TFF na BMT mpo serious kweli? Hivi Kagere na Morrison wanaliuaje Soka letu?

SankaraBoukaka

JF-Expert Member
Jul 2, 2019
910
1,394
Hili swala la wachezaji wa kigeni linaonekana kama zima moto lakini siyo mwarobaini wa Soka letu.

Hata tukiwa na mmoja wa kigeni soka letu bado lipo hapa hapa, tatizo letu kubwa ni ukuzaji wa vipaji tulivyonavyo. Kama tukiweza kusimamia hilo hata hao wa nje hakuna atakaosumbuka nao.

Cha muhimu ni kutafuta namna sahihi ya kuondokana na udumavu wa Elimu ya Soka.
Tengenezeni miongozo itakayoweza kusimamia FIFA CLUB LICENCING ambayo itafanya tubaki na timu ambazo zinauwezo wa kutengeneza vijana na kujiendesha. Ni bora muwe na ligi yenye timu chache hata 10 ambazo zitasaidia ukuaji wa soka letu.

Nafikiri kwa sasa swala muhimu ni vigezo vya ubora wa hao wachezaji wanaoletwa ambao hauna usimamizi unaoeleweka, hata kwenye ligi za Senegal, Ghana, Ivory Coast, Nigeria, Brazil, Argentina na Uruguay kuna wageni japo ni nchi ambazo zinazalisha wachezaji wengi duniani.

Kwa mtazamo wa haraka, ni kama tunatafuta visingizio ambavyo havitotutoa tulipo badala ya kuandaa msingi ambao utalitengeneza soka letu.

Halafu hii ligi yetu kiuhalisia inatakiwa kuwa na timu zisizidi 12. Maana kama vilabu hata kula ni shida ni vipi tupate Ligi Bora, na haya yote ndo yanatuporomosha. Timu nikiwa chache zitapata udhamini mnono that means zitaweza hata kuhudumia timu za vijana.

BMT na TFF kaeni chini mpange mipango ya kulisaidia SOKA acheni siasa.

Leo tunapigania wageni wakati hata ligi za vijana hakuna.
 
Wachezaji wa kigeni wapungue mpaka watano kwa klabu. Bora usajili wachezaji watano wa maana at least B+ kuliko kusajili 10 vilaza kama wabrazil wa Simba.
Kwani wale wabrazil wa simba bado wapo? Yaani mchezaji atoke Brazil aje kucheza mpira Tanzania? ni ajabu kweli. Ni sawa na kutoa ndizi Far upeleke kuziuza Mbeya!
 
Taasisi za Tz sio imara,kuna waziri tu kakurupuka. sasa hawa wenzangu kwa kukosa misimamo inabidi wafuatishe tamko la waziri. ujinga mtupu
 
Waziri anashindwa kuja na wazo la angalau kila wilaya kuwepo na academy ya soka.. Yeye anatoa wazo la hovyo hv.
Hawa wachezaji wetu wa bongo hawajitumi, hawana MAAJENTI wazuri, hata wacheze peke yao bila wageni bado hakuna kitu
 
Tatizo hapo ni usajili siyo idadi ya wachezaji,kama timu inasajili wachezaji wa nje wabovu hata kungekuwa na sheria za wachezaji watano wa nje wanaweza kusajili wote wabovu.

Hapo ni suala la usajili iangaliwe na siyo kupunguza idadi
Wachezaji wa kigeni wapungue mpaka watano kwa klabu. Bora usajili wachezaji watano wa maana at least B+ kuliko kusajili 10 vilaza kama wabrazil wa Simba.
 
Kungekuwa na timu 12 au 10 ligi ingekuwa bora ,na wadhamini wa vilabu na wa ligi wangekuwa wengi,halafu timu mpaka itoke ligi daraja la kwanza inakuwa iko vizuri sana na ushindani ungekuwa mkubwa mno,sasa hivi timu nyingi hata viwanja hamna havitoshi
Sijui kigezo gani kilitumika kuongeza teams ligi kuu hadi 20, !

TAFUTA MTU YOYOTE UMLAUMU...!
 
Hivi michezo mingine kama riadha,tennis,basketball yenye wenyeji tu tumefika wapi au ligi ya soka ya wanawake yenye wachezaji wa ndani tu tumefika wapi? Au ligi daraja za chini zenye wachezaji wa ndani tu tumefika wapi? Najaribu kuwaza tu
 
Hili swala la wachezaji wa kigeni linaonekana kama zima moto lakini siyo mwarobaini wa Soka letu.

Hata tukiwa na mmoja wa kigeni soka letu bado lipo hapa hapa, tatizo letu kubwa ni ukuzaji wa vipaji tulivyonavyo. Kama tukiweza kusimamia hilo hata hao wa nje hakuna atakaosumbuka nao.

Cha muhimu ni kutafuta namna sahihi ya kuondokana na udumavu wa Elimu ya Soka.
Tengenezeni miongozo itakayoweza kusimamia FIFA CLUB LICENCING ambayo itafanya tubaki na timu ambazo zinauwezo wa kutengeneza vijana na kujiendesha. Ni bora muwe na ligi yenye timu chache hata 10 ambazo zitasaidia ukuaji wa soka letu.

Nafikiri kwa sasa swala muhimu ni vigezo vya ubora wa hao wachezaji wanaoletwa ambao hauna usimamizi unaoeleweka, hata kwenye ligi za Senegal, Ghana, Ivory Coast, Nigeria, Brazil, Argentina na Uruguay kuna wageni japo ni nchi ambazo zinazalisha wachezaji wengi duniani.

Kwa mtazamo wa haraka ni kama tunatafuta visingizio ambavyo havitotutoa tulipo badala ya kuandaa msingi ambao utalitengeneza soka letu.

Halafu hii ligi yetu kiuhalisia inatakiwa kuwa na timu zisizidi 12. Maana kama vilabu hata kula ni shida ni vipi tupate Ligi Bora, na haya yote ndo yanatuporomosha. Timu nikiwa chache zitapata udhamini mnono that means zitaweza hata kuhudumia timu za vijana.

BMT na TFF kaeni chini mpange mipango ya kulisaidia SOKA acheni siasa.

Leo tunapigania wageni wakati hata ligi za vijana hakuna.

Wee ndio unajielewa na kuelewa soka.
 
Kwani wale wabrazil wa simba bado wapo? Yaani mchezaji atoke Brazil aje kucheza mpira Tanzania? ni ajabu kweli. Ni sawa na kutoa ndizi Far upeleke kuziuza Mbeya!
Ndiyo hapo Sasa .... Waste of forex.
 
Tatizo hapo ni usajili siyo idadi ya wachezaji,kama timu inasajili wachezaji wa nje wabovu hata kungekuwa na sheria za wachezaji watano wa nje wanaweza kusajili wote wabovu.

Hapo ni suala la usajili iangaliwe na siyo kupunguza idadi
Kupunguza idadi ni njia ya kufacilitate umakini sawa na kuweka salary cap inavyotumiwa kuzidisha ushindani baina ya timu eg. In NBA
 
Back
Top Bottom