Thamani ya Dawa na Vifaa Tiba Vilivyo Expaya MSD ni Zaidi ya Tsh 20 Billion; CAG Hajaripoti

Stuxnet

JF-Expert Member
Feb 12, 2011
10,228
17,440
Wakati wananchi wanalalamika ukosefu wa dawa kwenye hospitali na zahanati, yasemekana kwenye Bohari Kuu ya Madawa (MSD) kuna dawa zilizo expaya za thamani ya zaidi Tsh Bilion 20. Nimepitia ripoti ya CAG ya mwaka 2019/20 kwa haraka haraka sijaona hoja ya ukaguzi kuhusu dawa zilizo expaya.

Je timu ya CAG iliyotumwa MSD haikuliona hili?

Ushauri:
Hata kama CAG hakuliweka Wabunge waliopo kwenye Kamati ya Huduma za Jamii wanaweza kumuuliza Waziri wa Afya alitolee majibu kwa vile kiasi hicho ni kikubwa sana kuharibika wakati wananchi wanakosa hata dozi ya Panadol kwenye zahanati
 
Hiyo ripoti hukutakiwa kuipitia haraka haraka, unatakiwa uipitie kwa makini uje na habari complete hapa jf.

Hao MSD nao nasikia wanaidai serikali pesa zao hawalipwi, kama ni kweli hii taarifa yako basi na serikali itakuwa inachangia kuimaliza MSD kwa kulimbikiza madeni.
 
Wewe taarifa za madawa kuexpire umezipata wapi?
Kama hamuitaki mwaka huu basi mtakutana nayo mwaka kesho. Anyway kipindi cha Mwendazake taarifa zilikuwa zinafunikwa sana ndiyo maana wabunge akina Msukuma na Deo Sanga walidhani Magufuli anadhalilishwa
 
Wewe taarifa za madawa kuexpire umezipata wapi?
Hapo ndipo tofauti ya ma great thinker wa JF na watu wa kawaida. Nina chanzo changu ndicho kimenijuza.

Uzuri ni kwamba MSD ni public parastatal na hizi siyo Siri. Ukienda kununua dawa kwenye maghala yao utaambiwa hakuna. Lakini unaziona zimejaa kwenye maghala ya Dar, Moshi na Tanga. Ukiwauliza wanakuambia zime expaya. Ndiyo nilivyopata taarifa hii
 
Hapo ndipo tofauti ya ma great thinker wa JF na watu wa kawaida. Nina chanzo changu ndicho kimenijuza.

Uzuri ni kwamba MSD ni public parastatal na hizi siyo Siri. Ukienda kununua dawa kwenye maghala yao utaambiwa hakuna. Lakini unaziona zimejaa kwenye maghala ya Dar, Moshi na Tanga. Ukiwauliza wanakuambia zime expaya. Ndiyo nilivyopata taarifa hii
Kuwa great thinker ni kuleta ushahidi na sio majungu. Leta ushahidi.
 
Kuhusu madeni kwenye ripoti ya CAG yako covered vizuri na Serikali imeahidi kuyalipa baada ya kuyahakiki. Nilichoshangaa ni kiasi kikubwa cha dawa ku expaya bila kutumika wakati wananchi wanakosa dawa kwenye vituo vya afya.
Hiyo ripoti hukutakiwa kuipitia haraka haraka, unatakiwa uipitie kwa makini uje na habari complete hapa jf.

Hao MSD nao nasikia wanaidai serikali pesa zao hawalipwi, kama ni kweli hii taarifa yako basi na serikali itakuwa inachangia kuimaliza MSD kwa kulimbikiza madeni.
 
hospitali za serikali wapo radhi kukwambia dawa hakuna ili ulipe wakati dawa zinazoza stoo
 
Mnamuonaga CAG Mungu mtu.
Utajajua hujui kumbe nae mla rushwa kubwakubwa tu.
 
Wakati wananchi wanalalamika ukosefu wa dawa kwenye hospitali na zahanati, yasemekana kwenye Bohari Kuu ya Madawa (MSD) kuna dawa zilizo expaya za thamani ya zaidi Tsh Bilion 20. Nimepitia ripoti ya CAG ya mwaka 2019/20 kwa haraka haraka sijaona hoja ya ukaguzi kuhusu dawa zilizo expaya.

Je timu ya CAG iliyotumwa MSD haikuliona hili?

Ushauri:
Hata kama CAG hakuliweka Wabunge waliopo kwenye Kamati ya Huduma za Jamii wanaweza kumuuliza Waziri wa Afya alitolee majibu kwa vile kiasi hicho ni kikubwa sana kuharibika wakati wananchi wanakosa hata dozi ya Panadol kwenye zahanati
Binadamu ni katili sana. Hizo dawa ni kusaidia na kuimarisha afya na maisha ya watanzania. Waliopewa dhamana huko kwenye bohari ninmaselfish wa aina yake.
 
Ukienda kwa MSD na OS yako wanakupa kibali kwenda kwa mshitiri ASTRA kwamba wao hawana dawa kisa hawajalipwa na user department hapo Sasa ndo wanachemka midawa inadodea stoo, hii Inji hii!!
 
Back
Top Bottom