Thadeus Mkamwa aeleza kuhusu mabadiliko ya mtazamo katika hoja anazozitoa Mrishi Gambo

aseenga

Senior Member
Jul 13, 2011
106
86
Kwa siku kadhaa zilizopita, tumemshuhudia mheshimiwa mbunge wa Arusha mjini Mrisho Gambo akichangia hoja bungeni. Hoja zake zimeibua hisia tofauti kati ya wengi kutokana na sababu mbalimbali.

Moja ya sababu hizo inaonekana ni mabadiliko ya ghafla ya mtazamo wake kiutendaji kabla na baada ya kuwa mbunge. Kama mkuu wa mkoa mstaafu, wengi wanadhani na wana haki ya kudhani kwamba alikuwa sehemu ya utekelezaji wa dhuluma mbalimbali walizofanyiwa watu waliokuwa katika himaya ya utawala wake. Hii ni kwa sababu yeye alikuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa.

Swali la kujiuliza kati ya maswali mengi ni, je mtazamo huu wa kwamba Gambo alikuwa sehemu ya udhalimu ni sahihi au sio sahihi? Maswali mengine muhimu ni, Je Gambo anapotoa hoja Bungeni, hoja zake zipuuzwe au zifanyiwe kazi? Je ni haki kumuandama Gambo kwa mchango wake kama mwakilishi wa wananchi wa Jimbo la Arusha mjini?

Ni wazi kwamba, kama Mkuu wa Mkoa wa Arusha, mwajiri wake mkuu alikuwa serikali/Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kama mbunge, yeye ni mwakilishi na msemaji wa wananchi anaowawakilisha bungeni. Je aache kusema madhambi kwa sababu ataonekana kigeugeu? au aseme madhambi na uonevu uliotekelezwa na “Task force” ili aokoe jahazi la roho yake na wale ambao wameumizwa?

Nina imani kwamba Gambo ametafakari kwa kina hoja zake na ufunuo (revelations) wa yale ambayo yangepita kama ndwele. Lakini kuganga yajayo bila kufanyia kazi hoja zake, na kuandama nafsi yake bila ushahidi wa kutosha kwamba na yeye alikuwa mstari wa mbele kupora watu mali zao kwa sheria na kanuni kandamizi, itafanya watu wa Arusha na watanzania kwa ujumla tuendelee kushangaa kimetokea nini kwa Mrisho Gambo.

Kuungama au kutaja hadharani maovu ambayo mtu aliyafanya au alishiriki kuyafanya sio kitu kipya. Ipo mifano mingi tu hata katika vitabu vitakatifu. Mtakatifu Paulo awali aliitwa Sauli na alitesa watu wa Mungu. Baadaye, akapata wokovu na akawa Mtakatifu Paulo. Akaaza kuwa chombo chema na akaacha uovu wake.

Mtakatifu Augustino wa Hippo ni mfano mwingine. Baada ya kuishi maisha yasiyompendeza Mungu, alitubu hadharani akaandika kitabu cha The Confessions of Saint Augustine na akaongoka.

Ni imani yangu kwamba, Gambo hatoi hoja zake ili kuchochea taharuki kwa watu, wala hatoi hoja zake ili kukwepa maswali na uchunguzi kama ule wa viongozi wengine ambao unaendelea, bali ana nia ya dhati ya kuchangia katika kurekebisha hali ya haki na usawa katika jamii.

Ni wazi kwamba pale msalabani, mwizi aliyetubu kwa Yesu alipata msamaha na akaonja pepo haraka sana akilinganishwa na mwizi ambaye aliendelea kumtukana Yesu badala ya kuomba msamaha kwa makosa yake.

Hali kadhalika, mwana mpotevu aliporudi kwa baba yake na kutubu, alisamehewa haraka sana kuliko mwana mkubwa ambaye alijiona ana haki na hivyo hakupenda hata ndugu yake arudi nyumbani. Mwana huyo aliangalia mabaya ya kaka yake tu.

Kwa kusema hivi, sio kwamba namtuhumu Gambo kwa ubaya wowote, bali nampongeza kwa ushujaa anaouonesha licha ya changamoto ambazo atazipata kutoka kwa wengi ambao watamuona msaliti, mnafiki au kigeugeu. Nadhani sio haki kumtazama yeye kama sehemu ya uovu, bali kumtazama katika nafasi mbili za uongozi (ubunge na ukuu wa mkoa) ambazo kwa bahati mbaya zinafungamana sana.

Hoja na ujasiri wa Gambo pia ni dalili kwamba hata wale ambao walikuwa watiifu bila kutumia hulka zao na utashi wao binafsi, kuna wakati wanaangaziwa na mwanga wa ukweli na wanarudi kwenye mstari. Nionavyo mimi, mbunge Gambo ni wa kumpongeza, ni wa kumpa sikio letu ili atusaidie kujua mengi ambayo yeye kama mla kiapo cha utii kwa Rais, ameona awe muwazi na aweze kuliponya taifa.

Jambo la muhimu katika haya yote, ni kwamba Gambo ana kinga za kibunge na hivyo hatuwezi kumuadhibu nje ya Bunge kwa sababu anayotamka yana kinga za kibunge. Labda Bunge lenyewe liamue kinyume chake kwa mfano kumfukuza Bungeni ili akitoka nje ya Bunge serikali imshughulikie.

Je, kuna mbunge mwenye nia ya kusikiliza hoja za Gambo au wabunge wengi wanakimbilia kutoa taarifa na kuomba mwongozo ili Gambo ashindwe kuendelea kuongelea mambo ambayo yeye mwenyewe anayaita ‘ya maana’?

Je, kugonga meza bungeni wakati mbunge anatoa hoja, iwe hoja chanya au hasi, ni ishara kwamba Bunge litatoa maamuzi na mwelekeo kuhusu hoja, au ni sehemu ya ushereheshaji kama ambavyo tumeshuhudia katika mabunge mengine? Binafsi, napendekeza meza za Bungeni ziwe za chuma ili tupunguze milio ya wagonga meza, au ziwe za kioo, ili kuwe na tahadhari kati ya ushangiliaji hoja na uchangiaji hoja.!
 
Mimi napendekeza juu ya Mesa watandike SPONJI.

MKUU KWA ANDIKO LAKO HAYA NI MUHIMU;
Katiba mpya,
Mkuu wa mkoa ni kiini macho,kifutwe.
GAVANA luoga awajibike,shahidi mkuu wa mkoa.
Viapo kwa rais vifutwe.
Rais awe anateua then waapishwe na jaji
 
All in all, he knows his position kama mbunge is curiously & seriously at stake because alishinda ubunge kwa hoja kubwa kwamba JPM ni mtendaji madhubuti na wala hayumbishwi wala hababaishi katika utekelezaji wa mipango na miradi ya maendeleo ya taifa, tofauti kabisa na watangulizi wake plus huyu Bi Mkubwa mwenyewe.

Lakini sasa hawezi kutumia hoja hiyo tena kwa sababu mwenyekiti wake, obviously, yuko kwenye harakati za kujenga brand yake mwenyewe na kuwafurahisha masponsa na mapromota wachache wakubwa tena kwa kukinzana na yule ambaye kimsingi amempa cheo hicho cha Urais kwa dhamana, so to speak.

Sasa, kwa mantiki hiyo, mbunge wako huyu hana option yoyote nyingineyo, kwa mtazamo wake, isipokuwa kubaki kuwa, as you rightly said, kigeugeu, mnafiki, mbinafsi, mwoga na mwenye mtazamo finyu na dufu.
 
Kama mkuu wa mkoa mstaafu
Neno mstaafulina heshima zake, naona mwandishi unaanza kulitumia vibaya, huyu atafutiwe la kwake kama Mwendazake, hivi Makonda, Sabaya nk utawaita wastaafu kweli?
 
Gambo simwelewi na sitakaa nimuelewe. Mrisho Gambo alipokua mkuu wa mkoa wa Arusha alionea watu wengi sana. Alitumia madaraka yake kibabe, alikua hapatani na viongozi wenzake. Na kwa kua alikua anatafuta kua mbunge kwa nguvu zake zote alikua anaumiza mwananchi yeyote Ili kufikia adhma yake.

Mfano alitoa Amri mama mjane anyang'anywe Mali yake. Tena alinyanyaswa Sana Sana Mali yake ilifungiwa kwenye maduka ya halmashauri na gambo akamwanzishia zengwe eti yule mjane wa watu ni chadema. Hakujali yule mama Ana mkopo wa bank, Ana watoto, anatakiwa alipe TRA, Bali alijali interests zake yeye binafsi.

Mrisho Gambo alkua anajua kabisa Yale ni maduka ya halmashauri na wajenzi waliojenga pale MIKATABA yao ilikwisha kitambo, lakini alkua anazuia halmashauri isipate mapato,, aliruhusu wale kakikundi Cha watu wachache wahofhi Mali ya Jiji na kufukuza wafanyabiashara. Hakujali utu Wala thamani yao. Aliwanyanyasa haswa Wanawake. Wengi Sana walinyanyaswa na Gambo.

Mrisho Gambo ni mnafiki, kama anataka Mali za bureau de change zirudishwe, ahakikishe na Mali za yule mjane zinarudi. Yule mjane hajawahi kuwa CHADEMA ( ingawa kua chadema sio dhambi na ni haki ya mwananchi kufanya maamuzi) yule ni CCM siku zote, sisi wenyewe tulishangaa. Na ahakikishe wamama na watu wote ambao alitoa Amri wanyang'anywe Mali zao huku akijua hawadaiwi hata mia wanarudishiwa Mali zao.

Na aseme ni kwanini alikua anaponda mbele ya wale wafanyabiashara serkali ya awamu ya nne?? Hana fadhila kabisa, je alisahau kwamba SERIKALI ya JK ndo ilimwona na ikampa nafasi ya UDC?

Anachofanya saizi ni Anatafuta uwaziri na hafai, hafai, hafai kwakuwa ni mtu wa majungu na fitna.
 
Kwanza atoke hadharani atubu madhambi yake si kutetewa na wapambe ama watumwa wake.

Kama hakutubu na kuomba radhi bado tutamuona MNAFIQ si kinyume chake kwani "ukifuatana na mwizi hatutaona utakatifu wako.."
 
Kwa hiyo kura za ubunge alipataje ikiwa hakuwa na mahusiano na wananchi.
Jina lake huko CCM Arusha lilipitaje?
Je, kamati ya maadili haikuona hayo.
Nani mnafiki Gambo au Wapiga kura wa Arusha.
 
Kwanza atoke hadharani atubu madhambi yake si kutetewa na wapambe ama watumwa wake...
Kama hakutubu na kuomba radhi bado tutamuona MNAFIQ si kinyume chake kwani "ukifuatana na mwizi hatutaona utakatifu wako.."
Kama GAMBO ni mkweli basi ajiuzulu ubunge kwani alishinda kwa dhuluma tu.Au anasubiri muda wa miaka mitano iishe aanze kutuambia uongo wake tena kuwa haikuwa haki yeye kuwa mbunge na aliingia kwa kulazimishwa.Tuwaogope kama ukoma watu kama hawa.
 
Well said my friend!!!

Nashukuru sana kwamba umejitahidi kuwazungumzia baadhi ya watumishi wa Mungu kwamba hapo mwanzo walikuwa wakatili sana lakini badae wakabadilika na kuwa watu wema sana machoni pa Mungu na wanadamu. Umewataja kama akina; Paulo, St. Augustine, yule mwana mpotevu n.k.

Lakini kumbuka kuwa the bottom line here ni kwamba hao uliowataja walitubu kwanza makosa yao au dhambi zao ndipo wakaongoka na jamii pamoja na Mungu wakawapokea.

Haifai Mr. Mrisho Gambo aendelee kuyakosoa matendo mabaya ya Serikali iliyopita kwa wananchi wake wakati yeye mwenyewe alikuwa miongoni mwa watendaji wakuu wa Serikali hiyohiyo tena katika ngazi ya Mkuu wa Mkoa.

Tunataka Mrisho Gambo ajitokeze hadharani na atubu kwanza mambo ya hovyo aliyoyafanya kwa wananchi akiwa kiongozi wa Serikali, laa sivyo ataonekana ni MNAFIKI.

Asante!
 
Back
Top Bottom