TFF ya Malinzi yashikishwa adabu

Odili

JF-Expert Member
Feb 8, 2015
1,764
1,378
Ninayo furaha kuwafahamisha kuwa leo TFF ya malinzi imenyoshwa mara baada ya Yanga kuruhusu watu waingie bure kwenye mechi ya TP Mazembe na Yanga.

Hapa kilichonifurahisha ni kile kipengere cha kugawana mapato. Kwa hiyo kama pato ni Tshs 0 basi wanagawana hiyo 0 kila mmoja na asilimia zake. Malinzi ajifunze aache figisu katika soka la bongo analiua.

Nampongeza sana Manji kwa mikakati yake madhubuti ya kupambana na hili kupe la soka hapa nchini.
 
Akili za Kibongo.
Tff anakosa mapato na Yanga anakosa mapato. Hakuna aliyefanikiwa kwa sababu mwisho wa siku club inahitaji fedha, si ya kumywezesha kubaki hapo ila kuifanya ikue zaidi.

Wakati "masikini Yanga na Tff" mkishindanisha umasikini yeye Manji yanamnyookea.

Kwa sababu haitaji vipesa vya Yanga wala Tff, yeye anataka kuendeleza jina lake kubwa kwa manufaa ya biashara zake.

Kalaghabaho..
 
Manji anajua kuwanyoosha TFF

Kwenye uchaguzi wa yanga napo kupe lilitaka kuleta mafigisu aise sikutegemea bonge la counter attack kali toka kwa Manji lingemnyong'onyeza bwana kupe. Kupe kabamizwa na uchaguzi ukafanyika kama yanga walivyotaka.

Sasa hivi kupe limenusa ulaji pale stand united ya Shinyanga tayari limevurugavuruga kila kitu pale na linataka kupenyeza mirija ya kunyonya pesa za mdhamini ambaye nadhani ni ACCACIA.

Soka letu linatakiwa lipate watu aina ya Tenga siyo haya makupe yananyonya afya ya soka letu linadhoofika mbaya.
 
Yale Mafurushi ya Ticket feki ya TFF na Makomandoo feki wa milangoni walizojipanga kuziuza leo wakawauzie wapika supu wa pale Opposite na Msimbazi police central wawashie moto.
Mnyoosho wa Manji nimeukubali
 
Yale Mafurushi ya Ticket feki ya TFF na Makomandoo feki wa milangoni walizojipanga kuziuza leo wakawauzie wapika supu wa pale Opposite na Msimbazi police central wawashie moto.
Mnyoosho wa Manji nimeukubali
Wakiwepo watu aina ya Manji kama 6 tu kupe atanyoka zaidi ila ndo hivyo tena vilabu vingine vinamtetemekea as if kashushwa toka mbingu ya 7.
 
Ninayo furaha kuwafahamisha kuwa leo TFF ya malinzi imenyoshwa mara baada ya Yanga kuruhusu watu waingie bure kwenye mechi ya TP Mazembe na Yanga.

Hapa kilichonifurahisha ni kile kipengere cha kugawana mapato. Kwa hiyo kama pato ni Tshs 0 basi wanagawana hiyo 0 kila mmoja na asilimia zake. Malinzi ajifunze aache figisu katika soka la bongo analiua.

Nampongeza sana Manji kwa mikakati yake madhubuti ya kupambana na hili kupe la soka hapa nchini.
Bora tujifariji boss wetu MANJI
 
Bora tujifariji boss wetu MANJI
Hongereni sana na kwa hakika mmepata bosi fundi wa mikakati. Nashauri na vilabu vingine waige mikakati ya yanga ktk kupambana na unyonyaji na ubabaishaji ktk soka. Mtu kashindwa kuongoza masumbwi huko ataweza kuongoza soka ambalo halijui??? Vituko uswahilini for sure.
 
...kwa hiyo na CAF nao hawajapata kitu?!, ila naamini mmejifunza kitu,mpira siku zote unachezwa uwanjani!, wala hauchezwi na mashabiki jukwaani!.

Mmeingizwa wengi kwa lengo la kushangilia ushindi,badala yake mmemwagilia nyasi za uwanja wa taifa kwa machozi!
 
...kwa hiyo na CAF nao hawajapata kitu?!, ila naamini mmejifunza kitu,mpira siku zote unachezwa uwanjani!, wala hauchezwi na mashabiki jukwaani!.

Mmeingizwa wengi kwa lengo la kushangilia ushindi,badala yake mmemwagilia nyasi za uwanja wa taifa kwa machozi!
Mkuu bila shaka umenifananisha na mashabiki wa yanga. Utakua hauko sahihi, mimi si mshabiki wa yanga ila ni mpinga ukupe na unyonyaji unaofanywa na tff. Kama utafuatilia vizuri kwa sasa vilabu vingi vina mgogoro na tff ila yanga ndo angalau wameonyesha uthubutu wa kupambana na upuuzi wa tff. Kwa hiyo hapa nazungumzia unyonyaji wa kupe la tff kwa vilabu vya soka Tanzania.
 
Mm nilicho "NOTE" leo ni kuwa ni bora MAGUFULI aachie tu BUNGE LIVE!! Make Uwanja Taifa (60,000 SEAT CAPACITY) ulijaa saa 2:00 asubuhi tena siku ya J4!! Siku ya kazi!!!

Hata MAGU alete matrekta na Majembe hatulimiii WALAI!!!!
 
Manji ana elimu ya kuelimika,Magu mwenyewe ana mbembeleza aachie coco beach
 
Ndugu hakuna kilichoingia bure hapo. Manji amenunua mechi ile kalipia siti zote za uwanjani.

Tambua kuwa:
Kuna makato ya uwanja
Kuna kodi ya Magu
Kuna hela ya CAF.

Kwa hiyo maji hana mamlaka ya kusema watu waingie bure isipokuwa tu pale akinunua siti zote na kwa hiyo mapato ya wadau wote wa mchezo yako palepale.

Cc. Odili platozoom Rio Tinto Pohamba makedonia bruno castol jd41 Enzymes BONGOLALA
 
SHIRIKISHO la Soka barani Afrika (CAF) na
Shirikisho la Soka nchini (TFF), limeitaka
Yanga kulipa fidia ya gharama za mchezo
wake na TP Mazembe Sh milioni 530.
CAF na TFF imefikia hatua hiyo baada ya
Yanga kufuta kiingilio katika mchezo wao
huo wa makundi wa Kombe la Shirikisho
Afrika unaotarajiwa kuchezwa leo kwenye
Uwanja wa Taifa Dar es Salaam na sasa
mashabiki wataingia bure.
Katika kikao chao cha jana kilichofanyika
kwenye hoteli ya Coral Beach jijini na
kukutanisha maofisa wa CAF, uongozi wa
TFF, Polisi, Wizara ya Habari, Utamaduni,
Sanaa na Michezo na viongozi wa Yanga
wakiongozwa na Katibu mkuu wa klabu
hiyo, Baraka Deusdetit wametakiwa kulipa
kiasi hicho cha fedha kama gharama za
mchezo.
Makato katika mchezo huo wa hatua ya
makundi Kombe la Shirikisho asilimia 15
ya fedha hizo zitaenda CAF, asilimia 15
nyingine gharama ya uwanja, TFF asilimia
tano, Baraza la Michezo la Taifa (BMT),
asilimia 10, na Chama cha soka Dar es
Salaam (DRFA) asilimia tano.
Tayari Yanga ilikuwa imechapisha tiketi
31,000 ambazo zingeuzwa kwa Sh7,000
ambazo zingeingiza Sh 217,000,000 huku
zile za Sh 25,000 zilikuwa zimechapishwa
tiketi 8,200 zingeingiza Sh milioni 205
huku VIP zilikuwa tiketi 5,000 ambazo
zingeingiza Sh milioni 150 jumla ya fedha
zote ambazo zingepatikana katika
mchezo huo ni Sh milioni 572.
Pia Yanga wametakiwa kuingiza
mashabiki wasiozidi 40,000 wakizidi
kiwango hicho mchezo huo utafutwa na
Yanga watalazimika kuwajibishwa.
 
Ninayo furaha kuwafahamisha kuwa leo TFF ya malinzi imenyoshwa mara baada ya Yanga kuruhusu watu waingie bure kwenye mechi ya TP Mazembe na Yanga.

Hapa kilichonifurahisha ni kile kipengere cha kugawana mapato. Kwa hiyo kama pato ni Tshs 0 basi wanagawana hiyo 0 kila mmoja na asilimia zake. Malinzi ajifunze aache figisu katika soka la bongo analiua.

Nampongeza sana Manji kwa mikakati yake madhubuti ya kupambana na hili kupe la soka hapa nchini.
SHIRIKISHO la Soka barani Afrika (CAF) na
Shirikisho la Soka nchini (TFF), limeitaka
Yanga kulipa fidia ya gharama za mchezo
wake na TP Mazembe Sh milioni 530.
CAF na TFF imefikia hatua hiyo baada ya
Yanga kufuta kiingilio katika mchezo wao
huo wa makundi wa Kombe la Shirikisho
Afrika unaotarajiwa kuchezwa leo kwenye
Uwanja wa Taifa Dar es Salaam na sasa
mashabiki wataingia bure.
Katika kikao chao cha jana kilichofanyika
kwenye hoteli ya Coral Beach jijini na
kukutanisha maofisa wa CAF, uongozi wa
TFF, Polisi, Wizara ya Habari, Utamaduni,
Sanaa na Michezo na viongozi wa Yanga
wakiongozwa na Katibu mkuu wa klabu
hiyo, Baraka Deusdetit wametakiwa kulipa
kiasi hicho cha fedha kama gharama za
mchezo.
Makato katika mchezo huo wa hatua ya
makundi Kombe la Shirikisho asilimia 15
ya fedha hizo zitaenda CAF, asilimia 15
nyingine gharama ya uwanja, TFF asilimia
tano, Baraza la Michezo la Taifa (BMT),
asilimia 10, na Chama cha soka Dar es
Salaam (DRFA) asilimia tano.
Tayari Yanga ilikuwa imechapisha tiketi
31,000 ambazo zingeuzwa kwa Sh7,000
ambazo zingeingiza Sh 217,000,000 huku
zile za Sh 25,000 zilikuwa zimechapishwa
tiketi 8,200 zingeingiza Sh milioni 205
huku VIP zilikuwa tiketi 5,000 ambazo
zingeingiza Sh milioni 150 jumla ya fedha
zote ambazo zingepatikana katika
mchezo huo ni Sh milioni 572.
Pia Yanga wametakiwa kuingiza
mashabiki wasiozidi 40,000 wakizidi
kiwango hicho mchezo huo utafutwa na
Yanga watalazimika kuwajibishwa.
 
SHIRIKISHO la Soka barani Afrika (CAF) na
Shirikisho la Soka nchini (TFF), limeitaka
Yanga kulipa fidia ya gharama za mchezo
wake na TP Mazembe Sh milioni 530.
CAF na TFF imefikia hatua hiyo baada ya
Yanga kufuta kiingilio katika mchezo wao
huo wa makundi wa Kombe la Shirikisho
Afrika unaotarajiwa kuchezwa leo kwenye
Uwanja wa Taifa Dar es Salaam na sasa
mashabiki wataingia bure.
Katika kikao chao cha jana kilichofanyika
kwenye hoteli ya Coral Beach jijini na
kukutanisha maofisa wa CAF, uongozi wa
TFF, Polisi, Wizara ya Habari, Utamaduni,
Sanaa na Michezo na viongozi wa Yanga
wakiongozwa na Katibu mkuu wa klabu
hiyo, Baraka Deusdetit wametakiwa kulipa
kiasi hicho cha fedha kama gharama za
mchezo.
Makato katika mchezo huo wa hatua ya
makundi Kombe la Shirikisho asilimia 15
ya fedha hizo zitaenda CAF, asilimia 15
nyingine gharama ya uwanja, TFF asilimia
tano, Baraza la Michezo la Taifa (BMT),
asilimia 10, na Chama cha soka Dar es
Salaam (DRFA) asilimia tano.
Tayari Yanga ilikuwa imechapisha tiketi
31,000 ambazo zingeuzwa kwa Sh7,000
ambazo zingeingiza Sh 217,000,000 huku
zile za Sh 25,000 zilikuwa zimechapishwa
tiketi 8,200 zingeingiza Sh milioni 205
huku VIP zilikuwa tiketi 5,000 ambazo
zingeingiza Sh milioni 150 jumla ya fedha
zote ambazo zingepatikana katika
mchezo huo ni Sh milioni 572.
Pia Yanga wametakiwa kuingiza
mashabiki wasiozidi 40,000 wakizidi
kiwango hicho mchezo huo utafutwa na
Yanga watalazimika kuwajibishwa.
Hapa nimechoka kabisa kwa hii habari.
 

Similar Discussions

3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom