana kunirudishia furaha yangu naahidi kuto rudia kosa mke wangu sito kuacha ata nzi akukere sitakaa mbali nawe tena” Richard alimkumbatia zaidi mkewe na
kumpiga mabusu mfululizo ya kichwa huku Wini akionekana kutulia akaiweka risasi katika chemba na kuipachika kichwani
tayari kwa kufyatua. Richard wala hakuwa na wazo lingine zaidi ya kujiua hakuwaza kumtikisa mkewe hakuwaza kumpeleka hospitali hakuwaza kubahatisha kuokoa maisha yamkewe kwa sababu aliamini asilimia mia kuwa mkewe ni marehemu hivyo hakuwa na mpango tofauti zaidi ya kujiua.
Baada ya kuweka vizuri akafumba macho huku mkono mmoja ukiwa begani mwa mkewe, “Mke wangu ngoja tu nikufate
maana nikibaki nitakuwa nimevunja ahadi yangu” alipo kuwa anaendeleaa kulia kwa uchungu na kujiongelesha mwenyewe
mwili wa Wini ukaanza kutikisika, Richard wa watu alibaki akitazama kwa mshangao akiwa na hali ya furaha akatulia
kumuangalia mkewe vizuri, Wini akajigeuza tena hukukujinyoosha huku akiyafumbua macho yake. Richard akamvamia mkewe na kuanza kumtingisha na kumuita kwa
jina huku akimgusa mapigo ya moyo “…Ooh asante Mungu mke wangu hujafa?!!” Richard akaitupa bastola ukutani na
kumnyanyua mkewe kumkalisha kitako huku akiwa anahema hovyo hovyo akimuita mfululizo “Mke wangu …mke
wangu…jamani mke wangu… ooh jamani mke wangu”. Richard alimkumbatia kwa furaha mkewe, Wini yeye alibaki
kumtazama tu usoni mumewe bado akiwa na wenge la kuponyoka na kifo alionekana kama mtu asiyejielewa alibaki kumtazama tu usoni. “Mke wangu sina thibitisho la kunipendainatosha usifanye hivi tena tafadhari, najua mwenyezi Mungu
amenipendelea sana kunirudishia furaha yangu naahidi kuto rudia kosa mke wangu sito kuacha ata nzi akukere sitakaa
mbali nawe tena” Richard alimkumbatia zaidi mkewe na kumpiga mabusu mfululizo ya kichwa huku Wini akionekana kwenye sofa maana alipigwa la kushtukiza alitulia kajishika shavu akiugulia maumivu makali. “Mpumbavu wewe usiongee
upuuzi mbele yangu shwaini” alifoka Richard huku akimuangalia Eva kwa jicho lenye hasira sana. “Sikiliza Richard najua unaongea kwa kujiamini sana kwa kuwa tupo kwako, lakini tambua kuwa sisi ndugu zako tunakupenda sana halafu kingine kaa ukijua kuwa unapoteza muda bure na huyo mwanamke” Ester aliingilia kuongea kwa utulivu sana na sio kwa kupayuka kila mtu pale sebureni aliweza kusikia vizuri hapakuhitajika kurudiwa, yalikuwa ni maneno mazito kwa
kijana Rich yalitibua tibua chungu ya moyo akashindwa kujizuia alijikuta anapayuka kwa nguvu “Nasema ondokeni
nyumbani kwangu sasa hivi” “Hatuondoki lolote fanya mpaka utuelewe” Ester nae aliongea kwa jazba tena kwa kujiamini,
Richard aliona anapotezewa muda aliamua kuchukua simu mfukoni mwa suruali yake na kutafuta namba na kupiga, dada zake walibaki wakimtazama tu. “Hallow…yes afande maunaomba mje nyumbani kwangu kuna uvamizi hapa… okay sawa” Richard alitoka eneo hilo na kusogea pahala ambapo meza ya chakula ilikuwepo na ndipo mkewe alikuwa
amejituliza akishuhudia malumbano yanayo sababishwa na yeye. ‘Roho inaniuma sana matatizo yangu leo yana
wapelekea ndugu kugombana’ Winifrida alijisemea nafsini.
Richard alisogea na akaanza kupakuwa chakula na kumnawisha mkewe na kuanza kula huku akimlisha na mkewe kwa tabu tabu. Ndugu wakabaki wakitazama tu kwa mishangao.
Chakula hakikuisha kwenye sahani nje kulisikika honi kali, Juma akiwa hana hili wala lile alitazama katika ukuta kupitia kifaa maalumu “Hee magwanda tena” aliongea na kuchapuka kutoka mbio “Jamani polisi wamekuja…” kauli hiyo ndo ya kwanza kumtoka baada ya kufungua mlango na kuingia ndani huku akihema bila mpangilio macho yakimtoka na kushangaa shangaa “Waruhusu waingie tu” aliongea Richard akiwa hana
wasiwasi kabisa, dada zake walibaki wakitazamana kwa mshangao. Jumaa huyo akatoka, punde Juma na maaskari
watatu wakawa wapo ndani ya nyumba ya Richard “Karibuni sana maafisa nawaomba mnitolee hao watu kwa sababu wanatishia usalama wa familia yangu na muwaambie wasije
wakakanyaga tena hapa ni hilo tu wala msiwapelekerumande” Richard aliongea huku akionesha kidole kwa dada
zake “Jamani Richard wewe wakutuitia polisi leo ama kweli dunia hadaa walimwengu shujaa, wewe niliyekuachia ziwa wewe ukanyonya unanitoa kwako kwa kutumia polisi?” Ester aliongea kwa uchungu mkubwa huku machozi yakimlenga, dada huyu yeye hakuamini kama kweli ndugu yake atafikia
hatua hiyo sasa ndipo alipo amini kuwa basi nia yake imefeli, aligeuza sura akamtazama wifi yake kwa jicho la hasira sana akarudisha uso kwa ndugu yake Eva, “Mdogo wangu naona umejionea amechagua penzi na ndugu kawaacha basi kuanzia sasa sisi sio ndugu zake” Eva alitingisha kichwa huku jicho la chuki likiwa kwa wifi yake, polisi hawakuacha ngonjera ziendelee waliwasogelea na kuwaamuru watoke na wao wakatii. “Tafadhari naomba muhakikishe habari hizi haziwafikii waandishi wa habari kwa gharama zozote…mnajua wazi watu wananiwinda kuchafua sifa yangu…vizuri” Richard alimaliza kuongea akakata simu huku akirudishia pazia alilokuwa amelipenyua.“Mke wangu pole, hakuna atakae kuja kututenganisha zaidi ya
Mungu na wala sio watu, sipo tayari kukukosa kabisa” aliongea Mheshimiwa huku akimvutia mkewe kifuani hii
baada ya kukaa sofani. “Haa Fatuma …” Wini akatahamaki na kujinasua kifuani akanyanyuka na kumfata Fatuma ambaye
alionekana kujiegemeza ukutani akitabasamu huku ameushika mkono wake uliojeruhiwa akamkumbatia “Pole
jamani pole mdogo wangu” aliongea Winifrida huku akimshika bega Fatuma na kumvutia kifuani “Hamna dada
usiwe na hofu kikubwa wewe ni mzima ndio jambo la kushukuru” Fatuma aliongea huku kichwa kikiwa begani mwa
Wini, Richard alikuwa hajaelewa kitu hivyo alibaki kuwatazama tu kwa furaha. Wini alijinasua katika kifua cha Fatuma na kumuangalia mumewe, “Mume wangu Fatuma alikuwa ananizuia nisijiumize pindi nilipokuwa nampokonya kisu nikamjeruhi katika kiganja chake inaniuma sana” Richard ndipo akazibuka masikio nakushangaa akanyanyuka kujionea
“Asante sana Fatuma kwa moyo wako haya jiandae basi nikupeleke hospitali ukatazamwe majeraha” “Sawa kaka
ngoja nimuwekee chakula Jumaa aje kula bado hajakula nilisahau kumuita” “Ooh hapana nitafanya na uende Hospitali
mpendwa” alidakia Winifrida.Tatizo la mtoto katika nyumba ya mheshimiwa Richardlilianza kuzoeleka, lakini haikuwa rahisi katika moyo wa Winifrida liliendelea kuishi na kuitafuna subira na imani yake
iliyobakia ndani ya moyo wake. Winifrida aliendelea kucheka, kufurahi, kula na kuendelea na shughuli zake za kila siku
lakini yote yalikuwa ni maigizo. Usiku mmoja, Winifrida akiwa kajilaza macho juu, alijigeuza na kumuangalia mumewe aliyekuwa mbali kwa usingizi akamtazama jinsi alivyo “Wewe ni Handsome sana mume wangu ukilala hata ukiamka” alijiongelea Winifrida na kutabasamu akaanza kumshika shika mashavu mumewe na lips, alifanya hivyo mpaka Richard alipofumbua macho na
kumtazama “Vipi mke wangu mbona hulali” aliongea bwana Richard kwa sauti ya kichovu chovu, Winifrida alichukua
muda wa takribani dakika tatu akimuangalia tu ndipo alipoamua kusema “Mume wangu najua hupendi kuniona
naongelea tatizo hili ila mimi nimepata njia” “Umepata njia” Richard usingizi ulimpaa macho yakamtoka na akajinyanyua kukaa kitako, “Njia gani mke wangu” Wini nae alifata kwa kunyanyuka na kukaa kitako, “Sio njia nzuri sana…ni kuwa mume wangu, mi naomba utafute mwanamke mwingine uzae nae mi uniache…” kabla haja malizia, Richard alishtushwa sana, hali yake ilianza kubadilika moyo ulimbana pumzi
zikaanza kutoka kwa tabu, akaanza kutweta akikohoa hovyo huku mkono ukiwa katika koo lake kama mtu aliyebanwa kwa loba kooni. Wini alishtuka na kuogopa sana akaanza kumpiga
piga mgongoni kumtuliza lakini wapi akachukua nguo na kuanza kumpepea huku akilalamika “Mume wangu unanini…
jamani mume wanguu” mwisho hali ikaanza kupungua huku Richard macho yakiwa mekundu yamemtoka na machozi
yakimteremka, Wini alimsogeza na kumkumbatia “Basi mume wangu sitataka kukuacha tena sitarudia nakupenda mume wangu, sitasema tena nilichokisema basi tujaribu kumuhasili
mtoto” Richard akiwa kakiweka kichwa kwenye mapaja ya mkewe alisikia lakini uwezo wa kujibu hakuwa nao kwa taabani aliyokuwa nayo, ama kweli mapenzi ni uchawi wa ajabu.
Siku nazo zikaanza kusonga zikienda mbio mbio kama zinakimbizwa, watu mbali mbali wakaanza kumshauri Winifrida kuhusu kuingia katika masuala ya waganga wa jadi kujaribu bahati yake maana wengi hubahatika waliongea kwa
majivuno. Maneno mengi aliambiwa yeye aliishia kuwajibukuwa atafikiria, upande wa mumewe nae mambo yalikuwa
sawa tu na kwa mkewe marafiki na jamaa wengine walimshauri kuhusu kutafuta waganga nae aliwajibu atafikiria.
Kadri siku zilivyokwenda na wao walianza kulewa na maneno ya watu imani ikawatoka na kuanza kuamini mambo ya
waganga wa jadi na sio Mungu tena kama awali. Hatua ya kwanza ilikuwa ni kuwatembelea hao waganga waliokuwa
wanasifika tena bila kukata tamaa, walichanjwa chale wakalishwa madawa ya kila namna wakapewa masharti ya
namna tofauti kulala chini, kuoga na nguo, kwenda kutupa vitu makaburini na mambo mengine ya ajabu kibao kama kawaida ya waganga wengi walivyo. Marafiki na jamaa zao baada ya kuona hakuna mfanikio wala mabadiliko yoyote ndipo wakayaweka wazi midomoni kuwa Winifrida atakuwa
ni tasa kabisa hakuna la ziada. Kama ilivyo marafiki si wakufanana wapo wazuri na wabaya, kati yao kuna waliojikuta wakimkosea sana Richard kwa kuthubutu
kumshawishi amsaliti mkewe na kuzaa nje ya nyumba yake kisiri ili tu awe na mbegu ambayo itakuja kurithi mali zake, jambo hilo lilipelekea kutofautiana baina yake na hao marafiki na hata kuvunja mahusiano kabisa. Richard alikuwa mkali sana hakuwa tayari. Richard na Winifrida walikaa wakachambua wakawaza mioyo yao nayo ilianza kubadilika taratibu na kuanza kusalimu amri kukubali hali halisi kuwa mtoto ni zawadi na hupewa yoyote endapo mwenyezi Mungu akipenda na sio kuwa inatoka kwa binadamu wenzao,
walitubu kwa tabia mbaya walioyoifanya kwa kumkosea mola wao na kuanza maisha mapya.“Ni balaa zito! Tumemuona Bwana Fanuel Mkwasi akiwa makaburini dhahiri ni mtu mwenye uchungu na familia yake aliyoipoteza, alimvamia Mzee
Ishengoma akihitaji ukweli kuhusu familia yake lakini aliukosa na kuishia kumuua huku akibaki na kiapo cha sehemu ya ukweli uliobaki. MheshimiwaRichard nae alifanikiwa kushinda kesi dhidi ya washindani wake bila kutegemea huku akipewa taarifa na wakili wake kuhusu kufojiwa kwa ushahidi na kuhitajika kukutana na mheshimiwa raisi haraka, lakini hatujajua walikutana au hawakukutana na kama walikutana waliongea nini! Miaka mitano ikapita, Winifrida mke wa Richard anaonekana kuwa na kitu kinachomnyima raha kwa miaka mingi hadi kufikia kukumbuka namna ndoa yao ilivyofungwa bila kubainisha, na mwisho wa siku alimshawishi mumewe kuishi maisha ya kawaida na kuyatupilia mbali maisha ya Siasa, je! kwanini? Waliwapunguza walinzi na wafanyakazi na kumuajiri mlinzi mmoja ambaye hatukujua alimtolea wapi, lakini alionekana mheshimiwa Richard kuwa na
walinzi wa siri wakimlinda kila aendapo bila mkewe kujua. Mgongoni mwa
mheshimiwa Richard anaonekana akifatiliwa na watu wa Raisi kwa siri kupitia waziri Mwijaku aliyetumwa kumshawishi bila mafanikio pamoja na Kijana aliyemuamini na kumuajili kuwa mlinzi wa nyumba yao naye kuoneakana
kuwa na kazi ya ziada tofauti na ulinzi. Huzuni ya kukosa mtoto ilimtawala
Richard na mkewe na kuamua kufanya matibabu wanaligundua tatizo na
kuamua kuishi nalo lakini changamoto nyingi zakuingiliwa na ndugu, jamaa
na marafiki hazikukoma kuwaandama. Je! Kijana Jumaa anampango gani na
familia ya Richard na aliwezaje kuishi humo? Je! wanandoa hao wataweza
kuvumiliana kwa hali hiyo ya kukosa mtoto na kudumisha mapenzi yao? Je!
Fanuel Mkwasi atawezakufanikisha ataweza upata ukweli anao utafuta?”
Itaendeleaaaa....
Mijadara inaruhusiwa