Thamani ya shilingi yapaa Gavana adai Uchumi umepaa pia mimi nasema hapana wewe je ?

Chingwanji

Member
Oct 18, 2006
54
2
2008-03-15 08:54:40
Na Dunstan Bahai

Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Profesa Benno Ndulu, amesema thamani ya Shilingi imepanda kutokana na benki hiyo kujitahidi kudhibiti mfumuko wa bei.

Aliyasema hayo jana jijini Dar es Salaam ikiwa ni mara ya kwanza katika utaratibu aliyojiwekea wa kuzungumza na waandishi wa habari kila baada ya miezi mitatu kuhusu shughuli za benki hiyo na hali ya uchumi nchini.

Alisema dola moja awali ilikuwa ni Sh. 1,300 lakini sasa ni Sh. 1,160.

Hata hivyo, alisema kupanda kwa shilingi pia kumechangiwa na kukuwa kwa uchumi hasa kwa sekta mbalimbali kwa kuwa na mchango mkubwa katika pato la Taifa.
Alisema kilimo kimepitwa sana na sekta nyingine katika kuchangia pato la taifa.

Alisema katika mwaka uliopita wa fedha, pato la taifa kwa mauzo ya bidhaa nje ya nchi na huduma lilifikia dola bilioni 3.5 ambapo mazao ya kilimo thamani yake ilikuwa ni dola milioni 300 sawa na asilimia 10 tu ya pato la Taifa.

Kwa upande wa usafirishaji, sekta hiyo alisema iliingiza dola milioni 340, viwanda dola milioni 350 wakati sekta ya madini dola milioni 800.

Kuhusu matumizi ya dola ndani ya nchi, Profesa Ndulu alisisitiza kuwa sheria mpya za benki hiyo zinamkataza mtu au taasisi yoyote kumshurutisha Matanzania aliyeko ndani ya mipaka ya nchi kutumia dola.
Alisema atakayebainika, sheria iko wazi ya kumshtaki au kumchukulia hatua nyingine yoyote.
Kuhusu akaunti ya madeni ya nje (EPA) alisema BoT imekwisha unda kamati kuchunguza na kwamba upouwezekana hata akauti hiyo ikafutwa.

``Kuna shughuli nyingine zimeingia BoT kama mzigo kwani si kazi ya benki Kuu kuzifanya. Kazi kuu za BoT zimeainishwa bayana kama vile kusimamia uchumi wa nchi, kusimamia na kuangalia usalama wa benki na taasisi nyingine za kifedha, kudhibiti mfumuko wa bei, kuhakikisha malipo yako salama,`` alisema.
Alitoa mfano wa shughuli zilizokuwa zinafanywa na BoT ambazo si za msingi kama za ununuzi wa dhahabu uliokuwa ukifanywa na benki hiyo katikati ya miaka ya 1992 na 1994.

Kwa mujibu wa Gavana huyo, BoT iliingia kichwa kichwa kufanya biashara hiyo pasi kuijua ingawa hakutaja hasara labda iliyojitokeza hadi kusitisha kuendelea na biashara hiyo.

Alisema zipo shughuli nyingi zinazofanywa na benki hiyo ambazo si za msingi na hivyo kuna kazi ya kuzichunguza na zipo ambazo zitafutwa.

Kuhusu mikopo inayofanywa na benki za biashara na taasisi za kifedha, alisema BoT inajitahidi kupunguza riba kwa taasisi hizo ili nao washawishike kuwapunguzia riba wakopaji.

Kuhusu uvumi kuwa wapo waajiriwa wa BoT ambao hawana sifa, alisema kazi inafanywa ya kuwachunguza na ikibainika ni kweli, wataachana nao.

SOURCE: Nipashe
 
actually kwa watu wenye kipato cha juu....na wananchi wahali ya juu wafanyabiashara wakubwa na hasa waagizao bidhaa nje(magari nk) watakubaliana na gavana! mfano mtu anayeagiza gari la dola 10,000 wakati dola ilikuwa 1300 anglipa milion 13,000,000 wakati sasa ambapo dola ni sh 1160 atalipa 11,600,000TOFAUTI YA MILION MOJA NA LAKI NNE SI HABA 1,400,000......
TUJE KWA MTANZANIA WA KAWAIDA NA WA HALI YA CHINI.......HIZI STATISTICS HAZIMSAIDII CHOCHOTE...NDO KWANZA MAISHA YANAPANDA...mtu huyu huwezi kumshawishi kuwa uchumi umekuwa huku maisha ni magumu....so kwa mtanzania wa chini uchumi haujakuwa na kwa wala nchi uchumi umekuwa........! nimeeleweka hapo......!
 
Ukweli ni kwamba fungu la mchicha kupanda bei au kilo ya mchele haiwahusu BOT, wao wanaangalia dhahabu, almasi tanzanite, mafuta na takataka zingine.
Nadhani hawa BOT hawana muda wa kuangalia sekta nyingine ambazo zinaweza kusaidia kupandisha uchumi wetu, Ninaweza nikajitolea kuwapa darasa waone how arts and crafts inaweza kusaidia kuipandisha chati shilingi yetu. Wasifikirie kuuza mahindi na pamba nje tu itatosha, kuna vitu hambavyo hawaviweki ktk rekodi ya comodities za kuexport.

Pia nadhani hawa BOT wanafanya kazi ktk mzingo wa twintowers, yaani sijaona kama wanaleta data zenye uhalisia wa real situation.

Prof. Ndulu, usifikiri akiba ya fedha za kigeni itakuja kwa kuexport hewa...
 
actually kwa watu wenye kipato cha juu....na wananchi wahali ya juu wafanyabiashara wakubwa na hasa waagizao bidhaa nje(magari nk) watakubaliana na gavana! mfano mtu anayeagiza gari la dola 10,000 wakati dola ilikuwa 1300 anglipa milion 13,000,000 wakati sasa ambapo dola ni sh 1160 atalipa 11,600,000TOFAUTI YA MILION MOJA NA LAKI NNE SI HABA 1,400,000......
TUJE KWA MTANZANIA WA KAWAIDA NA WA HALI YA CHINI.......HIZI STATISTICS HAZIMSAIDII CHOCHOTE...NDO KWANZA MAISHA YANAPANDA...mtu huyu huwezi kumshawishi kuwa uchumi umekuwa huku maisha ni magumu....so kwa mtanzania wa chini uchumi haujakuwa na kwa wala nchi uchumi umekuwa........! nimeeleweka hapo......!


upuuuuuuuuzi mtupu, sijui hata mnajaribu kumdanganya nani??
ukweli ni kwamba $$$ ndio imeporomoka na sio shillingi kupanda!! ebu jaribu ku-compare shillingi ya TZ na ile ya Kenya, then compare na pesa nyingine kama Yen, Pound n.k ktk same time frame......kisha rudi tena hapa na hizo hadithi zako za chekechea!! watu wengine bwana, ovyooooooo....
 
upuuuuuuuuzi mtupu, sijui hata mnajaribu kumdanganya nani??
ukweli ni kwamba $$$ ndio imeporomoka na sio shillingi kupanda!! ebu jaribu ku-compare shillingi ya TZ na ile ya Kenya, then compare na pesa nyingine kama Yen, Pound n.k ktk same time frame......kisha rudi tena hapa na hizo hadithi zako za chekechea!! watu wengine bwana, ovyooooooo....
HAPA TUTAWAJUA TU WALA NCHI NA WALALAHOI....!
 
HAPA TUTAWAJUA TU WALA NCHI NA WALALAHOI....!

sasa hiyo hapo juu maana yake nini??.......huu upuuzi wenu unaitwa 'dumb economics' ambayo alwayz ni fools paradise!! its a shame, msomi kama gavana wa BOT anapotosha watu namna hii.
Angalia bei ya mafuta na gold ktk soko la dunia, yote hiyo ina reflect kuanguka kwa $$. Kuna sehemu za kitalii in India hasa Taj Mahal hawakubali $$ tena kwa malipo.......europeans na euro zao wanakuja kufanya shopping US kwasababu wanapata bargain nzuri juu ya kwamba $$ imeporomoka!!
Bottomline hapa tena kwa makelele ni $$ NDIO IMEPOROMOKA na ni URONGO KUSEMA KUWA Tshillingi IMEPANDA!!.
 
Huyu Jamaa Baada Ya Kusema Dola Imeshuka Thamani Anasema Shilingi Imepanda Thamani.ni Sawa Sawa Na Mtu Aliyekuwa Anaendesha Baisikeli Akafika Kwenye Mteremko Baiskeli Ikaenda Bila Kuchochewa Alafu Mwingine Anasema Jama Anachochea Baiskeli Kumbe Ni Nguvu Ya Mteremko.
 
Huyu Jamaa Baada Ya Kusema Dola Imeshuka Thamani Anasema Shilingi Imepanda Thamani.ni Sawa Sawa Na Mtu Aliyekuwa Anaendesha Baisikeli Akafika Kwenye Mteremko Baiskeli Ikaenda Bila Kuchochewa Alafu Mwingine Anasema Jama Anachochea Baiskeli Kumbe Ni Nguvu Ya Mteremko.

....kwikwikwikwikwikwikwikwi..........

.......some professors bana!!.....hizi justification nyingine sikupata namna nzuri ya kuielezea zaidi ya ndugu yangu tgeofrey!

dah kwikwikwikwikwi
 
actually kwa watu wenye kipato cha juu....na wananchi wahali ya juu wafanyabiashara wakubwa na hasa waagizao bidhaa nje(magari nk) watakubaliana na gavana! mfano mtu anayeagiza gari la dola 10,000 wakati dola ilikuwa 1300 anglipa milion 13,000,000 wakati sasa ambapo dola ni sh 1160 atalipa 11,600,000TOFAUTI YA MILION MOJA NA LAKI NNE SI HABA 1,400,000......
TUJE KWA MTANZANIA WA KAWAIDA NA WA HALI YA CHINI.......HIZI STATISTICS HAZIMSAIDII CHOCHOTE...NDO KWANZA MAISHA YANAPANDA...mtu huyu huwezi kumshawishi kuwa uchumi umekuwa huku maisha ni magumu....so kwa mtanzania wa chini uchumi haujakuwa na kwa wala nchi uchumi umekuwa........! nimeeleweka hapo......!

yournameisYOURS na OGAH......MMEELEWA HIYO BOLD....!?
 
THANKS TOO yourname......!
As mahesabu always and always my standings will be firm to advocate the exploited,embaraced,terrorised,weakened,poor,TANZANIA,our culture,......etc.....and not mafisadi,walanchi,magabacholi,waroho wa madaraka....nk!
NAOMBA KUELEWEKA HIVYO....!
 
upuuuuuuuuzi mtupu, sijui hata mnajaribu kumdanganya nani??
ukweli ni kwamba $$$ ndio imeporomoka na sio shillingi kupanda!! ebu jaribu ku-compare shillingi ya TZ na ile ya Kenya, then compare na pesa nyingine kama Yen, Pound n.k ktk same time frame......kisha rudi tena hapa na hizo hadithi zako za chekechea!! watu wengine bwana, ovyooooooo....

huo ndo ukweli wenyewe $$$$$$ imeshuka, subirini $$ ipande sijui tutaambiwa nini??
 
Kuna uwezekano mkubwa kabisa kwamba nchi hii ina wasomi waongo, la sivyo imejaa wahuni sehemu nyeti ama ina mbumbu wenye vyeti vizuri. Sina uhakika kabisa kuwa gavana mwenye kufikiria kwa makini anweza kusimama na kudai kuwa uchumi umepanda. Shilingi haijapata nguvu yoyote na wala hakuna kudanganya mtu hapa kwani tunafahamu kuna ku-dorora kwa dola kunakoifanya shilingi kupanda dhidi ya dola na si shilingi tu, bali hata hela za nchi nyi9ngine zimekuwa hivyo. Kuna sababu nyingine za wapumbavu waliodai kuwa inflation inasababishwa na kupanda kwa bei ya vyakula. Huu ni upumbavu uliopindukia. Vyakula vinapanda bei kutokana na kupanda kwa gharama mbalimbali ikiwemo ya kusafirisha bidhaa, iweje chakula kiwe chanzo cha inflation.
Ndugu gavana acha kudanganya umma huu kama yamekushinda toka ukapumzike nyumbani na uwadanganye watoto wako kwa hadithi za sungura na fisi, na si watanzania.
 
upuuuuuuuuzi mtupu, sijui hata mnajaribu kumdanganya nani??
ukweli ni kwamba $$$ ndio imeporomoka na sio shillingi kupanda!! ebu jaribu ku-compare shillingi ya TZ na ile ya Kenya, then compare na pesa nyingine kama Yen, Pound n.k ktk same time frame......kisha rudi tena hapa na hizo hadithi zako za chekechea!! watu wengine bwana, ovyooooooo....

Hivi akisema shilingi imepanda kwa kuwa thamani ya dollar katika soko la dunia imeporomoka ataonekana juha!? Je, shilingi hiyo hiyo iliyopanda ukilinganisha na dollar inafanyaje ukilinganisha na EURO, UK POUND na currencies nyingine mbali mbali duniani? Kudanganya Watanzania kila kukicha!
 
Huyu Profesa vipi, anatuona sisi watoto wa chekechea au? Angetuambia kuwa hela nyingine (kama GBP, Euro) zilikuwaje kwa kulinganisha na TZS na sasa hivi ziko bei gani. Na hata bei za vitu vinavyouzwa kwa USD zimepanda kwa kuwa USD imeshuka bei. Sasa kushuka uchumi wa US ndio tunaita kupanda thamani hela ya Tz? Masikhara haya!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom