TGIF: Unajua umeanza kuzeeka pale ambapo...

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,460
39,928
1. Ukiulizwa wimbo wa mapenzi unaoupenda sana unasema "Mv. Mapenzi meli ya wapendanao"

2. Ukiambiwa uchague wimbo wa kusindikiza salamu kwa yule umpendaye unasema "Karolina" yeah.. ule wa "siku ulipoondoka ewe Karolina"..

3. Ukiambiwa ni mwanasoka gani wa Tanzania ambaye ni nyota wa zama zote.. bila kusita unasema "Gibson Sembuli"...

4. Ukiulizwa na chombo gani cha kielektroniki ambacho unatumia kusikiliza muziki kila uendako na kinatumia betri kwa haraka unasema "Radio ya National Bendi 4"!

5. Ni mcheza filamu gani unayemhusudu sana kupita wote. Unafikiri mara moja na kusema "Amita Bachichani".. na anayefuatia unasema "Govinda"

6. Ukiulizwa filamu ya mapenzi ambayo unaikumbuka sana unasema "Disco Dancer" hasa pale pa gitaa la umeme!

7. Ukiulizwa kuhusu mwanamuziki mahiri kabisa kutokea katika Tanzania ambaye amefariki kijana bila kuchelewa unamkumbuka "Nico Zengekala"

8. Ukiulizwa ukumbi ambao ulikuwa unapenda kujimwaga kila weekend huchelewi kusema ule wa pale Ubungo (nasikia uligeuzwa Kanisa)

9. Ukiulizwa ni bendi gani unaipenda unasema "Juwata Jazz - Baba ya Muziki"

10 Ukiulizwa ni kikatuni gani ambacho unakumbuka hadi leo kwa tabasamu... unasema ile sherehe aliyoandaa Kipepe Bush na kuwawekea TV za Bush kina Lodi Lofa..
 
Tell me what you read and I will tell you what you are.
Whats the meaning of all that?I didnt get what you are trying to tell us.[/I]
 
Whats the meaning of all that?I didnt get what you are trying to tell us.[/I]

And the article is on the SIASA column.
Is it just an error or the smthg to it.


And bye the way,Huu ukumbi wa ubungo uliobadilishwa kua kanisa ni upi au unamaana ya 92 Hotel pale USHIRIKA TANZANIA STARS (watu njata njata )walipokua wanapiga?

Lakini kama ni hapo
 
Na pale ambapo "Unajua umeanza kuzeeka pale ambapo............., inapowekwa kwenye Jukwaa la siasa.

Am I wrong to assume kwamba haikutakiwa kuwa kwenye Siasa? If I'm wrong, then sorry Mkuu, may be ndio nimeanza kuzeeka.


It's Friday, almost MONDAY, Ooops, almost Week end.
 
Kwa maelezo yako Mwanakijiji hata mimi nadhani umeanza kuzeeka pia manake majina mengi uliyoyataja hapo binafsi siyajui hivyo naweza hitimisha kwa kusema kuwa mimi bado sijazeeka.

Film bora kwangu nitakutajia Blood diamond, mwanamuziki bora nitakutajia Lil wyne, Bendi bora Twanga, mchezaji bora Kaseja, mcheza filam bora denzel washington nk..

Tehe tehe tehe!

Babu Mwanakijiji shikamoo!
 
dance bora itakuwa twisti

halafu viatu vyangu vilikuwa raizoni na travolta ... shati bugaloo au slim fit
 
11.Ukiulizwa nani aliyeimba wimbo wa 'Mapenzi Yanitesa,nikikufikiri wewe....sasa nashangaa....' kabla hata hujameza mate unaitikia 'Mbaraka Mwaruka Mwinshehe wa Moro Jazz'
 
Nafikiri pia ni uzee kama kutokujua leo ni TGIF... nadhani hii inaweza kupelekwa kokote kule...
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom