Thomas David
Member
- Aug 22, 2008
- 51
- 3
Let me be too hard on these friends of mine today (TGNP,TAMWA et al)
Hata kama leo mtapewa 50% ya uwakilishi bungeni na huo upendeleo kwa asilimia kubwa lazima utoke CCM (iwe kwa viti maalum au kuteuliwa) sidhani kama utaleta mabadiliko yeyote.
Kwanini?
Hamtaweza kutetea maslahi ya taifa.Uhuru wenu (wanawake wenye nia-aspirants) ulishaporwa hata kabla ya kuingia bungeni.
Bila shaka mnataka kuingia mjengoni kuganga njaa!
Ni masikitiko makubwa, hata baada ya mahakama ya rufaa kukimbia wajibu wake wa kulinda haki za msingi za raia wa nchi hii (Kuacha hukumu ya mbuzi kwa chui au mbwa mwitu au fisi) na kusema jambo lile ni la kisiasa (mimi sijui la kisheria ni lipi-Mahakama ya rufaa inapaswa kutupa jibu) sijaona juhudi zozote kutoka kwenye civil society kulipigia hili kelele ukiachana na tamko la LHRC.
CSO's mko wapi?
TGNP,TAMWA kama hili la mgombea binafsi hamtalisemea na mnataka asilimia 50/50 basi mmepoteza mwelekeo na hakuna tofauti na waganga njaa wengine ambao tunawafahamu na matangazo kwenye televisheni yanayolipiwa na fedha za walipa kodi wa nchi za kigeni basi mwazichezea bure bila hata matokeo ya maana na ole wenu...
Oneni aibu na fungueni vinywa vyenu na mpaze sauti zenu kupita fikra na mikakati ya mwovu ambaye kila kukicha anapanga kila hila kupora haki za mwananchi wa Tanzania ambaye bado yuko kizani
Macho yetu yapo kwenu na twapenda kuona wanawake waingie bungeni kwa kugombea kupitia mgombea binafsi na wawe na uhuru wa kusema na kutetea maslahi ya taifa bila aibu na hiana ya aina yeyote.
Anne Kilango Malecela ni mpiganaji lakini uhuru wake ulishanyakuliwa ndio maana hata mwisho alinywea kabisa na heri asingethubutu kutuhadaa kama alivyofanya. Huzuni na masikitiko yetu na yawe juu yake milele.
Hivyo hatutaki akina Anne Kilango Malecela waingie bungeni kwani hakuna lolote ambalo watatuletea zaidi ya kelele ambazo mwisho wake twaufahamu sisi sote.
Na basi mtoe vichwa vyenu nje ya wingu hilo nene na angalieni mbele nini kinatakikana kufanyika kuwakomboa wanawako ambao mnawapigania kiume.
Kama TAMWA na TGNP wana malengo ya kutuletea akina Anne Kilango Malecela na basi washindwe na kulegea kabisa.
Nawasilisha
Hata kama leo mtapewa 50% ya uwakilishi bungeni na huo upendeleo kwa asilimia kubwa lazima utoke CCM (iwe kwa viti maalum au kuteuliwa) sidhani kama utaleta mabadiliko yeyote.
Kwanini?
Hamtaweza kutetea maslahi ya taifa.Uhuru wenu (wanawake wenye nia-aspirants) ulishaporwa hata kabla ya kuingia bungeni.
Bila shaka mnataka kuingia mjengoni kuganga njaa!
Ni masikitiko makubwa, hata baada ya mahakama ya rufaa kukimbia wajibu wake wa kulinda haki za msingi za raia wa nchi hii (Kuacha hukumu ya mbuzi kwa chui au mbwa mwitu au fisi) na kusema jambo lile ni la kisiasa (mimi sijui la kisheria ni lipi-Mahakama ya rufaa inapaswa kutupa jibu) sijaona juhudi zozote kutoka kwenye civil society kulipigia hili kelele ukiachana na tamko la LHRC.
CSO's mko wapi?
TGNP,TAMWA kama hili la mgombea binafsi hamtalisemea na mnataka asilimia 50/50 basi mmepoteza mwelekeo na hakuna tofauti na waganga njaa wengine ambao tunawafahamu na matangazo kwenye televisheni yanayolipiwa na fedha za walipa kodi wa nchi za kigeni basi mwazichezea bure bila hata matokeo ya maana na ole wenu...
Oneni aibu na fungueni vinywa vyenu na mpaze sauti zenu kupita fikra na mikakati ya mwovu ambaye kila kukicha anapanga kila hila kupora haki za mwananchi wa Tanzania ambaye bado yuko kizani
Macho yetu yapo kwenu na twapenda kuona wanawake waingie bungeni kwa kugombea kupitia mgombea binafsi na wawe na uhuru wa kusema na kutetea maslahi ya taifa bila aibu na hiana ya aina yeyote.
Anne Kilango Malecela ni mpiganaji lakini uhuru wake ulishanyakuliwa ndio maana hata mwisho alinywea kabisa na heri asingethubutu kutuhadaa kama alivyofanya. Huzuni na masikitiko yetu na yawe juu yake milele.
Hivyo hatutaki akina Anne Kilango Malecela waingie bungeni kwani hakuna lolote ambalo watatuletea zaidi ya kelele ambazo mwisho wake twaufahamu sisi sote.
Na basi mtoe vichwa vyenu nje ya wingu hilo nene na angalieni mbele nini kinatakikana kufanyika kuwakomboa wanawako ambao mnawapigania kiume.
Kama TAMWA na TGNP wana malengo ya kutuletea akina Anne Kilango Malecela na basi washindwe na kulegea kabisa.
Nawasilisha