baaaaaasiiiiii tokeo hilo la kidato cha nne na wengne tayari wamekua wakulima kwa mfano mwanafunzi alie somea igunga day Jonh mrefu kaona matokeo yanachelewa ile mbaya
Matokeo ya kidato cha nne kwa mitihani iliyofanyika October mwaka jana yanakaribia kutoka. Katika matokeo hayo ambayo vikao vyake vya mwisho ndio vinafanyika,ufaulu umnaonekana kushuka.Nyaraka zinaonesha kuwa Shule za Seminari,kama ilivyo ada,zinaoongoza.Baadhi ya Shule za Serikali zinajikongoja ingawa ufaulu katika Shule zetu za Kata ni wa utata mtupu.
Matokeo hayo ambayo nimefanikiwa kuyachungulia kiintelijensia yanaonesha kuwa wanafunzi wa Sayansi ndio waliofaulu zaidi ya wale wa masomo ya Sanaa. Wasichana,katika ufaulu wa kitaifa,wameng'ara kuliko wavulana. Hali katika Shule zetu za Serikali hasa za Kata si nzuri hata kidogo. Yakitoka,hapatatosha!
Matokeo hayo yanatarajiwa kutangazwa muda wowote hasa kuanzia tarehe 1/2/2013.
ANGALIZO: Siwezi kutaja kwa majina Shule za kwanza na za mwisho na wanafunzi wa namna hiyo kwakuwa matokeo rasmi hutangazwa na Serikali.
Amefanya kosa gani?unajua umefanya kosa kubwa kisheria lakini mtoa mada?