Slim5
JF-Expert Member
- Jan 7, 2014
- 28,108
- 37,641
Juzi kati hapa, nilikuwa naangalia mechi moja ya La Liga, Bacca walishinda 4 au 5, lakini ndani ya dk 30 za mwanzo walikuwa wamebanwa! Matokeo yakiwa 0-0 Messi akiwa ndani ya 18 akapewa cross ambayo mpira ulikuwa ushatoka dhahiri, hata mpigaji aliona umetoka, na timu pinzani yote walishanyoosha mikono na kuanza kuondoka wakijua goalkick! Mchazaji mmoja akafanya kama anausukuma kwa kipa ili auchukue aweke goalkick, mpira ukatinga nyavuni! Bacca wala Messi hawakushangilia Goal, wale jamaa sijui Alaves wale, wakamvaa lineman, lakini wapi! Natamani Manara awe msemaji wa ile timu!