TFF Kuwaleta Eto’o, Kaka Kuchezea Simba Na Yanga

Babuji

Senior Member
Nov 27, 2008
197
3
2716554.jpg

Samuel Eto'o 8/3/2009 5:56:57 AM
SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF), limesema litaweka utaratibu wa kuwaalika wachezaji wanaocheza soka la kulipwa Ulaya kuja Tanzania kuchezea timu za hapa kwa lengo la kuinua kiwango cha soka nchini. Rais wa TFF, Leodegar Tenga alisema lengo la mpango huo ni kukuza kiwango cha soka nchini mara baada ya wachezaji hao kuja kufanya mazoezi ya pamoja na timu za hapa.

"Tunaelekea kwenye soka la kulipwa na hili nadhani ni la msingi. Mfano, tunamchukua Samuel Eto'o aliyeko Inter Milan au Kaka wa Real Madrid au hata Ronaldinho, tunamwuingiza kwenye timu kama Simba au Yanga, wanafanya mazoezi na baadaye mechi, lengo hapa ni kuona utaalamu wake,” alisema Tenga.

"Hawa wenzetu wako mbali na sisi tuwatumie...najua wakati ligi zinaendelea inakuwa ngumu, tunaweza kuweka ka-program baada ya ligi zote kumalizika wachezaji hawa wakaja na inawezekana. Tuna wadhamini wengi, lakini tunasimamia palepale, tunataka kutengeneza mpira wetu," aliongeza Rais huyo wa TFF.

Akizungumzia hali ya soka Tanzania, Tenga alisema kwa sasa anafurahi kuona imepiga hatua kutokana na kuwepo kwa programu mbalimbali za vijana.

Alirejea kauli yake ya awali kuwa anamalizia kutengeneza misingi ili kwa watakaokuja baadaye waweze kuendeleza badala ya kuanza moja.

"Tanzania inao wapenzi wengi wa soka na hili ndilo naweza kusema, msingi wake ni huu, tunajenga na tunaimarisha misingi," alisema Tenga.

Source: http://www.nifahamishe.com/NewsDetails.aspx?NewsID=2716554&&Cat=6
 
Bongo kumbe mna hela za kuchezea haya..Kumbe ndio maana nchi inadidimia!!

Hizo hela kwa nini zisipelekwe kule kijijini kwa wale wasiojiweza???Nchi gani hiyo isiyokuwa na mwelekeo hata wa kuwaonea watu huruma???
 
Sikutegemea mtu kama Tenga anaweza kuwa na mawazo ya ajabu kiasi hicho. Aende Senegal, Ivory Coast, Nigeria, Ghana na Misri akaulize wenzetu wamefanikiwaje hadi wanaweza kucheza na mataifa makubwa kisoka duniani. Haina maana yoyote kumleta Etoo hapa, ni sawa na kuwaambia wachezaji wetu waige wachezaji wa Ulaya kwa kuangalia kwemye Tv au Video. Kile unachoona kwenye TV ni kitu ambacho kimefanyiwa kazi kwa zaidi ya miaka mitano na kuendelea, ni sawa na kuwaambia wanasiasa uchwara popote walipo katika hii sayari wamwangalie Obama anapohutubia halafu wamuige nao wahutubie kama yeye (contents and articulation).
 
Back
Top Bottom