TFF wakanusha taarifa za kujillipa mamilioni. Majina ya watu 10 waliosambaza habari hizo kupelekwa Polisi

Kunguru Mjanja

JF-Expert Member
Aug 22, 2012
2,036
3,929
TFF.jpg

Akizungumza leo Mubashara na kituo cha televisheni cha Azam Tv channeli ya Azam Sport 2, Kaimu Katibu Mkuu wa TFF akanusha tuhuma za kujilipa mamilioni na Kiernan unapoacha jambo la uongo lisambae mwisho litaonekana ni lakweli.

Rejea hapa; Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kujilipa posho mil. 438 kwa mwaka

Anaendelea Kaimu Katibu wa TFF kuwa

"Toka uongozi mpya uingie, tumejitahidi kuhakikisha tunaondoa makandokando hususan ya malipo na rushwa"

"Nataka niwahakikishieni suala la nyongeza ya posho halijawahi kuzungumziwa kabisa,"

"...Ndio kulikuwa na mjadala mkubwa juu ya posho ya kujikimu Rais na Makamu wake. Rais aligoma kupewa posho na kuandaa waraka wa kwanini hataki na amesisitiza mapato yote ya TFF yaende kwenye mpira moja kwa moja,"

"Posho pekee ambayo Rais amekubali iendelee ni Sh1.5 milioni kwa wajumbe wa kamati kuu kila baada ya miezi 3 na si milioni 1 kwa mwezi kama inavyodaiwa,"

"Hatukatai kukosolewa, lakini tukosolewe kwa haki. Siyo kutaka kuchafuliwa bila ya sababu. Tupo tayari kubaldilika. Ukipata habari kuhusu sisi njoo uthibitishe nasi,"

"Lazima tubadili utamaduni wetu wa kuongoza mpira ndani na nje ya TFF. Hivyo, baada ya kikao hiki mwanasheria wetu anaenda kuwaripoti kwenye vyombo husika watu wote waliokuwa wanasambaza taarifa hizi za uongo na kuchafua sura ya TFF,"

"Tayari tuna majina 10 ya watu ambao walikuwa wanasambaza taarifa hizi za uongo na kutuchafua kinyume kabisa na Sheria ya Mitandao. Tunataka wakathibitishe tuhuma hizi kwenye vyombo vya dola,"

"Naamini kuna watu watakaochukia kwa hizi hatua tunzochukua, lakini hatuwezi kurudi nyuma kwenye hili, hakuna aliye juu ya sheria. Lazima, kama mwanahabari uwe na uhakika na unachokiandika, hauwezi kukurupuka tu..."

"Tupo makini sana katika nidhamu ya kifedha, kwa mara ya kwanza TFF imeajiri mkaguzi wa ndani wa hesabu. Leo hii TFF hatulipani kwa 'cash' malipo yote yanafanyika kupitia benki, hii ni sehemu ya uwazi wa kifedha tunaopigania,"
 
Laki tano kwa mwezi ndio iwatoe roho kugombania vyeo namna hiyo? Na hapa naona mmeshaanza kumchafua wambura
 
Kaimu Katibu Mkuu wa TFF Wilfred Kidao ametolea ufafanuzi ujumbe uliosambaa kwenye mitandao ya kijamii ukiituhumu taasisi hiyo inayoongoza soka la Tanzania kuongeza posho kwa wajumbe wa kamati ya utendaji pamoja na kuanzisha malipo ya mishahara kwa Rais na makamu wake.

1. Viwango vya posho za vikao vya Kamati ya Utendaji havijawahi kujadiliwa wala kubadilishwa (kuongezwa). Bado vipo vilevile.

2. Wajumbe wa kamati ya utendaji wanawezeshwa kutekeleza majukumu yao kwenye kanda zao. Ujumbe wa Kamati ya Utendaji ni kazi ya kujitolea watakuwa wakipewa Tsh. 1.5 milioni kwa miezi mitatu kwa ajili ya kutekeleza majukumu yao kwenye Kanda zao (Tsh. 1.5 milioni ni sawa na Tsh. 500,000 kwa mwezi).

3. Kuhusu mshahara wa Rais wa TFF na makamu wake jambo hilo halikufikiwa mwafaka na Kamati ya utendaji. Wajumbe wa kamati ya Utendaji walishauri ofisi ya Rais ihudumiwe na TFF kama ilivyo kwa ofisi za marais wa FIFA na CAF.

Rais wa TFF Wallace Karia alikataa kwa kusema, anaamini sio wakati mwafaka wa yeye kuchukua posho hadi taasisi itakapokaa vizuri na taratibu zote kufuatwa.

Hatua zilizochukuliwa

Kidao amwagiza mwanasheria wa TFF kufungua mashtaka (leo) kwa wale waliosambaza ujumbe kwenye mitandao ya kijamii wenye lengo la kuichafua taasisi hiyo.
Chanzo: Shaffih Dauda blogs
 
Back
Top Bottom