Thanx God....17 yrs...Still getting stronger

Hongera sana.Mungu awajalie miaka mingine yenye amani na furaha tele
 
Hongera sana dear Mungu azidi kuwa pamoja nanyi. umenitia moyo sana kumbe inawezekana!
 
GAga yaani unatupa mfano mzuri sana wa jinsi kuwa Panapo Nia pana njia: Ukiamua ndoa yako idumu itadumu. Ubarikiwe sana mpendwa na MUNGU akushibishe kwa mema yote ya nchi.
 
Hongera aisee! yaani miaka 17 kama umefeli darasa la saba unaweza ukahitaji kalkuleta kuihesabu, jambo ambalo ni adimu sana kwa ndoa za kileo.

kuna kajirani kangu hapa majuzi kaliachana na mume wake hata CD ya halusi haijamaliza kuwa edited. Balaaa!
 
Hongera sana kwa kudumisha ndoa kwa miaka 17! Nina imani wengine wameshaoa/kuolewa na kuachika mara kadhaa ktk miaka 17. Bid up, Gaga.
Ila endelea kuzikabili changamoto za ndoa na usibweteke na miaka 17 kwani Al Gore na mkewe wameachana mwaka jana baada ya ndoa ya zaidi ya miaka 30. Mwombe Mungu akusaidie muishi pamoja hadi kifo kitakapowatenganisha.
On top of that sio vibaya ukitumegea siri ya ndoa yenu kuwa imara
 
Hongera Gaga, najua kila ulipojitokeza uchungu ulistruggle kurudisha raha.
Mungu akujalie paradiso njema duniani na mwisho wewe na mumeo mumuimbie yeye milele.
Asante kwa ushuhuda na hadithi nzuri kuwa yote yanawezekana.
 
Gaga hongereni sana,...
duh,you're like a mama to me aiseee,sijui ntaanza lini kusebu na mimi pia
so nice counting,hope utakua mama mkwe hahaha
 
Gaga nahisi uliolewa under age lol.. (Joke)...... Hongera mwaya.. miaka 17 si mchezo!
 
hongera sana Gaga!

Miaka 17 sio mchezo ndugu yangu.. Mungu azidi kuwabariki mpendwa. Wewe mfano wa kuigwa!
 
Back
Top Bottom