Thanks God for Giving us Kikwete

Rev. Kishoka

JF-Expert Member
Mar 7, 2006
4,526
1,529
Katika hiki Kitab Alf Layla wa Layla, napenda kutoa shukrani kwa Mwenyezi Mungu, Subhana Wataala kwa kutupa Jakaya Mirisho Kikwete kuwa Raisi wetu.

We need to thank God for so much blessings to have Kikwete as man in charge.

Yes I have been critical of his leadership, I have mocked him, I have challenged him for his in-activeness and forgot that it was blessings in disguise from our Lord God!

Mungu ni wa ajabu sana, na nafikiri ni mapenzi yake tumepewa Kikwete awe kiongozi wetu. Ni mapenzi ya Mungu leo hii tupo hapa tukipiga kelele na baragumu tukitumia vinubi, zumari na tarumbeta kufukuta hasira zetu, vilio vyetu, aibu yetu na umoja wetu.

Si kwa mapenzi yake Jakaya Kikwete, bali ni mapenzi ya Mungu, kuwa yanayotokea sasa hivi, yalipangwa mapema na Mola.

Nasi tumkubali Jakaya Mrisho Kikwete kwa mapungufu yake yote, ukimya, uzembe, uvivu, uzubaaji, kutokuchangamka, kutokuwajibika na dhana kuwa analinda wale wahujumu. Mapungufu yake, ndiyo ngao na silaha yetu tuliyopewa na Mungu dhidi ya wale wenye kutaka kutufanyia dhuluma na kutuumiza.

Kuporomoka kwa Mawaziri wakubwa na mashuhuri wanne si mapenzi yake Kikwete, maana alitoa machozi. Lakini ni mapenzi ya Mungu leo hii nchi nzima si vilio kuhusu ufisadi tuu, bali mazungumzo ya kutaka uwajibikaji, mazungumzo ya kuimarisha ufanisi, na kulitakia Taifa letu maisha mema na Baraka za Mungu ndiyo yaliyotawala.

Tunataka mshikamano, tunataka uongozi madhubuti, tunataka tufaidi matunda ya utajiri wetu wa asili, uhuru wetu na matunda ya jasho letu bila kunyonywa, kudhulumiwa, kuonewa au kudhihakiwa.

Haya yote yasingetokea kama Kikwete wetu, mtalii, Vasco Da Gama, Sinbad, Chekacheka, Kisura asingekuwa madarakani.

Najiuliza je tungekuwa na mwamko mkubwa namna hii wa kutetea haki zetu kama tungekuwa chini ya Nyerere? Labda ungekuwako, lakini tungekuwa na woga.

Najiuliza je tungekuwa na ukali namna hii wakati wa Mwinyi, yawezekana, lakini bado tungekuwa na woga.

Najiuliza tena tungekuwa na uwezo wa kuchambua mambo muhimu kwa Taifa letu, kuishupalia Serikali, kutafuta ushahidi na hata kuimbua Serikali yetu wakati wa Mkapa? tungeweza, lakini angetupuuza na angetumia ujeuri na dharau zake kutokutusikiliza.

Sidhani kama Kikwete ni msikilizaji mzuri, ila ni baraka za Mungu kuwa kujivuta vuta kwake ambao wengine wamekuita Uyakhe yakhe, Ukwerekwere na Usaigon, ndio umetusaidia sana.

Yeye mwenyewe sijui kama analijua hili, lakini tafadhali sana wewe uliye mwakilishi wa Mheshimiwa Kikwete unayepita kuchungulia JF wamesema nini, mnapoamka Ijumaa hii na kujiandaa na Gwaride la Muungano, mwambie Mheshimiwa Raisi, tunamshukuru Mungu kwa kuwa yeye ni Raisi wetu.

Mapambano yetu bado hayajaisha. Tuendelee kutumia kudra, rehema na baraka hizi za Mwenyezi Mungu, kuendeleza Libeneke la kutaka uwajibikaji, ufanisi, umahiri kupiga vita Uhujumu, Uzembe, Dhuluma, Umasikini, Ujinga na Maradhi.

Kila jamii ina njia yake ambayo Mungu kawatengenezea. Njia yetu ya Ukombozi ni wakati huu wa ndugu yetu Muungwana akiwa Raisi!

Tutumie fursa hii kupigana na wale mahasidi wasiotutakia mema, tuendeleze shinikizo letu kwa viongozi wetu wawe watii wa sheria, walinzi wa katiba, wafuata haki na wanaothamini utu.

Through Jesus Christ our Lord, Amen, Amen, Amen
Through Muhamed our Lord, Amen, Amen Amen
By the Grace of Allmighty Lord, Amen, Amen, Amen

Mungu Ibariki Afrika, Mungu Ibariki Tanzania, Tubariki watoto wa Tanzania.
 
Kwani ni Mungu "alitupa" Kikwete? Kumshukuru Mungu kwa kufanya kitu ambacho labda hakukifanya haiwezi kuwa kumdhihaki? Wewe Carmalenge ambaye unatangazia dunia "Habeamus Papam" unaamini kweli Mungu angetupa Kikwete? Kwani tumemkosea nini?

Mungu alijua, kabla ya wakati, kwamba JK agekuwa Rais wetu. Alijua hivyo hata kabla baba yake JK hajazaliwa. Lakini unataka kusema ni yeye alichora dili la kuchukua fedha BoT kwa ajili ya takrima za kumfanya JK akubalike? Hapana, Mungu hakutupa JK. Tumejitwalia huyu ndugu wenyewe baada ya kunogewa na takrima.

Kilichobaki ni kumwomba Mungu aendelee kumpa JK ujasiri wa kuruhusu mafisadi wafichuliwe. Ampe hata nguvu ya kuwavaa Mkapa, Yona na Rostam Aziz. Akiwavaa hao basi hata mimi nitaanza kudhani labda ni Mungu ametupa huyu mwenzetu.
 
Kwani ni Mungu "alitupa" Kikwete? Kumshukuru Mungu kwa kufanya kitu ambacho labda hakukifanya haiwezi kuwa kumdhihaki? Wewe Carmalenge ambaye unatangazia dunia "Habeamus Papam" unaamini kweli Mngu angetupa Kikwete? Kwani tumemkosea nini?

Mungu alijua, kabla ya wakati, kwamba JK agekuwa Rais wetu. Alijua hivyo hata kabla baba yake JK hajazaliwa. Lakini unataka ksema ni yeye alichora dili la kuchukua fedha BoT kwa ajili ya takrima za kumfanya JK akubalike? Hapana, Mungu hakutupa JK. Tumejitwalia JK wenyewe baada ya kunogewa na takrima.

Kilichobaki ni tumwombe Mungu aendelee kumpa JK ujasiri wa kuruhusu mafisadi wafichuliwe. Ampe hata nguvu ya kumvaa Rostam. Akimvaa huyo basi hata mimi nitaanza kudhani labda ni Mungu ametupa mtu wetu.

Prof. , you are too serious....I don't think he meant it like that..
 
duh!!

sijui malaika gani amemtokea Mchungaji! Maana ni yeye alisema "screw Muungwana", "vua gloves" n.k n.k sasa yawezekana mwenzetu amepata ufunuo wa aina fulani. Ila huyu Mungu huyu siku moja atatuzaba vibao.

On the other hand, labda wachungaji walisema kweli walipodai kuwa Kikwete ni "chaguo la Mungu"... Maana hata Farao alisimamishwa saa na wakati wa Musa ili wana wa Israel watoke utumwani na ni Mungu tunaambiwa aliufanya "moyo wa Farao kuwa mgumu" ili aoneshe utukufu wake.

So, Amen...!
 
duh!!

sijui malaika gani amemtokea Mchungaji! Maana ni yeye alisema "screw Muungwana", "vua gloves" n.k n.k sasa yawezekana mwenzetu amepata ufunuo wa aina fulani. Ila huyu Mungu huyu siku moja atatuzaba vibao.

On the other hand, labda wachungaji walisema kweli walipodai kuwa Kikwete ni "chaguo la Mungu"... Maana hata Farao alisimamishwa saa na wakati wa Musa ili wana wa Israel watoke utumwani na ni Mungu tunaambiwa aliufanya "moyo wa Farao kuwa mgumu" ili aoneshe utukufu wake.

So, Amen...!

mchungaji amefurahi sana leo baada ya kusikia serikali ya JK imeamua kulivalia njuga suala la tuhuma zinazomhusu BWM.
 
Jamani mumemuelwewa vibaya,sio kama anamsifie Kikwete,someni upya mutafahamu nini anamaanisha.
Ni tungo tata mno inayohitaji uyakinifu kuipembua,hicho ni kiswhili cha mafumbo.
Mungu wabariki wazaramo.
 
Mungu anapanga kila kitu na ana makusudi yake.Alimuweka JK kuwa Rais kwa makusudi kabisa sasa tuyasubiri hayo makusudi.Kuna kitu anataka kutuonesha.BWANA ASIFIWE
 
Mungu anapanga kila kitu na ana makusudi yake.Alimuweka JK kuwa Rais kwa makusudi kabisa sasa tuyasubiri hayo makusudi.Kuna kitu anataka kutuonesha.BWANA ASIFIWE

Nitaendelea kupinga kuwa kauli kuwa Mungu alimweka JK, i still believe that JK ni product ya mtandao and dirty politics( unless unataka kuniambia kwako hii ndio maana ya Mungu).

Nakubaliana na Rev Kishoka kuwa tumshukuru mungu kuwa laana iliyotupata huenda ni blessing in desguise, effectaulity yote tunayoiona imesaidia sana kufunua yale ambayo outsiders hatukuyaona. ABSOLUTE POWER CORRUPTS ABSOLUTELY, huko ndiko walikofikia watawala wetu walikuwa na power kupita kiasi baada ya kuona watanzania wamekuwa kondoo kupita kiasi, sasa mambo yameanza kugeuka watanzania wenye uchungu na nchi wameanza kuona kuwa kukaa kimya na kusema tusubiri Yesu arudi au tusubiri imani ya mtume Muhamad itakuwa way toooo late.

Kwa hiyo sioni kama ni kazi Mungu, ni kazi ya mtandao na evil spirit na matokeo yake tunaendelea kuyaona!
 
Mchugaji naona you said all. Mpe muheshimiwa brake on muungano day. We came the long way, but we have a long way to go.Tumeona mengi in our life time, we saw a lot of status quo get drawned.

Tanzania inaongozwa na mungu and inshallah hawa wezi wote wataondoka tuu kwenye system. Mungu ibariki Tanzania kipindi hiki cha kusherekea muungano.
We have a log way to go, but we're going to make it.
HAPPY MUUNGANO TO ALL JF CREW
 
Nakubaliana Na Rev Na Ninaendelea Kumshukuru Mungu Kwa Kumeweka Jk Hapo Naama Kwa Ni Njia Rahisi Ya Kuyajua Maovu Yaviongozi Wetu Na Kupata Ushahidi
 
Labda niseme kwamba tumshukuru Mungu na tuzidi kumuomba aendelee kumfanya Kikwete azidi kusikia vilio vya watanzania!! Kwani kuna mengi tu bado anayafumbia macho, mfano: kulikuwa na kilio cha wengi kuhusu Chenge na alikuwa pia kwenye list of shames pamoja na Tangold yake lakini Rais alimrudisha kwenye Cabinet!!
Hivyo tumuombe sana Mungu ili macho na masikio ya Kikwete yazidi kuwa wazi aweze kuona na kusikia na mafisadi wake.
 
Rev
Nami nikaona chini ya jua kwamba si wenye mbio washindao ktk michezo,wala si walio hodari washindao vitani,wala si watu wa ufahamu wapatao mali lakini wakati na bahati huwapata wote.
Maana mwanadamu naye hajui wakati wake kama samaki wanaokamatwa ktk nyavu mbaya mfano wa ndege wanaonaswa mtegoni,kadhalika wanadamu hunaswa ktk wakati mbaya unapowajilia kwa ghafula.Asomaye na afahamu.Amen!!!
 
Hizi ni habari za kufikirika kwani nothing can stop revolution, Mafisadi wataumbuka kwa namna yeyote tu TIME WILL TELL
 
Katika hiki Kitab Alf Layla wa Layla, napenda kutoa shukrani kwa Mwenyezi Mungu, Subhana Wataala kwa kutupa Jakaya Mirisho Kikwete kuwa Raisi wetu.

We need to thank God for so much blessings to have Kikwete as man in charge.

Yes I have been critical of his leadership, I have mocked him, I have challenged him for his in-activeness and forgot that it was blessings in disguise from our Lord God!

Mungu ni wa ajabu sana, na nafikiri ni mapenzi yake tumepewa Kikwete awe kiongozi wetu. Ni mapenzi ya Mungu leo hii tupo hapa tukipiga kelele na baragumu tukitumia vinubi, zumari na tarumbeta kufukuta hasira zetu, vilio vyetu, aibu yetu na umoja wetu.

Si kwa mapenzi yake Jakaya Kikwete, bali ni mapenzi ya Mungu, kuwa yanayotokea sasa hivi, yalipangwa mapema na Mola.

Nasi tumkubali Jakaya Mrisho Kikwete kwa mapungufu yake yote, ukimya, uzembe, uvivu, uzubaaji, kutokuchangamka, kutokuwajibika na dhana kuwa analinda wale wahujumu. Mapungufu yake, ndiyo ngao na silaha yetu tuliyopewa na Mungu dhidi ya wale wenye kutaka kutufanyia dhuluma na kutuumiza.

Kuporomoka kwa Mawaziri wakubwa na mashuhuri wanne si mapenzi yake Kikwete, maana alitoa machozi. Lakini ni mapenzi ya Mungu leo hii nchi nzima si vilio kuhusu ufisadi tuu, bali mazungumzo ya kutaka uwajibikaji, mazungumzo ya kuimarisha ufanisi, na kulitakia Taifa letu maisha mema na Baraka za Mungu ndiyo yaliyotawala.

Tunataka mshikamano, tunataka uongozi madhubuti, tunataka tufaidi matunda ya utajiri wetu wa asili, uhuru wetu na matunda ya jasho letu bila kunyonywa, kudhulumiwa, kuonewa au kudhihakiwa.

Haya yote yasingetokea kama Kikwete wetu, mtalii, Vasco Da Gama, Sinbad, Chekacheka, Kisura asingekuwa madarakani.

Najiuliza je tungekuwa na mwamko mkubwa namna hii wa kutetea haki zetu kama tungekuwa chini ya Nyerere? Labda ungekuwako, lakini tungekuwa na woga.

Najiuliza je tungekuwa na ukali namna hii wakati wa Mwinyi, yawezekana, lakini bado tungekuwa na woga.

Najiuliza tena tungekuwa na uwezo wa kuchambua mambo muhimu kwa Taifa letu, kuishupalia Serikali, kutafuta ushahidi na hata kuimbua Serikali yetu wakati wa Mkapa? tungeweza, lakini angetupuuza na angetumia ujeuri na dharau zake kutokutusikiliza.

Sidhani kama Kikwete ni msikilizaji mzuri, ila ni baraka za Mungu kuwa kujivuta vuta kwake ambao wengine wamekuita Uyakhe yakhe, Ukwerekwere na Usaigon, ndio umetusaidia sana.

Yeye mwenyewe sijui kama analijua hili, lakini tafadhali sana wewe uliye mwakilishi wa Mheshimiwa Kikwete unayepita kuchungulia JF wamesema nini, mnapoamka Ijumaa hii na kujiandaa na Gwaride la Muungano, mwambie Mheshimiwa Raisi, tunamshukuru Mungu kwa kuwa yeye ni Raisi wetu.

Mapambano yetu bado hayajaisha. Tuendelee kutumia kudra, rehema na baraka hizi za Mwenyezi Mungu, kuendeleza Libeneke la kutaka uwajibikaji, ufanisi, umahiri kupiga vita Uhujumu, Uzembe, Dhuluma, Umasikini, Ujinga na Maradhi.

Kila jamii ina njia yake ambayo Mungu kawatengenezea. Njia yetu ya Ukombozi ni wakati huu wa ndugu yetu Muungwana akiwa Raisi!

Tutumie fursa hii kupigana na wale mahasidi wasiotutakia mema, tuendeleze shinikizo letu kwa viongozi wetu wawe watii wa sheria, walinzi wa katiba, wafuata haki na wanaothamini utu.

Through Jesus Christ our Lord, Amen, Amen, Amen
Through Muhamed our Lord, Amen, Amen Amen
By the Grace of Allmighty Lord, Amen, Amen, Amen

Mungu Ibariki Afrika, Mungu Ibariki Tanzania, Tubariki watoto wa Tanzania.

Rev Kishoka leo umeongea kifalsafa na watu wengi hawajakuelewa ila kwa watu waliosoma falsafa kidogo Rev Kishoka umetukumbusha mwana Falsafa mmoja aitwaye Rev Thomas Robert Malrhus.

Rev Thomas Robert Malthus (Principle of Population) alizungumzia njia mbili za kupunguza population nazo ni Preventive check (au uzazi wa Mpango) na Posive check ( Majanga kama Matetemeko ya Ardhi)

Ukisoma Positive check Malthus anasema "Natural Calamies are blessed in disguise to man". Kwa tafsiri isiyo sahihi "Majanga ya Asili Ni Rehema kwa binadamu". Haina maana kwamba Rev Malthus alikuwa anafagilia au anasifia hayo Majanga lahasha bali alikuwa anatoa mchango wake katika namna ya kupambana na Population.

So Kikwete is blessed in disguise to Sauti za wanyonge na Wanaharakati.

Again thank God for giving us Kikwete
 
13 Reactions
Reply
Back
Top Bottom