Thamani ya baba yangu ni kubwa kuliko thamani ya mama yangu.

kitokololoo

JF-Expert Member
Nov 26, 2018
704
813
Ninaandika huu uzi japokuwa wengi hawatakubariana na hichi nachosema.

Mimi nimezaliwa mpaka najitegemea sijawahi uona upendo wa mama yangu

My story: Baba yangu na mama yangu walitengana nikiwa na miaka miwili mama aliondoka na kwenda kuolewa na mwanaume mwingine toka hapo baba yangu alikuwa ndiyo mama yangu ndiyo baba yangu.

Baba alihakikisha nakula,navaa,nasoma miaka ikapita nami Mwenyezi Mungu akanijaharia nikamaliza chuo na kupata kazi na kujitegemea.

Mpaka naandika uzi huu wazazi wangu wote wameshafariki Mwenyezi Mungu awapumzishe kwa amani

Kipindi cha msiba wa marehem baba yangu nililia sana kwa uchungu sana maana nilikuwa peke yangu mama yangu kanitenga kaka ambao tumechangia baba tu walikuwa botswana migodini huko hivyo walichelewa kufika msibani niliumia sana kumzika baba yangu peke yangu bila mama yangu kuja msibani.

Baada ya msiba nilisikia ndugu zangu wakisema huyu mtoto kalia sana kwa sababu mama yake alimwacha mdogo sana pia wakati mama yake anaondoka alitamka maneno makali sana kwamba mama yangu alitamka kwamba mimi naondoka namwacha mtoto wenu akifa mtajua nyinyi akipona mtajua nyinyi hayo ni maneno ya mama yangu mbele ya baba yangu na ndugu zangu.

Sababu kubwa ya mama kuondoka nyumbani ni kuwa hali ilikuwa ngumu ya kiuchum nyumbani lakini hata kama ndiyo hivyo mama yangu hakunionea huruma mimi na kuniacha nikiwa na umri mdogo kiasi kile mpaka aniache na baba yangu kweli?

Baadae baba alipata kazi shirika la reli maisha na akawa pia pale nyumbani anafuga kuku nakumbuka na ng'ombe na kulima pia kaka zangu walikuwa wanamsaidia sana kidogo maisha yakabadirika nyumbani lakini baba yangu hakuamua kuoa tena mpaka anapofariki.


Huwa naumia ile kauli aliyotamka mama yangu kwamba kama ndugu zangu wakiniacha nife sawa nikikuwa sawa lakini bado nampenda kama mtu aliyenizaa.

Lakini kwangu thamani ya baba ni kubwa kuliko ya mama katika maisha yangu sijawahi pata upendo wa mama zaidi ya wema wa kunizaa.

Japo ntakosolewa kwa nilichokiandika ila hayo ndiyo maisha yangu na ndiyo nionavyo mimi.

Mwenyezi Mungu awape pumziko la milele wazazi wangu na wazazi wa wengine waliofariki Amen..
 
mwana wa adam huwa anaweka mapenzi na upendo wake kwa aliye fanya kikubwa hadi alipofikia pasipokujua ni nani kwake na ndo maana baadhi ya watu huwajali na kuwathamini zaidi wale waliowalea pasipo kujali ni mjomba ama jirani, hiyo ndo asili ya mtu
 
Msamehe mama na uwaombee wote pumziko la amani. Baba ana credits kubwa kwenye maisha yako kwasababu ali sacrifice mno. Apumzike kwa amani.
 
Hata kama hivyo hutakiwi kuongea hivyo hiyo mimba yako mama yako alikuwa na uwezo wa kuitoa wakati wowote na Leo usinge kuwepo kuandika upuzi wako

Pia unasema mama yako ameondoka ukiwa na miaka 2
Sasa kwa taarifa yako hakuna kipindi ambacho mama anapata shida kulea mtoto kama kutoka anapozazaliwa hadi miaka 2 ndio kipindi kigumu mno
Kama yupo hai kamuombe msama maana akisoma uzi wako akisikitika hautakuwa na baraka
 
Ninaandika huu uzi japokuwa wengi hawatakubariana na hichi nachosema.

Mimi nimezaliwa mpaka najitegemea sijawahi uona upendo wa mama yangu

My story: Baba yangu na mama yangu walitengana nikiwa na miaka miwili mama aliondoka na kwenda kuolewa na mwanaume mwingine toka hapo baba yangu alikuwa ndiyo mama yangu ndiyo baba yangu.

Baba alihakikisha nakula,navaa,nasoma miaka ikapita nami Mwenyezi Mungu akanijaharia nikamaliza chuo na kupata kazi na kujitegemea.

Mpaka naandika uzi huu wazazi wangu wote wameshafariki Mwenyezi Mungu awapumzishe kwa amani

Kipindi cha msiba wa marehem baba yangu nililia sana kwa uchungu sana maana nilikuwa peke yangu mama yangu kanitenga kaka ambao tumechangia baba tu walikuwa botswana migodini huko hivyo walichelewa kufika msibani niliumia sana kumzika baba yangu peke yangu bila mama yangu kuja msibani.

Baada ya msiba nilisikia ndugu zangu wakisema huyu mtoto kalia sana kwa sababu mama yake alimwacha mdogo sana pia wakati mama yake anaondoka alitamka maneno makali sana kwamba mama yangu alitamka kwamba mimi naondoka namwacha mtoto wenu akifa mtajua nyinyi akipona mtajua nyinyi hayo ni maneno ya mama yangu mbele ya baba yangu na ndugu zangu.

Sababu kubwa ya mama kuondoka nyumbani ni kuwa hali ilikuwa ngumu ya kiuchum nyumbani lakini hata kama ndiyo hivyo mama yangu hakunionea huruma mimi na kuniacha nikiwa na umri mdogo kiasi kile mpaka aniache na baba yangu kweli?

Baadae baba alipata kazi shirika la reli maisha na akawa pia pale nyumbani anafuga kuku nakumbuka na ng'ombe na kulima pia kaka zangu walikuwa wanamsaidia sana kidogo maisha yakabadirika nyumbani lakini baba yangu hakuamua kuoa tena mpaka anapofariki.


Huwa naumia ile kauli aliyotamka mama yangu kwamba kama ndugu zangu wakiniacha nife sawa nikikuwa sawa lakini bado nampenda kama mtu aliyenizaa.

Lakini kwangu thamani ya baba ni kubwa kuliko ya mama katika maisha yangu sijawahi pata upendo wa mama zaidi ya wema wa kunizaa.

Japo ntakosolewa kwa nilichokiandika ila hayo ndiyo maisha yangu na ndiyo nionavyo mimi.

Mwenyezi Mungu awape pumziko la milele wazazi wangu na wazazi wa wengine waliofariki Amen..
Mimi nitakuwa tofauti na wengine. Sitakulaumu kabisa ila nitakupa ushauri. Kwa amara ya kwanza nakutana na mtu anayethamini uwepo wa baba. Hakuna aliyefanya jitihada yeyote kuzaliwa dume au aliyefanya uzembe wowote kuzaliwa jike. Sote tuna thamani sawa mbele ya Mungu. Mimi pia nilijishitukia tu nina mapenzi karibu sawa tu kwa baba na mama ingawa wakati fulani kama yalizidi kwa baba zaidi na sijui kwanini. Uislam unaonekana kumuweka mama juu zaidi ya baba na ukristo nimeona ukisema waheshimu baba na mama upate miaka mingi na heri duniani. Hapa haikusemwa baba aliyekulea vizuri au mama aliyekutunza vizuri, imesemwa tu waheshimu baba na mama baaasi. Kuhusu walikukosea au hawakukulea vizuri, hilo sio haki yako kuhukumu watahukumiwa na aliyewaumba kwa kutotimiza wajibu wao. Na kuhusu kubeba mimba kwa taabu au kujifungua kwa uchungu au baba kwenda kufanya kazi za hatari ili watoto wale wengine hufikia hadi kufirwa sorry lakini ili familia yake ipate salama, kwa hili hatupaswi kulijadili baina ya sisi wanadamu maana hakuna aliyepanga kati yetu iwe hivi. Mie ningekuwa na uwezo ningeamua mke wangu ajifungue kwa urahisi tu kama kunya au wakati wa kujifungua angekuwa anapata raha kama ile aipatayo wakati wa kunanihiliwa. Lakini siwezi sababu sie mie ninayepanga na kuulalamikia utaratibu uliopo naona kulingana na imani yangu ni kama kumkosoa Muumba. LA MSINGI BINADAMU TUEPUKE SANA KUHUKUMU MAANA NA SIE TUTAHUKUMIWA. NA PIA TUEPUKE KUKOSOA UTARATIBU WA ASILI TULIOUKUTA MAANA TUTAKUWA TUNAMKOSOA ALIYEUWEKA
 
Ishhh kuna jamaaa mama yake hampendi kabisaa na yupo hai tenaa mzeee alivyofariki ndiyo kabisaa mazaa hana habari nae.


Nikiri tu Mimi mwenyewe nimelelewa na mzee via mama wa kambo. Kiufupi na wapenda wote.
 
Unajua ni maumivu gani anayopata mama yako pale kichwa chako kinapotoka ukeni wakati wa kukuzaa ? je unaweza lipa nini mpaka mama asahau yale maumivu? what is baba ..yeye si anapumzika tu?
 
Unajua ni maumivu gani anayopata mama yako pale kichwa chako kinapotoka ukeni wakati wa kukuzaa ? je unaweza lipa nini mpaka mama asahau yale maumivu? what is baba ..yeye si anapumzika tu?
Hayo maumivu anayoyapata hayamuhusu mtoto kwa namna yeyote ile. Kama kuna wa kulaumiwa kuhusu hayo maumivu, basi huyo aliyeweka utaratibu kwa mwanamke kuzaa kwa ucungu. Huyo ndo mtupieni lawama zote. Ama sie waume ingelikuwa tuna uwezo basi tungeamrisha kuzaa kuambatane na utamu kama wa kugegedwa vile
 
nilipoona kichwa cha habari nilijua umeniandikia,uzuri wangu wote wapo kila nikitaka kitu babangu hutekeleza haraka na kwa ufanisi lakini mamangu ni mwenye hila mpaka leo hii.ngoja niishie hapa.
 
Unajua ni maumivu gani anayopata mama yako pale kichwa chako kinapotoka ukeni wakati wa kukuzaa ? je unaweza lipa nini mpaka mama asahau yale maumivu? what is baba ..yeye si anapumzika tu?
mkuu hiyo avatar viiipi?
 
nilipoona kichwa cha habari nilijua umeniandikia,uzuri wangu wote wapo kila nikitaka kitu babangu hutekeleza haraka na kwa ufanisi lakini mamangu ni mwenye hila mpaka leo hii.ngoja niishie hapa.
doh!!
pole sana ndugu
 
Inasikitisha ila ni pepo tu lilimpitia mama , akubebe tumboni miezi tisa ashindwe kukutunza ?? Ni pepo !! Nalikemea kwa jina la aliye juu ! Msamehe bure !!
 
Back
Top Bottom