Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,315
- 33,109
DAWA BANDIA aina tano zilizoingizwa nchini kwa ajili ya kutibu ugonjwa wa Malaria zimekamatwa
Dawa hizo zimekamatwa na Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA) kwa kugundulika kuwa ni dawa bandia na hazijasajiliwa
Mkurugenzi Mkuu wa TFDA, Hiiti Sillo, alisema kuwa, dawa hizo zilikamatwa kufuatia ukaguzi uliofanywa na mamlaka hiyo katika maeneo 390 ya kuuzia dawa na kutolea huduma za afya yaliyopo katika mikoa 13 nchini.
Alisema ukaguzi ambao ulifanyika kuanzia Agosti 21 hadi Septemba 8, mwaka huu, ulilenga kubaini ubora na usalama wa dawa zilizopo katika soko na kuchukua hatua stahiki.
Mikoa iliyofanyiwa ukaguzi huo Dar es Salaam, Kigoma, Ruvuma, Dodoma, Mwanza, Mtwara, Lindi, Morogoro, Mbeya, Kagera, Manyara, Pwani naTanga.
Alisema dawa hizo ziliisha muda wa matumizi na kukosekana harufu ya penicillin inayotakwia iwepo kwenye vidonge
Mamlaka hiyo imewataka wananchi kuwa makini na ununuzi wa dawa kuepuka madhara yanayoweza kutokea kutokana na matumizi ya dawa zisizokidhi ubora na usalama.
Dawa bandia zilizokamatwa ni za aina ya Artemether + Lumefantrine (ALU) yenye jina la biashara Coartem, dawa ya kutuliza maumivu ya Ibuprofen, ambayo inauzwa kama Erythromycin Stearate BP 250mg; Penizin-V; Elphedrin, Elphedren na Laifin (Sulphamethoxazole + Pyrimethamine) zote zikiwa katika mfumo wa vidonge.
Chanzo: Nifahamishe.comaya ndugu zangu tujihadhari na Madawa Feki.
Dawa hizo zimekamatwa na Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA) kwa kugundulika kuwa ni dawa bandia na hazijasajiliwa
Mkurugenzi Mkuu wa TFDA, Hiiti Sillo, alisema kuwa, dawa hizo zilikamatwa kufuatia ukaguzi uliofanywa na mamlaka hiyo katika maeneo 390 ya kuuzia dawa na kutolea huduma za afya yaliyopo katika mikoa 13 nchini.
Alisema ukaguzi ambao ulifanyika kuanzia Agosti 21 hadi Septemba 8, mwaka huu, ulilenga kubaini ubora na usalama wa dawa zilizopo katika soko na kuchukua hatua stahiki.
Mikoa iliyofanyiwa ukaguzi huo Dar es Salaam, Kigoma, Ruvuma, Dodoma, Mwanza, Mtwara, Lindi, Morogoro, Mbeya, Kagera, Manyara, Pwani naTanga.
Alisema dawa hizo ziliisha muda wa matumizi na kukosekana harufu ya penicillin inayotakwia iwepo kwenye vidonge
Mamlaka hiyo imewataka wananchi kuwa makini na ununuzi wa dawa kuepuka madhara yanayoweza kutokea kutokana na matumizi ya dawa zisizokidhi ubora na usalama.
Dawa bandia zilizokamatwa ni za aina ya Artemether + Lumefantrine (ALU) yenye jina la biashara Coartem, dawa ya kutuliza maumivu ya Ibuprofen, ambayo inauzwa kama Erythromycin Stearate BP 250mg; Penizin-V; Elphedrin, Elphedren na Laifin (Sulphamethoxazole + Pyrimethamine) zote zikiwa katika mfumo wa vidonge.
Chanzo: Nifahamishe.comaya ndugu zangu tujihadhari na Madawa Feki.