Tetesi za Usajili Ulaya

M6 Media Tz

New Member
Jul 14, 2022
3
7
Chelsea wamefufua nia yao ya kumnunua mlinzi wa Sevilla ya Ufaransa Jules Kounde, 23, baada ya Manchester City kuamua kutomuuza mlinzi wa Uholanzi Nathan Ake, 27 kwa timu ya Thomas Tuchel.

Matumaini ya Chelsea kumsajili Serge Gnabry wa Bayern Munich yamepata pigo baada ya mshambuliaji huyo wa Ujerumani mwenye umri wa miaka 27 kuamua kusalia katika klabu hiyo.


Baada ya kumpata winga wa Leeds United wa Brazil Raphinha, Barcelona wanapiga hatua katika majaribio yao ya kumsajili mshambuliaji mahiri wa Poland Robert Lewandowski, 33.

Arsenal wako tayari kumuuza Nicolas Pepe kwa chini ya ada ya rekodi ya klabu ya £72m waliyomlipa, huku winga huyo wa Ivory Coast mwenye umri wa miaka 27 akiwa sio sehemu ya mipango ya meneja Mikel Arteta.

Mshambulizi wa zamani wa Manchester United Jesse Lingard, 29, anafikiria kuhamia Saudi Arabia ambako anaweza kulipwa £10m kwa mwaka. Mkataba wa mchezaji huyo wa Uingereza United ulimalizika mwezi uliopita.

Arsenal wana matumaini ya kufikia makubaliano ya kumsajili mchezaji mahiri wa Manchester City Oleksandr Zinchenko, 25.

AC Milan wanajaribu kumjaribu winga wa Ureno Rafael Leao kwa kandarasi mpya huku kukiwa na nia ya kumnunua mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23 kutoka Chelsea.

Everton wako kwenye mazungumzo na Burnley iliyoshuka daraja ili kumsajili winga wa Ivory Coast Maxwel Cornet, 25, ambaye alifunga mara tisa katika mechi 26 za Premier League akiwa na Clarets.

AC Milan wanakaribia kutangaza mkataba mpya kwa mshambuliaji wa Sweden Zlatan Ibrahimovic, 40.

Mshambulizi wa Chelsea na Albania Armando Brojo, 20, bado analengwa na Newcastle United, lakini mkufunzi Eddie Howe ameonya kuhusu ugumu wa "bei ya juu na upatikanaji mdogo" huku akijaribu kuimarisha kikosi chake.

Tottenham wanakaribia kumtangaza beki wa timu ya taifa ya England chini ya umri wa miaka 21, Djed Spence kama usajili wao mkuu wa sita msimu huu wa joto. Mchezaji wa Middlesbrough mwenye umri wa miaka 21 amefanyiwa vipimo vya afya katika klabu hiyo ya Premier League kabla ya kununuliwa kwa pauni milioni 15.
IMG_20220716_074036_293.jpg
IMG_20220716_074046_673.jpg
IMG_20220716_074042_384.jpg
 

Attachments

  • IMG_20220716_074042_384.jpg
    IMG_20220716_074042_384.jpg
    24.6 KB · Views: 9
Asante mkuu kwa uzi wako mzuri kuhusu tetesi za Ulaya hiyo Sevilla sijui kwanini wanambania mchezaji wao Kounde ikiwa mchezaji mwenyewe ameshaonesha mlango wakuama team yao?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom