TFF na ufisadi mzito

Kyaruzi

Member
Mar 23, 2007
83
1
Baada ya gazeti la Tanzania Daima kufichukua wizi wa TFF kwenye mapato ya uwanja wa Taifa,wizara husika baadaye iliahidi kushughulikia suala la upotevu wa mapato ya clubs na timu ya Taifa.Rais wa Tff akaahidi kuomba ushirikiano wa wanachi kujua nani anawaibia fedha zao.

Hivi juzi kiongozi mwandamizi wa TFF bwana Daniel Msangi amekamatwa akiwa na vitabu feki kwenye mechi ya Yanga.kuwa bwana Msangi ndiye anayekaa na vitabu vya tiketi feki kiasi cha kuhujumu mapato ya timu na taifa kwa ujumla.

lakini pamoja na Msangi kukamatwa na kulala rumande kwa siku moja badaye TFF ilimrudisha ofisini na sasa anaendelea na kazi zake kama kawaida wakati ana kesi mahakamani.kwa hali hiyo anaweza kuharibu upelelezi wa kesi hii.

Daniel Msangi amewekwa TFF na waziri mmoja kigogo ambaye ni rafiki wa dada ya Daniel Msangi.ndio maana Daniel amekuwa akipewa kila aina ya cheo au wadhifa TFF mara Meneja wa TIMU ya Taifa.

Hivi sasa KaTIBU MKUU wa TFF bwana Mwakalebela anasema kuwa TFF haina senti tano kuandaa timu ya Taifa ya Vijana.wakati hivi karibuni wamepewa mamilioni ya pesa ili kuendeleza mpira na idara nzima ya TFF.

Kutokana na TIMU ya TAIFA kuwa na sapoti kubwa ya serikali viongozi wa TFF wamepata eneo la kuficha na kufanya ufisadi wao.Msangi anaendelea na kazi kwa kisingizio anakabidhi ofisi.

majumba na mali za ajabu anazomiliki Mwakalebela, Tenga na Daniel Msangi ni ushahidi wa kutosha kuthibitisha kuwa TFF kuna ufisadi mkubwa.
http://www.mwananchi.co.tz/newsrids.asp?id=18827
 
Mkaguzi mkuu wa Mahesabu wa serikali inabidi apige hodi kwenye ofisi hii.
 
TENGA inabidi awe mwangalifu sana na kuichunguza timu anayofanya nayo kazi.nashangaa Mwakalebela anatumia ma milioni ya pesa kwenye kampeni zake za ubunge-Iringa wakati TFF inasema haina kitu.
 
Back
Top Bottom