TFF na Karia wachunguzwe. Timu nyingi za ligi kuu masikini.Sababu kuipa haki ya kurusha ligi kuu TV moja tu

Umaskin wa vilabu unatokana na uzembe wa viongoz wa klabu husika,wengi wao si wabunifu wanategemea kwa kiwango kikubwa ufadhil wa NBC na azam pamoja na mapato ya mlangon tu
 
Sijaisoma yote ila hao dstv na hzo channel nyingine walikataa kurusha matangazo ya ligi ya bongo wakidai haina malipo leo imekuwa imara wanaleta unafiki wao wakutaka kurusha hakuna chizi atakae Kubali wakae na hela zao tubaki na njaa zetu.
 
League yetu inahadhi ya kugombaniwa na hizo TV’s ?
Hizo TV’s zimelalamika kwamba zimenyimwa haki ya kurusha league?
Baada ya zabuni kutangazwa zilijitokeza kuomba?
 
Sina shaka hata chembe juu ya uwezo na commitment ya Azam Sports, na ukweli ni kwamba, ingawaje mkataba ni mrefu sana lakini sioni any tv station or media house ambayo ingeweza kufanya ilichofanya Azam Media in terms of ukubwa wa ufadhili (monetary value) na commitment ya kuhakikisha wanaonesha karibu kila mechi! Hakuna kwa sasa ambae angeweza kufanya anayofanya Azam
Unataka niambie Dstv wangeshindwa?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa ufupi tu naomba vyombo vinavyohusika na michezo na RUSHWA WACHUNGUZE MKATABA KATIKA YA TFF NA TV MOJA KURUSHA LIVE MATANGAZO YA LIGI KUU TENA KWA MIAKA 10.GHARAMA WALIZOLIPA NI TAKRIBAN BILLIONI 200 NA USHEE.DUNIANI KOTE HAKUNA TV MOJA INAYOPEWA HAKI BILA YA KUZISHINDANISHI TV ZINGINE.TUNAO STAR TIMES,DSTV, AMBAO INASEMEKANA WALIOMBA LAKINI WAKAKATALIWA.NDIO MAANA TIMU NYINGI NI MASIKINI KWANI HAWAWEZI KUSHINDANA NA TIMU KUBWA SIMBA NA YANGA.ILITAKIWA IWE HIVI ,WOTE HAWA 3 WANAPEWA HAKI KWA KILA TV KUTOA OFA HALAFU WANAPEWA MICHEZO YA KUONYESHA KUTOKANA NA MALIPO.UKIWAJUMLISHA HAWA 3,MFANO AZAM ATATOA BILIONI 200,STAR TIMES BILIONI 200,DSTV BILLIONI 300,JUMLA UNAPATA HAKI ZA MATANGAZO PEKEE BILIONI 700.BADO KUNA PESA ZA WADHAMINI WENGINE KAMA NBC N.K TIMU ZENYE MAPATO MADOGO YATAFAIDIKA SANA.ANGALIA LIGI KUU YA UINGEREZA AMBAYO NI GHALI DUNIANI TIMU ZOTE 18 ZINAFAIDIKA NA MATANGAZO YA TV PEKEE.WAMESHINDANISHWA HIVYO DAU LIKAPANDA SANA.LIGI HIYO ALMAARUFU PREMIER LEAGUE MATANGAZO PEKEE YA TV YANAWAINGIZIA DOLA BILIONI 12.MCHAKATO WAO NI WA MIAKA 3 MITATU TU,SIO KUMI KAMA WA TFF,KARIA NA AZAM.SKYSPORTS WANA ASILIMIA 60,BT SPORTS 20 NA AMAZON 20.HUU MKATABA WA MIAKA 10 WA KARIA,TFF NA AZAM TENA KWA MIAKA 10 UNATIA SHAKA SANA.DAIMA YANGA,SIMBA,AZAM NDIO WATAKAOTAWALA.ISITOSHE WAN'GEGAWANYA KWA TV HIZI 3 AJIRA NYINGI ZINGEPATIKANA.PIA TUNA DSTV AMBAO WANAONEKANA HADI ULAYA,KODI ZINGEONGEZEKA.JAMANI WAZIRI WA MICHEZO AMKA TWENDE NA SPIDI YA DUNIA YA SASA.NAOMBA TENA WAHUSIKA WALICHUNGUZE HILI SUALA.FOOTBALL IS TOP BUSINESS EARNER DUNIANI.HATA TRA AMKENI.NAOMBA KUWASILISHA.
Hakuna tv hapa bongo yenye uwezo wa kurusha matangazo ya moja kwa moja ya mpira zaidi ya azam,, unajua bei ya camera moja tu pale uwanjani?? Mana umeandika kwa chuki na ghababu au wewe unajua tff ndio wanarusha mpira?? Hizo tv hata kama zitapewa hiyo haki lkn sharti wajiunge na azam kurusha hayo matangazo la sivyo wafunge camera zao uwanjani na ndio maana hili jambo linakuwa gumu,,,
 
Nilivyomwelewa mtoa mada, issue sio TV Rights kupewa kituo kimoja bali kutoa TV Rights bila kushindanisha! Kwamba, je TFF just picked Azam na kupewa hizo tv rights au Azam, Star Times, DStv, na wengineo walishindanishwa lakini Azam ndo akaibuka kidedea?! Na kama hawashindanishi, basi jamaa ana hoja!! Na ukiwasikia TFF walivyoingia mkataba na GSM kuna kila dalili hakuna kushindanisha kwa sababu, kama na kwa Azam walipiga hodi kuomba udhamini kama walivyofanya kwa GSM, ina maana hapakuwa na ushindanishi wowote ule.

Hata hivyo, hoja ni kama kweli ziliwepo taasisi zingine kama hao DSTV ambao nao walitaka hizo tv rights lakini TFF wakafunga vioo?!
Kurusha matangazo walishindanishwa na tangazo liliwekwa humu tafuta utaliona
 
Azam ni kama maji usipo itumia kwako utaitafuta hata kwa kibanda umiza shwaini
 
Dstv walishawahi kushindanishwa wakachemka kwa Azam kwa dau na idadi ya mechi watakozoonesha Kama una Dstv kwako angalia ligi za Afrika wanazoonesha na idadi ya mechi kwenye ligi husika, Azam anaupiga Mwingi anatuonesha hata mechi ambazo ni za kawaida kabisa ambapo DStv wasingezionesha

Azam wamejitahidi kuutangaza mpira wetu ndani na nje ya nchi wana Channel mbili za mpira wa ndani ambapo Tv za TBC, ITV, GO TV walishindwa kuonesha, wamepangilia mechi kiasi kwamba tunaziona zote nachowaomba Azam ni kuongeza channel ya 3 ili waondoe mechi za saa 8 mchana haswa katika ukanda wa pwani hazina maana kwasababu ya jua na joto kali, hivyo mechi ziwe zinaanza saa 10 jioni hadi saa 6 usiku maana maeneo kama Dodoma mechi inaweza kuanza saa 4 usiku kwasababu hakuna foleni kali na mji haujapanuka sana na hata pale Mbeye CCm ikiweka taa kwenye uwanja wao basi tunaweza kuangalia mechi hadi saa 6 usiku
Channel mbona zinazidi kuongezwa kwanzia jana tarehe 1 imeeongezwa channel mpya Azam sportHD3 imewashwa
 
Huyo mwanamke alikuwa amekondaaa.
Kapata bwana kamnenepesha anapendeza mnamuona mzuri.
Jiulize Kati ya Azam tv na DStv Nani wa kwanza kuingia BONGO?
ukipata jibu Rudi
 
Kwa ufupi tu naomba vyombo vinavyohusika na michezo na RUSHWA WACHUNGUZE MKATABA KATIKA YA TFF NA TV MOJA KURUSHA LIVE MATANGAZO YA LIGI KUU TENA KWA MIAKA 10.GHARAMA WALIZOLIPA NI TAKRIBAN BILLIONI 200 NA USHEE.DUNIANI KOTE HAKUNA TV MOJA INAYOPEWA HAKI BILA YA KUZISHINDANISHI TV ZINGINE.TUNAO STAR TIMES,DSTV, AMBAO INASEMEKANA WALIOMBA LAKINI WAKAKATALIWA.NDIO MAANA TIMU NYINGI NI MASIKINI KWANI HAWAWEZI KUSHINDANA NA TIMU KUBWA SIMBA NA YANGA.ILITAKIWA IWE HIVI ,WOTE HAWA 3 WANAPEWA HAKI KWA KILA TV KUTOA OFA HALAFU WANAPEWA MICHEZO YA KUONYESHA KUTOKANA NA MALIPO.UKIWAJUMLISHA HAWA 3,MFANO AZAM ATATOA BILIONI 200,STAR TIMES BILIONI 200,DSTV BILLIONI 300,JUMLA UNAPATA HAKI ZA MATANGAZO PEKEE BILIONI 700.BADO KUNA PESA ZA WADHAMINI WENGINE KAMA NBC N.K TIMU ZENYE MAPATO MADOGO YATAFAIDIKA SANA.ANGALIA LIGI KUU YA UINGEREZA AMBAYO NI GHALI DUNIANI TIMU ZOTE 18 ZINAFAIDIKA NA MATANGAZO YA TV PEKEE.WAMESHINDANISHWA HIVYO DAU LIKAPANDA SANA.LIGI HIYO ALMAARUFU PREMIER LEAGUE MATANGAZO PEKEE YA TV YANAWAINGIZIA DOLA BILIONI 12.MCHAKATO WAO NI WA MIAKA 3 MITATU TU,SIO KUMI KAMA WA TFF,KARIA NA AZAM.SKYSPORTS WANA ASILIMIA 60,BT SPORTS 20 NA AMAZON 20.HUU MKATABA WA MIAKA 10 WA KARIA,TFF NA AZAM TENA KWA MIAKA 10 UNATIA SHAKA SANA.DAIMA YANGA,SIMBA,AZAM NDIO WATAKAOTAWALA.ISITOSHE WAN'GEGAWANYA KWA TV HIZI 3 AJIRA NYINGI ZINGEPATIKANA.PIA TUNA DSTV AMBAO WANAONEKANA HADI ULAYA,KODI ZINGEONGEZEKA.JAMANI WAZIRI WA MICHEZO AMKA TWENDE NA SPIDI YA DUNIA YA SASA.NAOMBA TENA WAHUSIKA WALICHUNGUZE HILI SUALA.FOOTBALL IS TOP BUSINESS EARNER DUNIANI.HATA TRA AMKENI.NAOMBA KUWASILISHA.
kitendo ch kutuandikia kwa herufi kubwa hiyo ni sawa na kutufokea, huna adabu.
 
Azam wenyewe Wana camera za kizamani,angalia picha zao zinavyoonekana zimefifia rangi,
Azam gani yenye camera za kizamani unayo izungumzia wewe? Azam channel zote za Mpira ni HD hakuna picha inayofifia ila ni mandhari na pitch mbovu ya viwanja vya mikoani
Alafu uache kutumia TV za chogo ndo maana unaona picha zinafifia kumbe tatizo ni we mwenyewe
 
Dstv walishawahi kushindanishwa wakachemka kwa Azam kwa dau na idadi ya mechi watakozoonesha Kama una Dstv kwako angalia ligi za Afrika wanazoonesha na idadi ya mechi kwenye ligi husika, Azam anaupiga Mwingi anatuonesha hata mechi ambazo ni za kawaida kabisa ambapo DStv wasingezionesha
exactly. niliwahi kuambiwa sababu za dstv kukosa kushinda tena ya kuonyesha mpira wa
miguu tz.

moja ya kigezo cha kukosa kwao tenda kinatokana na maelezo uliyotoa hapo juu. ni kwamba dstv ili base kwenye kuonyesha potential match tu za simba, yanga na azam.
 
Kwenye muongozo wa kutumia jf, kipengele namba 3 kinaeleza kuhusu matumizi ya herufi kubwa! Sasa kinapokiukwa sijui ni kwa nini mods hawachukui hatua…
IMG_0619.jpg
 
Back
Top Bottom