TGIF: Je unaijua Misingi iliyoliunda Taifa letu?

Nitarudi kujibu baadhi ya maswali ya Mwijage hapo juu.

Kuhusu swali la msingi kwa ufupi jibu ni kuwa Tanzania imejengwa katika msingi wa UTU wa MWANADAMU (THE DIGNIqTY OF MAN). Hii ni falsafa ya juu kidogo kuliko wale waliopigania tu "USAWA NA HAKI ZA WATU". Fikiria kidogo; mtu anaweza kukubali kuwa uko sawa naye mbele ya haki (equality in justice) lakini asikuthamini kama mtu mwenzie. Kwa mfano, mtu anaweza akasema "binadamu wote ni sawa" lakini inapokuja swali la kukuozesha binti yake au binti yako kuolewa kwao anakuona hauko sawa kwa sababu ya rangi, dini, hadhi, cheo n.k Kimsingi anakubali mko sawa kisheria lakini hamna utu sawa! !

MMM,

Umegusa kwenyewe kabisa!!

Na nilazima jaribio lolote la kuikomboa hii nchi kuirudisha kwenye HESHIMA na USTAWI wake wa Kweli kwa kila Mwanachi Lianzie hapo ...lipitieee hapo na kumalizikia hapo!! ...KWENYE UTU!!

Inatakiwa Tafakari ya Kitaifa kuhusu hasa maana ya UTU,*Lazima kuwa na MJADALA WA KITAIFA KUHUSU UTU NI NINI

Unajua nini ... Ingawa UTU ni tunu muhimu kwa mwandamu ... Ni ajabu tukisema tujadii UTU ni Nini ...Utasikia Kuna mtu hajui kuwa UTU ni Nini,...Ambayo Its shame...Mtu kutojitambua kiasi hicho.... UTU hauko kwa mnyama yeyote ila kwa mtu tu!! Na hilo ndilo linaufanya Ubinadamu na Unyama kuwa Tofauti ..Ndio ..UTU NI UUNGU NDANI YA MTU ...Thamani ambayo hakuna kiumbe chcochcote kinachoweza kutambua na kufikia. Hivyo , Lazima hiyo dhamani ijitokeze kwenye kila nyanja ya Ustawi na maisha ya jamii ya kitanznaia.

NB .. Ni Muhimu kuwepo tafakari ya kitaifa kuhusu DHANA YA UTU!! Mjadala wa kitaifa kuhusu UTU NI NINI KAMA MSINGI NA NGUZO YA UJENZI WA TAIFA!!

Hivi kweli Tunajidili vipi kuhusu Kupata katiba ya Nchi Huku Hatujui FOUNDING PRINCIPLE za TAIFA... I am telling you we will miss it all again!*Maana hiyo katiba kwa kifupi ni ingekuwa ni Tafsiri ya utu kwenye nyanja zote za katiba hiyo!!

Vinginevyo tutatengeneza katiba inayowafaa Nyani na tumbili wa mwituni kwani Pasipo na UTU kuna ufisadi usio na tofauti kubwa na unyama wa porini.

Lakini katiba iliyosimamia misinigi ya UTU ni katiba iliyosimamia UUNGU na kutupa kiburi kuimba MUNGU ibariki Tanzania. Na UTU hauna dini, hauna itikadi ya chama, UTU hauna Kabila , UTU hauna JINSIA, UTU hauna Kanda, UTU ni MMOJA KWA KILA MTU ...Nani haoni maana ya Utanzania_

Utanzania ni UTU ...Utanznaia ..sio kabila, Utanznaia, sio dini, Utanznaia sio Ukanda, Utanzania sio Jinsia UTANZANIA NI UTU!!

MIMI NAABUDU KWENYE UTU NA DINI YANGU NI UTANZANIA ... !!
 

Katiba ya mwaka gani!? kati ya hiyo katiba unayoisema na Taifa la Tanganyika na Tanzania ili ilianza kuwepo kabla ya nyingine?
1. Katiba ya mwaka 1977 ambayo pamoja na marekebisho mbalimnali yaliyofanyika Utangulizi haukufanyiwa marekebisho yoyote
2. Hakuna Taifa linaloitwa Tanganyika na hata mtoa mada amezungumzia taifa la Tanzania soma tena hoja ndugu..!
 
1. Katiba ya mwaka 1977 ambayo pamoja na marekebisho mbalimnali yaliyofanyika Utangulizi haukufanyiwa marekebisho yoyote
2. Hakuna Taifa linaloitwa Tanganyika na hata mtoa mada amezungumzia taifa la Tanzania soma tena hoja ndugu..!

Mwaka 1977!!

Iwaje hiyo Katiba ya Mwaka 1977 ndio itoe mwongozo sahihi wa Msingi ya Taifa Letu!?
 
Msingi wa kutunga Katiba yetu umetokana na Misingi iliyojenga Taifa letu ambayo kwenye Utangulizi wa Katiba yetu imetamkwa kama...... UHURU, HAKI, UDUGU na AMANI. Sasa kama kila mtu atachukua kile anachokipenda na kukifanya ndio Misingi ya Utaifa wetu tutakuwa tunazidi kuwachanganya zaidi Watanzania. Nakuu Utangulizi unasema hivi..

UTANGULIZI
MISINGI YA KATIBA

KWA KUWA SISI Wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania tumeamua rasmi na kwa dhati kujenga katika nchi
yetu jamii inayozingatia misingi ya uhuru, haki, udugu na
amani:



Katiba ya mwaka gani!? kati ya hiyo katiba unayoisema na Taifa la Tanganyika na Tanzania ili ilianza kuwepo kabla ya nyingine?

1. Katiba ya mwaka 1977 ambayo pamoja na marekebisho mbalimnali yaliyofanyika Utangulizi haukufanyiwa marekebisho yoyote
2. Hakuna Taifa linaloitwa Tanganyika na hata mtoa mada amezungumzia taifa la Tanzania soma tena hoja ndugu..!

Mwaka 1977!!

Tayari Tanganyika na Tanzania ilikwisha kuwepo kabla ya hiyo katiba, hivyo kumbe hatukutafuta uhuru kwa kuongozwa na hiyo katiba!
 
Mkuu, swali lako ni rahisi kwa kulitazama juujuu lakini ni gumu. Watu wengi ni kweli hatujui. Nisawa na mtu kuuliza kwa nini Tanzania tuna amani. Najiuliza swali hili kila mara, sipati majibu. Siamini kama tunayo ambiwa kuwa ni majibu niyenyewe/siyo.
 
Mwaka 1977!!

Tayari Tanganyika na Tanzania ilikwisha kuwepo kabla ya hiyo katiba, hivyo kumbe hatukutafuta uhuru kwa kuongozwa na hiyo katiba!
Kwa maana hiyo unataka kuniambia kuwa Taifa lolote misingi yake hujengwa wakati wa kutafuta uhuru na si wakati mwingine wowote? kwanini iwe wakati wa kutafuta Uhuru tu na si vinginevyo..? au unataka tufanane na Marekani? Kuna ajabu gani kuainisha misingi ya Taifa baada ya Uhuru..? misingi ilikuwepo lakini imewekwa kwenye official documentation 1977 na hakuna sehemu nzuri zaidi ya kuiweka zaidi ya kwenye Katiba...niambie wewe misingi uliyoitaja imeandikwa wapi?
 
Wasiwasi wangu ni kwamba utaishia ku-quote speeches na maandiko za mwana jumuia mwenzako (a.k.a. mtakatifu nyerere) kama mising ya taifa...too late no going back..<br />
<br />
Taifa letu si yeye na wala yeye siyo authority ya kuunda taifa letu..<br />
<br />
Tutaandaa mising yetu yenyewe wala si matokeo ya ccm ya nyerere a.k.a chadema
<br />
<br />
kila kitu kina mwanzo,we mwanzo wa taifa ili ni upi? Hapa umeulizwa misingi,iwe ilikizi haja au la.mchango wako ni muhimu hadi sasa hujachangia kitu mkuu.
 
Nimefuatia hii discussion with interest. Ninachoshangaa, mtu pekee anayeongelea hiyo 'founding principle' ni Nyerere. Na hata yeye haiongelei directly bali ni quotations katika speeches zake mbali mbali. Sasa nashangaa kweli hii inaweza kuwa a founding principle kama imegusiwa kwa mbali tu na kiongozi mmoja?
Nina maswali kadhaa ambayo nadhani ni muhimu katika ku-discuss hiyo 'founding principle'.
Ni lazima taifa liwe na a founding principle? Ivi 'taifa' la Tanzania lilianza mwaka gani? Nyerere ndio waliunda hilo Taifa au ni lilitokana na kugawanywa kwa Africa mwaka 1884? What makes me a Tanzanian?
Huo UTU WA MWANADAMU ulikuwaje a founding principle katika nchi yenye ma-chief? Wao hawakujiona kuwa na UTU zaidi ya wengine?
Kwa maoni yangu Tanzania haina a 'founding principle'. Hapa ni watu wamejaribu ku-create moja out of the blue.
 
Nimefuatia hii discussion with interest. Ninachoshangaa, mtu pekee anayeongelea hiyo 'founding principle' ni Nyerere. Na hata yeye haiongelei directly bali ni quotations katika speeches zake mbali mbali. Sasa nashangaa kweli hii inaweza kuwa a founding principle kama imegusiwa kwa mbali tu na kiongozi mmoja?
Nina maswali kadhaa ambayo nadhani ni muhimu katika ku-discuss hiyo 'founding principle'.
Ni lazima taifa liwe na a founding principle? Ivi 'taifa' la Tanzania lilianza mwaka gani? Nyerere ndio waliunda hilo Taifa au ni lilitokana na kugawanywa kwa Africa mwaka 1884? What makes me a Tanzanian?
Huo UTU WA MWANADAMU ulikuwaje a founding principle katika nchi yenye ma-chief? Wao hawakujiona kuwa na UTU zaidi ya wengine?
Kwa maoni yangu Tanzania haina a 'founding principle'. Hapa ni watu wamejaribu ku-create moja out of the blue.

Nina shaka kama umesoma posti zote...! soma posti namba 57
 
Msingi wa kutunga Katiba yetu umetokana na Misingi iliyojenga Taifa letu ambayo kwenye Utangulizi wa Katiba yetu imetamkwa kama...... UHURU, HAKI, UDUGU na AMANI. Sasa kama kila mtu atachukua kile anachokipenda na kukifanya ndio Misingi ya Utaifa wetu tutakuwa tunazidi kuwachanganya zaidi Watanzania. Nakuu Utangulizi unasema hivi..

UTANGULIZI
MISINGI YA KATIBA

KWA KUWA SISI Wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania tumeamua rasmi na kwa dhati kujenga katika nchi
yetu jamii inayozingatia misingi ya uhuru, haki, udugu na
amani:


Mwanzomatatu,

Nakubaliana na wewe kwa kiasi chote ...

@ Red .. UHURU, HAKI, UDUGU, AMANI *NI COMPONETS ZA UTU

UTU *ni Uhuru, haki, Udugu, amani .... na zaidi ya Uhuru, Haki, udugu na amani ... Neno Utu lina uzito ..unaopitiliza hapo ... Lakini kwa kuwa matamshi uliyoyaleta yamenukuliwa kwenye katiba inabidi kuafiki lakinio haituzuii sasa kuyaangalia kwa undani na makini zaidi ili kuboresha chochote ambacho kinaihitaji kuboreshwa.*
Bado Napendekeza UTU kuwa ndio founding princilple ya Taifa hili. Na hapo hapo napendekez akuwe na majada wa kutosha kuhusu founding principle hata kabala ya kukimbilia kuijadili katiba. kwa kuwa kama katiba iatkuwa nje hata kidogo tu nje ya Uasili wa mwanadamu ambao ndio Utu wake ..tutakuwa hatujafanya lolote.

Dhana hii sio mali ya Nyerere peke akama wengine wanavyojaribu kuonyesha ...Utu ni dhana pana, iliyoibeba jamii iliyo staarabika, pevu na yenye maendeleo ya kweli. Dhanahii haiwezi kuwa mali ya mtu mmoja au kikundi.*


 

Nina shaka kama umesoma posti zote...! soma posti namba 57

The same question applies to your reasoning. Kwa vile ipo kwenye Katiba basi ndio Misingi? Unaweza kutoa application za hiyo misingi katika Maisha ya taifa letu changa? Au kwa vile tuligombea uhuru basi tumekuwa na msingi wa uhuru? Msingi wa haki umetokea wapi? Au ni watu wameamua tu? Je msingi Amani? na Undugu?
 
Kila taifa lina misingi yake. Misingi ambayo husimama kama maono ya aina ya taifa gani watu wanalitaka kujenga na wananchi wake hujitahidi kuifikia hiyo. Kwa mfano Wamarekani wanachukulia Tangazo la Uhuru na kauli za waasisi wao kuweza kuona misingi yao. Mambo kama Uhuru (liberty) na haki za mtu (individual rights) ni misingi ya Wamarekani.

Je Tanzania ina misingi gani? Je unaifahamu? Je unafahamu Kanuni Nne za mahusiano ya Tanzania? Je unajua ilimaanisha nini kusema wewe ni Mtanganyika au Mtanzania (baada ya Muungano)?

Je umewahi kujifunza misingi hiyo ukiwa shuleni au chuoni?

PICHA ZA IGUNGA

View attachment 37470View attachment 37471View attachment 37472View attachment 37473

Picha za Igunga Mgongoro, Kata ya Igunga

View attachment 37508View attachment 37509View attachment 37510

Kweli Igunga imepata maendeleo. Huyu mzee sasa ana baiskeli mbili.

Mkapa alipokuwa nafungua kampeni za CCM alisema hivi ``wakati yeye anasoma shule alikuwa anatembea kwa miguu lakini sana watoto wanakwenda shule kutumia baiskeli``.

Wenye akili zao wataelewa alikuwa na maana gani.
 
MMM,

Umegusa kwenyewe kabisa!!

Na nilazima jaribio lolote la kuikomboa hii nchi kuirudisha kwenye HESHIMA na USTAWI wake wa Kweli kwa kila Mwanachi Lianzie hapo ...lipitieee hapo na kumalizikia hapo!! ...KWENYE UTU!!

Inatakiwa Tafakari ya Kitaifa kuhusu hasa maana ya UTU,*Lazima kuwa na MJADALA WA KITAIFA KUHUSU UTU NI NINI

Unajua nini ... Ingawa UTU ni tunu muhimu kwa mwandamu ... Ni ajabu tukisema tujadii UTU ni Nini ...Utasikia Kuna mtu hajui kuwa UTU ni Nini,...Ambayo Its shame...Mtu kutojitambua kiasi hicho.... UTU hauko kwa mnyama yeyote ila kwa mtu tu!! Na hilo ndilo linaufanya Ubinadamu na Unyama kuwa Tofauti ..Ndio ..UTU NI UUNGU NDANI YA MTU ...Thamani ambayo hakuna kiumbe chcochcote kinachoweza kutambua na kufikia. Hivyo , Lazima hiyo dhamani ijitokeze kwenye kila nyanja ya Ustawi na maisha ya jamii ya kitanznaia.

NB .. Ni Muhimu kuwepo tafakari ya kitaifa kuhusu DHANA YA UTU!! Mjadala wa kitaifa kuhusu UTU NI NINI KAMA MSINGI NA NGUZO YA UJENZI WA TAIFA!!

Hivi kweli Tunajidili vipi kuhusu Kupata katiba ya Nchi Huku Hatujui FOUNDING PRINCIPLE za TAIFA... I am telling you we will miss it all again!*Maana hiyo katiba kwa kifupi ni ingekuwa ni Tafsiri ya utu kwenye nyanja zote za katiba hiyo!!

Vinginevyo tutatengeneza katiba inayowafaa Nyani na tumbili wa mwituni kwani Pasipo na UTU kuna ufisadi usio na tofauti kubwa na unyama wa porini.

Lakini katiba iliyosimamia misinigi ya UTU ni katiba iliyosimamia UUNGU na kutupa kiburi kuimba MUNGU ibariki Tanzania. Na UTU hauna dini, hauna itikadi ya chama, UTU hauna Kabila , UTU hauna JINSIA, UTU hauna Kanda, UTU ni MMOJA KWA KILA MTU ...Nani haoni maana ya Utanzania_

Utanzania ni UTU ...Utanznaia ..sio kabila, Utanznaia, sio dini, Utanznaia sio Ukanda, Utanzania sio Jinsia UTANZANIA NI UTU!!

MIMI NAABUDU KWENYE UTU NA DINI YANGU NI UTANZANIA ... !!

AMIRI KUU KULIKO ZOTE NI MPENDE BWANA MUNGU WAKO................................... NA NYINGINE INAYOFANANA NA HIYO NI MPENDE JIRANI YAKO KAMA NAFSI YAKO.

BILA YA KILA MTU KUFUATA HII AMRI BASI HAKUNA CHOCHOTE KIZURI KATIKA JAMII YEYOTE ILE.

In addition, napenda kunakili Editor wa gazeti la post la Zambia hapa kutoka kwenye makala yake kuhusu uchaguzi unaofanyika sasa huko Zambia. Hii makala inafaa sana kwa Tanzania pia. Kwa bahari zaidi link yake hii hapa http://www.postzambia.com/post-read_article.php?articleId=23160

Ila kipande hiki nilichoweka hapa ndio naona kinafaa kwa hii hoja.

``
Many outstanding citizens of our country, including the founding father of our Republic Dr Kenneth Kaunda, have spoken on the need for peace. They have stressed the message of love, the very heart of the good news, as being most fundamental to our survival and growth as a nation. That message is timeless. Only love unites. Love leads to honesty in everything. Those who love their neighbours cannot engage in electoral fraud, deception, cheating, manipulation. They cannot engage in acts that amount to rigging of elections.

Honesty, in everything, is the deep desire of all who seek to walk the path of peace. A nation united in purpose, in the pursuit of true ideals such as justice, truth and honest elections, cannot fail to enjoy the blessings of peace. To live together peacefully and harmoniously requires responsible behaviour and honesty in the conduct of elections and other political contests.
If, in any way, you are engaged in electoral malpractices, stop it, don't do it, back out. There is no peace that can be maintained without honest dealings.

Each one of us can only contribute to the maintenance of peace in our country by building the ark of peace in our own hearts. Peace in our country is only possible if there is peace inside our hearts.

It is pointless to call our people to peace, to deplore disorder in our country if we fail to pinpoint the part each of us individually plays in the creation of a political environment that leads to conflict. Electoral malpractices, fraud, manipulation, deceit lead to conflict. Fair political competition, free and fair elections, accurate election results that truly reflect the wishes of the people is what guarantees peace before, during and after elections.

Those who have contributed or are working to contribute to the denial of these things are not working for peace, are promoters of conflict and should be held accountable for the absence of peace in our country.

It is important to realise that the source of conflicts is not solely out there. It is first and foremost located inside the hearts. Conflicts spring from the hearts that are full of hatred and full of greed for power. Peace, as recent world events remind us so vividly, is a frail and fragile possession. So much in us and about us conspires against peace and unity.

Progress would be destroyed by greed for power that leads us to cheat in elections to keep ourselves in power. The forces of discord that unleash themselves in the blood and destruction of conflict are hidden in every human heart. Too often, they surface, to the great distress of others, in the frequently lamented evils of electoral fraud, injustice in all its sordid and selfish guises``
 
Kweli Igunga imepata maendeleo. Huyu mzee sasa ana baiskeli mbili.

Mkapa alipokuwa nafungua kampeni za CCM alisema hivi ``wakati yeye anasoma shule alikuwa anatembea kwa miguu lakini sana watoto wanakwenda shule kutumia baiskeli``.

Wenye akili zao wataelewa alikuwa na maana gani.

Hata wewe Mwanakijiji inawezekana hujui misingi ya kuanzishwa kwa Taifa letu.Je,unajua kupata uhuru mwaka 1961 kulikuwa na maana gani? Why 1961.Je unajua kwa nini TANU ilianzishwa tarehe 7/7/1954(7+7+1+9+5+4=33)?Je unajua kwa nini tunasherehekea 2011 kama mwaka wa hamsini wa uhuru wa Tanganyika?I could go on and on.Kama hujui majibu ya maswali hayo, na mengine yanayofanana na hayo, hujui misingi ya Taifa la Tanganyika.
 
Kwa maana hiyo unataka kuniambia kuwa Taifa lolote misingi yake hujengwa wakati wa kutafuta uhuru na si wakati mwingine wowote? kwanini iwe wakati wa kutafuta Uhuru tu na si vinginevyo..? au unataka tufanane na Marekani? Kuna ajabu gani kuainisha misingi ya Taifa baada ya Uhuru..? misingi ilikuwepo lakini imewekwa kwenye official documentation 1977 na hakuna sehemu nzuri zaidi ya kuiweka zaidi ya kwenye Katiba...niambie wewe misingi uliyoitaja imeandikwa wapi?

Kimsingi Bwana MawazoMatatu, ninachotaka ni kukuweka sawa tu ili husiwe kipofu ndani ya Box la Katiba.

Ukumbuke kuwa Katiba hiyo ilijengwa wakati wa chama kimoja ambapo mifumo ya katiba nchni za Kijamaa na chama kimoja ilikuwa siyo nguzo mama na dira ya kuongoza nchni bali ilikuwa kama mojawapo ya nyezo ikifayakazi kwa pamoja na nyezo zingine kuu ambazo katika mifumo ya vyama vya Kijamaa ikijulikana kama Maazimio ya chama, maana chama ndicho kilichoshika hatamu. Mojawapo la azimio lililo kuwa linatafsiri vyema misingi ya Taifa letu likijulikana kama Azimio la Arusha, na hapa ndipo tulipokosea zaidi, nadhani kabla ya kubadili aina ya siasa mwaka 1992 awali ya yote tulitakiwa kuunda katiba mpya ambayo ingejengwa kwa mfumo wa vyama vingi na siasa za Liberari ambapo katika mfumo huo katiba ndio kila kitu na ndio uhai wa Taifa husika.

Ndio maana utaona watu wana-feel gap kutokuwepo kwa Azimio la Arusha ingawa Katiba ipo! maana vivyo vilifanya kazi kama nyezo tofauti zinazotegemeana. Kwa siasa tunazofuata leo tunapaswa kuwa sasa na katiba ambayo imekamilika na ambayo inaweza kufanya kazi yenye kama nguzo mama ya Taifa hili ikianisha yote na kila kitu.
 
Uhuru na Umoja ulikiuwa Msingi Mkuu wa Nchi yetu. Hata kabla haijatangazwa azimio la Arusha na siasa ya Ujamaa, msingi na katika kauli mbalimbali ilikuwa ni Uhuru na Umoja.

Ikaja kuingizwa hata katika siasa ya Ujamaa, na sehemu mojawapo ya maandiko ya ujamaa kulikuwa na sentensi hii " Msingi wa Ujamaa ni kuamini umoja wa watanzania na kwamba watu huinuka pamoja na huanguka pamoja"
 
AMIRI KUU KULIKO ZOTE NI MPENDE BWANA MUNGU WAKO................................... NA NYINGINE INAYOFANANA NA HIYO NI MPENDE JIRANI YAKO KAMA NAFSI YAKO.

BILA YA KILA MTU KUFUATA HII AMRI BASI HAKUNA CHOCHOTE KIZURI KATIKA JAMII YEYOTE ILE.

In addition, napenda kunakili Editor wa gazeti la post la Zambia hapa kutoka kwenye makala yake kuhusu uchaguzi unaofanyika sasa huko Zambia. Hii makala inafaa sana kwa Tanzania pia. Kwa bahari zaidi link yake hii hapa http://www.postzambia.com/post-read_article.php?articleId=23160

Ila kipande hiki nilichoweka hapa ndio naona kinafaa kwa hii hoja.

``
Many outstanding citizens of our country, including the founding father of our Republic Dr Kenneth Kaunda, have spoken on the need for peace. They have stressed the message of love, the very heart of the good news, as being most fundamental to our survival and growth as a nation. That message is timeless. Only love unites. Love leads to honesty in everything. Those who love their neighbours cannot engage in electoral fraud, deception, cheating, manipulation. They cannot engage in acts that amount to rigging of elections.

Honesty, in everything, is the deep desire of all who seek to walk the path of peace. A nation united in purpose, in the pursuit of true ideals such as justice, truth and honest elections, cannot fail to enjoy the blessings of peace. To live together peacefully and harmoniously requires responsible behaviour and honesty in the conduct of elections and other political contests.
If, in any way, you are engaged in electoral malpractices, stop it, don't do it, back out. There is no peace that can be maintained without honest dealings.

Each one of us can only contribute to the maintenance of peace in our country by building the ark of peace in our own hearts. Peace in our country is only possible if there is peace inside our hearts.

It is pointless to call our people to peace, to deplore disorder in our country if we fail to pinpoint the part each of us individually plays in the creation of a political environment that leads to conflict. Electoral malpractices, fraud, manipulation, deceit lead to conflict. Fair political competition, free and fair elections, accurate election results that truly reflect the wishes of the people is what guarantees peace before, during and after elections.

Those who have contributed or are working to contribute to the denial of these things are not working for peace, are promoters of conflict and should be held accountable for the absence of peace in our country.

It is important to realise that the source of conflicts is not solely out there. It is first and foremost located inside the hearts. Conflicts spring from the hearts that are full of hatred and full of greed for power. Peace, as recent world events remind us so vividly, is a frail and fragile possession. So much in us and about us conspires against peace and unity.

Progress would be destroyed by greed for power that leads us to cheat in elections to keep ourselves in power. The forces of discord that unleash themselves in the blood and destruction of conflict are hidden in every human heart. Too often, they surface, to the great distress of others, in the frequently lamented evils of electoral fraud, injustice in all its sordid and selfish guises``

Hisia kali nimevutiwa sana na mtizamo wako na ninaafikiana nao kabisa. Kwa haraka utafkiri unatofautina na dhana ya utu kwa msingi wa taifa la tanzania. Laki jibu ni kuwa kwenye dhana ya Utu hali nzima ya upendo imezingatiwa.

Kwenye nembo ya taifa Kuna alama nyingi moja wapo ni mwenge wa uhuru, ambo kwenye post yangu nimeufafanulia kuwa ni alama ya UTU WA TAIFA ...ingawa sasa unafanyiwa mzaha mkubwa.

Ukifanya utafiti wa dhati utagundua kuwa alama hiyo ya Taifa ilikisimamia msingi ya kuzaliwa kwa Taifa la Tanzani ilisimamia Matamshi Matatu yote yakiwa nguzo ya UTU na Ubinaadamu kutafsiriwa kwenye kila nyaja ya kijamii.*

Matamshi hayo ni ... UPENDO MATUMAINI na HESHIMA

...Kuleta UPENDO ...pale penye chuki
...Kuleta HESHIMA ...palipo na dharau
... MATUMAINI ... Kukata tamaa ..

Kwahiyo UTU unaelelezwa na UPENDO, UTU unaelelezwa na HESHIMA na UTU unaelelezwa na MATUMAINI

Kwannii neno UTU ... Lisimame badala ya meatamshi mengine yote kwenye Thread hii ...Hilo ndio jambo la kujadiliwa!!!
 
The same question applies to your reasoning. Kwa vile ipo kwenye Katiba basi ndio Misingi? Unaweza kutoa application za hiyo misingi katika Maisha ya taifa letu changa? Au kwa vile tuligombea uhuru basi tumekuwa na msingi wa uhuru? Msingi wa haki umetokea wapi? Au ni watu wameamua tu? Je msingi Amani? na Undugu?
Mkuu Chapakazi, Ofcoz Misingi ya Taifa lolote lazima watu wakae waamue, na Application ya hiyo misingi ndio kama nilivyonukuu kwamba katiba yetu imetungwa kwa Kuzingatia misingi ya Taifa letu kwa maana ya uhuru wa watu wake, haki sawa kwa wote Udugu na Amani ulitaka application gani tena..? Hata misingi iliyounda taifa la Marekani ilibuniwa na Viongozi wao vilevile yaani Life,Liberty, pursuit of Happiness.
 
Tikerra,

Ninadhani misingi, au 'UTU', anaouzungumzia Mzee Mwanakijiji (na wengine waliochangia mada hii) ni values ambazo huwa ni msingi wa kulisimika taifa-hali. Misingi hiyo mara nyingi huwa haina uhusiano wa karibu na itikadi za vyama katika jamii ya kisiasa. Na, ingawaje, katika jamii hiyo huwepo vyama mbali mbali vyenye mirengo tofauti, values (misingi) ambapo taifa limesimikwa haibadiki kutokana na chama kingine kuja madarakani.

Kwa hiyo utakuta, mathlan, nchini Denmark, Sweden, Norway, Finland na Iceland vyama vya mhafidhini (Conservative Parties), vinatofautiana sana na vyama vya mhafidhini vya huko Marekani na United Kingdom. Kwa maana, hata kama chama cha mhafidhini kikichaguliwa kushika madaraka, hakiwezi kufuta sera muhimu za kijamii ambazo kwa pamoja, huwa ndiyo misingi ambapo mataifa haya yamejengwa. Na, kuna suala la usawa baina ya watawala na watawaliwa. viongozi wa mataifa niliyoyataja mwanzo huchanganyika na raia wao bila ulinzi. Hata pale mkasa unapotokea, bado hausababishi nchi hizi kuacha msingi huu. Chukua mifano hii.


Kunako saa tano na dakika ishiri na moja hivi, usiku wa tarehe 28 Februari 1986, Waziri Mkuu wa Sweden, Olaf Palme, alipigwa risasi na kuuwawa katika mtaa mmoja, mjini Stockholm. Mkewe, Lisbeth, alinusurika kifo ingawa alijeruhiwa. wapo wanaodai kwamba Olof Palme aliuawa kwa kuwa hakuwa na wapambe. Lakini pamoja na hoja hii (na uzito wa tukio lenyewe) jamii ya Kiswede, ilikataa kubadili msingi huu. Mambo hayakuishia hapo.


Asubuhi ya tarehe 11 Septemba 2003, Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa wakati huo (na aliyekuwa akitumainiwa kuwa baadaye angelikuwa Waziri Mkuu wa nchi hiyo), Anna Lindh, alichomwa kisu mara kadhaa na mtu aliyesemekana kuwa na maradhi ya kichwa. Alikufa kutokana na majeraha ya kuchomwa kisu. Kama Waziri Mkuu Palme, Anna Lindh alikuwa akifanya shopping peke yake bila walinzi. Lakini pamoja na uzito wa tukio hili pia, serikali ya Sweden haikufikiria kubadili msingi huu. Hata leo, karibu mataifa yote ya ki-Nordic viongozi wa kisiasa na serikali huchanganyika na raia wao. Ni msingi ambapo taifa lao limejengwa. Kwa hiyo, tiba na elimu kwa kila mkazi na raia wa nchi hizi n.k. kwao ndiyo 'Utu' anaouzungumzia Mzee Mwanakijiji, na wengineo. Dhahiri, mataifa mengine wanauona 'Utu' huo kupitia macho yao; na, hii ndio sababu mojawapo misingi ambapo taifa-hali hujengwa, huwa ni tofauti kati ya nchi na nchi. Lakini la muhimu, huwa misingi hii haibadiliki.


Swali ni ilikuwaje misingi hiyo ikabadilika nchini mwetu? Au, bado ipo? Kama ipo kweli, inamfaa namna gani raia wa kawaida ambaye ni mlengwa? Kwa nini katika nchi nyingine isiwe rahisi kubadilisha misingi hiyo lakini iwe rahisi nchini mwetu? Si, misingi (ya 'Utu') inasemekana kuwemo katika katiba ya taifa letu kama baadhi ya wana JF walivyoonyesha? Au umuhimu wa katiba si maandiko yenyewe bali nguvu za kisheria inazopewa katiba na hao wanaoiendesha kwa niaba yetu? Je! viongozi wetu wanapoipuuza misingi hiyo na kujaribu kujenga misingi mipya wanafanya hiyo kwa faida ya taifa au..? Je! nguvu za kufanya hivi, bila kujali maoni ya Mtanzania kwa ujumla, zinatokana na ukweli kwamba Mhimili wa Utawala (ambao hutekeleza sheria) umejilimbikizia madaraka mengi mno kuliko Mihimili mingine? Je! raia afanyeje maoni yake yakipuuzwa miaka nenda rudi? Je! ategemee vyama vya upinzani tu kurekebisha hali hii? Je! vyama vikishindwa kutimiza ahadi kwa mpiga kura (imepata kutokea) kabwela afanyeje? Na Mhilimili wa Nne je unaowahusisha waandishi wa habari kwa umma? Si ni Mhihimili huu unaopashwa kuhakikisha kwamba viongozi wa kuchaguliwa wanalinda viapo vya ofisi zao na ahadi zao kwa mpiga kura? Hau vidole havikunyooshwa wakati sahihi-kabla ya mambo kutoka nje ya mkono? Je! uongozi wa taifa unaposhindwa kusikiliza kilio cha Mtanzania unafanya hivyo kwa hiyari zao au kutokana na msukumo wa nje? Kama la mwisho ni kweli, msukumo huo unatokana na nini? Je! inawezekana wafadhili ambao kwa miaka 50 hivi sasa wamekuwa wakituazima kasma, wanapendelea viongozi wetu wawajibike kwao zaidi, ili walao waweze kuwahakikishia walipa kodi wa nchi hizo (za kifadhili) kwamba maslahi yao yako salama nchini Tanzania? Kama upo ukweli katika hili, je, tulichukua mikopo hiyo bila ya kufahamu kwamba tunaiweka Tanzania 'poni'? Hivi, mikopo hiyo yote tuliitumiaje? Kuendeleza ustawi wa jamii yetu au kuwasaidia wenzetu ambao bado walikuwa chini ya ukoloni mkongwe ili nao wajitawala nasi tujiridhishe kwamba sasa uhuru wetu ni 'kamili'? Vipi, huko kwenye mataifa tuliyoyakomboa Watanzania hawawezi kwenda huko kuweka vitega uchumi? Je! hawawezi ku reciprocate kinamna kutusaidia gharama za a luta continua, kama nazo zinachangia madeni yetu? Tayari tunajua tuliko toka na tulipo, tuithibitije hali?

Hata wewe Mwanakijiji inawezekana hujui misingi ya kuanzishwa kwa Taifa letu.Je,unajua kupata uhuru mwaka 1961 kulikuwa na maana gani? Why 1961.Je unajua kwa nini TANU ilianzishwa tarehe 7/7/1954(7+7+1+9+5+4=33)?Je unajua kwa nini tunasherehekea 2011 kama mwaka wa hamsini wa uhuru wa Tanganyika?I could go on and on.Kama hujui majibu ya maswali hayo, na mengine yanayofanana na hayo, hujui misingi ya Taifa la Tanganyika.
 
Back
Top Bottom