The Boiling Point

Rev. Kishoka

JF-Expert Member
Mar 7, 2006
4,526
1,529
Maji yanapoanza kukolea joto, msuguano wa chembe chembe zinazounda maji huanza kusuguana na kuanza kutoa mvuke. Kadri jinsi moto unavyoendelea kwa kiwango kile kile au kuongezeka, msuguano wa chembe chembe hizi huongezeka, mvuke huongezeka na kama chombo ambacho maji haya yanachemshiwa kina mfuniko, mluzi mwepesi na fukuto la mvuke huanza kuinua ule mfuniko.

Hitimisho la kupata joto huku kwa maji, ni maji kuchemka, yakiwa na joto la hadi nyuzi 100 sentigredi. Inapofikia hatua hiyo, maji haya pamoja ni salama kiafya kwa kunywa, lakini ni hatari maana huweza unguza na hata kuhatarisha maisha ya mwanadamu.

Mfano huu wa maji kuchemka, ni kuoanisha hali iliyofikia mchemko kwa kupitia Wanafunzi tangu shule za msingi, sekondari mpaka ngazi ya vyuo hususan Chuo Kikuu Dar Es Salaam.

Katika kipindi cha miezi minne iliyopita, kumekuwa na wimbi la wanafunzi kufanya fujo ambazo zimefikia hatua ya kuharibu mali na hata kupotea kwa maisha.

Pamoja na kuwa sikubaliani na njia walizotumia Wanafunzi hawa, anzia wa kule Mtwara au Lindi waliochoma shule kwa ajili ya Sukari, Kantalamba ambao walikasirikana kuvunja vunja mali za shule na magari kisa kufungwa kwenye mechi ya mpira na mwenzao kuchapwa viboko, Green Acres ya Dar ambao wamefanya uharibifu wa karibu Shillingi 100 Millioni kisa Muziki na kupewa pasi za kwenda kutembea na mwisho Baba lao UDSM ambao wamefanya vurugu na migomo kutokana na kukosekana maji, umeme, calculator, kusimamishwa uchaguzi wa serikali ya wanafunzi na sababu nyingine nyingi, lakini naelewa chimbuko la hasira zao na kamwe si jambo la kupuuzia.

Ninachojiuliza, Serikali inajifunza nini kutokana na hili? Je jamii yetu inajifunza nini kutokana na haya mambo yaliyotokea?

Wanafunzi hawa wanachofanya ni active resistance, na wamekimbilia kufanya fujo na kuharibu mali kama tamati ya hasira na kuchoshwa kwao kwa kuendelea kutokusikilizwa au maombi na matakwa yao kutokufanyiwa kazi.

Sisi hapa JF, tunatumia passive resistance, ingawa si kwa nguvu zote, ila mazungumzo yetu ya kuuchambua mfumo wa kiutawala na maswala yanayohusu jamii na athari zake, ndiyo yanatufanya tuwe kwenye kundi la passive resistance, non violent resistance.

Hata walioandamana majuzi kule Buzwagi, waliomzomea Mkapa na wale wa Morogoro walimzomea Ngasongwa ni sehemu ya civil disobidience kudai haki.

Maji yameanza kuchemka, sehemu moja ya jamii yetu imefika ngazi ya juu ya kusubiri haki itumike ili mahitaji na vilio visikilizwe.

Ukiangalia kesi zote za hawa wanafunzi, chimbuko la fujo zao ni UONGOZI wa shule na vyuo vyao.

Sisi hapa JF, magazetini na sehemu nyingine, chimbuko la vilio vyetu ni UONGOZI na VIONGOZI.

Swali linabakia, je Taifa na Jumuia zetu zina matatizo gani ya Uongozi? Inakuwaje kunakuwa na msukumo mkubwa wa Jamii kutokuridhika na Uongozi?

Kilichoshtua zaidi ni vijana wa Green Acres, shule binafsi ambao wanalipia ada kwenda kwenye hiyo shule. Nikajiuliza, kawaida ya migomo na vurugu katika Shule hutokea kwenye Shule za Serikali. Sasa kama hata kwenye Shule binafsi kunaanza kuwa na vurugu, je ni ugonjwa gani katika ngazi za uongozi Taifa letu inalikosa?

Sizungumzii Ufisadi au Uhujumu, bali ni Upeo wa Uongozi Mahiri ulioambatana na Hekima, Busara, Uwajibikaji, Ufanisi na Unyenyekevu.

Inaelekea viongozi wengi wa Tanzania wa ngazi mbali mbali tangia mitaa, kijiji, taasisi, shule, mashirika na hata serikali kuu na Kiongozi Mkuu, Rais, ni vipofu, viziwi na pua zao hazi fanyi kazi vizuri kung'amua kuwa kuna fukuto la Jamii na Taifa lililochoshwa na adha, mahangaiko na kukosa amani kwa kutokujua Kesho wataamka wakiwa katika hali gani.

Tulipoandamana kulienzi Azimio la Arusha, Viongozi na Wananchi walikuwa bega kwa bega wakiungana Kulijenga Taifa linalojitegemea, lenye watu wenye juhudi na maarifa katika kupiga vita Ujinga, Umasikini na Maradhi.

Lakini sasa inaelekea Mwananchi anachapwa mjeledi na kiongozi wake, kushurtishwa avumilie machungu na makali ya maisha kama kukosekana kwa huduma nzuri za elimu kwa watoto, kinga ya afya, ajira, bei punjifu ya mazao, mishahara midogo, kukosekana kwa miundo mbinu mizuri kwa sekta kama za umeme, maji, usafiri wa matata anzia reli hata barabara na kutwa kuchwa akiambiwa "vumilia kidogo" lakini kukiwa hakuna tumaini.

Mwananchi anaambiwa "Vumilia Kidogo" huku akikamuliwa na serikali yake na Viongozi wake, kuchangia kila kitu kwa kipato haba, kushurtishwa kufanya mambo yanayokidhi matakwa ya Viongozi na si ya Jamii au Taifa.

Tumekosa viongozi wasikivu, wenye kung'amua haraka kuwa maji yakikaa kwenye moto kwa muda mrefu, hufukuta na katika safari yake ya kubadilika kutoka kuwa kimiminika kuwa hewa, mvuke huleta msukumo ambao hufanya maji yachemke.

Asilani tusikimbilie kusema eti ni mbegu mbaya tuliyoipanda kutoka tupate uhuru, au ni mipango mibovu ya viongozi wa kwanza. Kuendelea kulaumu ya kale na kuyafanya kuwa ndiyo sababu kuu ya udhaifu wa viongozi wa sasa, ni kuwapa viongozi hawa sababu za kukwepa uwajibikaji kwa kuwa watakimbilia kusema kuwa wao ni "Walevi" kwa kuwa Baba na Bau zao walikuwa ni "Walevi".

Taifa sasa hivi liko njia panda na kwenye ncha ya kuangukia kwenye vurugu mithili ya wanafunzi. Kila mtu anajifunza kutokana na fujo hizi na mwishowe kila mmoja wetu atasema imetosha, ngoja nami nichukue "kitofa" na kufanya vurugu.

Ikiwa Viongozi walishindwa kusoma mambo ya nyakati wakati Shamba la Ballali alilolipata halali liligawanywa na wananchi wenye hasira kama vazi la Yesu, basi tuendako ni hatari na kunanikumbusha nilichokiona na kusikia pale Kariakoo nyuma ya CCM Lumumba.

Ilikuwa ni November ya 2004, nimetoka Kanisani nikiwa na Mzee Kishoka na wake zetu, tukaenda kununua nyama. Kulikuwa na vikundi vya watu wakibarizi asubuhi kusugoa.

Nilichokisikia kutoka kwa hawa ndugu na nilichokiona kutoka machoni mwao, kimenikaa mpaka leo, na ikawa ndio ongezo la hasira zangu kwa ugoigoi wa Serikali.

Tuliposhuka kwenye gari, jamaa wakatutazama, kisha wakaanza kusema, "Ruksa hiyo, Ruksa hiyo", nikaangalia nyuma sikuona mtu, ila kelele hizo zilielekezwa kwetu. Nikawaangalia na kuwakazia macho mithili Bush alivyomkazia macho Putin, nikaona hasira tupu zilizotokana na kushindwa kusikilizwa kwa kero zao ambazo zimeendeleza wao kuwa wanyonge na kuhisi kuwa ni masikini wasio na haki au sehemu katika nchi yao.

Nikasema, ikiwa kuvalia kwa utanashati kunatoa tafsiri ya "Ruksa" wakati huo, basi tunapoenda na kubaya sana ikiwa Serikali na Viongozi hawatafanya juhudi kufanya kazi zao ili kuondoa hizi zana potofu kuwa kila mwenye tai ni "Ruksa" au kwa leo "Fisadi".

Kwa nyie wapambe wa viongozi, kina Salva, Balile na wenginewe, mkisoma maandiko haya, nendeni mkawaamshe mnaowasaidia.

Waambieni maji yameanza kuchemka na hatari yake ni kuungua. Watuepushie balaa na kufanya kazi kwa umakini ikiwa ni pamoja na kuchukua hatua kuondoa kero kwa wananchi na kushughulikia uzembe,dhuluma, hujuma na ufisadi. Waambieni kama hawawezi kazi za uongozi, ni heri wang'atuke na si kuendelea kutulaghai na miezi 18 ijayo watuambie wanataka kura zetu waendelee kuwa Viongozi (Watawala).

Nawatakia wiki njema.
 
Maji yanapoanza kukolea joto, msuguano wa chembe chembe zinazounda maji huanza kusuguana na kuanza kutoa mvuke. Kadri jinsi moto unavyoendelea kwa kiwango kile kile au kuongezeka, msuguano wa chembe chembe hizi huongezeka, mvuke huongezeka na kama chombo ambacho maji haya yanachemshiwa kina mfuniko, mluzi mwepesi na fukuto la mvuke huanza kuinua ule mfuniko.

Hitimisho la kupata joto huku kwa maji, ni maji kuchemka, yakiwa na joto la hadi nyuzi 100 sentigredi. Inapofikia hatua hiyo, maji haya pamoja ni salama kiafya kwa kunywa, lakini ni hatari maana huweza unguza na hata kuhatarisha maisha ya mwanadamu.

Mfano huu wa maji kuchemka, ni kuoanisha hali iliyofikia mchemko kwa kupitia Wanafunzi tangu shule za msingi, sekondari mpaka ngazi ya vyuo hususan Chuo Kikuu Dar Es Salaam.

Katika kipindi cha miezi minne iliyopita, kumekuwa na wimbi la wanafunzi kufanya fujo ambazo zimefikia hatua ya kuharibu mali na hata kupotea kwa maisha.

Pamoja na kuwa sikubaliani na njia walizotumia Wanafunzi hawa, anzia wa kule Mtwara au Lindi waliochoma shule kwa ajili ya Sukari, Kantalamba ambao walikasirikana kuvunja vunja mali za shule na magari kisa kufungwa kwenye mechi ya mpira na mwenzao kuchapwa viboko, Green Acres ya Dar ambao wamefanya uharibifu wa karibu Shillingi 100 Millioni kisa Muziki na kupewa pasi za kwenda kutembea na mwisho Baba lao UDSM ambao wamefanya vurugu na migomo kutokana na kukosekana maji, umeme, calculator, kusimamishwa uchaguzi wa serikali ya wanafunzi na sababu nyingine nyingi, lakini naelewa chimbuko la hasira zao na kamwe si jambo la kupuuzia.

Ninachojiuliza, Serikali inajifunza nini kutokana na hili? Je jamii yetu inajifunza nini kutokana na haya mambo yaliyotokea?

Wanafunzi hawa wanachofanya ni active resistance, na wamekimbilia kufanya fujo na kuharibu mali kama tamati ya hasira na kuchoshwa kwao kwa kuendelea kutokusikilizwa au maombi na matakwa yao kutokufanyiwa kazi.

Sisi hapa JF, tunatumia passive resistance, ingawa si kwa nguvu zote, ila mazungumzo yetu ya kuuchambua mfumo wa kiutawala na maswala yanayohusu jamii na athari zake, ndiyo yanatufanya tuwe kwenye kundi la passive resistance, non violent resistance.

Hata walioandamana majuzi kule Buzwagi, waliomzomea Mkapa na wale wa Morogoro walimzomea Ngasongwa ni sehemu ya civil disobidience kudai haki.

Maji yameanza kuchemka, sehemu moja ya jamii yetu imefika ngazi ya juu ya kusubiri haki itumike ili mahitaji na vilio visikilizwe.

Ukiangalia kesi zote za hawa wanafunzi, chimbuko la fujo zao ni UONGOZI wa shule na vyuo vyao.

Sisi hapa JF, magazetini na sehemu nyingine, chimbuko la vilio vyetu ni UONGOZI na VIONGOZI.

Swali linabakia, je Taifa na Jumuia zetu zina matatizo gani ya Uongozi? Inakuwaje kunakuwa na msukumo mkubwa wa Jamii kutokuridhika na Uongozi?

Kilichoshtua zaidi ni vijana wa Green Acres, shule binafsi ambao wanalipia ada kwenda kwenye hiyo shule. Nikajiuliza, kawaida ya migomo na vurugu katika Shule hutokea kwenye Shule za Serikali. Sasa kama hata kwenye Shule binafsi kunaanza kuwa na vurugu, je ni ugonjwa gani katika ngazi za uongozi Taifa letu inalikosa?

Sizungumzii Ufisadi au Uhujumu, bali ni Upeo wa Uongozi Mahiri ulioambatana na Hekima, Busara, Uwajibikaji, Ufanisi na Unyenyekevu.

Inaelekea viongozi wengi wa Tanzania wa ngazi mbali mbali tangia mitaa, kijiji, taasisi, shule, mashirika na hata serikali kuu na Kiongozi Mkuu, Rais, ni vipofu, viziwi na pua zao hazi fanyi kazi vizuri kung'amua kuwa kuna fukuto la Jamii na Taifa lililochoshwa na adha, mahangaiko na kukosa amani kwa kutokujua Kesho wataamka wakiwa katika hali gani.

Tulipoandamana kulienzi Azimio la Arusha, Viongozi na Wananchi walikuwa bega kwa bega wakiungana Kulijenga Taifa linalojitegemea, lenye watu wenye juhudi na maarifa katika kupiga vita Ujinga, Umasikini na Maradhi.

Lakini sasa inaelekea Mwananchi anachapwa mjeledi na kiongozi wake, kushurtishwa avumilie machungu na makali ya maisha kama kukosekana kwa huduma nzuri za elimu kwa watoto, kinga ya afya, ajira, bei punjifu ya mazao, mishahara midogo, kukosekana kwa miundo mbinu mizuri kwa sekta kama za umeme, maji, usafiri wa matata anzia reli hata barabara na kutwa kuchwa akiambiwa "vumilia kidogo" lakini kukiwa hakuna tumaini.

Mwananchi anaambiwa "Vumilia Kidogo" huku akikamuliwa na serikali yake na Viongozi wake, kuchangia kila kitu kwa kipato haba, kushurtishwa kufanya mambo yanayokidhi matakwa ya Viongozi na si ya Jamii au Taifa.

Tumekosa viongozi wasikivu, wenye kung'amua haraka kuwa maji yakikaa kwenye moto kwa muda mrefu, hufukuta na katika safari yake ya kubadilika kutoka kuwa kimiminika kuwa hewa, mvuke huleta msukumo ambao hufanya maji yachemke.

Asilani tusikimbilie kusema eti ni mbegu mbaya tuliyoipanda kutoka tupate uhuru, au ni mipango mibovu ya viongozi wa kwanza. Kuendelea kulaumu ya kale na kuyafanya kuwa ndiyo sababu kuu ya udhaifu wa viongozi wa sasa, ni kuwapa viongozi hawa sababu za kukwepa uwajibikaji kwa kuwa watakimbilia kusema kuwa wao ni "Walevi" kwa kuwa Baba na Bau zao walikuwa ni "Walevi".

Taifa sasa hivi liko njia panda na kwenye ncha ya kuangukia kwenye vurugu mithili ya wanafunzi. Kila mtu anajifunza kutokana na fujo hizi na mwishowe kila mmoja wetu atasema imetosha, ngoja nami nichukue "kitofa" na kufanya vurugu.

Ikiwa Viongozi walishindwa kusoma mambo ya nyakati wakati Shamba la Ballali alilolipata halali liligawanywa na wananchi wenye hasira kama vazi la Yesu, basi tuendako ni hatari na kunanikumbusha nilichokiona na kusikia pale Kariakoo nyuma ya CCM Lumumba.

Ilikuwa ni November ya 2004, nimetoka Kanisani nikiwa na Mzee Kishoka na wake zetu, tukaenda kununua nyama. Kulikuwa na vikundi vya watu wakibarizi asubuhi kusugoa.

Nilichokisikia kutoka kwa hawa ndugu na nilichokiona kutoka machoni mwao, kimenikaa mpaka leo, na ikawa ndio ongezo la hasira zangu kwa ugoigoi wa Serikali.

Tuliposhuka kwenye gari, jamaa wakatutazama, kisha wakaanza kusema, "Ruksa hiyo, Ruksa hiyo", nikaangalia nyuma sikuona mtu, ila kelele hizo zilielekezwa kwetu. Nikawaangalia na kuwakazia macho mithili Bush alivyomkazia macho Putin, nikaona hasira tupu zilizotokana na kushindwa kusikilizwa kwa kero zao ambazo zimeendeleza wao kuwa wanyonge na kuhisi kuwa ni masikini wasio na haki au sehemu katika nchi yao.

Nikasema, ikiwa kuvalia kwa utanashati kunatoa tafsiri ya "Ruksa" wakati huo, basi tunapoenda na kubaya sana ikiwa Serikali na Viongozi hawatafanya juhudi kufanya kazi zao ili kuondoa hizi zana potofu kuwa kila mwenye tai ni "Ruksa" au kwa leo "Fisadi".

Kwa nyie wapambe wa viongozi, kina Salva, Balile na wenginewe, mkisoma maandiko haya, nendeni mkawaamshe mnaowasaidia.

Waambieni maji yameanza kuchemka na hatari yake ni kuungua. Watuepushie balaa na kufanya kazi kwa umakini ikiwa ni pamoja na kuchukua hatua kuondoa kero kwa wananchi na kushughulikia uzembe,dhuluma, hujuma na ufisadi. Waambieni kama hawawezi kazi za uongozi, ni heri wang'atuke na si kuendelea kutulaghai na miezi 18 ijayo watuambie wanataka kura zetu waendelee kuwa Viongozi (Watawala).

Nawatakia wiki njema.


Uongozi ndio changamoto kubwa tulionayo nchini hivi sasa. Mada na maneno mazuri sana Rev! Changamoto ya Uongozi
 
Asante sana Mkuu

Hatuna budi kurudi katika msingi mzima wa sheria mama ili kuweza kuziba mianya inayoonekana sasa kuna sehemu zinavuja mojawapo ikiwa maadili ya viongozi na watawala kuanzia ngazi za chini mpaka ngazi za juu.

Tunahitaji kuandika sheria hizi upya kulingana na experience inayotukuta sasa hivi.

Kunahitajika watanzania wawekewe vipengele vilivyowazi vitakavyoweza kumwajibisha kiongozi yeyote wakati watakapoona atendi yale waliyoyategemea kuanzia ngazi za chini mpaka za juu bila kuvunja sheria.
 
Rev Serikali ya Tanzania haijawai kusoma chochote kutokana na lolote. Kama tungekuwa tunasoma mambo tungeweza kutengeneza miswada itakayokomesha hayo mambo kujiludia over and over baadae.

Mlimani wameanza kugoma tangu enzi za mwalim, lakini ni strategy gani serikali ilichukua kuzuia hiyo migomo? Nothing

Ufisadi haujaanza jana, sema umescalade kwa 100% for the past 10 years. Hii inatokana serikali haikuweka strong rules wakati wa huo ufisadi ulipoanza. That is matatizo ya kutokuchukua strong measures enzi hizo.

Hatujawai kusoma chochote kile, iwe ni wizi wa mitihani ya darasa la saba au taifa stars kunyolewa kama kichwa cha mwenda wazimu. Sakata la wanaCCM kuibia Taifa halijaanza jana wala juzi, lakini sababu ya do nothing government then tumefika hapa tulipo.

Wanaserikali wachache wanaamini wanamiliki Tanzania, wanaimani kabisa Tanzania ni sawa na kiwanda na wao ndio top stakeholder's so, they can do whatever they wanna do. Wewe kumbuka kashafa za Lowassa na ufisadi zimeanza mwaka gani? Kumbuka jengo la balozi ya south africa, EL alikuwa anajulikana kabisa ndio mmiliki. Na mwalim ashawai kusema huyu jamaa hafai, lakini what measures were taken by serikali? Nothing

Haya ndio madhara ya slow bleeding ndani ya brain, sasa nchi ipo kwenye COMA, there is nothing we can do about. Tutakufa tuu.
 
Upofu wa Viongozi wetu ni wa kujitakia na makusudi ili waendeleze uzembe na ukosefu wa maadili.
 
Mtanganyika,

Kwa kuongeza, Uongozi unalea mizengwe, unafiki na uzandiki, ndio maana tunashindwa kujenga Taifa la watu makini.

Just imagine hawa wanafunzi ambao in 20-30 years from today ndio watakuwa viongozi wetu. Kama wanaanza jifunza kwa makosa, tunatarajia kujenga Taifa la namna gani?
 
Mtanganyika,

Kwa kuongeza, Uongozi unalea mizengwe, unafiki na uzandiki, ndio maana tunashindwa kujenga Taifa la watu makini.

Just imagine hawa wanafunzi ambao in 20-30 years from today ndio watakuwa viongozi wetu. Kama wanaanza jifunza kwa makosa, tunatarajia kujenga Taifa la namna gani?


Mfumo wa Tanzania haujengi viongozi, bali viongozi wanajijenga ndani ya mfumo. Sasa kinachonitisha waheshimiwa walifanya analysis zao wakaona hakuna umuhimu wa kuwa na vyuo vya kati ( DIT, Mbeya Tech, DSA na nk), wao wakafanya university boom. Kila chuo pale Tanzania sasa ni University, cha kusikitisha asilimia 100 ya wakufunzi wa hivi vyuo wana degree moja au mbili au CPA, madhara yake ni tutakuwa na wahitimu wengi walio hitimu nothing.

Hapo ndio CCM watakapo jua aliyeleta idea ya kuturn kila karatasi kuwa hela alikosea sana. Hiki kiini macho kitawatafuna CCM kwa miaka mingi sana hijayo. Fikiria hivi vyuo ndani ya miaka 4 vinaanza kumwaga wahitimu ambao ni unpropotion na demand ya kazi. Sasa what happen ni supply ya wahitimu inakuwa kubwa and then demand ya kazi ni chini. Kwanza mishahara ya watu inaanza kwenda kwenye tube.

University boom ndani ya Tanzania itakuwa source ya matatizo mengi sana kwa serikali ya CCM. Nawaambia watu kama unaweza wewe andaa kahawa yako na kashata then let us watch the movie. Jini liwajualo CCM safari hii litawala mpaka liwamalize.
 
Mtanganyika,

Niko njia panda. sijui kama haya ni kukosea mahesabu kulikofanywa awali na CCM na kunaendelea mpaka sasa au ni kuwa walikosea mahesabu awali, sasa wanaopuuzia kurekebisha mfumo wa Uongozi wa kuwajibika.

Mathlani Rais wetu kabadilisha mawaziri katika miezi Miwili na nusu. Hili ni badiliko la tatu katika miaka miwili na nusu ya "uongozi" wake. Je ni wapi Raisi wetu alipigwa kanyaboya kwenye somo la Uongozi?

Je si yeye alisema alijifua na kujipika ili awe tayari?

Same can be said on many "leaders" and administrators. We have poor quality people, who are lacking motivation to work, to be risk takers and think and act outside the box. Hawa ndio wanatulelea Umasikini Ujinga na Maradhi na kuhalalisha dhuluma na uhujumu (Ufisadi).

I hope I am wrong kuwa Uongozi uliopo haufanyi huu uzembe wa kila kitu delibarately!
 
Rev, over the weekend nilikuwa na Zitto. Baada ya mazungumzo marefu nikamuuliza the same question kuhusu leaders ndani ya Tanzania.

I asked him about JK and his potential. Kwangu mimi na wewe tunaamini asilimia 100 kwamba JK alipoteza direction the same day alivyohapishwa pale uwanja wa Taifa kuwa raisi wa Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania.

JK hajawai kuongoza chochote kikafanikiwa, CV yake ni partial kama ile ya waziri wake wa mambo ya ndani. Tatizo letu watanzania tukipenda kitu hatusikii la shekh wala mnadi swala.

JK alipovunja baraza la mawaziri mwezi wa mbili kama sikosei, wengi tuliandika suggestion kuhusu ukubwa wa baraza, kuhusu njia bora za kuchagua viongozi na mengine mengi. Lakini muheshimiwa kama kawaida yake alitumia strategy maarufu ya CCM katika kuchagua viongozi, trial and error method. Mimi na wewe tulijua Fika Chenge ni mzandiki na mwizi, tukapiga mayowe kumwambia muheshimiwa asimuweke kwenye team yake, lakini kwa kiburi chake cha kikwere akamchagua kwa vishindo bila kujibu maswali ya waandishi.

Niliuliza are people born to be leaders or lean to be leaders. Kama watu wanazaliwa viongozi then Tanzania tusahau kwasababu tunazaa nightmares. Na kama watu wanasoma ili wawe viongozi then we need to close Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam maana hakitoi hata kiongozi mmoja.

We in the lose lose situation, it doesn't make any difference to thing about changes ndani ya Tanzania
 
Mtanganyika,

Watakuambia walisomea masualaya uongozi Kivukoni, Nyegezi, Marangu, ESAMI, Ngurdoto, Mlimani na sehemu kibao.

Niliposema tubinafsishe Serikali, watu walichukulia kimzaha, aah Mchungaji kakolea mvinyo, ameanza changanyikiwana maneno kibao.

Ukweli ni kuwa Tanzania (si CCM pekee) ina tatizo kubwa sana la kukosekana watu wenye uwezo wa UONGOZI.

Viongoziwetu hawana uwezo, ni waoga wa kufanya maamuzi magumu na mazito, ni wanafiki, wazembe na wenye kukataa kukubali wanapofanya makosa.

Tunakoelekea ni jehanamu, na kama hatutakuwa na dhamira ya kweli na kutumia nguvu zote kubadilika, basi tumelogwa!
 
Kwa nyie wapambe wa viongozi .... .

Waambieni maji yameanza kuchemka na hatari yake ni kuungua. Watuepushie balaa na kufanya kazi kwa umakini ikiwa ni pamoja na kuchukua hatua kuondoa kero kwa wananchi na kushughulikia uzembe,dhuluma, hujuma na ufisadi. Waambieni kama hawawezi kazi za uongozi, ni heri wang'atuke ....

REV!

Ni natural law and there is no going back, you will come to recall thise words one day!

Kuwa, inafikia wakati Mama mja mzito aingie kwenye uchugu mkali ili furaha ya kupata kiumbe kipya ikamilike. Breaking point ya maji lazima ifikiwe kabla "maji kimiminika" hayajabadilika kuwa "maji mvuke". Kipindi kigumu cha kufanya mtihani kwa mwanafunzi lazima kitangulie furaha ya kufaulu na kumaliza mtihani, shule na kuanza maisha mapya ya kufanya kazi. ....etc

The point is .... There is no way we can avoid pains in the processes of expansional - development.

Kinachotokea kwenye nyanja ya UONGOZI WA TAIFA letu kwa sasa ni sawa na yai linalongojewa kuanguliwa kifaranga.... katika siku ya 15 .... siku ya 21 yai litavunjika tu hata nini kitokee...kama kifaranga ni lazima kipatikane. Na kitapatika!

Upya fulani ndani ya nchi Tanzania haukwepeki tena! The breaking point is just there.. just there..near the coner!

That means mwenye fikra sahihi anajua fika kuwa lazima kuna maumivu yanayoendana na hilo!

And you know what?

Watu wengi wanajaribu kuyakwepa haya maumivu au kuya modify prematurely!

Ujumbe hapa ni kuwa dont waste your time...mambo yalipofikia bado five degree centgrade maji yachemke au mama ajifungue etc...No going back.

Kwa kawaida ...hii michakato ikishaanza hairudi nyuma...hakuna mtu mzima anaye weza kurudua utotoni tena..!

VIONGOZI mlioko madarakani ... get this very clear ..YOU ARE DONE!!!!

Kwa wananchi wengine...ujumbe ni huu, Jueni ukweli wa sheria za asili... yaani Vumilieni kwa busara na kufanya lile linalopaswa kufanya... maana maumivu haya yakitumiwa vizuri KITOTO KICHANGA KIPYA TANZANIA KITATOKEA!

Na tutakuwa tumeyasahau yote yaliyopita kwa kujitwalia UONGOZI MPYA!!!

MUNGU IBARIKI TANZANIA MPYA!!!
 
Azimio,

We could as well state that after Boiling Point, next is Melting Pot!
 
Absence ya Uongozi makini unatufikisha pale ambapo Azimio anasema ni lazima tupitie, tutoe chozi, ngeu kabla ya kuana kujiumba upya.

Niliongelea suala la fujo za Wanafunzi kama kianzio. Lakini sasa kuna mengine ambayo yametokea ambayo yanaonyesha wazi udhaifu wa Uongozi wa nchi yetu.

Mambo haya yametokea katika kipindi cha wiki moja na nusu, na bado mambo yanaendelea. Swali kwa Mtanzania ni mpaka lini tuendelee kusubiri boiling point ipasue pandora box na kuishia kuwa melting point kama si melting the pot?
  • Vijana Tanga kutaka Mawaziri waliojiuzulu kwa tuhuma wavuliwe ubunge na kuondolewa kwenye ngazi zote za CCM.
  • Warioba kutoa kauli kuhusu Ufisadi na muafaka.
  • Kingunge na Makamba kudai Warioba hana wasifu kuzungumzia suala la Muafaka.
  • Wananchi wa Pemba waliokwenda UNDP kulalamika, wameanza kukamatwa na kutiwa ndani na Usalama wa Taifa.
  • CUF wamechoka kuhadaiwa na CCM, wametoa siri za vikao vilivyoigarimu serikali yetu mamilioni ya fedha.
  • Kamati ya EPA inaomba muda zaid kuendelea kufanya uchunguzi, huku wanalipwa "alaunsi" za kila siku kwa kuwa wajumbe wa kamati.
  • UVCCM wametoa vitisho kuwashughulikia CUF na yeyote atakayewabeza CCM. Vitisho hivi si vita vya kauli na sera bali ni ubabe wa mikong'oto!
  • Wanafunzi kule Kigoma wanapewa adhabu kutazama jua! http://www.majira.co.tz/kurasa.php?soma=tanzania&habariNamba=6653
Sasa ukiangalia kila kitu hapo juu, tatizo lake ni uongozi. Sasa kama Uongozi na mbovu namna hii, kwa nini basi tusidai Serikali ibinafsishwe?
 
Back
Top Bottom