Thamani ya Ukuu wa Wilaya yazidi kushuka. Wasaliti, waliokataliwa majimboni na wananchi ndio wanaoteuliwa

Ukiacha kulipwa Mshahara mzuri na marupurupu mengine , likiwemo V 8 labda na Mamlaka ya kiofisi , ukweli ni kwamba wengi wanaoteuliwa kwenye cheo hiki kwa sasa hawaakisi ukubwa wa cheo chenyewe .

Wateuliwa wengi ni wale waliosaliti walikotoka baada ya kuahidiwa vyeo hata kama tabia zao ni za "Kisela" ukiwemo ulevi na ukosefu wa adabu na maadili , jambo ambalo linawafanya wananchi kupigwa na bumbuwazi huku wakishindwa kuendelea kukiheshimu cheo hicho , kiukweli sisi tulio mtaani ndio tunaojua nani ni nani , sasa unapoteua mtu kuwa DC kwa vile tu aliwahi kuvaa fulana ya chama hata kama uadilifu wake ni sifuri inaletea ukakasi mno

Ukiacha Protocal ya kuheshimu Mamlaka ya Uteuzi , ukweli ni kwamba Wakuu wengi wa wilaya wanaoteuliwa hawaheshimiwi na wananchi kutokana na vituko vyao kabla ya teuzi , wengi tumeishi nao na tunawafahamu kuliko hata anayewateua na wala hatudanganyiki

NAKULILIA TANZANIA
Wataje basi na kuainisha maovu yao ili tulifanyie kazi lalamiko lako
 
Ukiacha kulipwa Mshahara mzuri na marupurupu mengine , likiwemo V 8 labda na Mamlaka ya kiofisi , ukweli ni kwamba wengi wanaoteuliwa kwenye cheo hiki kwa sasa hawaakisi ukubwa wa cheo chenyewe .

Wateuliwa wengi ni wale waliosaliti walikotoka baada ya kuahidiwa vyeo hata kama tabia zao ni za "Kisela" ukiwemo ulevi na ukosefu wa adabu na maadili , jambo ambalo linawafanya wananchi kupigwa na bumbuwazi huku wakishindwa kuendelea kukiheshimu cheo hicho , kiukweli sisi tulio mtaani ndio tunaojua nani ni nani , sasa unapoteua mtu kuwa DC kwa vile tu aliwahi kuvaa fulana ya chama hata kama uadilifu wake ni sifuri inaletea ukakasi mno

Ukiacha Protocal ya kuheshimu Mamlaka ya Uteuzi , ukweli ni kwamba Wakuu wengi wa wilaya wanaoteuliwa hawaheshimiwi na wananchi kutokana na vituko vyao kabla ya teuzi , wengi tumeishi nao na tunawafahamu kuliko hata anayewateua na wala hatudanganyiki

NAKULILIA TANZANIA
Donald Trump alikuwa mcheza kamari mwenye kuishi maisha ya kila aina ya starehe. Alipofikisha umri wa miaka 70 akapigiwa kura na wamarekani na akawa rais wao. Kaliongoza taifa hilo kwa miaka minne na sasa anafurahia maisha ya ustaafu.

Mtume Paulo alikuwa muuaji kabla ya kubadilika na kuwa kiongozi wa kiroho, kila Jumapili makanisani jina lake halikosi kutamkwa na mapadre pamoja na wachungaji.

Ukimwangalia samaki namna alivyoishi ndani ya maji huwezi kupata hamu ya kumla. Tubadilike, tuachane na hizi dhana za kuishi kimajungu, maisha yale ya umbeya wa facebook na instagram.
 
Tusubiri wakurugenzi Sasa, kikubwa namwombea mama wakurugenzi ageukie watumishi wa umma Kama taratibu zinavyotaka.Kuteua makada kwenye ukurugenzi Ni kuvuruga utumishi wa umma
Ni kweli DED na DAS wanafaa kuwa senior civil/public servants ili watekeleze vilivyo majukumu yao. Walau wenye miaka 10 ktk utumishi.
 
Unamchukulia poa ? Amepiga shule kutosha DC....kuimba ni ajira tu ila kichwani madini yapo


Ni zaidi ya kuwa na elimu.

Ndiyo maana kazi rasmi duniani wafanyakazi wanapatikana kwa process ya usaili hata kama waloomba wote wana first class za kwanza

Unazani kwa nini kwenye ajira watu huwa wanafanyiwa usaili na kutafuta the best to fits?
Je kigezo ni elimu pekee?

Ni zaidi ya elimu.

Sababu mtu aweza kuwa na elimu lakini sifa nyingine na namna ya kukabiliana na changamoto hawezi .

Na hiyo ni utafiti wa kisayansi umethibitisha hayo.
 
Hivi kwa nini hawawapandishi hawa watu waliopo chini?
Ingekuwa ni njia moja wapo ya kuongeza ajira, unampandisha aliyepo, anaacha gap, unaliziba kwa ajira mpya; sasa wao wanapeana ulaji kisiasa kulipana fadhila za waliyotendeana kabla.
 
Tatizo siyo ukuu wa wilaya tatizo majukumu ya ukuu wa wilaya

Jukumu kubwa ambalo DC analo ni kuwa mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama wa wilaya

Haya unapowuweka mvuta bange, Mlevi kwenda kuongoza hii kamati unategemea nini zaidi ya Yale Yale ya kina ole sabaya kujitokeza upya

..pia wakati wa magufuli wako ma-dc na ma-rc ambao waliteuliwa kwa malengo mahsusi ya kwenda kuwahujumu wabunge upinzani, pamoja na halmashauri zilizokuwa zinaongozwa na madiwani wa upinzani.
 
Et Nikki wa pili nae DC , hii nchi hii imekosa maono
Cha ajabu kipi Sasa!??
Umeambiwa jamaa ni graduate mwenye matokeo yake toka shuleni.
Kijana ametumia kipaji badala ya kupanga foleni kusubiria ajira. Kwangu hiyo ni credit.
Anajitambua halingano Ni vijana wanaoazima pasi wananyoosha Kisha wanabeba bahasha kuzunguka kila ofc kuomba kaz.

Nashauri tungoje matokeo. Hata Jokate walimdiss na kumzushia Mambo kibao lakini Leo hi Yuko kwenye 10 bora
 
..pia wakati wa magufuli wako ma-dc na ma-rc ambao waliteuliwa kwa malengo mahsusi ya kwenda kuwahujumu wabunge upinzani, pamoja na halmashauri zilizokuwa zinaongozwa na madiwani wa upinzani.
Swali kwa Sasa je unafikilia nini kinaenda tokea ni ugovi wakugombea wasichana wao kwa wao Wakurugenzi na madc nk ngoja uone
 
Swali kwa Sasa je unafikilia nini kinaenda tokea ni ugovi wakugombea wasichana wao kwa wao Wakurugenzi na madc nk ngoja uone

..nadhani safari hii ma-dc watapooza sana kwasababu hakuna wabunge na madiwani wa upinzani wa kuwadhulumu na kuwadhalilisha.

..huu ndio wakati tutaelewa kwamba dc ni ngazi ya utawala ambayo haihitajiki hapa nchini na ni mzigo kwa wananchi walipa kodi.
 
..nadhani safari hii ma-dc watapooza sana kwasababu hakuna wabunge na madiwani wa upinzani wa kuwadhulumu na kuwadhalilisha.

..huu ndio wakati tutaelewa kwamba dc ni ngazi ya utawala ambayo haihitajiki hapa nchini na ni mzigo kwa wananchi walipakodi.
Naunga mkono hoja tukutane badae kwenye mkeka wa Wakurugenzi mama anakauli yake zege halilali
 
Back
Top Bottom