Thamani ya chupi yako. Ilinde chupi, imebeba maagano, imebeba laana, imebeba baraka, imebeba mapepo

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,633
697,754
Ni muda sahihi wa kujongea vitandani mwetu, nyumbani chumbani ama ugenini kwa ndugu jamaa na marafiki ama nyumba za wageni.

Usiku huu kama ilivyo siku nyingine zozote ama mchana wake kuna mambo yameendelea, yanaendelea na yataendelea.

Ni ndani ya nyumba na vyumba vetu milango ikiwa imetiwa komeo na madirisha yakiwa yameshushwa pazia
Katika hili inategemea una nani na mnafanya nini ama mmefanya nini
Nazungumzia thamani ya chupi yako na yule unayemvulia.

Kwa muktadha huu kuvua kwa maana ya kufanya matusi aka ngono
Mnapokutana kwenye hili tendo lenye asili ya Eden kuna watu watatu wanahusika na kuhusishwa kimwili na kiroho.

Wewe na mwenza wako mnakuwa kwenye nafsi ya kimwili. Mungu na shetani wanakuwa kwenye nafsi ya kiroho!!

Kwanini Mungu...? Kama hamfanyi ngono kwa usahihi na nia ovu ya kutamaniana tu na sababu zingine kama rushwa ya kitu fulani ama nia ya kupata faida fulani, kipato nk

Kwanini shetani? Kama ukitokea ugomvi kati yenu, ama kufanya kwa nia ya kukidhi tamaa za kimwili, ulafi, na kwa nia ya kufaidika kifedha, ajira, nafuu ama msaada fulani.

Wote tunatambua dhima, furaha na raha ya kumvua mtu chupi, kukuvulia ama kuvuana kwa hiari, bila lazima, bila kulazimishana, bila sababu fulani bali kwa heshima, upendo, tafakuri, ladha na kujali.

Bila tamaa za kimwili bali hisia za kweli na upendo toka rohoni. Hapa shetani hukaa mbali na ukuu wa Mungu hutamalaki...

Ngono ni ibada na tendo la kiroho linalobeba maana kubwa mno... Ndio maana zile sehemu zinazohusika na tendo hili huitwa sehemu za siri. Yaani si kwa kila mtu. Ngono si tendo la kufanya na kila mmoja ama watu wengi.

Ni faragha ya wawili wapendanao na wenye kunia umoja, misimamo, upendo na hisia za ndani kabisa. Hapa huwezi kupata mapepo ama mashambulizi ya maroho kinzani...!

Sasa basi mapepo ya ngono yanatoka wapi? Nuksi kwenye ngono inatoka wapi!? Kimavi na mikosi je? Ngono ina mahusiano makubwa sana na mambo ya kiroho.

Kwa kila tendo moja la kingono linalofanyika kuna falme mbili zinahusika.Ufalme wa nuru na ufalme wa giza
Mapepo ya ngono ni matokeo ya ufalme wa giza.

Kwa kila mwenza mnayevuana chupi ni pepo jipya mnalizalisha... Wewe ni roho kamili, sasa imagine roho yako inapokutana na roho mpya daily kila siku unatengeneza kitu gani?

Ni kama maroho yaliyo kwenye vilevi, kwenye starehe nyinginezo nk nk.

Haya ni mapepo yanazaliwa kukua na kustawi. Lakini kwanini pepo la ngono ndio lina nguvu zaidi?

Ungana nami sehemu ya pili kukipambazuka japo mada hii haijatendewa haki kwa kuwekwa jukwaa la imani na dini.



SEHEMU YA PILI....!

Kuna hisia za ajabu na raha ya aina yake pale inapofikia sehemu muhimu ya kuchojoa chupi... Ni moment yenye ladha ya aina yake hasa ikiwa ni kwa mara ya kwanza ama kwa yule umpendaye....
Uvuaji huu wa chupi ni ibada ya kiroho yenye pande mbili hasi na chanya...

Inategemea unamvulia nani na kwa nini...
Kuvua chupi kwa muktadha huu kuna tafsiri moja tu kukamilisha tendo lenye vinasaba na dhambi ya asili
Kwenye maingiliano ya kimwili kuna mgeni na kuna mwenyeji... Yeyote kati ya hawa anaweza kuwa si mwema... Na kadiri unavyofanya ngono na watu wengi ndio umajimaliza nguvu zako za kiroho huku ukistawisha mamlaka za giza kwakuwa mojawapo ya chakula chao kikuu ni manii.. Hivyo kwakuwa unazo za kutawanya basi unajikuta unashikiliwa mateka na mapepo husika ili uwe mtumwa za kuzalisha na kuzalisha

Makundi yenye manii zenye nguvu sana kiroho ni makundi mawili
Kundi la kwanza ni kundi lililokula kiapo na yamini kwenye madhabahu ya kidini.... Unapokula kile kiapo cha useja unajiundia nguvu ya kiroho kuanzia wewe mwenyewe mpaka kila kitu chako.... Sasa mamlaka za giza zinapokukamata sidhani kama utaweza kuchomoka.... Watakubarikia pesa umaarufu na kila kitu lakini vyote vitaishia kwenye chupi... Na kamwe hutakuwa na mwisho mwema... Waangalie kwa mfano mapadre, manabii na mitume wa kileo

Kundi la pili ni kundi la wanandoa.. Wale waliokula kiapo cha kiimani... Hapa napo kuna shida, kiroho kwa upande wa nguvu za giza ni aina fulani ya ubinafsi na uchoyo... Wanandoa sio carefree na manii zao zina kiapo hivyo nazo ni malighafi zenye nguvu mno... Kwahiyo nao wakitetereka kidogo tu kwasababu yoyote ile hutekwa mazima....
Nitaendelea sehemu ya tatu

SEHEMU YA TATU NA YA MWISHO

Chupi inatumika kama kielelezo ama mlinzi wa kufunika ama kuficha utupu... (Chupi kwa maana yake halisi na sio hivi vikamba vya siku hizi.... Na pia chupi imetumika kama kipitio cha kutekeleza tendo la ngono isiyorasimishwa kisheria, kiimani wala kimila

Kama kuna malighafi inaweza kutumika kwa haraka na kuwa ufanisi wa hali ya juu basi ni chupi ilibeba ute wa utupu, manii, nywele za siri, jasho hata vinyweleo ama damu ya hedhi

Zaidi ni kwamba kupitia chupi hiyo hiyo, utupu wako unaweza kutumika kuzalisha mapepo, kuyafuga, kutupiwa kimavi au gundu, na hata kubeba maroho ambayo yanaweza kuja kukusumbua sana baadae
Wengi wamevuruga kazi, maisha na hata familia kwasababu tu ya chupi... I mean kuvuana chupi kwa nia ya kufanya ngono

Nihitimishe tu kwa kusema chupi yako ina thamani kubwa na imebeba dhamana kubwa katika maisha yako bila kujali wewe ni jinsia gani... Chupi yako ni sehemu ya uhai wako
Haipaswi kuonwa na kila mtu... Haivuliwi kwa kila mtu... Unavua kwa wakati sahihi na mtu sahihi.... Si kila mmoja ni wa kuvulia chupi la hasha kwa kufanya hivyo unavunja kuta na kingo imara za kinga za kiroho.... Heshima, raha na ladha ya chupi ni pale unapomvulia anayepaswa kuvuliwa tuu.....

Kwaherini

Jr
 
Nimetafuta kitufe cha kuripoti sikioni... Lakini Moderator, jamiiforum hii ni mada kweli ya kuwekwa jukwaa la dini?

Jr
mwenyew siku na access ya jukwaa la DINI ila nime jikuta nauona huu uzi jukwaa la Dini ivo nime kua granted na hiyo access sasa najiuliza apa nime pewa na access ya jukwaa la wakubwa au laaa wacha niendelee kuangalia kwenye haya majukwaa labda ntalionaaa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mshana Jr ni mtu mshirikina mshirikina tu hapa jukwani,,sio mtu mzuri sana hapa jukwani ,kama mnafahamiana akija kwako kama una mtoto mchanga usimpe abebe,, usikubali asalimiane na mke wako kwa kushikana mikono (Hapa ndipo alipo mpatia Demis) ,huyu mtu ni mlozi sana,, asijue kazi yako huyu Mkuu anaweza loga ukafukuzwa au kupewa barua ya onyo ,kushushwa cheo ,kutokupata safari ,huyu mtu hapana aise .Mitambo yake ya maangamizi iko msata ndo maana anaishi msata na kufanya kazi Dar .Huyu Mkuu tuwe nae makini hata kuchangia nyuzi zake huenda ndo unabeba mikosi yenyewe kwa kuchangia ,


Unisamehe sana Mkuu kama utakuwa umekwazika na sio kupata wateja wengi ,usinifanyie chochote maana wewe ni kama Baba yangu tu ,maana baba yangu mwezi wa sita mwaka huu anatimiza miaka 49 na wewe ni around umri huo tu ,, wewe ni Kama Baba yangu mazazi tofauti tu wewe ni mganga mganga,mshirikina mshirikina ,mchawi mchawi na mambo yafananayo na hayo:
 
....zinaa ni kama mkopo/deni hivi ata ukifa litaandkwa baddebt na litaenda kupunguza faida (profit) katka record zako..na ndomana kiimani tunaamini zinaa ni deni na lazima litalipwa,

naunga mkono hoja ya apo juu,
 
Back
Top Bottom