Thamani ya Kombe la Ligi Kuu.

Mbao za Mawe

JF-Expert Member
May 11, 2015
23,373
54,755
Kwema waungwana.

Nimekuwa najiuliza bila mafanikio yeyote kuhusu hii ligi ya VPL, Kwanza naomba kufahamu ni kiasi gani mshindi wa ligi ya vodacom anapewa pale anapotwaa taji hilo.

Gharama ambazo vilabu vinatumia wakati wa ligi zinaweza kuwa sawa na Thamani ya kikombe?
 
Vpl ni million 70

Gharama zinazotumia timu mfano yanga ni karibu million 500 katika usajiri

Kombe halirudishi gharama ila linakupa mwanya wa kupata wadhamini watakaotia mzigo wa maana

Kombe linakupa mwanya wa kushiriki michuano ya kimataifa ambapo ukifika hata makund tu ukawa wa mwisho unaingiza almost million 900-billion 1

Na mengine mengi tu ,

Hii ni the same na EPL uingereza, EPL lina thamani ya Paund million 30

Ila timu kama man u zinafanya usajiri wa paun million 200

Na mwisho wa msimu wanafunga mahesabu kwa faida

Kutoka ktk mauzo ya jezi

Haki za matangazo

Kushiriki uefa

N.k

Yote hayo chanzo ni kufanya vizuri ktk ligi

Hivo usije kushangaa YANGA anamnunua chirwa million 200 ukazani lengo ni kugombea million 70 pekee hapana, kuna malengo mengi hapo ,kupiga faida
 
Back
Top Bottom